Unaweza Kumkaribia Mungu
BAADHI YA WATU HUHISI KWAMBA . . .
Mungu hajishughulishi sana na sisi au yeye ni mkuu sana, mtakatifu, na hatuwezi kumkaribia.
BIBLIA INASEMA HIVI
“Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.
“[Tupeni] mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.”—1 Petro 5:7.
UNAWEZA KUFANYA NINI ILI USITAWISHE UHUSIANO WA KARIBU NA MUNGU?
Ongea naye.—Zaburi 145:18, 19.
Msikilize.—Zaburi 32:8.
Fuata mwongozo wake.—Methali 3:5, 6.
Usikate tamaa.—Mathayo 7:7, 8.