Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umutegemee Yehova ili Uishi!

Umutegemee Yehova ili Uishi!

“Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote, na usitegemee uelewaji wako mwenyewe.”​—MEZ. 3:5.

NYIMBO: 3, 8

1. Juu ya nini sisi wote tuko na lazima ya faraja?

SISI wote tuko na lazima ya faraja ao kitulizo. Pengine maisha yetu yamejaa mambo mengi yenye kuleta wasiwasi, yenye kuvunja moyo, na mahangaiko. Pengine tunateseka kwa sababu tuko na ugonjwa fulani, tumezeeka, ao mutu mwenye tunapenda amekufa. Wamoja kati yetu wanatendewa mubaya na wengine. Zaidi ya hilo, watu wenye kutuzunguka wanaendelea kuwa wenye jeuri zaidi. Kwa kweli, hizi “nyakati za hatari” zinahakikisha kama tunaishi “katika siku za mwisho” na kama kila siku yenye kupita tunakaribia ulimwengu mupya. (2 Ti. 3:1) Lakini, pengine tumengojea kwa muda murefu ahadi za Yehova zitimie, na pengine tunapatwa na magumu mengi zaidi. Kwa hiyo, ni wapi tunaweza kupata faraja?

2, 3. (a) Tunajua nini juu ya Habakuki? (b) Juu ya nini tutazungumuzia kitabu cha Habakuki?

2 Tuzungumuzie basi kitabu cha Habakuki ili kupata jibu la ulizo hilo. Hata kama Maandiko hayatuambie mambo mengi juu ya maisha ya Habakuki, kitabu chake ni chenye kutia moyo kabisa. Pengine jina Habakuki linamaanisha “Kumbatio Changamufu.” Hilo linaweza kumaanisha kumbatio changamufu la Yehova lenye linafariji waabudu wake. Ao linaweza pia kumaanisha namna waabudu wake wanashika Yehova kwa nguvu sana. Habakuki alizungumuza na Mungu na kumuuliza maulizo fulani. Yehova alimuongoza Habakuki kupitia roho yake ili aandike mazungumuzo hayo kwa sababu alijua kama yanaweza kutuletea faida.​—Hab. 2:2.

3 Jambo moja tu lenye Biblia inatuambia juu ya Habakuki, nabii mwenye alikuwa na huzuni, ni mazungumuzo hayo kati yake na Yehova. Lakini kitabu chake ni sehemu ya “mambo yote yenye yaliandikwa zamani” katika Neno la Mungu, “ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.” (Ro. 15:4) Namna gani kitabu cha Habakuki kinaweza kusaidia kila mumoja kati yetu? Kinaweza kutusaidia tuelewe maana ya kumutegemea Yehova. Na unabii wa Habakuki unatuhakikishia kama tunaweza kupata amani ya akili, hata kama tunapambana na magumu ao majaribu ya namna gani.

USALI KWA YEHOVA

4. Juu ya nini Habakuki alikuwa na huzuni?

4 Soma Habakuki 1:2, 3. Habakuki aliishi katika kipindi cha magumu sana. Watu wenye walikuwa wanamuzunguka walikuwa wabaya na wenye jeuri, na jambo hilo lilimufanya akuwe na huzuni sana. Kila mahali kwenye aliangalia, aliona Waisraeli wanatendeana bila huruma na bila haki. Habakuki alijiuliza hivi: ‘Mambo haya ya mubaya yataisha wakati gani? Juu ya nini Yehova anakawia sana kufanya jambo fulani juu ya hali hii?’ Alijisikia kuwa anaishiwa kabisa. Kwa hiyo, alimuomba sana Yehova afanye jambo fulani. Pengine Habakuki alianza kuwaza kama Yehova hakuhangaikia tena watu wake ao kama hangetenda. Umekwisha kujisikia vile?

5. Kitabu cha Habakuki kinaweza kutufundisha nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari hii.)

5 Habakuki aliuliza maulizo hayo kwa sababu alikuwa ameacha kumutegemea Yehova na ahadi zake? Hapana kabisa! Habakuki alikuwa anamuambia Yehova amusaidie kupiganisha mashaka na magumu yake, hilo linaonyesha kama alikuwa hajapoteza tumaini lakini alikuwa angali anamutegemea Yehova. Ni wazi kwamba Habakuki alikuwa na mahangaiko na alikuwa mwenye kuvurugika. Hakuelewa ni juu ya nini Yehova alikuwa anangojea mbele ya kutenda na juu ya nini alikuwa anamuacha ateseke sana. Kwa sababu Yehova alimuongoza Habakuki kupitia roho yake ili aandike mahangaiko yake, hilo linatufundisha jambo fulani la maana. Hatupaswe kuogopa kumuambia Yehova mahangaiko ao mashaka yetu. Kwa kweli, anatualika kwa upendo tusali na kumuambia namna tunajisikia kabisa. (Zb. 50:15; 62:8) Andiko la Mezali 3:5 linatutia moyo sisi wote hivi: “Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote, na usitegemee uelewaji wako mwenyewe.” Habakuki alitumia maneno hayo katika maisha yake.

