Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Usihukumu Mutu Kulingana na Namna Anaonekana kwa Inje

Usihukumu Mutu Kulingana na Namna Anaonekana kwa Inje

“Muache kuhukumu kulingana na namna mutu anaonekana kwa inje, lakini muhukumu kwa hukumu ya haki.”​—YOH. 7:24.

NYIMBO: 142, 123

1. Isaya alitabiri nini juu Yesu, na sababu gani jambo hilo linatutia moyo?

UNABII wa Isaya juu ya Yesu Kristo unatutia moyo na kutupatia tumaini. Isaya alitabiri kama Yesu “hatahukumu kulingana na mambo yenye anaona kwa macho yake, wala kukaripia kulingana tu na mambo yenye anasikia kwa masikio yake” na kama “atawahukumu kwa haki watu wa hali ya chini.” (Isa. 11:3, 4) Sababu gani jambo hilo linatutia moyo? Kwa sababu tunaishi katika ulimwengu wenye kujaa ubaguzi, na watu wanahukumu wengine kulingana na mambo yenye wanaweza kuona. Tuko kabisa na lazima ya Yesu, Muamuzi mukamilifu, mwenye hatatuhukumu kulingana na namna tunaonekana kwa inje!

2. Yesu alituamuru tufanye nini, na tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Kila siku, tunakuwa na mawazo mbalimbali juu ya wengine. Yesu yeye alikuwa mukamilifu, lakini sisi hatuko wakamilifu, kwa hiyo mawazo yetu pia hayakamilike. Mambo yenye tunaona yanatuchochea haraka. Hata hivyo, Yesu alituamuru hivi: “Muache kuhukumu kulingana na namna mutu anaonekana kwa inje, lakini muhukumu kwa hukumu ya haki.” (Yoh. 7:24) Kwa hiyo, Yesu anapenda tumuige na tuepuke kuhukumu wengine kulingana na namna wanaonekana kwa inje. Katika habari hii, tutazungumuzia mambo tatu yenye yanaweza kuchochea mawazo yetu: rangi ya ngozi ya mutu ao inchi yake, kiasi cha feza zenye iko nazo, na miaka yake. Juu ya kila jambo, tutajifunza namna tunaweza kumutii Yesu na kuepuka kuhukumu wengine kulingana na namna wanaonekana kwa inje.

USIHUKUMU MUTU KULINGANA NA RANGI YAKE YA NGOZI AO INCHI YAKE

3, 4. (a) Sababu gani Petro alibadilisha mawazo yake juu ya Watu wa Mataifa? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Ni jambo gani la mupya lenye Yehova alimufundisha Petro?

3 Wazia namna mutume Petro alijisikia wakati aliombwa kuenda Kaisaria, kwenye nyumba ya Mutu wa Mataifa mwenye aliitwa Kornelio! (Mdo. 10:17-29) Tangu wakati Petro alikuwa anakomaa, aliamini kama Watu wa Mataifa hawakukuwa safi. Lakini mambo fulani yalikuwa tu yametokea, na yalifanya abadilishe mawazo yake. Kwa mufano, alikuwa amepata maono kutoka kwa Mungu. (Mdo. 10:9-16) Katika maono hayo, Petro aliona kitu fulani chenye kilikuwa kama kitambaa kikubwa kinashuka kutoka mbinguni; kilikuwa kinajaa wanyama wenye walionwa kuwa hawakukuwa safi. Kisha sauti ikamuambia hivi: “Petro, simama, chinja na ukule!” Petro alikataa kabisa. Kwa hiyo, sauti hiyo ilimuambia hivi: “Acha kuita vitu vyenye Mungu ametakasa kuwa ni vichafu.” Kisha kuona maono hayo, Petro hakuelewa mambo yenye sauti hiyo ilikuwa inajaribu kumuambia. Palepale, watu wenye Kornelio alituma wakafika. Roho takatifu ilimuambia Petro aende kwenye nyumba ya Kornelio, kwa hiyo, akaenda pamoja na watu hao.

4 Petro angehukumu watu ‘kulingana na namna walionekana kwa inje,’ hangeenda hata kidogo kwenye nyumba ya Kornelio. Wayahudi hawakukuwa wanaenda hata kidogo kwenye nyumba za Watu wa Mataifa. Sasa, sababu gani Petro alienda? Hata kama alikuwa anabagua Watu wa Mataifa, maono yenye alikuwa ameona na muongozo wa roho takatifu, vilifanya abadilishe mawazo yake. Kisha kumusikiliza Kornelio, Petro alisema hivi: “Sasa ninaelewa kabisa kwamba Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.” (Mdo. 10:34, 35) Jambo hilo la mupya lenye Petro alielewa lilimufurahisha sana, na lingesaidia Wakristo wote. Namna gani?

