Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uvumilivu​—Onyesha Sifa Hii na Uko na Tumaini

Uvumilivu​—Onyesha Sifa Hii na Uko na Tumaini

KWA SABABU maisha yamekuwa nguvu sana katika hizi “siku za mwisho,” tunapaswa kuonyesha uvumilivu kuliko wakati mwingine wowote. (2 Ti. 3:1-5) Watu wengi wenye kutuzunguka hawana uvumilivu. Wanajipenda wenyewe, wanapenda mabishano, na hawana sifa ya kujizuia. Kwa hiyo, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Nimeanza kukosa uvumilivu kama vile watu wenye kunizunguka? Kuwa muvumilivu maana yake nini kabisa? Ninaweza kufanya nini ili uvumilivu ukuwe sehemu ya utu wangu?’

UVUMILIVU MAANA YAKE NINI?

Neno “uvumilivu” lenye kutumiwa katika Biblia maana yake nini? Linamaanisha mambo mengi zaidi ya kuvumilia tu magumu fulani. Mutu muvumilivu anavumilia na iko na tumaini, ni kusema, anatumaini kama mambo yatakuwa muzuri. Hajifikirie yeye mwenyewe, lakini anafikiria pia namna wengine wanajisikia, hata wale wenye pengine walimukasirisha ao kumutendea mubaya. Anaendelea kutumaini kama uhusiano wao utakuwa muzuri tena. Haishangaze kuona kama Biblia inasema kwamba upendo unatusaidia kuvumilia. * (Ona maelezo ya chini.) (1 Ko. 13:4) Uvumilivu pia ni sehemu ya “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23) Kwa hiyo, tunapaswa kufanya nini ili tukuwe na uvumilivu kabisa?

MAMBO YA KUFANYA ILI TUKUWE NA UVUMILIVU

Ili tukuwe na uvumilivu, tunapaswa kusali ili kuomba musaada wa roho takatifu ya Yehova, yenye anapatia watu wenye kumutumainia. (Lu. 11:13) Roho hiyo ni yenye nguvu sana, lakini tunapaswa kutenda kulingana na sala zetu. (Zb. 86:10, 11) Maana yake, tunapaswa kujikaza sana ili kuonyesha uvumilivu kila siku na kufanya sifa hiyo ikuwe sehemu ya utu wetu. Lakini, wakati fulani tunaweza kushindwa kufanya vile. Ni nini inaweza kutusaidia?

Tunapaswa kujifunza mufano mukamilifu wa Yesu na kuiga mufano huo. Wakati mutume Paulo alizungumuzia “utu mupya,” wenye kutia ndani uvumilivu, alitutia moyo kwa kusema hivi: “Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu.” (Kol. 3:10, 12, 15, maelezo ya chini) Ili kufanya vile, tunapaswa kufuata mufano wa Yesu na kutumaini kabisa kama Mungu atatengeneza mambo kwa wakati wenye kufaa. Kama tuko na tumaini hilo, hatatupoteza uvumilivu wetu, hata kutokea hali gani.​—Yoh. 14:27; 16:33.

Sisi wote tunapenda kabisa dunia mupya ikuje haraka sana kadiri inawezekana. Lakini tunajifunza kuwa na uvumilivu zaidi wakati tunafikiria namna Yehova ametuvumilia sana. Biblia inatuhakikishia hivi: “Yehova hakawie kuhusiana na ahadi yake, kama vile watu fulani wanaona kukawia, lakini yeye ni muvumilivu kuwaelekea ninyi kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Kwa hiyo, wakati tunafikiria namna Yehova ametuvumilia, sisi pia tutavumilia zaidi wengine. (Ro. 2:4) Ni hali gani fulani zenye kutuomba tuonyeshe uvumilivu?

