Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ni Nani Iko Upande wa Yehova?”

“Ni Nani Iko Upande wa Yehova?”

“Unapaswa kumuogopa Yehova Mungu wako, unapaswa kumutumikia yeye, unapaswa kushikamana naye.”​—KUM. 10:20.

NYIMBO: 28, 32

1, 2. (a) Sababu gani ni jambo la hekima kuwa upande wa Yehova? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

NI JAMBO la hekima kwetu kuendelea kubakia karibu na Yehova. Hakuna mutu mwenye kuwa na nguvu, hekima, na upendo zaidi kuliko yeye! Kwa kweli, sikuzote tunapenda kuwa washikamanifu kwake na kuwa upande wake. (Zb. 96:4-6) Lakini, watu fulani wenye walikuwa wanamuabudu Mungu walishindwa kufanya vile.

2 Katika habari hii, tutazungumuzia mifano ya watu fulani wenye walisema kama walikuwa upande wa Yehova, lakini wakati uleule walikuwa wanafanya mambo yenye Yehova anachukia. Mambo ya maana yenye mifano yao inatufundisha yanaweza kutusaidia tubakie washikamanifu kwa Yehova.

YEHOVA ANACHUNGUZA MOYO WETU

3. Sababu gani Yehova alijaribu kumusaidia Kaini, na Yehova alimuambia nini?

3 Fikiria mufano wa Kaini. Hakukuwa anaabudu miungu ya uongo, lakini Yehova hakukubali ibada yake. Sababu gani? Yehova aliona kama Kaini alikuwa na mawazo ya mubaya katika moyo wake. (1 Yo. 3:12) Kwa hiyo, alimuonya hivi: “Ukibadilika na kutenda mambo ya muzuri, je, hautakubaliwa? Lakini kama haubadilike na kutenda mambo ya muzuri, zambi inashutama kwenye mulango, na inatamani sana kukutawala; lakini je, utaishinda?” (Mwa. 4:6, 7) Yehova alipenda kuonyesha wazi kama ikiwa Kaini angetubu na kuchagua kuwa upande wake, yeye pia angekuwa upande wa Kaini.

4. Kaini alifanya nini wakati alikuwa na nafasi ya kuwa upande wa Yehova?

4 Kaini angebadilisha mawazo yake, Yehova angekubali tena ibada yake. Lakini, Kaini hakumusikiliza Mungu, na mawazo na tamaa yake ya mubaya vilimuongoza kwenye matendo ya mubaya. (Yak. 1:14, 15) Wakati Kaini alikuwa kijana, pengine hakuwazia hata kidogo kama siku moja angemupinga Yehova. Lakini hakusikiliza onyo la Mungu, alimuasi Mungu, na kumuua ndugu yake!

5. Ni mawazo ya namna gani yenye yanaweza kufanya tusikubaliwe tena na Yehova?

5 Kama Kaini, leo Mukristo fulani anaweza kusema kama anamuabudu Yehova lakini wakati uleule anafanya mambo yenye Yehova anachukia. (Yud. 11) Pengine anahubiri na kukusanyika kwa ukawaida. Lakini wakati uleule, anaweza kuruhusu mawazo machafu, mawazo ya pupa, ao mawazo ya chuki yatawale akili yake. (1 Yo. 2:15-17; 3:15) Mawazo kama hayo yanaweza kumuongoza afanye zambi. Pengine watu wengine hawajue mambo yenye tunawaza ao kufanya, lakini Yehova anayajua. Anajua ikiwa hatuko upande wake kwa moyo wetu wote.​—Soma Yeremia 17:9, 10.

6. Namna gani Yehova anatusaidia tuachane na tamaa za mubaya?

6 Hata wakati tunafanya makosa, Yehova hatuache mara moja. Kama tunaelekea upande wenye kuwa hatari, Yehova anatuambia hivi: “Munirudilie, na mimi nitawarudilia.” (Mal. 3:7) Yehova anaelewa kama tuko na uzaifu wenye tunapiganisha. Lakini anapenda tukuwe imara na kukataa mambo ya mubaya. (Isa. 55:7) Kama tunafanya vile, anatuahidi kama atatusaidia na kutupatia nguvu zenye tuko nazo lazima ili tuachane na tamaa zetu za mubaya.​—Mwa. 4:7.