5. (a) Yehova anapenda Wakristo wote waelewe jambo gani? (b) Hata kama tunajua kweli, pengine tungali na mawazo gani?

5 Yehova alimutumia Petro ili kusaidia Wakristo wote waelewe kama Yeye hana ubaguzi. Yehova haangalie rangi yetu ya ngozi, inchi yetu, kabila letu ao luga yetu. Kama tu tunamuogopa Mungu na kufanya mambo yenye kuwa sawa, anatukubali. (Gal. 3:26-28; Ufu. 7:9, 10) Pengine tayari unajua jambo hilo. Lakini, tuseme nini ikiwa ulikomalia katika inchi ao familia yenye kuwa na ubaguzi sana? Hata kama unafikiri kuwa hauna ubaguzi, je, inawezekana kuwa ungali na mawazo fulani ya ubaguzi? Hata kisha kusaidia wengine waone kama Mungu hana ubaguzi, Petro alionyesha tena ubaguzi. (Gal. 2:11-14) Kwa hiyo, namna gani tunaweza kumutii Yesu na kuacha kuhukumu wengine kulingana na namna wanaonekana kwa inje?

6. (a) Ni nini inaweza kutusaidia kuacha ubaguzi? (b) Ripoti ya muzee mumoja ilionyesha nini juu yake?

6 Ili kujua ikiwa tuko na mawazo yoyote ya ubaguzi, tunapaswa kujichunguza. Tunapaswa kulinganisha mawazo yetu na mambo yenye tunajifunza katika Neno la Mungu. (Zb. 119:105) Pia, tunaweza kumuuliza rafiki fulani ikiwa ametambua kama tuko na wazo lolote la ubaguzi, lenye sisi wenyewe hatuwezi kuona. (Gal. 2:11, 14) Tunaweza kushindwa kutambua kama tuko na ubaguzi kwa sababu tumezoea kuwa na mawazo hayo! Jambo hilo lilimufikia muzee mumoja. Aliandikia biro ya tawi ripoti fulani juu ya bibi na bwana fulani wenye bidii wenye walikuwa katika utumishi wa wakati wote. Bwana alikuwa wa kabila fulani lenye watu wengi waliona kuwa la hali ya chini. Muzee huyo aliandika mambo ya mingi ya muzuri juu ya bwana huyo. Kisha akaongeza hivi: “Hata kama iko wa [inchi hii], tabia zake na namna yake ya kuishi vinasaidia wengine waelewe kama, kuwa wa [kabila hili] hakumaanishe kuwa muchafu kimwili, kuwa na maisha ya hali ya chini, kama vile wengine wengi wa kabila [hilo] wanakuwaka.” Jambo hilo linatufundisha nini? Hata kama tuko na madaraka gani katika tengenezo la Yehova, tunapaswa kujichunguza na kukubali musaada wenye tunapewa ili tutambue mawazo yoyote ya ubaguzi yenye tunaweza kuwa tungali nayo. Ni jambo gani lingine tunaweza kufanya?

7. Namna gani tunaweza kuonyesha kama “tumefungua wazi moyo wetu”?

7 Kama “tumefungua wazi moyo wetu,” tutaacha ubaguzi na tutakuwa na upendo. (2 Ko. 6:11-13) Unafurahia kupitisha tu wakati pamoja na watu wenye kuwa na rangi ya ngozi kama yako, wa inchi yako, kabila lako ao wenye kuzungumuza luga yako? Kama ni vile, ujikaze kupitisha wakati pamoja na watu wengine. Unaweza kualika ndugu na dada wa desturi tofauti na yako ili muhubiri pamoja nao. Ao unaweza kuwaalika kwenye nyumba yako ili kula chakula ao ili kupitisha wakati pamoja nao. (Mdo. 16:14, 15) Kisha wakati fulani, upendo utajaa katika moyo wako na hautakuwa na ubaguzi tena. Sasa, tuzungumuzie njia ingine yenye tunaweza kuhukumu wengine ‘kulingana na namna wanaonekana kwa inje.’

USIHUKUMU MUTU KULINGANA NA UTAJIRI AO UMASKINI WAKE

8. Andiko la Mambo ya Walawi 19:15 linaweza kutufundisha nini juu ya namna utajiri ao umaskini unaweza kuchochea namna tunaona wengine?

8 Tunaweza kuwa na mawazo fulani juu ya wengine kwa sababu wako matajiri ao maskini. Andiko la Mambo ya Walawi 19:15 linasema hivi: “Haupaswe kubagua maskini ao kuonyesha upendeleo kwa matajiri. Unapaswa kumuhukumu mwenzako kwa haki.” Namna gani utajiri ao umaskini wa mutu unaweza kuchochea namna tunamuona?

