Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Yehova Alibariki Sana Uamuzi Wangu

Yehova Alibariki Sana Uamuzi Wangu

Ilikuwa mwaka wa 1939. Tuliamuka katikati ya usiku na tukatembeza motokari zaidi ya saa moja ili kuenda mu muji mudogo wa Joplin kusini-mangaribi mwa Missouri, inchi ya Amerika. Kule tulianza kuweka kimya-kimya trakte chini ya kila mulango katika eneo. Kisha tu kumaliza, tuliingia mu motokari na kuenda kukutana na vikundi vingine. Ilikuwa sasa asubui sana. Lakini, juu ya nini siku hiyo tulienda mu mahubiri mbele jua litokee na kutoka mu eneo haraka sana? Nitaeleza kisha.

NILIZALIWA mu mwaka wa 1934. Wazazi wangu, Fred Molohan na Edna, walikuwa tayari Wanafunzi wa Biblia (Mashahidi wa Yehova) kwa miaka 20. Niko mwenye shukrani juu walinifundisha kumupenda Yehova. Tulikuwa tunaishi Parsons, muji mudogo kusini-mashariki mwa Kansas. Katika kutaniko letu, karibu kila mutu alikuwa mutiwa-mafuta. Familia yetu ilikuwa inaenda ku mikutano kwa ukawaida na ilihubiri kwa ukawaida. Siku ya Posho kisha midi, tulizoea kufanya mahubiri ya barabarani, yenye kuitwa leo mahubiri ya mahali pa watu wengi. Wakati fulani tulikuwa tunachoka, lakini sikuzote Baba alikuwa anatuuzia kreme ya baridi kisha mahubiri.

Kutaniko letu ndogo lilikuwa na eneo kubwa lenye lilikuwa na miji ya kidogo-kidogo na mashamba mengi. Kuliko kutupatia feza kwa ajili ya vichapo vyetu, watu fulani wenye walikuwa na mashamba walikuwa wanatupatia mboga za majani zenye zililimwa ku nyumba, mayai (yenye yalitoka palepale katika chicha), ao hata kuku wazima. Baba alikuwa amekwisha kutoa muchango wa feza kwa ajili ya vichapo, kwa hiyo chakula hicho kilisaidia familia.

KAMPANYE ZA KUHUBIRI

Wazazi wangu waliuza fono ya kutumia mu kazi ya mahubiri. Singeweza kuitumia juu nilikuwa mudogo sana, lakini nilifurahia kusaidia Baba na Mama ili kusikilizisha watu wenye tulirudilia na wanafunzi wa Biblia hotuba za Ndugu Rutherford zenye zilikuwa zimerekodiwa.

Mimi pamoja na baba yangu na mama yangu karibu na motokari yetu yenye kutoa sauti

Baba aliweka chombo kikubwa cha kutoa sauti ku motokari, na akaifanya kuwa motokari yenye kutoa sauti. Ilikuwa ya muzuri sana kwa ajili ya kazi ya kuhubiri. Mara nyingi, tulitia kwanza muziki ili kuvutia watu, na kisha tuliwasikilizisha hotuba yenye kutegemea Biblia. Kisha pale, tulitolea watu wenye kupendezwa vichapo.

Katika muji mudogo wa Cherryvale, Kansas, Baba alitembeza motokari yenye kutoa sauti mupaka mu bustani ya muji, mahali kwenye watu wengi walikuwa wanapumuzikia Siku ya Yenga. Kisha, polisi mumoja alikuja na akamuambia kama angeweza kutumia motokari yenye kutoa sauti inje tu ya bustani. Baba alihamishia motokari ku barabara yenye ilikuwa karibu na bustani hiyo ili watu wenye walikuwa mule waendelee tu kusikia muzuri programu. Nilifurahia sana kuwa pamoja na Baba na Jerry, ndugu yangu mukubwa, wakati kama huo.

Katika miaka hiyo, tulifanya kampanye za pekee mu maeneo kwenye watu walikuwa wanapinga sana kweli. Kama vile nilisema ku mwanzo wa habari hii, tulikuwa tunaamuka katikati ya usiku na tulikuwa tunatia kimya-kimya trakte ao vijitabu chini ya milango ya nyumba za watu. Kisha, tulikuwa tunakutana inje ya muji ili kuona ikiwa polisi hawakufunga mutu yeyote kati yetu.