USIDANGANYWE

7. Sababu gani Sulemani alipoteza urafiki wake pamoja na Yehova?

7 Wakati Sulemani alikuwa kijana, alikuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova. Mungu alimupatia Sulemani hekima nyingi sana na mugao wa maana wa kujenga hekalu la muzuri sana katika Yerusalemu. Lakini Sulemani alipoteza urafiki wake pamoja na Yehova. (1 Fa. 3:12; 11:1, 2) Sheria ya Mungu ilisema kama mufalme hakupaswa kuoa “bibi wengi, ili moyo wake usipotoke.” (Kum. 17:17) Sulemani hakutii sheria hiyo. Kisha, akafikia kuwa na bibi 700 na masuria 300! (1 Fa. 11:3) Wengi kati ya wanamuke hao hawakukuwa Waisraeli na walikuwa wanaabudu miungu ya uongo. Kwa hiyo, Sulemani hakutii pia sheria ya Mungu yenye ilikataza kuoa wanamuke wenye hawakukuwa Waisraeli.​—Kum. 7:3, 4.

8. Sulemani alifanya mambo gani yenye yalimuchukiza Yehova?

8 Pole kwa pole, Sulemani aliacha kupenda sheria za Yehova. Mwishowe, alifikia kufanya mambo ya mubaya sana. Alijenga mazabahu kwa ajili ya mungu mwanamuke wa uongo mwenye kuitwa Ashtoreti na mungu wa uongo mwenye kuitwa Kemoshi. Kisha aliabudu miungu hiyo ya uongo pamoja na bibi zake. Sulemani alijenga hata mazabahu hizo kwenye mulima wenye ulikuwa mbele tu ya muji wa Yerusalemu, kwenye alikuwa amejenga hekalu la Yehova! (1 Fa. 11:5-8; 2 Fa. 23:13) Pengine Sulemani alijidanganya kwa kuwaza kama Yehova angeachilia mambo yote ya mubaya yenye alikuwa anafanya kwa sababu tu aliendelea kutoa zabihu kwenye hekalu.

9. Ni nini ilitokea kwa sababu Sulemani hakusikiliza maonyo ya Mungu?

9 Lakini Yehova hawezi kuachilia zambi hata kidogo. Biblia inasema hivi: “Yehova akamukasirikia sana Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umegeuka na kuacha Yehova.” Mungu alikuwa amejaribu kumusaidia Sulemani. “Alikuwa amemutokea mara mbili na alikuwa amemuonya juu ya jambo lilelile, kwamba hapaswe kufuata miungu mingine. Lakini hakutii mambo yenye Yehova alikuwa ameamuru.” Kwa hiyo, Yehova hakumukubali tena na hakumutegemeza tena. Yehova hakuruhusu wazao wa Sulemani watawale juu ya taifa lote la Israeli, na kwa mamia ya miaka walikuwa na magumu ya nguvu sana.​—1 Fa. 11:9-13.

10. Ni nini inaweza kutufanya tupoteze urafiki wetu pamoja na Yehova?

10 Kama tunachagua marafiki wenye hawaelewe na kuheshimia kanuni za Mungu, wanaweza kutufanya tukuwe na mawazo ya mubaya na tupoteze urafiki wetu pamoja na Yehova. Wanaweza kuwa katika kutaniko lakini hawana urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova. Ao wanaweza kuwa watu wa jamaa, majirani, wafanyakazi wenzetu, ao wanafunzi wenzetu wenye hawamuabudu Yehova. Kama watu wenye tunapitisha wakati pamoja nao hawaishi kulingana na kanuni za Yehova, wanaweza kutufanya tukuwe na mawazo ya mubaya na tupoteze urafiki wetu pamoja na Yehova.

Watu wenye unapitisha wakati pamoja nao wako na matokeo gani juu ya urafiki wako pamoja na Yehova? (Picha hii inapatana na fungu la 11)

11. Ni nini inaweza kutusaidia kuchagua marafiki?

11 Soma 1 Wakorinto 15:33. Watu wengi wako na sifa fulani za muzuri. Na wale wenye hawamutumikie Yehova, pengine hawafanye mambo ya mubaya sikuzote. Pengine unajua watu fulani kama hao. Je, hilo linamaanisha kama wako marafiki wazuri? Wako na matokeo gani juu ya urafiki wako pamoja na Yehova? Je, wanakusaidia umukaribie Mungu? Ni mambo gani yenye wanaona kuwa ya maana sana? Wanazungumuzia mambo gani? Je, wanazungumuzia sana mitindo ya nguo, feza, vyombo vya kielektroniki vya hali ya juu, mambo ya kujifurahisha, na mambo mengine kama hayo? Je, mara nyingi wanasema-sema mubaya juu ya wengine? Wanapenda kusema mizaha michafu? Yesu alionya hivi: “Kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo.” (Mt. 12:34) Ukiona kama watu wenye unapitisha wakati pamoja nao wanaharibu urafiki wako pamoja na Yehova, tenda bila kukawia! Punguza wakati wenye unapitisha pamoja nao, na kama ni lazima, ukate urafiki huo.​—Met. 13:20.