9. Ni jambo gani la kuhuzunisha lenye Sulemani aliandika, na hilo linatufundisha nini?

9 Sulemani aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika jambo hili lenye kuhuzunisha: “Maskini anachukiwa hata na majirani wake, lakini tajiri iko na marafiki wengi.” (Mez. 14:20) Mezali hiyo inatufundisha nini? Kama hatuko waangalifu, tunaweza kupenda kufanya urafiki na ndugu ao dada wenye kuwa matajiri na kuepuka wale wenye kuwa maskini. Sababu gani ni hatari kuhukumu watu kulingana na vitu vyenye wako navyo ao vyenye hawana?

10. Yakobo alionya Wakristo juu ya jambo gani?

10 Kama tunahukumu ndugu na dada zetu kulingana na utajiri ao umaskini wao, tunaweza kuleta migawanyiko katika kutaniko. Jambo hilo lilitokea katika makutaniko fulani ya wakati wa mitume, na Yakobo alionya Wakristo hao juu ya jambo hilo. (Soma Yakobo 2:1-4.) Hatuwezi kuruhusu migawanyiko ikuwe katika kutaniko letu. Sasa, namna gani tunaweza kuepuka kuhukumu watu kulingana na vitu vyenye wako navyo?

11. Vitu vya kimwili vinafanya mutu akuwe na uhusiano pamoja na Yehova? Fasiria.

11 Tunapaswa kuona ndugu na dada zetu kama vile Yehova anawaona. Yehova haone kuwa mutu fulani iko wa maana kwa sababu iko tajiri ao maskini. Uhusiano wetu pamoja na Yehova hautegemee kiasi cha feza zenye tuko nazo ao vitu vya kimwili vyenye tuko navyo. Yesu alisema kama “itakuwa vigumu kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni,” lakini hakusema kama haiwezekane. (Mt. 19:23) Yesu alisema pia hivi: “Wenye furaha ni ninyi maskini, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wenu.” (Lu. 6:20) Lakini maneno hayo hayakumaanisha kama watu wote wenye kuwa maskini wangemusikiliza Yesu na kupata baraka za pekee. Kulikuwa maskini wengi wenye hawakumufuata Yesu. Jambo la kweli ni hii: Hatuwezi kusema kama mutu iko na uhusiano wa muzuri pamoja na Yehova ao hapana kulingana na vitu vya kimwili vyenye iko navyo.

12. Biblia inafundisha matajiri na maskini nini?

12 Kati ya watu wa Yehova, kuko ndugu na dada wenye kuwa matajiri na wengine wenye kuwa maskini. Lakini wote wanamupenda Yehova na wanamutumikia kwa moyo wote. Biblia inaambia matajiri “wasiweke tumaini lao katika utajiri wenye hauko hakika, lakini katika Mungu.” (Soma 1 Timoteo 6:17-19.) Neno la Mungu linaonya pia watumishi wote wa Yehova, matajiri na maskini, kama ni hatari kupenda feza. (1 Ti. 6:9, 10) Wakati tunaona ndugu na dada zetu kama vile Yehova anawaona, hatutawahukumu kulingana na vitu vyenye wako navyo ao kulingana na vitu vyenye hawana. Lakini, tuseme nini juu ya miaka ya mutu? Hiyo ni sababu ya kuhukumu wengine?

USIHUKUMU MUTU KULINGANA NA MIAKA YAKE

13. Biblia inafundisha nini juu ya kuonyesha heshima watu wenye kuzeeka?

13 Mara nyingi, Biblia inasema kama tunapaswa kuheshimia watu wenye kuzeeka. Andiko la Mambo ya Walawi 19:32 linasema hivi: “Unapaswa kusimama mbele ya kichwa chenye imvi, na unapaswa kumuheshimia mutu mwenye kuzeeka, na unapaswa kumuogopa Mungu wako.” Mezali 16:31 inatuambia kama “imvi ni taji la uzuri wakati zinapatikana katika njia ya haki.” Paulo alimuambia Timoteo asikaripie kwa ukali wanaume wenye kuzeeka lakini awatendee kama baba. (1 Ti. 5:1, 2) Hata kama Timoteo alikuwa na mamlaka fulani ya kutolea ndugu wenye kuzeeka muongozo, sikuzote alipaswa kuwatendea kwa huruma na kwa heshima.