Sehemu ingine ya kazi yetu ya kuhubiri yenye ilifurahisha sana iliitwa matembezi ya kutangaza habari. Tulikuwa tunavaa alama kubwa-kubwa na kutembea mu muji fulani. Ninakumbuka kama wakati fulani ndugu walikuja mu muji wetu na walitembea wakiwa wenye kuvaa alama zenye zilikuwa na maandishi yenye kusema “Dini Ni Mutego na Hila.” Walianzia kwetu, walitembea kilometre karibu moja na nusu mu muji, na kisha wakarudia tena kwetu. Jambo la kufurahisha ni kwamba, hakuna mutu mwenye aliwasimamisha, lakini watu wengi walikuwa wanapenda kujua kulikuwa nini.

MIKUSANYIKO WAKATI NILIKUWA KIJANA MUDOGO

Mara nyingi familia yetu ilikuwa inafanya safari za kuenda Texas kwa ajili ya mikusanyiko. Juu Baba alikuwa anatumika mu kompanyi ya njia ya treni, tulikuwa tunabeba treni bila kulipa ili kuenda ku mikusanyiko na kutembelea watu wa jamaa yetu. Ndugu mukubwa wa mama yangu, Fred Wismar, na bibi yake, Eulalie, walikuwa wanaishi mu muji wa Temple, Texas. Mujomba Fred alijua kweli wakati fulani kisha mwaka wa 1900 wakati alikuwa kijana. Alibatizwa, na aliambia wadogo yake, kutia ndani mama yangu, juu ya mambo yenye alikuwa anajifunza. Ndugu wenye waliishi katikati ya Texas walikuwa wanamujua muzuri Mujomba Fred juu wakati fulani alikuwa mutumishi wa eneo (mwenye kuitwa sasa mwangalizi wa muzunguko). Alikuwa mutu muzuri, mwenye furaha, na mwenye bidii na alinionyesha mufano muzuri.

Katika mwaka wa 1941, tulifanya safari kwa treni ili kuenda mu muji wa St. Louis, Missouri, kwa ajili ya mukusanyiko mukubwa. Kwenye mukusanyiko huo, watoto wote waliombwa wakae pamoja karibu na jukwaa ili wasikilize hotuba ya Ndugu Rutherford yenye ilikuwa na kichwa “Watoto wa Mufalme.” Ku mwisho wa hotuba yake, watoto wote 15 000 walipata kitu fulani chenye hawakuwazia kabisa. Ndugu Rutherford na wasaidizi wake walipatia kila mumoja wetu kitabu cha mupya chenye kichwa Watoto (katika Kiingereza).

Katika Mwezi wa 4, 1943, tulihuzuria Mukusanyiko wenye kichwa “Mwito wa Kutenda” mu muji wa Coffeyville, Kansas. Kule, tulisikia tangazo lenye lilisema kama makutaniko yote yatakuwa na masomo ya mupya, ni kusema, Shule ya Huduma ya Kiteokrasi. Pia, tulipata kijitabu cha mupya chenye kilikuwa na somo 52 zenye tungetumia wakati wa masomo. Ku mwisho wa mwaka huo, nilifanya mugao wangu wa kwanza kwenye masomo hayo. Mukusanyiko huo ulikuwa pia wa pekee kwangu, juu mimi pamoja na watu wengine kidogo, tulibatizwa mu kiziwa cha maji ya baridi karibu na shamba fulani.

NILIPENDA KUTUMIKIA KU BETELI

Nilimaliza masomo ya segondere mu mwaka wa 1951 na nilipaswa kuamua namna nitatumia maisha yangu. Ndugu yangu Jerry alikuwa ametumikia ku Beteli. Mimi pia nilipenda kabisa kuenda ku Beteli, kwa hiyo nilituma ombi langu. Bila kukawia, nilialikwa na nikaanza kutumikia ku Beteli tarehe 10 Mwezi wa 3, 1952. Huo ulikuwa uamuzi wa muzuri sana; umenisaidia nijitoe sana mu kazi ya Yehova.