6. Juu ya nini ni jambo la maana kusali?

6 Habakuki alimutegemea Yehova, Rafiki na Baba yake, na akakamata hatua ya kumukaribia. Hakuhangaikia tu hali yake na hakujaribu kutengeneza mambo yeye mwenyewe. Lakini, alisali juu ya mahangaiko yake na juu ya namna alikuwa anajisikia. Huo ni mufano muzuri kwetu. Yehova, Musikiaji wa sala, anatualika tuonyeshe kama tunamutegemea kwa kusali na kumuambia mahangaiko yetu. (Zb. 65:2) Wakati tunafanya vile, tutaona namna Yehova anajibu sala zetu. Tutajisikia kama vile anatukumbatia wakati anatufariji na kutuongoza. (Zb. 73:23, 24) Atatusaidia tuelewe namna anaona hali yetu hata kama tunateseka namna gani. Kusali kwa Yehova ni njia moja kati ya njia za muzuri zaidi za kuonyesha kama tunamutegemea.

UMUSIKILIZE YEHOVA

7. Yehova alitenda namna gani wakati Habakuki alimuambia mahangaiko yake?

7 Soma Habakuki 1:5-7. Kisha Habakuki kumuambia Yehova mahangaiko yake, pengine alijiuliza ikiwa Yehova angetenda namna gani. Kwa sababu Yehova ni Baba mwenye upendo, alielewa namna Habakuki alikuwa anajisikia. Alijua kama Habakuki alikuwa anateseka na alikuwa anaomba sana musaada. Kwa hiyo, Yehova hakumukaripia lakini alimuambia mambo yenye alikaribia kufanya juu ya Wayahudi wenye kukosa uaminifu. Kwa kweli, pengine Habakuki alikuwa mutu wa kwanza mwenye Yehova aliambia kama alikuwa karibu kupatia Wayahudi malipizi.

8. Juu ya nini jibu lenye Yehova alitoa haiko njo lenye Habakuki alikuwa anangojea?

8 Yehova alimuambia Habakuki kama alikuwa tayari kufanya jambo fulani. Angepatia malipizi watu wa Yuda wenye jeuri na wabaya. Wakati Yehova alisema kama jambo hilo lingetokea “katika siku zenu,” Yehova alionyesha kama hukumu yake ingekuja wakati Habakuki alikuwa angali anaishi ao wakati Waisraeli wa wakati wake walikuwa wangali wanaishi. Jibu la Yehova haiko njo lenye Habakuki alikuwa anangojea. Wakaldayo, ao Wababiloni, walikuwa wanatenda bila huruma. Walikuwa wenye jeuri sana kupita Waisraeli, wenye walikuwa wanajua kanuni za Yehova kwa kadiri fulani. Kwa hiyo, juu ya nini Yehova angetumia taifa la wapagani wenye jeuri ili kupatia watu wake malipizi? Hilo lingeletea tu watu wa Yuda mateso zaidi. Kama ulikuwa Habakuki, ungejisikia namna gani?

9. Pengine Habakuki alijiuliza maulizo gani mengine?

9 Soma Habakuki 1:12-14, 17. Hata kama Habakuki alielewa kama Yehova angetumia Wababiloni ili kupatia malipizi watu wabaya wenye walikuwa wanamuzunguka, aliendelea kuwa mwenye kuvurugika. Lakini alikuwa munyenyekevu na aliazimia kuendelea kumutegemea Yehova. Kwa kweli, alisema kama Yehova aliendelea kuwa “Mwamba” wake. (Kum. 32:4; Isa. 26:4) Habakuki alikuwa hakika kama Mungu ni mwenye upendo na mwenye fazili, kwa hiyo, hakuogopa kumuuliza maulizo mengine fulani, kama vile: Juu ya nini Yehova anaacha mambo yaharibike hata zaidi katika Yuda na watu wateseke zaidi? Juu ya nini hafanye jambo fulani mara moja? Juu ya nini Mweza-Yote ‘ananyamaza’ na kuvumilia mambo ya mubaya yenye kufanyika kila mahali? Yehova ni “Mutakatifu,” na ‘macho yake ni safi sana, hayawezi kuendelea kuangalia ubaya,’ kwa hiyo, juu ya nini anaacha mambo hayo yatokee?