YEHOVA ANATUOMBA TUKUWE WASHIKAMANIFU KWAKE

12. (a) Kisha tu Waisraeli kutoka Misri, Yehova aliwaambia nini? (b) Waisraeli walisema nini wakati Mungu aliwaomba wakuwe washikamanifu kwake?

12 Mambo yenye yalitokea kisha Yehova kukomboa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri yanaweza pia kutufundisha jambo fulani. Wakati watu walikusanyika mbele ya Mulima Sinai, Yehova alijionyesha kwao katika njia ya ajabu sana! Waliona wingu nzito, umeme wa radi, na moshi, na wakasikia mungurumo na sauti kubwa kama ya baragumu. (Kut. 19:16-19) Kisha, walisikia Yehova anatangaza kwamba yeye ni “Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.” Aliahidi kama atakuwa mushikamanifu kwa wale wenye wanamupenda na kutii amri zake. (Soma Kutoka 20:1-6.) Yehova alipenda Waisraeli wajue kama, ikiwa wanabakia upande wake, yeye pia angekuwa upande wao. Kama ulikuwa kati ya watu hao, ungetenda namna gani kisha kusikia maneno ya Yehova? Pengine ungejibu kama Waisraeli hao wenye walisema hivi: “Maneno yote yenye Yehova amesema, tuko tayari kuyafanya.” (Kut. 24:3) Lakini bila kukawia, jambo fulani lilitokea lenye lilijaribu ushikamanifu wao kwa Mungu. Ni jambo gani?

13. Ni jambo gani lilijaribu ushikamanifu wa Waisraeli?

13 Namna Mungu alionyesha nguvu yake kwa njia ya ajabu iliogopesha sana Waisraeli. Kwa hiyo, Musa alipanda kwenye Mulima Sinai na akazungumuza na Yehova kwa ajili yao. (Kut. 20:18-21) Lakini wakati ulipita, na Musa hakurudia mbio katika kambi. Ilionekana kama watu walibakia katika jangwa bila kiongozi wao. Wangefanya nini? Pengine Waisraeli walitegemea sana kiongozi mwanadamu, ni kusema, Musa. Walianza kuhangaika na kumuambia Haruni hivi: “Ututengenezee mungu mwenye ataenda mbele yetu, kwa sababu hatujue kile kimemufikia huyu Musa, ule mutu mwenye alitutosha katika inchi ya Misri.”​—Kut. 32:1, 2.

14. Waisraeli walijidanganya kwa kuwaza nini, na Yehova alitenda namna gani?

14 Waisraeli walijua kama ilikuwa mubaya kuabudu sanamu. (Kut. 20:3-5) Lakini, bila kukawia walianza kuabudu sanamu ya zahabu ya kitoto-dume cha ngombe! Hata kama walikosa kutii amri za Yehova, walijidanganya kwa kuwaza kama walikuwa wangali upande wa Yehova. Hata Haruni aliita ibada hiyo ya kitoto-dume cha ngombe kuwa “sikukuu kwa ajili ya Yehova”! Yehova alifanya nini? Alimuambia Musa kama watu walikuwa “wamejipotosha” na kuacha njia yenye “aliwaamuru wafuate.” Yehova alikasirika sana na alifikiria hata kuua taifa lote.​—Kut. 32:5-10.

15, 16. Namna gani Musa na Haruni walionyesha kama walikuwa upande wa Yehova kwa moyo wao wote? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

15 Lakini, Yehova ni Mungu mwenye rehema. Aliamua kama hataharibu taifa hilo la Waisraeli. Kuliko kuwaharibu, aliwapatia nafasi ya kuonyesha ikiwa walipenda kuwa upande wake. (Kut. 32:14) Wakati Musa aliona watu wanafanya makelele, wanaimba, na kucheza mbele ya sanamu hiyo ya zahabu, aliiponda-ponda na kuifanya kuwa vumbi. Kisha akawaambia hivi kwa sauti kubwa: “Ni nani iko upande wa Yehova? Akuje hapa kwenye niko!” Na “Walawi wote wakakusanyika kumuzunguka” Musa.​—Kut. 32:17-20, 26.

