Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unajua Ukweli wa Mambo?

Unajua Ukweli wa Mambo?

“Wakati mutu anajibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo, huo ni upumbavu na haya.”​—MEZ. 18:13.

NYIMBO: 126, 95

1, 2. (a) Tunapaswa kuwa na uwezo gani wa maana, na sababu gani? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

SISI wote tunapaswa kujifunza namna ya kuchunguza habari muzuri na kuitumia ili kufikia maamuzi ya muzuri. (Mez. 3:21-23; 8:4, 5) Kama hatufanye vile, inaweza kuwa mwepesi kwa Shetani na ulimwengu wake kuharibisha mawazo yetu. (Efe. 5:6; Kol. 2:8) Kwa kweli, ili kufikia maamuzi ya muzuri, tunapaswa kujua ukweli wa mambo. Mezali 18:13 inasema hivi: “Wakati mutu anajibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo, huo ni upumbavu na haya.”

2 Katika habari hii, tutaona ni nini inaweza kufanya ikuwe nguvu kujua ukweli wa mambo na kufikia maamuzi ya muzuri. Tutajifunza pia kanuni za Biblia na mifano yenye itatufundisha namna ya kuchunguza habari muzuri.

USIAMINI “KILA NENO”

3. Sababu gani tunapaswa kutumia kanuni ya Biblia yenye kupatikana katika Mezali 14:15? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Leo, tunapata habari kupitia njia nyingi sana. Tunapata habari kupitia Enternete, televizyo, na vyombo vingine vya kutangaza habari. Marafiki wetu pia wanaweza kututumia ujumbe mwingi kupitia Enternete, telefone, na habari mbalimbali. Wakati fulani inaonekana kuwa habari hizo zote hazina mwisho. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu. Pengine marafiki wetu wako na nia ya muzuri, lakini kuko watu wengine wenye wanaeneza kwa makusudi habari zenye hazifae ao habari zenye kuwa na uongo fulani. Ni kanuni gani ya Biblia yenye inaweza kutusaidia kuchunguza muzuri habari zenye tunasikia? Mezali 14:15 inasema hivi: “Mujinga anaamini kila neno, lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.”

4. (a) Namna gani andiko la Wafilipi 4:8, 9 linatusaidia kuchagua habari zenye tunasoma? (b) Sababu gani ni jambo la maana kupata habari za kweli? (Ona pia kisanduku “ Vyombo Fulani vya Kutusaidia Kupata Habari za Kweli.”)

4 Ili kufikia maamuzi ya muzuri, tunapaswa kuwa na habari za kweli. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu wakati tunachagua habari za kusoma. (Soma Wafilipi 4:8, 9.) Hatupaswe kupoteza wakati kwa kuchunguza site za Enternete zenye hazitumainike ao kwa kusoma kwenye Enternete ao kwenye telefone ujumbe wenye kueneza habari zenye haziko za kweli. Ni jambo la maana zaidi tuepuke site za Enternete zenye waasi-imani wanatumia ili kueneza mawazo yao. Wanapenda kufanya imani ya watu wa Mungu ikuwe zaifu na kupotosha kweli. Habari zenye hazitumainike zinaongoza kwenye maamuzi ya mubaya. Usiwaze hata kidogo kama habari za uongo hazitakuletea matokeo yoyote.​—1 Ti. 6:20, 21.

5. Waisraeli walisikiliza habari gani ya uongo, na habari hiyo iliwaletea matokeo gani?

5 Habari za uongo zinaweza kuleta matokeo ya mubaya sana. Wakati wa Musa, wapelelezi 12 walienda katika Inchi ya Ahadi. Wapelelezi 10 walisema habari za mubaya wakati walirudia. (Hes. 13:25-33) Walitilia sana chumvi mambo yenye waliona, na watu wa Yehova wakaogopa sana na kuvunjika moyo. (Hes. 14:1-4) Sababu gani watu waliogopa sana na kuvunjika moyo? Pengine waliwaza kama habari hiyo ilikuwa ya kweli kwa sababu wengi kati ya wapelelezi hao walisema jambo lilelile. Kwa hiyo, watu walikataa kusikiliza mambo ya muzuri yenye wapelelezi wengine 2 walisema juu ya Inchi ya Ahadi. (Hes. 14:6-10) Kuliko kuchunguza habari muzuri na kumutumainia Yehova, watu walitenda kwa upumbavu kwa kuamini habari ya uongo.