10. Juu ya nini wakati fulani tunaweza kujisikia kama vile Habakuki alijisikia?

10 Wakati fulani tunaweza kujisikia kama vile Habakuki alijisikia. Tunamusikiliza Yehova. Tunamutegemea na tunasoma na kujifunza Neno lake, lenye linatia nguvu tumaini letu. Tunajifunza pia mambo mengi juu ya ahadi zake wakati tunasikiliza mambo yenye tengenezo lake linatufundisha. Lakini, pengine tunaweza kuendelea kujiuliza hivi: ‘Mateso yetu yataisha wakati gani?’ Jambo lenye Habakuki alifanya kisha pale, linaweza kutufundisha jambo fulani.

UMUNGOJEE YEHOVA ATENDE

11. Habakuki aliazimia kufanya jambo gani?

11 Soma Habakuki 2:1. Mazungumuzo kati ya Habakuki na Yehova yalimupatia amani ya akili. Yalimusaidia aazimie kumungojea Yehova atende. Habakuki alirudilia tena azimio lake wakati alisema hivi: “Ninangojea kimya-kimya siku ya taabu.” (Hab. 3:16) Watumishi wengine waaminifu wa Mungu waliendelea pia kumungojea Yehova kwa uvumilivu ili atende. Mufano wao unatutia moyo kwa sababu unaonyesha kama sisi pia tunaweza kufanya vile.​—Mik. 7:7; Yak. 5:7, 8.

12. Mufano wa Habakuki unaweza kutufundisha nini?

12 Jambo lenye Habakuki aliazimia kufanya linaweza kutufundisha nini? Kwanza, hatupaswe kuacha hata kidogo kusali kwa Yehova hata kama tuko na magumu ya namna gani. Pili, tunapaswa kusikiliza mambo yenye Yehova anatuambia kupitia Neno lake na tengenezo lake. Na tatu, tunapaswa kumungojea Yehova kwa uvumilivu ili atende na tunapaswa kuwa na tumaini kama atamaliza maumivu yetu kwa wakati wake mwenyewe. Kama tunamuiga Habakuki, tutakuwa na amani ya akili na tutaweza kuvumilia. Tumaini letu litatusaidia kuwa na uvumilivu na kuwa na furaha hata kama tuko na magumu ya namna gani. Tuko hakika kama Baba yetu wa mbinguni atatenda.​—Ro. 12:12.

13. Namna gani Yehova alimufariji Habakuki?

13 Soma Habakuki 2:3. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova alifurahi kwa sababu Habakuki aliamua kumungojea ili atende. Mweza-Yote alijua kabisa sababu gani Habakuki alikuwa anateseka. Kwa hiyo, alimufariji nabii huyo na kumuhakikishia kwa upendo kama angejibu maulizo yake yenye kutoka mu moyo. Mahangaiko yote ya Habakuki yalikuwa karibu kuisha. Ni kama vile Yehova alikuwa anamuambia Habakuki hivi: “Uvumilie tu na unitegemee. Nitajibu sala yako, hata kama jibu linaonekana kuwa linakawia.” Yehova alimukumbusha Habakuki kama tayari alikuwa ameamua ni wakati gani angetimiza ahadi zake. Kwa hiyo, alimutia Habakuki moyo aendelee kungojea. Mwishowe, nabii huyo hangevunjika moyo.

Juu ya nini tunaazimia kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote? (Picha hii inapatana na fungu la 14)

14. Tunapaswa kuazimia kufanya nini wakati tunapatwa na magumu?

14 Sisi pia tunapaswa kumungojea Yehova atende. Tunapaswa pia kusikiliza kwa uangalifu mambo yenye anatuambia. Kisha tutakuwa na tumaini na amani ya akili hata kama tunapatwa na magumu ya namna gani. Yesu alitutia moyo tusikaze akili yetu juu ya “nyakati ao vipindi” vyenye Mungu hajatuambia jambo fulani juu yavyo. (Mdo. 1:7) Tunapaswa kuwa hakika kama Yehova anajua wakati wa muzuri zaidi wa kutenda. Kwa hiyo, hatupaswe kupoteza tumaini lakini tunapaswa kuonyesha unyenyekevu na uvumilivu na kuwa na imani katika Mungu. Na wakati tunaendelea kungojea, tunapaswa kutumia wakati wetu kwa hekima ili kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote.​—Mk. 13:35-37; Gal. 6:9.

YEHOVA ATAPATIA UZIMA WA MILELE WALE WENYE KUMUTEGEMEA

15, 16. (a) Ni ahadi gani zenye kupatikana katika kitabu cha Habakuki? (b) Ahadi hizo zinatufundisha nini?

