Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Zawadi Gani Tunaweza Kumutolea Yehova?

Ni Zawadi Gani Tunaweza Kumutolea Yehova?

WAKATI fulani, Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Kweli hiyo ya musingi inahusu urafiki wetu pamoja na Yehova. Juu ya nini? Yehova ametupatia zawadi nyingi zenye zinatuletea furaha, lakini tunaweza kuwa wenye furaha hata zaidi wakati tunamutolea Yehova zawadi. Ni zawadi gani tunaweza kumutolea Yehova? Mezali 3:9 inasema hivi: “Umuheshimie Yehova kupitia vitu vyako vyenye samani.” ‘Vitu vyetu vyenye samani’ vinatia ndani wakati wetu, uwezo wetu mbalimbali wa kizalikio, nguvu zetu, na vitu vyetu vya kimwili. Wakati tunatumia mambo hayo yote ili kufanya ibada ya kweli iendelee, tunamutolea Yehova zawadi, na kufanya vile kunatuletea furaha kubwa.

Kuhusu vitu vyetu vya kimwili, ni nini inaweza kutusaidia tuone kama ni jambo la maana kumutolea Yehova zawadi yetu? Mutume Paulo aliambia Wakristo wa kutaniko la Korinto ‘waweke kitu fulani pembeni’ kwa ajili ya muchango. (1 Ko. 16:2) Unaweza kufanya nini kama unapenda kupata habari zaidi juu ya njia mbalimbali za kutoa michango zenye kutumiwa mu eneo lenu? Tafazali, ona kisanduku hapa chini.

Njia ya kutoa michango kupitia Enternete haitumike katika inchi zote. Lakini, unaweza kupata habari juu ya njia zingine za kutoa michango kwenye ukurasa wa kutoa michango. Katika inchi fulani, kuko document kwenye ukurasa huo, yenye inatoa majibu kwa maulizo yenye watu wanazoea kuuliza juu ya michango.