6. Sababu gani hatupaswe kushangaa wakati tunasikia habari za kuchukiza zenye watu wanasema juu ya watumishi wa Yehova?

6 Tunapaswa kuwa waangalifu zaidi sana wakati tunasikia habari fulani juu ya watumishi wa Yehova. Kumbuka kama adui yetu, Shetani, anaitwa “mushitaki wa ndugu zetu.” (Ufu. 12:10) Yesu alionya kwamba wapinzani ‘wangetusingizia kila namna ya uovu.’ (Mt. 5:11) Kama tunakamata onyo hilo kwa uzito, hatutavunjika moyo wakati tunasikia habari za kushangaza zenye watu wanasema juu ya watumishi wa Yehova.

7. Tunapaswa kujiuliza maulizo gani mbele ya kutumia wengine habari fulani kupitia Enternete ao kupitia telefone?

7 Je, unafurahia kutumia marafiki wako ujumbe kupitia Enternete ao kupitia telefone? Wakati unaona habari fulani yenye kupendeza kwenye vyombo vya kutangaza habari ao wakati unasikia jambo fulani la kushangaza, unajisikia kama mutangazaji wa habari mwenye kupenda kujulisha wengine habari bila kukawia? Mbele ya kutumia wengine habari hiyo kupitia Enternete ao kupitia telefone, ujiulize hivi: ‘Niko hakika kama habari hii ni ya kweli? Ninajua kabisa maelezo yote?’ Kama hauko hakika, unaweza kueneza habari ya uongo. Kwa hiyo, ikiwa haujue kama habari fulani ni ya kweli, usiitume. Uivute!

8. Wapinzani wetu wamefanya nini katika inchi fulani, na namna gani tunaweza kuwasaidia bila kujua?

8 Kutumia wengine bila kufikiri ujumbe fulani wenye tulipata kwenye Enternete ao kwenye telefone ni jambo la hatari. Ona sababu ingine. Katika inchi fulani, kazi yetu imewekewa vizuizi ao imekatazwa kabisa. Wapinzani wetu katika inchi hizo wanaweza kueneza kwa makusudi habari zenye wametayarisha ili kutuogopesha ao kutufanya tukuwe na mashaka juu ya wenzetu. Fikiria jambo lenye lilitokea katika Muungano wa Sovieti wa zamani. Polisi wa siri, wenye waliitwa KGB, walieneza habari zenye haziko za kweli kwamba ndugu fulani wenye kujulikana sana wamekana imani yao. * (Ona maelezo ya chini.) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, ndugu wengi waliamini habari hizo za uongo na wakaacha tengenezo la Yehova. Kisha wakati fulani, wengi kati yao walirudia katika tengenezo, lakini wengine hawajarudiaka. Waliruhusu habari hizo za uongo ziharibu imani yao. (1 Ti. 1:19) Namna gani tunaweza kuepuka hatari hiyo? Epuka kueneza habari za uongo ao zenye haziko hakika. Usiamini kila jambo lenye unasikia. Lakini, ukuwe hakika kama unajua ukweli wa mambo.

HABARI YENYE HAINA MAELEZO YOTE

9. Ni nini ingine inaweza kufanya ikuwe nguvu kupata habari ya kweli?

9 Wakati fulani tunasikia habari zenye kuwa na uongo fulani. Habari zingine hazina maelezo yote. Hilo linafanya ikuwe nguvu kupata habari ya kweli. Hatuwezi kuamini hata kidogo habari yenye kuwa na uongo fulani! Tunaweza kufanya nini ili tusidanganywe na habari kama hizo?​—Efe. 4:14.

10. Sababu gani Waisraeli fulani walikuwa karibu kupigana vita na ndugu zao, na ni nini iliwasaidia waepuke kufanya vile?

10 Jambo lenye lilifikia Waisraeli wenye walikuwa ngambo ya mangaribi ya Muto Yordani katika siku za Yoshua, linaweza kutufundisha jambo fulani. (Yos. 22:9-34) Walisikia kama Waisraeli wenye walikuwa ngambo ya mashariki ya Yordani walikuwa wamejenga mazabahu kubwa karibu na muto huo. Sehemu hiyo ya habari ilikuwa ya kweli, lakini haikukuwa ndiyo habari yote. Na jambo hilo lilifanya Waisraeli wenye walikuwa ngambo ya mangaribi wafikiri kama ndugu zao wenye walikuwa ngambo ya mashariki walikuwa wamemuasi Yehova. Kwa hiyo, walikusanyika pamoja ili kupigana vita nao. (Soma Yoshua 22:9-12.) Lakini, mbele ya kuwashambulia, Waisraeli wenye walikuwa ngambo ya mangaribi walituma kwanza wanaume fulani ili kujua ukweli wa mambo. Wanaume hao walivumbua nini? Walivumbua kama Waisraeli wa ngambo ya mashariki hawakujenga mazabahu hiyo ili kutolea zabihu miungu ya uongo. Walijenga mazabahu hiyo ili kuonyesha kila mutu kama walikuwa wanamuabudu Yehova. Waisraeli walipaswa kufurahi kabisa kwa sababu hawakuenda kupigana vita na ndugu zao, lakini walichukua wakati wa kuchunguza ukweli wa mambo.

