Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tunaweza Kumpa Yehova Zawadi Gani?

Tunaweza Kumpa Yehova Zawadi Gani?

PINDI moja, Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Ukweli huo wa msingi unahusu uhusiano wetu pamoja na Yehova. Jinsi gani? Yehova ametupatia zawadi nyingi zinazotufanya tuwe na furaha, lakini tunaweza kupata furaha nyingi hata zaidi kwa kumpa Yehova zawadi. Tunaweza kumpa Yehova zawadi gani? Andiko la Methali 3:9 linasema hivi: “Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani.” ‘Vitu vyetu vyenye thamani’ vinatia ndani wakati wetu, vipawa vyetu, nguvu zetu, na mali zetu za kimwili. Tunapotumia vitu hivyo kuendeleza ibada ya kweli, tunampa Yehova zawadi, na kufanya hivyo hutuletea furaha nyingi.

Ni nini kitakachotusaidia tusichukulie kivivihivi pendeleo letu la kumpa Yehova zawadi za mali za kimwili tulizo nazo? Mtume Paulo aliwaambia Wakorintho “[waweke] kando kitu fulani” kuwa mchango. (1 Kor. 16:2) Unaweza kufanya nini ikiwa ungependa kupata habari zaidi kuhusu njia mbalimbali za kutoa michango zinazotumiwa katika eneo lenu? Tafadhali tazama sanduku hapa chini.

Njia ya kutoa michango mtandaoni haitumiki katika nchi zote. Hata hivyo, unaweza kupata habari kuhusu njia unazoweza kutumia ili kutoa michango kwenye ukurasa wa kutoa michango. Katika nchi fulani, kuna hati kwenye ukurasa wa mwanzo inayojibu maswali yanayoulizwa mara nyingi kuhusu michango.