HALI FULANI ZENYE KUTUOMBA TUONYESHE UVUMILIVU

Katika maisha yetu ya kila siku, kuko hali nyingi zenye kutuomba tuonyeshe uvumilivu. Kwa mufano, inaomba uvumilivu ili tusikatize wengine katika mazungumuzo wakati tunaona kama tuko na jambo fulani la maana la kusema. (Yak. 1:19) Tunapaswa pia kuonyesha uvumilivu wakati mutu fulani anatukasirisha. Kuliko kukasirika haraka, ni muzuri kukumbuka namna Yehova na Yesu wanatenda juu ya uzaifu wetu. Hawakazie uangalifu makosa ya kidogo-kidogo yenye tunafanyaka. Lakini, wanaona sifa za muzuri zenye tuko nazo na kwa uvumilivu, wanatupatia wakati wa kubadilika.​—1 Ti. 1:16; 1 Pe. 3:12.

Tunapaswa pia kuonyesha uvumilivu wakati mutu fulani anatuambia kama tulisema ao kufanya jambo fulani la mubaya. Pengine tunaweza kwanza kukasirika na kujitetea. Lakini, Neno la Mungu linatuambia tutende kwa njia tofauti. Linasema hivi: “Ni muzuri zaidi kuwa muvumilivu kuliko kuwa na roho yenye majivuno. Usikuwe haraka kukasirika, kwa maana kukasirika ni tabia ya mupumbavu.” (Muh. 7:8, 9, maelezo ya chini) Kwa hiyo, hata kama mutu fulani anatusingizia jambo la uongo, tunapaswa kuonyesha uvumilivu na kufikiri kwa uangalifu mbele ya kutenda. Ni vile Yesu alifanya wakati wengine walimusingizia mambo ya uongo.​—Mt. 11:19.

Zaidi sana wazazi wanapaswa kuwa na uvumilivu wakati wanapaswa kusaidia watoto wao wabadilishe mawazo fulani ao waepuke tamaa za mubaya. Tuzungumuzie mufano wa Mattias, mwenye kutumikia kwenye Beteli katika Skandinavia. Wakati Mattias alikuwa kijana mudogo, wanafunzi wenzake walikuwa wanamuchekelea kwa sababu ya mambo yenye anaamini. Kwanza, wazazi wake hawakujua jambo hilo. Lakini kisha waliona kama alianza kuwa na mashaka juu ya mambo yenye anaamini. Gillis, baba ya Mattias, anasema kama yeye na bibi yake walipaswa kuonyesha uvumilivu sana katika hali hiyo. Mattias alikuwa anauliza maulizo kama vile: “Mungu ni nani? Halafu kama Biblia haiko Neno la Mungu? Ni nini inaonyesha kama ni Mungu ndiye anatuomba tufanye hivi ao vile?” Pia, alikuwa anamuuliza baba yake hivi: “Sababu gani mutu fulani anihukumu kwa sababu tu tusijisikie namna unajisikia ao siamini mambo yenye unaamini?”

Gillis anaeleza hivi: “Wakati fulani, mutoto wetu mwanaume aliuliza maulizo yake kwa hasira, hakukasirikia mama yake wala mimi, lakini alikasirikia kweli, yenye aliona kama ilifanya maisha yake kuwa nguvu sana.” Namna gani Gillis alimusaidia mutoto wake? Anasema hivi: “Mimi na mutoto wangu tulikuwa tunakaa na kuzungumuza kwa saa nyingi.” Mara nyingi, Gillis alimusikiliza tu Mattias na alimuuliza maulizo ili ajaribu kuelewa mawazo yake na namna alijisikia. Wakati fulani, Gillis alimuelezea mutoto wake jambo fulani na alimuambia afikiri juu ya jambo hilo kwa siku moja hivi mbele walizungumuzie tena. Wakati mwingine, Gillis alikuwa anasema kama yeye pia alikuwa na lazima ya siku fulani ili afikiri juu ya jambo fulani lenye mutoto wake alisema. Mazungumuzo hayo ya mara kwa mara, yalimusaidia Mattias aanze kuelewa maana ya bei ya ukombozi na kuelewa kama Yehova anatupenda na iko na haki ya kuwa mutawala wetu. Baba yake anasema hivi: “Iliomba wakati, na mara nyingi ilikuwa vigumu, lakini, pole kwa pole, upendo kwa Yehova ulikomaa katika moyo wake. Mimi na bibi yangu tuko wenye furaha sana kwa sababu bidii yenye tulifanya kwa uvumilivu ili kumusaidia mutoto wetu wakati alikuwa kijana mudogo ilizaa matunda na iligusa moyo wake.”