11. (a) Namna gani Mefibosheti alitendewa kwa ukosefu wa haki? (b) Daudi angefanya nini ili amutendee Mefibosheti kwa haki?

11 Wakati fulani, tunaweza kuumizwa kwa sababu watu wameeneza juu yetu habari zenye kuwa na uongo fulani. Jambo hilo lilimufikia Mefibosheti. Mufalme Daudi alimupatia kwa ukarimu shamba lote lenye lilikuwa la Sauli, tate (nkambo) yake. (2 Sa. 9:6, 7) Lakini, kisha Daudi alisikia habari ya uongo juu ya Mefibosheti. Hakuchunguza ili kujua ikiwa habari hiyo ilikuwa ya kweli, na akamunyanganya Mefibosheti vitu vyake vyote. (2 Sa. 16:1-4) Kisha, wakati Daudi alizungumuza na Mefibosheti, alitambua kama alikuwa amekosea. Basi akamurudishia Mefibosheti sehemu fulani ya vitu. (2 Sa. 19:24-29) Ikiwa Daudi angechukua wakati wa kuchunguza mambo yote kuliko kutenda haraka-haraka kulingana na habari yenye haikukuwa na maelezo yote, Mefibosheti hangetendewa hata kidogo kwa njia hiyo ya ukosefu wa haki.

12, 13. (a) Yesu alifanya nini wakati watu walimusemea uongo? (b) Tunaweza kufanya nini kama mutu fulani anatusemea uongo?

12 Unaweza kufanya nini kama mutu fulani anaeneza habari za uongo juu yako? Jambo hilo lilimufikia Yesu na Yohana Mubatizaji. (Soma Matayo 11:18, 19.) Yesu alifanya nini? Hakupoteza wakati wake wote na nguvu yake yote ili kusadikisha watu kama habari hizo ni za uongo. Lakini alitia watu moyo wajionee ukweli wa mambo. Alipenda watu wakazie akili mambo yenye alifanya na mafundisho yake. Yesu alisema hivi: “Hekima inatetewa kupitia kazi zake.”​—Mt. 11:19, maelezo ya chini.

13 Namna Yesu alitenda inaweza kutufundisha jambo fulani. Wakati fulani, watu wanaweza kutusemea mambo yenye hayafae ao ya uongo, na tunaweza kuogopa kama hilo litatuharibishia sifa. Lakini namna yetu ya kuishi inaweza kusaidia wengine waone sisi ni watu wa namna gani kabisa. Kama vile mufano wa Yesu unatufundisha, mwenendo wetu wa muzuri unaweza kuonyesha kama habari yoyote yenye kuwa na uongo fulani na mambo yote yenye walitusingizia ni ya uongo.

UNAJITEGEMEA WEWE MWENYEWE?

14, 15. Sababu gani hatupaswe kutegemea uelewaji wetu wenyewe?

14 Tumejifunza kama inaweza kuwa nguvu kupata habari zenye kutumainika. Shida ingine ni hali yetu ya kukosa kukamilika. Pengine tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi na pengine tumeonyesha hekima katika njia fulani. Wengine wanaweza kutuheshimia kwa sababu tuko na uwezo wa kufikiri muzuri. Je, jambo hilo linaweza kutuletea shida?

15 Ndiyo. Tunaweza kuanza kutegemea uelewaji wetu wenyewe. Tunaweza kuacha namna tunajisikia na mawazo yetu viongoze namna tunafikiri. Tunaweza kuanza kuamini kama tunaelewa hali fulani hata kama hatujue ukweli wa mambo. Jambo hilo ni hatari sana! Biblia inatuonya waziwazi kwamba hatupaswe kutegemea uelewaji wetu wenyewe.​—Mez. 3:5, 6; 28:26.