16 Hata kama Haruni alikuwa ametengeneza sanamu ya zahabu ya kitoto-dume cha ngombe, alitubu, na yeye pamoja na Walawi wengine, walichagua kuwa upande wa Yehova. Watu hao washikamanifu walionyesha wazi kama hawakukuwa upande wa watenda-zambi. Huo ulikuwa uamuzi wa hekima, kwa sababu siku hiyo, maelfu ya watu wenye waliabudu sanamu hiyo ya zahabu waliuawa. Lakini wale wenye walikuwa upande wa Yehova waliokoka, na aliahidi kama atawabariki.​—Kut. 32:27-29.

17. Mambo yenye Paulo aliandika juu ya sanamu ya zahabu ya kitoto-dume cha ngombe yanatufundisha nini?

17 Jambo hilo linatufundisha nini? Mutume Paulo alisema hivi: “Mambo hayo yalikuwa mifano kwetu,” ili “tusikuwe waabudu-sanamu.” Paulo alieleza kama habari kama hizo ‘ziliandikwa ili kuwa onyo kwetu sisi wenye tumefikiwa na miisho ya mipangilio ya mambo. Sasa ule mwenye anawaza kama anasimama afanye angalisho asianguke.’ (1 Ko. 10:6, 7, 11, 12) Kama vile Paulo alisema, hata watu wenye kumuabudu Yehova wanaweza kujiingiza katika matendo ya mubaya. Wanaweza hata kuwaza kama Yehova angali anawakubali. Lakini, sikuzote Yehova hakubali mutu kwa sababu tu mutu huyo anataka kuwa rafiki yake ao kwa sababu anasema kuwa iko mushikamanifu kwake.​—1 Ko. 10:1-5.

18. Ni nini inaweza kutufanya tumuache Yehova pole kwa pole, na hilo linaweza kuwa na matokeo gani?

18 Waisraeli walianza kuwa na wasiwasi kwa sababu Musa hakushuka haraka kutoka kwenye Mulima Sinai kwa wakati wenye walitazamia. Kama mwisho wa mupangilio huu wa mambo haukuje mbio kama vile tulitazamia, sisi pia tunaweza kuwa na wasiwasi. Tunaweza kuanza kufikiri kuwa wakati muzuri sana wenye Yehova anatuahidi ungali mbali sana ao kufikiri kuwa ni ndoto tu. Kwa hiyo, tunaweza kuanza kukazia akili mambo yenye tunapenda kuliko kukazia akili mambo yenye Yehova anapenda. Kama hatuko waangalifu, tunaweza kumuacha Yehova pole kwa pole na kufanya mambo yenye hatukuwazia hata kidogo kama tunaweza kufanya.

19. Tunapaswa kukumbuka nini sikuzote, na sababu gani?

19 Yehova anatuomba tumutii kwa moyo wote na tumuabudu yeye tu. (Kut. 20:5) Sababu gani anatuomba tufanye vile? Kwa sababu anatupenda. Kama hatufanye mambo yenye Yehova anapenda, tutakuwa tunafanya mambo yenye Shetani anapenda, na hilo litatuletea matokeo ya mubaya. Paulo alisema hivi: “Hamuwezi kuwa munakunywa kikombe cha Yehova na kikombe cha pepo wachafu; hamuwezi kuwa munashiriki ‘meza ya Yehova’ na meza ya pepo wachafu.”​—1 Ko. 10:21.

BAKIA KARIBU NA YEHOVA!

20. Namna gani Yehova anaweza kutusaidia hata kama tumefanya kosa?

20 Kaini, Sulemani, na Waisraeli, wote walikuwa na nafasi ya kutubu na kubadilisha tabia yao. (Mdo. 3:19) Kwa kweli, Yehova haache watu mara moja kwa sababu tu wanafanya kosa. Fikiria namna alimusamehe Haruni. Leo, Yehova anatuonya kwa upendo ili kutulinda tusifanye mambo ya mubaya. Anatumia Biblia, vichapo vyetu, na hata Wakristo wenzetu. Wakati tunatii maonyo ya Yehova, tunaweza kuwa hakika kama atatuonyesha rehema.

21. Wakati ushikamanifu wetu kwa Yehova unajaribiwa, tunapaswa kufanya nini?

21 Fazili zenye hazistahiliwe za Yehova ziko na kusudi. (2 Ko. 6:1) Zinatupatia nafasi ya “kukataa matendo ya kukosa kumuogopa Mungu na tamaa za ulimwengu.” (Soma Tito 2:11-14.) Katika ulimwengu huu, sikuzote tutapambana na hali zenye zitajaribu ushikamanifu wetu kwa Yehova. Uazimie kubakia kabisa upande wa Yehova, na ukumbuke kama “unapaswa kumuogopa Yehova Mungu wako, unapaswa kumutumikia yeye,” na “unapaswa kushikamana naye”!​—Kum. 10:20.