Nilitumaini kama nitatumika mahali pa kuchapishia vichapo ili nisaidie mu kazi ya kutoa magazeti na vichapo vyetu vingine. Lakini sikupata nafasi ya kufanya vile hata siku moja. Nilipewa mugao wa kutolea watu chakula na kisha nilitumika mu chumba cha kupikia. Nilifurahia kazi hiyo na nilijifunza mambo mengi. Tulikuwa tunagomboana, na nilikuwa na wakati fulani wa kupumuzika wakati wa muchana. Mara nyingi, nilikuwa ninaenda mu chumba cha Beteli cha kuwekea vichapo na nilikuwa ninatumia vitabu vya mingi vyenye vilikuwa mule ili kufanya funzo langu la pekee. Kufanya vile kulinisaidia kutia nguvu imani yangu na urafiki wangu pamoja na Yehova. Niliazimia hata zaidi kumutumikia Yehova ku Beteli muda murefu kadiri ningeweza. Jerry alikuwa ametoka ku Beteli mu mwaka wa 1949 na akamuoa Patricia, lakini walikuwa wanaishi karibu na Brooklyn. Alinisaidia na kunitia moyo wakati nilikuwa ningali mupya ku Beteli.

Kisha tu kufika ku Beteli, ndugu walianza kutafuta Wanabeteli wenye wangeweza kuongeza ku liste ya wasemaji wa Beteli. Wasemaji hao walipewa mugao wa kutembelea makutaniko mupaka kwenye umbali wa kilometre 320 na Brooklyn. Wakati walitembelea makutaniko, walikuwa wanatoa hotuba ya watu wote na kuhubiri pamoja na kutaniko. Nilikuwa kati ya ndugu wenye walichaguliwa. Nilianza kutembelea makutaniko na kutoa hotuba za watu wote nikiwa na wasiwasi. Wakati huo, hotuba ya watu wote ilikuwa inafanya saa moja. Nilizoea kusafiri kwa treni ili kutembelea makutaniko. Ninakumbuka muzuri Siku ya Yenga moja kisha midi mu kipindi cha baridi mwaka wa 1954. Nilipanda mu treni ya kurudia New York na nilipaswa kufika ku Beteli mangaribi. Lakini wakati tulikuwa mu njia, kulikuwa zoruba ya upepo mukali na teluji. Motere ya treni ikaacha kutumika, na nikafika mu muji wa New York Siku ya Kwanza saa kumi na moja asubui (5:00). Kutokea mahali treni zinasimamaka mupaka Brooklyn, nilikamata treni ya chini ya udongo na mara moja nikaenda kutumika mu chumba cha kupikia. Nilifika nyuma kidogo na nilikuwa mwenye kuchoka sana juu sikulala usiku wote. Lakini furaha yenye nilipata kwa kutumikia makutaniko na kukutana na ndugu na dada wengi wapya ilipita sana namna nilijitoa.

Tuko mu studio ya WBBR, tunajitayarisha kwa ajili ya programu fulani ya kupitisha

Katika miaka yangu ya kwanza ku Beteli, nilianza pia kushiriki mu programu ya funzo la Biblia yenye ilitangazwa kila juma ku kituo chetu cha radio, WBBR. Studio zilikuwa ku gorofa ya pili ya jengo la 124 Columbia Heights. Ndugu Alexander Macmillan, mwenye alikuwa ametumikia ku Beteli kwa miaka mingi, alikuwa anashiriki kwa ukawaida mu programu hizo za radio. Tulizoea kumuita Ndugu Mac. Alituonyesha mufano muzuri sisi ndugu vijana ku Beteli juu alikuwa amebakia muaminifu hata kama alipatwa na magumu mengi.

Tulitumia mialiko hii ili kufanya matangazo kwa ajili ya WBBR

Katika mwaka wa 1958, mugao wangu ulibadilika na nilianza kutumika kwa ukaribu pamoja na ndugu wenye walimaliza Masomo ya Gileadi. Nilikuwa ninasaidia wanaume na wanamuke hao wenye bidii ili wapate viza zao, na nilikuwa ninafanya mipango kwa ajili ya safari zao. Wakati huo, safari ya ndege ilikuwa bei sana, kwa hiyo, ndugu wengi wenye walitumwa Afrika na Asia kisha masomo walikuwa wanasafiri katika mashua za kubeba mizigo. Kisha miaka fulani, wakati bei ya ndege ilishuka, wamisionere wengi walisafiri kwa ndege ili kuenda katika migao yao.