14. Ni wakati gani tunapaswa kumurekebisha mutu fulani mwenye kuwa na miaka mingi kutupita?

14 Tuseme nini kama ndugu fulani mwenye kuzeeka anafanya zambi kwa makusudi ao anachochea jambo fulani lenye halimupendeze Yehova? Yehova hawezi kuachilia mutu mwenye anafanya zambi kwa makusudi, hata kama mutu huyo ni mwenye kuzeeka ao ni mwenye kuheshimiwa. Ona kanuni yenye kuwa katika Isaya 65:20. Inasema hivi: “Mutenda-zambi atalaaniwa, hata kama iko na miaka mia moja.” Kanuni ingine yenye kufanana na hiyo inapatikana katika maono ya Ezekieli. (Eze. 9:5-7) Kwa hiyo, jambo la maana zaidi, ni kumuheshimia Yehova, Muzee wa Siku. (Da. 7:9, 10, 13, 14) Kumuheshimia Yehova kutatusaidia tukuwe na ujasiri wenye tuko nao lazima ili kumurekebisha mutu mwenye kuwa na lazima ya musaada, hata kama iko na miaka ngapi.​—Gal. 6:1.

Unaonyesha ndugu vijana heshima? (Picha hii inapatana na fungu la 15)

15. Mufano wa mutume Paulo unatufundisha nini juu ya kuonyesha ndugu vijana heshima?

15 Halafu kama ndugu ni kijana? Maana yake hastahili kuonyeshwa heshima? Hapana. Paulo alimuandikia Timoteo hivi: “Usiruhusu hata kidogo mutu yeyote azarau ujana wako. Lakini, ukuwe mufano kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, na katika mwenendo safi.” (1 Ti. 4:12) Wakati Paulo aliandika maneno hayo, pengine Timoteo alikuwa na miaka karibu 30. Lakini, Paulo alikuwa amekwisha kumupatia madaraka ya maana sana. Hilo linatufundisha nini? Hatupaswe kuhukumu vijana kulingana na miaka yao. Wazia mambo yote yenye Yesu alifanya wakati alikuwa tu na miaka 33!

16, 17. (a) Namna gani wazee wanaamua ikiwa ndugu fulani anastahili kuwa mutumishi wa huduma ao muzee? (b) Namna gani mawazo yetu wenyewe ao desturi za watu wa eneo letu zinaweza kupingana na mambo Biblia inasema?

16 Katika desturi fulani, watu hawaheshimie vijana wanaume. Kwa hiyo, wazee fulani hawawezi kumupendekeza kijana fulani ili akuwe mutumishi wa huduma ao muzee, hata kama anatimiza sifa zenye kuombwa. Lakini Biblia haiseme hata kidogo kama ndugu anapaswa kuwa na miaka fulani ili akuwe mutumishi wa huduma ao muzee. (1 Ti. 3:1-10, 12, 13; Tit. 1:5-9) Kama muzee anatia sheria juu ya jambo hilo kwa sababu ya desturi zake, hilo linaonyesha kama hafuate Neno la Mungu. Wazee hawapaswe kuhukumu vijana kwa kutegemea mawazo yao wenyewe ao desturi za eneo lao lakini wanapaswa kufuata kanuni za Neno la Mungu.​—2 Ti. 3:16, 17.

17 Kama wazee hawafuate kanuni za Biblia ili kuweka watumishi wa huduma ao wazee, wanaweza kuzuia ndugu wenye wanatimiza sifa zenye kuombwa. Katika inchi moja, mutumishi wa huduma mumoja alikuwa anatimiza muzuri madaraka fulani ya maana, na wazee wakaona kama anatimiza sifa zenye kutajwa katika Biblia ili kuwa muzee. Lakini, wazee fulani wenye kuzeeka walisema kama alionekana kuwa kijana sana, na kwa hiyo hawakumupendekeza. Jambo la kuhuzunisha ni hili: ndugu huyo hakupendekezwa, kwa sababu tu alionekana kuwa kijana. Na inaonekana kuwa namna hiyo ya kufikiri inaenea katika sehemu nyingi za dunia. Ni jambo la maana sana tufuate Biblia kuliko kufuata mawazo yetu wenyewe ao desturi za watu wa eneo letu. Kama tunafanya vile, hilo litaonyesha kama tunatii amri ya Yesu na tutaacha kuhukumu wengine kulingana na namna wanaonekana kwa inje.

MUHUKUMU KWA HUKUMU YA HAKI

18, 19. Ni nini itatusaidia kuona ndugu na dada namna Yehova anawaona?

18 Hatukamilike, lakini tunaweza kujifunza namna ya kutendea wengine bila ubaguzi kama vile Yehova anafanya. (Mdo. 10:34, 35) Kwa hiyo, sikuzote tunapaswa kutii mambo yenye Neno la Mungu linatukumbusha. Wakati tunafanya vile, tunatii amri ya Yesu ya ‘kuacha kuhukumu kulingana na namna mutu anaonekana kwa inje.’​—Yoh. 7:24.

19 Hivi karibuni, Mufalme wetu, Yesu Kristo, atahukumu watu wote. Hukumu yake itategemea kanuni za Mungu za haki, haitategemea mambo yenye anaona ao kusikia. (Isa. 11:3, 4) Tunangojea kwa hamu kabisa wakati huo wa muzuri sana!