Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Watu Wenye Kutoa kwa Ukarimu Ni Wenye Furaha

Watu Wenye Kutoa kwa Ukarimu Ni Wenye Furaha

“Kuko furaha . . . katika kutoa.”​—MDO. 20:35.

NYIMBO: 76, 110

1. Ni nini inaonyesha kama Yehova anaonyesha ukarimu?

WAKATI fulani, Yehova alikuwa peke yake. Kisha akaamua kupatia zawadi ya uzima viumbe vyenye kuwa na akili vyenye kuwa mbinguni na duniani. Yehova, “Mungu mwenye furaha,” anapenda kutoa vitu vya muzuri. (1 Ti. 1:11; Yak. 1:17) Na kwa sababu anapenda sisi pia tukuwe na furaha, anatufundisha kuonyesha ukarimu.​—Ro. 1:20.

2, 3. (a) Sababu gani tunakuwa na furaha wakati tunaonyesha ukarimu? (b) Tutajifunza nini katika habari hii?

2 Mungu aliumba wanadamu kwa mufano wake. (Mwa. 1:27) Ni kusema, wakati Yehova alituumba, alitupatia uwezo wa kuonyesha sifa zake. Ili tukuwe na furaha kabisa na kupata baraka za Yehova, tunapaswa kufuata mufano wake. Tunapaswa kupendezwa na watu wengine na kuwaonyesha ukarimu. (Flp. 2:3, 4; Yak. 1:5) Sababu gani? Kwa sababu ni vile Yehova alituumba. Hata kama hatukamilike, tunaweza kumuiga Yehova na kuonyesha pia ukarimu.

3 Sasa, tutazungumuzia mambo fulani yenye Biblia inafundisha juu ya ukarimu. Tutajifunza sababu gani Yehova anapendezwa wakati tunaonyesha ukarimu. Pia, tutajifunza namna gani kuonyesha ukarimu kunatusaidia kufanya kazi yenye Yehova ametupatia, na sababu gani tunakuwa na furaha wakati tunaonyesha ukarimu. Na tutazungumuzia sababu gani tunapaswa kuendelea kuonyesha ukarimu.

YEHOVA ANAPENDEZWA WAKATI TUNAONYESHA UKARIMU

4, 5. Yehova na Yesu wameonyesha ukarimu katika njia gani, na sababu gani tunapaswa kuwaiga?

4 Yehova anapenda tumuige, kwa hiyo, anafurahi wakati tunaonyesha ukarimu. (Efe. 5:1) Yehova anapenda pia wanadamu wakuwe na furaha. Tunajua jambo hilo kwa sababu alituumba kwa njia ya ajabu, na aliumba dunia yetu ya muzuri sana na vitu vyote vyenye kuwa katika dunia ili tuvifurahie. (Zb. 104:24; 139:13-16) Kwa hiyo, tunamutukuza Yehova wakati tunajikaza kufanya wengine wakuwe na furaha.

5 Tunamuiga pia Yesu, mwenye alionyesha mufano mukamilifu juu ya namna wanadamu wanaweza kuonyesha ukarimu. Alisema hivi: “Mwana wa binadamu hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine na atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” (Mt. 20:28) Na mutume Paulo alitia Wakristo moyo kwa kusema hivi: “Mukuwe na mutazamo huu wa akili ndani yenu wenye ulikuwa pia ndani ya Kristo Yesu . . . Alijiondolea hali yake na akachukua umbo ya mutumwa.” (Flp. 2:5, 7) Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninaweza kufuata mufano wa Yesu kwa ukaribu zaidi?’​—Soma 1 Petro 2:21.

6. Yesu alitufundisha nini kupitia habari ya Musamaria mwema? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

6 Yehova anapendezwa wakati tunafuata mufano mukamilifu wenye yeye na Yesu wametuonyesha. Tunafanya vile wakati tunapendezwa na watu na kutafuta njia za kuwasaidia. Yesu alionyesha kama jambo hilo ni la maana sana wakati alizungumuzia habari ya Musamaria mwema. (Soma Luka 10:29-37.) Alifundisha wanafunzi wake kama wanapaswa kusaidia wengine, hata kama ni watu gani ao wametoka wapi. Unakumbuka sababu gani Yesu alizungumuzia habari hiyo? Ni kwa sababu mwanaume mumoja Muyahudi alimuuliza hivi: “Kwa kweli jirani yangu ni nani?” Jibu la Yesu linatufundisha kama tunapaswa kuonyesha ukarimu kama ule Musamaria ikiwa tunapenda kumufurahisha Yehova.