Ninakusanya diplome za Gileadi mbele programu ya kumaliza masomo ianze

SAFARI ZA KUENDA KU MIKUSANYIKO

Katika mwaka wa 1960, nilifanya mipango ya kukodi ndege kutoka inchi ya Amerika mupaka Ulaya kwa ajili ya mikusanyiko ya kimataifa ya mwaka wa 1961. Nilisafiri kwa ndege ili kuenda Hamburg, Ujerumani ku mukusanyiko moja kati ya mikusanyiko hiyo. Kisha mukusanyiko huo, mimi na Wanabeteli wengine tatu tulikodi motokari na tukasafiri kutokea Ujerumani mupaka Italia na tukatembelea ofisi ya tawi ya Roma. Kutokea kule, tulienda Ufaransa, tulitambuka Milima ya Pyrénées, na tukaingia mu inchi ya Uhispania, kwenye kazi yetu ilikuwa inakatazwa. Tuliweza kutolea ndugu na dada wa Barcelona vichapo fulani, vyenye tulikuwa tumefunga muzuri ili vionekane kama zawadi. Tulifurahi sana kukutana nao! Kutokea kule, tulisafiri kwa motokari mupaka Amsterdam na tukasafiri kwa ndege ili kurudia New York.

Katika mwaka wa 1962, nilipewa mugao wa kufanya mipango kwa ajili safari za ndugu na dada 583 wenye wangeenda kwenye mikusanyiko ya pekee ya kimataifa yenye ilifanywa mu dunia yote. Huo ulikuwa mukusanyiko wa mwaka wa 1963 wenye ulikuwa na kichwa “Habari Njema za Milele.” Ndugu na dada hao wangehuzuria mikusanyiko mu Ulaya, Asia, na Pasifiki ya Kusini na wangeenda Honolulu katika Hawaii, na kisha wangeenda Pasadena katika Kalifornia. Pia, wangetembelea Lebanoni na Yordani ili kufanya matembezi ya pekee mu inchi fulani zenye kuzungumuziwa mu Biblia. Idara yetu ilifanya mipango kwa ajili ya safari hizo za ndege na kutafuta vyumba vya hoteli na viza zote zenye zilihitajiwa.

NINAPATA MUTU MUPYA WA KUSAFIRI PAMOJA NAYE

Kuko sababu ingine yenye ilifanya mwaka wa 1963 ukuwe wa maana sana kwangu. Tarehe 29 Mwezi 6, nilimuoa Lila Rogers wa Missouri; alifika ku Beteli mu mwaka wa 1960. Juma moja kisha ndoa yetu, mimi na Lila tulijiunga na wale wenye walisafiri mu dunia yote na tulitembelea Ugiriki, Misri, na Lebanoni. Kutokea kule, tulifanya safari fupi ya ndege ili kuenda Yordani. Lakini, kazi yetu ilikuwa inawekewa vizuizi kule, na wenye mamlaka hawakukuwa wanapatia Mashahidi wa Yehova viza. Kwa hiyo, hatukujua kutatokea nini wakati tutafika kule. Wazia namna tulifurahi na kushangaa sana wakati tuliona kikundi cha ndugu na dada wanasimama juu ya jengo ndogo sana kwenye uwanja wa ndege na walikuwa na kitambaa kikubwa chenye kilikuwa na maandishi yenye kusema “Karibu Mashahidi wa Yehova”! Tulifurahia sana kutembelea inchi zenye kuzungumuziwa mu Biblia na kuona mahali Abrahamu, Isaka, na Yakobo waliishi, mahali Yesu na mitume wake walihubiri, na mahali Ukristo ulianzia na kuenea mupaka “miisho ya dunia.”​—Mdo. 13:47.

Kwa miaka 55, Lila amenitegemeza kwa ushikamanifu mu migao yetu yote. Tulitembelea Uhispania na Ureno (Portugal) mara nyingi wakati kazi yetu ilikuwa inakatazwa kule. Tuliweza kutia moyo ndugu na dada zetu na kuwapelekea vichapo na vitu vingine vyenye walikuwa navyo lazima. Tuliweza hata kutembelea ndugu zetu fulani wenye walikuwa mu gereza katika Cádiz, mu inchi ya Uhispania. Nilifurahi sana kuona nilipata nafasi ya kuwatolea hotuba yenye kutia moyo.

