Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Atafanya Nini?

Mungu Atafanya Nini?

Kama ungekuwa mu magumu, bila shaka ungependa rafiki muzuri afanye jambo fulani ili kukusaidia. Ile imefanya watu fulani waseme kama Mungu haiko rafiki juu wanawaza kama Mungu hafanye jambo lolote ili kuwasaidia. Kwa kweli, Mungu amekwisha kufanya mambo mingi kwa faida yetu, lakini pia, atafanya jambo fulani ili kumaliza matatizo na mateso yenye kutupata leo. Mungu atafanya nini?

ATAMALIZA UOVU WOTE

Mungu atamaliza uovu wote kwa kuharibu mwenye kuuleta. Biblia inaonyesha mwenye kuleta ule uovu ni nani kwa kusema hivi: “Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Ule “muovu” njo ule mwenye Yesu aliita “mutawala wa ulimwengu huu,” ni kusema, Shetani Ibilisi. (Yohana 12:31) Shetani anachochea ulimwengu wa wanadamu, na ile njo sababu kubwa inafanya ku dunia kukuwe hali za mubaya. Mungu atafanya nini?

Hivi karibuni Yehova Mungu atatenda kupitia Mwana wake, Yesu Kristo, ili ‘kuharibu ule mwenye kuwa na uwezo wa kutokeza kifo, ni kusema, Ibilisi.’ (Waebrania 2:14; 1 Yohana 3:8) Kwa kweli, Biblia inaonyesha kama Ibilisi mwenyewe anajua kuwa “iko na kipindi kifupi cha wakati” mbele aharibiwe. (Ufunuo 12:12) Mungu ataondoa pia mambo yote ya mubaya na wale wote wenye kuileta.​—Zaburi 37:9; Mezali 2:22.

ATAFANYA DUNIA IKUWE PARADISO

Kisha kuondoa mambo yote ya mubaya ku dunia, Muumbaji wetu atatenda ili kutimiza kusudi lake la milele juu ya wanadamu na dunia. Ni mambo gani yenye tunachunga kwa hamu?

Amani na usalama wenye hauna mwisho. “Wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”​—Zaburi 37:11.

Chakula ya mingi na ya muzuri kwa afya. “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima.”​—Zaburi 72:16.

Nyumba za muzuri na kazi za muzuri. “Watajenga nyumba na kuishi ndani, na watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. . . . Wachaguliwa wangu watafurahia kwa ukamili kazi ya mikono yao.”​—Isaya 65:21, 22.

Je, unatamani kuona ile mambo? Hivi karibuni watu wote wataifurahia kila siku.

ATAMALIZA MAGONJWA NA KIFO

Leo, kila mutu anapatwa na magonjwa na kisha anakufa, lakini ile haitakuwa tena. Hivi karibuni, Mungu atafanya watu wapate faida kupitia bei ya ukombozi ya Yesu ili “kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Matokeo itakuwa nini?

Magonjwa itaisha kabisa. “Hakuna mukaaji mwenye atasema: ‘Niko mugonjwa.’ Watu wenye kukaa katika inchi hiyo watasamehewa kosa lao.”​—Isaya 33:24.

Wanadamu hawatapatwa tena na kifo. “Atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova atapanguza machozi kwenye nyuso zote.”​—Isaya 25:8.

Watu wataishi milele. “Zawadi yenye Mungu anatoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.”​—Waroma 6:23.

Wale wote wenye wamekufa watafufuliwa. “Kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” (Matendo 24:15) Zawadi ya Mungu ya bei ya ukombozi itawaletea faida.

Namna gani Mungu atatimiza ile mambo yote?

ATAWEKA SERIKALI KAMILIFU

Mungu atatimiza kusudi lake kwa ajili ya wanadamu na dunia kupitia serikali yenye kuwa ku mbingu. Mutawala wa ile serikali mwenye kuchaguliwa ni Yesu. (Zaburi 110:1, 2) Ile njo serikali ao ufalme wenye Yesu aliambia wanafunzi wake waombe kwa kutumia hii maneno: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, . . . Ufalme wako ukuje.”​—Matayo 6:9, 10.

Ufalme wa Mungu utatawala dunia na kumaliza maumivu na mateso yote. Ule Ufalme njo serikali ya muzuri zaidi yenye wanadamu wanaweza kupata! Njo maana Yesu alijitoa sana ili kuhubiri “habari njema ya Ufalme” wakati wa utumishi wake hapa ku dunia na aliambia wanafunzi wake wafanye vile.​—Matayo 4:23; 24:14.

Kwa sababu ya upendo wake mukubwa juu ya viumbe wake, ni kusema, wanadamu, Yehova Mungu ameahidi kuwafanyia ile mambo yote ya muzuri sana. Ile haikuchochee upende kumujua na kumukaribia? Kama unafanya vile, utapata faida gani? Habari yenye kufuata itafasiria.

MUNGU ATAFANYA NINI? Mungu atamaliza magonjwa yote na kifo, ataunganisha wanadamu wote chini ya Ufalme, ni kusema, serikali yake na kufanya dunia ikuwe paradiso