7. Namna gani tunaonyesha kama tunaamini kuwa mambo yenye Yehova anatuomba tufanye ndiyo ya muzuri zaidi? Eleza.

7 Tuko na sababu ingine ya kuonyesha ukarimu. Sababu hiyo inahusu jambo lenye lilitokea katika bustani ya Edeni. Shetani alisema kama Adamu na Eva wangekuwa na furaha ikiwa wangekosa kumutii Yehova na kujifikiria wao wenyewe tu. Eva alitafuta faida yake mwenyewe na alipenda kuwa kama Mungu. Adamu naye alitafuta faida yake mwenyewe na alitaka kumupendeza Eva zaidi kuliko kumupendeza Mungu. (Mwa. 3:4-6) Matokeo yalikuwa ya mubaya sana. Ni wazi, hakuna mutu mwenye anaweza kuwa na furaha kama anatafuta faida zake mwenyewe. Lakini, wakati tunatafuta faida za wengine na kuonyesha ukarimu, tunaonyesha kama tunaamini kuwa mambo yenye Mungu anatuomba tufanye ndiyo ya muzuri zaidi.

FANYA KAZI YENYE MUNGU AMETUPATIA TUFANYE

8. Sababu gani Adamu na Eva walipaswa kufikiria wengine?

8 Hata kama Adamu na Eva walikuwa peke yao katika bustani ya Edeni, walipaswa kufikiria wengine. Sababu gani? Yehova aliwapatia kazi ya kufanya. Aliwaambia wazae watoto na kujaza dunia na waifanye ikuwe paradiso. (Mwa. 1:28) Adamu na Eva walipaswa kupenda watoto wao wenye wangezaa wakuwe na furaha, kama vile tu Yehova alipenda wote wakuwe na furaha kwenye dunia. Wote, wangetumika pamoja ili kufanya dunia yote ikuwe paradiso. Hiyo ingekuwa kazi kubwa!

9. Sababu gani kazi ya kufanya dunia ikuwe paradiso ingepaswa kuletea wanadamu furaha?

9 Wanadamu wakamilifu walipaswa pia kutumika pamoja na Yehova ili kufanya dunia ikuwe paradiso na kutimiza kusudi lake. Kwa kufanya vile, wangeingia katika pumuziko lake. (Ebr. 4:11) Wazia namna kazi hiyo ingekuwa ya kufurahisha kabisa! Yehova alipaswa kuwabariki sana kama wangetafuta faida za wengine na kuwahangaikia.

10, 11. Ni nini itatusaidia ili tufanye kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi?

10 Leo, Yehova ametupatia kazi ya pekee ya kufanya. Anapenda tuhubiri na kufanya wanafunzi. Ili kufanya kazi hiyo, tunapaswa kabisa kuhangaikia watu. Kwa kweli, tunaweza kuendelea kufanya kazi hiyo kama tu tuko na nia ya muzuri, ni kusema, kumupenda Yehova na kupenda watu.

11 Paulo alisema kama yeye na Wakristo wengine wa wakati wa mitume walikuwa “wafanyakazi pamoja na Mungu” kwa sababu walikuwa wanahubiria watu na kuwafundisha kweli. (1 Ko. 3:6, 9) Leo, sisi pia tunaweza kuwa “wafanyakazi pamoja na Mungu” kwa kutoa kwa ukarimu wakati wetu, nguvu yetu, na vitu vyetu vya kimwili ili kufanya kazi ya kuhubiri yenye Mungu ametupatia. Hilo ni pendeleo kubwa!

Kusaidia mutu fulani ajue kweli kutakuletea furaha kubwa (Picha hii inapatana na fungu la 12)

12, 13. Wewe unaona kuwa kazi ya kufanya wanafunzi inakuletea baraka gani?