Tuko pamoja na Patricia na Jerry Molohan wakati tulikuwa tunaenda kwenye Mukusanyiko wa mwaka wa 1969 wenye kichwa “Amani Duniani”

Katika miaka kuanzia 1963, nimefanya mipango ya safari kwa ajili ya mikusanyiko ya kimataifa yenye ilifanyika mu Afrika, Australia, Amerika ya Kati na ya Kusini, Ulaya, Asia Mashariki, Hawaii, Nouvelle-Zélande, na Porto Rico. Mimi na Lila tumehuzuria mikusanyiko mingi yenye hatuwezi kusahau, kwa mufano mukusanyiko wa Varsovie, mu inchi ya Polandi, mwaka wa 1989. Ndugu na dada wengi kutoka Urusi waliweza kuja kwenye mukusanyiko huo mukubwa. Huo ndio ulikuwa mukusanyiko wao wa kwanza kabisa! Tulikutana na ndugu na dada wenye, juu ya imani yao, walikuwa wamefungwa mu gereza kwa miaka mingi katika Muungano wa Sovieti.

Mugao mwingine wenye nilifurahia kabisa ni kutembelea na kutia moyo familia za Beteli na wamisionere katika dunia yote. Mara ya mwisho, tulienda Korea ya Kusini na tulipata nafasi ya kukutana na ndugu 50 wenye walikuwa mu gereza katika Suwon. Wote walikuwa na mawazo ya muzuri kabisa na walikuwa wanangojea kwa hamu wakati watamutumikia tena Yehova bila vizuizi. Kukutana na ndugu hao kulitutia moyo sana!​—Ro. 1:11, 12.

ONGEZEKO LINALETA FURAHA

Nimejionea namna Yehova amebariki watu wake kwa miaka mingi. Wakati nilibatizwa mu mwaka wa 1943, kulikuwa wahubiri karibu 100 000. Sasa kuko wahubiri zaidi ya 8 000 000 wenye wako wanamutumikia Yehova mu inchi 240. Kazi ya bidii ya wale wenye walisoma Masomo ya Gileadi imesaidia sana kuleta ongezeko hilo. Kutumika kwa ukaribu pamoja na wengi kati ya wamisionere hao na kuwasaidia kufika katika migao yao kumeniletea furaha sana.

Niko mwenye furaha kwa sababu wakati nilikuwa ningali kijana, niliamua kutumia maisha yangu mu kazi ya Yehova na nilifanya ombi la kutumikia ku Beteli. Yehova amenibariki sana katika miaka hii yote. Zaidi ya mambo yote yenye tunafurahia katika utumishi wa Beteli, mimi na Lila tulifurahia pia kuhubiri pamoja na makutaniko mbalimbali katika Brooklyn kwa miaka zaidi ya 50 na tumejifanyia marafiki wengi wa kweli.

Ninaendelea kutumikia ku Beteli kwa musaada wa Lila kila siku. Hata kama niko sasa na miaka zaidi ya 84, niko mwenye furaha sana na ningali na uwezo wa kufanya kazi ya maana na kusaidia mu kazi ya tawi ya kushugulikia barua mbalimbali.

Mimi na Lila leo

Ni furaha sana kuwa mu tengenezo la Yehova la muzuri sana na kuona utimizo wa maneno yenye kuwa mu andiko la Malaki 3:18. Andiko hilo linasema hivi: “Mutaona tena tofauti kati ya mutu mwenye haki na mutu muovu, kati ya mutu mwenye kumutumikia Mungu na mwenye hamutumikie.” Kila siku, tunaona kama ulimwengu wa Shetani unaendelea kuharibika na kama watu hawana tumaini na furaha mu maisha yao. Lakini wale wenye wanamupenda Yehova na kumutumikia wako na furaha mu maisha, hata katika siku hizi za magumu, na wako na tumaini la kweli kwa ajili ya wakati wenye kuja. Ni pendeleo kabisa kuhubiria wengine habari njema! (Mt. 24:14) Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utageuza dunia hii kuwa paradiso. Tunangojea kwa hamu kabisa wakati huo! Kila mutu ku dunia atakuwa na afya ya muzuri na atakuwa mwenye furaha na ataishi milele.