15 Yehova anatoa ahadi hizi: “Mwenye haki ataishi kwa uaminifu wake,” na “dunia itajaa ujuzi juu ya utukufu wa Yehova.” (Hab. 2:4, 14) Kwa kweli, Yehova anaahidi kama atapatia uzima wa milele wale wenye wanavumilia na kumutegemea.

16 Ahadi hiyo yenye kupatikana katika Habakuki 2:4 ni ya maana sana; ndiyo sababu mutume Paulo aliitaja mara tatu katika barua zake. (Ro. 1:17; Gal. 3:11; Ebr. 10:38) Tunaweza kuwa hakika kama hata tupatwe na magumu ya namna gani, tutaona namna ahadi za Yehova zitatimia ikiwa tunamutegemea. Yehova anapenda tukaze akili yetu juu ya tumaini letu la wakati wenye kuja.

17. Yehova anatuhakikishia kama atatufanyia nini ikiwa tunamutegemea?

17 Kitabu cha Habakuki kinatufundisha somo kubwa sisi wote wenye kuishi katika siku za mwisho. Yehova anaahidi kama atapatia uzima wa milele mutu yeyote mwenye haki mwenye kumutegemea. Kwa hiyo, tuendelee basi kumutegemea kabisa Mungu, hata kama tuko na magumu ao mahangaiko ya namna gani. Mambo yenye Yehova alimuambia Habakuki yanatuhakikishia kama atatutegemeza na kutuokoa. Kwa upendo, anatuomba tumutegemee na kungojea kwa uvumilivu wakati wenye tayari ameweka ili Ufalme wake utawale dunia. Wakati huo, dunia itajaa watu wenye kumuabudu Yehova wenye kuwa na furaha na amani.​—Mt. 5:5; Ebr. 10:36-39.

UMUTEGEMEE YEHOVA NA UKUWE MWENYE FURAHA

18. Namna gani maneno ya Yehova yalimusaidia Habakuki?

18 Soma Habakuki 3:16-19. Mambo yenye Yehova aliambia Habakuki yalimusaidia sana. Habakuki alifikiri sana juu ya mambo ya ajabu yenye Yehova alikuwa amefanyia watu wake zamani. Sasa alimutegemea Yehova zaidi. Alikuwa hakika kama karibuni Yehova angetenda! Hilo lilimufariji nabii huyo, hata kama alijua kuwa pengine angeendelea kuteseka kwa wakati fulani. Habakuki hakukuwa tena na mashaka. Lakini, alikuwa na imani kabisa kama Yehova angemuokoa. Kwa kweli, maneno yenye alisema mu mustari wa 18 ni kati ya maneno yenye kuwa mu Biblia yenye kuonyesha sana sifa ya kumutegemea Yehova. Watu fulani wenye elimu wanaamini kama maana ya maneno hayo ni hii: “Nitaruka kwa sababu ya furaha katika Bwana; nitacheza-cheza kwa sababu ya furaha katika Mungu.” Hilo ni somo kubwa sana kwetu sisi wote! Zaidi ya kutupatia ahadi za muzuri sana juu ya wakati wenye kuja, Yehova anatuhakikishia pia kama hivi karibuni atatimiza ahadi hizo.

19. Tunaweza kufanya nini ili Yehova atufariji kama vile alimufariji Habakuki?

19 Somo la maana lenye tunajifunza katika kitabu cha Habakuki ni kumutegemea Yehova. (Hab. 2:4) Ili tuendelee kumutegemea Yehova, tunapaswa kutia nguvu urafiki wetu pamoja naye. Kwa hiyo, tunapaswa kufanya mambo haya: (1) Kuendelea kusali, kwa kumuambia Yehova mambo yote yenye kutuletea wasiwasi na mahangaiko yetu. (2) Kusikiliza kwa uangalifu mambo yenye Yehova anatuambia katika Neno lake, na kufuata muongozo wenye anatutolea kupitia tengenezo lake. (3) Kuwa waaminifu na kungojea Yehova kwa uvumilivu ili atimize ahadi zake. Habakuki alifanya vile. Hata kama alikuwa na huzuni sana wakati alianza kuzungumuza na Yehova, mwishowe, alikuwa mwenye kutiwa moyo na mwenye furaha! Kama tunamuiga Habakuki, sisi pia tutafarijiwa wakati Yehova, Baba yetu wa mbinguni, anatukumbatia kwa uchangamufu. Hiyo ni faraja kubwa sana yenye tunaweza kupata katika ulimwengu huu mubaya.