12 Kutoa kwa ukarimu wakati wetu na nguvu zetu wakati tunahubiri na kufundisha kunatuletea furaha kubwa. Ndugu na dada wengi wenye wamepata nafasi ya kuongoza mafunzo ya Biblia wanasema vile. Tuko na furaha sana kuona wanafunzi wetu wanafurahi wakati wanaelewa mambo yenye Biblia inatufundisha, wakati wanakomalisha imani ya kweli, wakati wanafanya mabadiliko katika maisha yao, na wakati wanaanza kuambia wengine mambo yenye wanajifunza. Yesu pia alifurahi sana wakati wahubiri 70 wenye alituma ‘walirudia wakiwa na furaha,’ kwa sababu ya mambo ya muzuri yenye walijionea.​—Lu. 10:17-21.

13 Ndugu na dada zetu katika dunia yote wanafurahi wakati wanaona namna ujumbe wa Biblia unasaidia watu katika maisha yao. Kwa mufano, dada mumoja kijana mwenye hajaolewa mwenye kuitwa Anna alipenda kufanya mengi katika kazi ya Yehova. * (Ona maelezo ya chini.) Kwa hiyo, alihamia katika eneo moja la Ulaya Mashariki kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Aliandika hivi: “Kuko nafasi nyingi za kuongoza mafunzo ya Biblia hapa, na ninafurahia sana jambo hilo. Kazi yangu ya kuhubiri inaniletea furaha kubwa. Wakati ninarudia nyumbani, sina wakati wa kuwaza juu ya magumu yangu. Ninafikiria watu wenye ninajifunza nao Biblia, magumu yao na mahangaiko yao. Ninatafuta namna za kuwatia moyo na kuwasaidia katika njia fulani. Na nimekuwa hakika kama ‘kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.’”​—Mdo. 20:35.

Wakati tunatembelea kila nyumba katika eneo letu, tunapatia watu nafasi ya kusikia ujumbe wa Ufalme (Picha hii inapatana na fungu la 14)

14. Tunaweza kufanya nini ili tufurahie kazi ya kuhubiri hata kama watu hawasikilize?

14 Hata kama watu hawatusikilize wakati tunahubiri, tunaweza kuwa na furaha kwa sababu tunawatolea nafasi ya kusikia habari njema. Yehova anatuomba tufanye jambo lilelile lenye alimuomba Ezekieli afanye. Alimuambia hivi: “Unapaswa kuwaambia maneno yangu, kama watasikiliza ao hapana.” (Eze. 2:7; Isa. 43:10) Kwa hiyo, hata kama watu wanasikiliza ao hapana, Yehova anafurahia bidii yetu. (Soma Waebrania 6:10.) Juu ya kazi yake ya kuhubiri, ndugu mumoja alisema hivi: “Tumepanda, tumetilia maji, na tumesali na kutumaini kama Yehova atasaidia wale wenye kupendezwa wapendezwe zaidi.”​—1 Ko. 3:6.

NAMNA TUNAWEZA KUPATA FURAHA

15. Tunapaswa kuonyesha ukarimu ikiwa tu watu wanatuonyesha shukrani? Eleza.

15 Yesu anapenda tuonyeshe ukarimu kwa sababu kufanya vile kunatuletea furaha. Wakati tunaonyesha ukarimu, watu wengi pia watatuonyesha ukarimu. Kwa hiyo, Yesu anatutia moyo hivi: “Muzoee kupatia watu, na watu watawapatia ninyi. Watawamwangia katika mufuko wa nguo zenu kipimo kizuri, chenye kushindiliwa, chenye kutikiswa, na kujaa sana. Kwa maana kwa kipimo chenye munapimia watu, wao pia watawapimia ninyi.” (Lu. 6:38) Kwa kweli, wakati unaonyesha ukarimu, haiko watu wote ndio wataonyesha shukrani. Lakini, hata kama hawaonyeshe shukrani, endelea kutoa. Hauwezi kujua matokeo ya muzuri yenye tendo lako moja la ukarimu linaweza kuleta.