16. Katika mufano huu, ni jambo gani linatokea kwenye restora, na Tom anawaza nini?

16 Kwa mufano, wazia mangaribi moja muzee fulani mwenye uzoefu mwenye kuitwa Tom anaenda kwenye restora na anamuona John, muzee mwingine. John anakaa mbele ya meza pamoja na mwanamuke mwenye haiko bibi yake. Wanaonekana kuwa wanafurahia maisha. Tom anawaona wako wanacheka na kukumbatiana. Anakuwa na wasiwasi na anajiuliza hivi: ‘John na bibi yake watavunja ndoa yao? Itakuwa namna gani juu ya watoto wao?’ Tom amekwisha kuona mambo kama hayo yanatokea. Kama ungekuwa Tom, ungejisikia namna gani?

17. Katika mufano huu, Tom alivumbua nini kisha, na jambo hilo linaweza kutufundisha nini?

17 Lakini fikiri kidogo. Hata kama Tom anawazia kuwa John anakosa uaminifu kwa bibi yake, je, anajua ukweli wa mambo? Mangaribi sana ya siku hiyo, Tom anamuita John na kuvumbua kama mwanamuke huyo ni dada yake, mwenye anatokea mbali, mwenye alikuja kumutembelea. John na dada yake wamefanya miaka mingi bila kuonana. Na kwa sababu dada yake angepitisha saa kidogo tu pamoja naye, John alikuwa tu na wakati wa kukutana naye kwenye restora ili wakule chakula. Bibi yake hakuweza kuenda pamoja nao. Tom alifurahi sana kuona kama hakuambia mutu yeyote juu mambo yenye aliwazia! Mufano huo unatufundisha nini? Hata kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi ao kidogo, tuko tu na lazima ya kujua ukweli wa mambo mbele ya kufikia uamuzi wa muzuri.

18. Ni nini inaweza kutufanya tuamini jambo fulani la uongo juu ya ndugu ao dada yetu?

18 Inaweza pia kuwa nguvu kuchunguza habari muzuri wakati inahusu ndugu ao dada mwenye hatuelewanake naye. Kama tunaendelea kufikiri juu ya mambo yenye kufanya tusielewane naye, tunaweza kuwa na mashaka juu ya ndugu ao dada yetu. Kisha, ikiwa tunasikia jambo fulani la mubaya juu yake, tunaweza kuwa tayari kuamini jambo hilo, hata kama hakuna ushuhuda wenye kuonyesha kama ni la kweli. Hilo linatufundisha nini? Kama tunajiacha tukuwe na mawazo ya mubaya juu ndugu ao dada zetu, hilo linaweza kutufanya tufikie maamuzi ya mubaya yenye hayategemee mambo ya kweli. (1 Ti. 6:4, 5) Hatupaswe kuruhusu mawazo ya mubaya, kama vile wivu, yabakie katika moyo wetu. Tusisahau hata kidogo kama Yehova anataka tupende ndugu na dada zetu na kuwasamehe kwa moyo wote.​—Soma Wakolosai 3:12-14.

KANUNI ZA BIBLIA ZITATULINDA

19, 20. (a) Ni kanuni gani za Biblia zenye zitatusaidia kuchunguza habari muzuri? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

19 Leo, ni nguvu sana kupata habari zenye kutumainika na kuzichunguza muzuri. Sababu gani? Habari nyingi zenye tunapata hazina maelezo yote ao ni zenye kuwa na uongo fulani, na pia hatuko wakamilifu. Ni nini inaweza kutusaidia? Kanuni zenye tunapata katika Neno la Mungu! Kwa mufano, kanuni moja inatuambia kama ni upumbavu kujibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo. (Mez. 18:13) Kanuni ingine inatusaidia kuelewa kama hatupaswe kuamini kila jambo lenye tunasikia bila kuchunguza ikiwa ni la kweli. (Mez. 14:15) Na hata kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi ao kidogo, hatuwezi kutegemea uelewaji wetu wenyewe. (Mez. 3:5, 6) Kanuni za Biblia zitatulinda kwa kutusaidia tuchunguze habari muzuri, tujue habari za kweli na kukamata maamuzi ya muzuri.

20 Lakini, kuko sababu ingine yenye kufanya ikuwe nguvu kwetu kujua kweli juu ya hali fulani. Sisi wanadamu, tunakuwaka haraka kuhukumu wengine kulingana na mambo yenye tunaona. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia ni katika njia gani mbalimbali tunaweza kufanya kosa hilo na tutajifunza namna tunaweza kuliepuka.

^ fu. 8 Ona Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2004, ukurasa wa 111-112, na Kitabu cha Mwaka cha 2008, ukurasa wa 133-135.