Wakati Gillis na bibi yake walikuwa wanamusaidia kwa uvumilivu mutoto wao mwanaume, walitumaini kama Yehova angewasaidia. Gillis anasema hivi: “Mara nyingi nilimuambia Mattias kama upendo wenye tuko nao kwake ulinichochea mimi na mama yake tumuombe Yehova kwa bidii hata zaidi ili amusaidie kuelewa.” Wazazi hao wako na furaha kabisa kwa sababu walikuwa na uvumilivu na hawakuchoka!

Tunapaswa pia kuonyesha uvumilivu wakati tunahangaikia mutu wa familia ao rafiki mwenye kuwa na ugonjwa wenye kukawia. Tuzungumuzie mufano wa Ellen * (ona maelezo ya chini). Yeye pia anaishi katika Skandinavia.

Miaka munane hivi yenye imepita, bwana ya Ellen amepatwa mara mbili na ugonjwa wa ubongo wenye kufanya sehemu fulani za mwili zipooze na ugonjwa huo umeharibisha ubongo wake. Kwa sababu ya ugonjwa huo, hawezi tena kusikia furaha, huzuni, wala huruma. Hali hiyo iko nguvu sana kwa Ellen. Anasema hivi: “Imeniomba nionyeshe uvumilivu sana na kusali sana.” Anasema tena hivi: “Andiko lenye ninapenda sana lenye linanituliza ni Wafilipi 4:13, lenye kusema hivi: ‘Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.’” Ellen anapambana na hali hiyo kwa uvumilivu kupitia nguvu na musaada wa Yehova.​—Zb. 62:5, 6.

IGA UVUMILIVU WA YEHOVA

Kwa kweli, Yehova mwenyewe ndiye mufano muzuri zaidi wa kuonyesha uvumilivu. (2 Pe. 3:15) Mara nyingi, Biblia inasema juu ya uvumilivu mwingi wa Yehova. (Ne. 9:30; Isa. 30:18) Je, unakumbuka namna Yehova alitenda wakati Abrahamu alimuuliza maulizo fulani juu ya uamuzi wake wa kuharibu Sodoma? Yehova hakumukatiza Abrahamu. Alisikiliza kwa uvumilivu maulizo na mahangaiko yote ya Abrahamu. Kisha, Yehova alionyesha kama alikuwa amesikia mahangaiko ya Abrahamu na alimuhakikishia kama hangeharibu Sodoma, hata kama kulikuwa tu watu kumi wenye haki katika muji huo. (Mwa. 18:22-33) Sikuzote, Yehova anasikiliza kwa uvumilivu, na hakasirike haraka hata kidogo!

Uvumilivu ni sehemu ya maana sana ya utu mupya yenye Wakristo wote wanapaswa kuwa nayo. Kama tunajikaza sana kuonyesha uvumilivu kabisa, tutamutukuza Yehova, Baba yetu mwenye kuonyesha uvumilivu na mwenye kutuhangaikia, na tutakuwa kati ya “wale wenye kupitia imani na uvumilivu wanariti ahadi.”​—Ebr. 6:10-12.

^ fu. 4 Sifa ya upendo ilizungumuziwa katika habari ya kwanza ya habari hizi kenda zenye kuzungumuzia tunda la roho ya Mungu.

^ fu. 15 Jina limebadilishwa.