16. Ni nani wenye tunapaswa kuonyesha ukarimu, na sababu gani?

16 Kwa kweli, watu wenye kuonyesha ukarimu hawatoe kwa sababu wanangojea wengine pia wawapatie kitu fulani. Yesu alisema hivi: “Wakati unatayarisha karamu, ualike maskini, viwete [ao vilema wa miguu], vilema, na vipofu; na utakuwa mwenye furaha, kwa sababu hawana kitu cha kukulipa.” (Lu. 14:13, 14) Biblia inasema pia hivi: “Mutu mukarimu atabarikiwa,” na “mwenye furaha ni mutu yeyote mwenye anamuhangaikia mutu wa hali ya chini.” (Mez. 22:9; Zb. 41:1) Tunapaswa kuonyesha ukarimu kwa sababu tunapenda kabisa kusaidia wengine.

17. Ni njia gani za kutoa zenye zitatufanya tukuwe na furaha?

17 Wakati Paulo alitaja maneno ya Yesu kwamba “kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea,” hakukuwa anazungumuzia tu kutolea wengine vitu vya kimwili. Tunaweza pia kutolea watu kitia moyo, shauri fulani la Biblia, na musaada fulani. (Mdo. 20:31-35) Kupitia mambo yenye Paulo alisema na kufanya, alitufundisha kama ni jambo la maana sana kuonyesha wengine ukarimu kwa kuwatolea wakati wetu, nguvu zetu, kuwahangaikia, na kuwaonyesha upendo.

18. Wachunguzi wengi wanasema nini juu ya kuonyesha ukarimu?

18 Wachunguzi wenye kujifunza tabia za watu wamevumbua kama kutoa kunafanya watu wakuwe na furaha. Habari moja inaonyesha kama watu wanasema kwamba wanajisikia kuwa wenye furaha sana wakati wanafanyia wengine mambo ya muzuri. Wachunguzi wanasema kama wakati tunasaidia wengine, tunajisikia kuwa maisha yetu yako na kusudi na maana. Kwa hiyo, wachunguzi fulani wanashauria watu wafanye kazi ya kujitolea ili wakuwe na furaha na afya ya muzuri. Kwa kweli, mambo hayo yenye wamevumbua hayatushangaze, kwa sababu Yehova, Muumbaji wetu mwenye upendo, ametuambia sikuzote kama kutoa kunatufanya tukuwe na furaha.​—2 Ti. 3:16, 17.

ENDELEA KUONYESHA UKARIMU

19, 20. Sababu gani unapenda kuonyesha ukarimu?

19 Wakati watu wenye kutuzunguka wanajihangaikia wenyewe, hilo linaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kuonyesha ukarimu. Lakini Yesu alitukumbusha kama amri mbili kubwa ni kumupenda Yehova kwa moyo wetu wote, kwa nafsi yetu yote, kwa akili yetu yote, na kwa nguvu zetu zote, na kumupenda jirani yetu kama sisi wenyewe. (Mk. 12:28-31) Katika habari hii, tumejifunza kama watu wenye kumupenda Yehova wanajikaza kumuiga. Yehova na Yesu wanaonyesha ukarimu. Wanatutia moyo tufuate mufano wao, kwa sababu wanajua kama kuonyesha ukarimu kutatuletea furaha kabisa. Kama tunaonyesha ukarimu katika mambo tunamufanyia Mungu na mambo tunafanyia majirani wetu, tutamutukuza Yehova na hilo litatuletea faida sisi wenyewe na wengine pia.

20 Kwa kweli, tayari uko unajikaza sana ili kuonyesha ukarimu na kusaidia wengine, zaidi sana ndugu na dada zako. (Gal. 6:10) Ukiendelea kufanya vile, watu watakuonyesha shukrani na watakupenda, na utakuwa na furaha. Biblia inasema hivi: “Mutu mukarimu atafanikiwa, na ule mwenye kuburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa.” (Mez. 11:25) Katika kazi yetu ya kuhubiri, kuko njia nyingi za kutoa bila uchoyo na kuonyesha wema na ukarimu. Tutazungumuzia njia fulani katika habari yenye kufuata.

^ fu. 13 Jina limebadilishwa.