Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Ni nini ilimusaidia mwanafunzi Stefano abakie mwenye kutulia kabisa wakati alikuwa anateswa?

STEFANO alipambana na kikundi cha wanaume wakali. Waamuzi hao 71 walikuwa kati ya wanaume wenye mamlaka zaidi katika taifa la Israeli, juu walifanyiza Sanhedrini, ni kusema, tribinali kubwa zaidi mu Israeli. Kuhani Mukubwa Kayafa, mwenye aliongoza mashitaka miezi kidogo yenye ilikuwa imepita wakati Yesu alipewa hukumu ya kifo, ndiye alikuwa amewakusanya. (Mt. 26:57, 59; Mdo. 6:8-12) Wakati walikuwa wanaleta watu wenye walikuwa wanamushitaki Stefano mambo ya uongo, mumoja kisha mwingine, waliona jambo fulani la kushangaza sana juu yake, uso wake ulikuwa “kama uso wa malaika.”​—Mdo. 6:13-15.

Ni nini ilimusaidia Stefano abakie mwenye kutulia kabisa mu hali kama hiyo ya kuogopesha? Mbele Stefano apelekwe mbele ya Sanhedrini, alikuwa amejitoa kabisa katika utumishi wake kupitia muongozo wa roho ya Mungu yenye nguvu. (Mdo. 6:3-7) Wakati alikuwa anasambishwa, roho ileile ilikuwa inafanya kazi ndani yake, ilikuwa inamufariji na kumukumbusha mambo fulani. (Yoh. 14:16; maelezo ya chini) Wakati Stefano alikuwa anajitetea bila woga, kama vile inaonyeshwa mu Matendo sura ya 7, roho takatifu ilimukumbusha maandiko 20 hivi ao zaidi yenye kuwa mu Maandiko ya Kiebrania. (Yoh. 14:26) Lakini imani ya Stefano ilitiwa nguvu zaidi wakati alipata maono; katika maono hayo alimuona Yesu anasimama ku mukono wa kuume wa Mungu.​—Mdo. 7:54-56, 59, 60.

Siku moja, tunaweza kuogopeshwa na kuteswa. (Yoh. 15:20) Wakati tunajilisha Neno la Mungu kwa ukawaida na kufanya kwa bidii kazi ya kuhubiri, tunaruhusu roho ya Yehova ifanye kazi ndani yetu. Sisi pia tutapata nguvu ya kuvumilia upinzani na kuendelea kuwa na amani ya akili.​—1 Pe. 4:12-14.