Unapokuwa na Ugonjwa Mbaya
IKIWA umeambiwa una ugonjwa unaoweza kusababisha kifo, au tatizo hilo limempata mtu unayempenda, basi unaelewa jinsi suala hilo linavyohangaisha. Zaidi ya kusumbuliwa na ugonjwa, bado unahitaji kupambana na hisia. Safari za kwenda kumwona daktari, ugumu wa kupata au wa kulipia matibabu, au madhara yanayosababishwa na dawa, ni mambo ambayo huongeza woga na wasiwasi. Hisia hizo zinaweza kumlemea sana mtu.
Tunaweza kupata wapi msaada? Watu wengi wametambua kwamba kumkaribia Mungu kupitia sala na kusoma mistari ya Biblia inayotia moyo huwafariji
sana. Msaada mwingine huenda ukatoka kwa washiriki wa familia na marafiki, wanapokuunga mkono na kukuonyesha upendo.MAMBO AMBAYO YAMEWASAIDIA WENGINE
Robert, aliye na umri wa miaka 58, anatoa ushauri huu: “Mwamini Mungu, naye atakusaidia kupambana na ugonjwa wako. Sali kwa Yehova. Mwambie jinsi unavyohisi. Mwombe akupe roho yake takatifu. Mwombe akupe nguvu ili uitie moyo familia yako na akuwezeshe kuwa na utulivu unapovumilia ugonjwa ulio nao.
“Inatia moyo sana washiriki wa familia yako wanapokuwa pamoja nawe unapowahitaji. Huwa ninapigiwa simu kila siku na kuulizwa, ‘Unaendeleaje?’ Marafiki kutoka sehemu mbalimbali hunitia moyo sana. Wao hunisaidia kupata nguvu, na hilo hufanya nisikate tamaa.”
Ikiwa unapanga kumtembelea mgonjwa, kumbuka jambo ambalo Linda anasema: “Bila shaka mgonjwa anatamani kuishi maisha ya kawaida kadiri awezavyo na huenda hangependa kuzungumzia ugonjwa wake kila wakati. Kwa hiyo, zungumza naye kuhusu mambo ya kawaida.”
Hivyo, tukitegemea nguvu kutoka kwa Mungu na faraja inayotolewa na Maandiko, na kupata msaada kutoka kwa marafiki na washiriki wa familia wanaotupenda, hatutakata tamaa ya maisha hata ikiwa tuna ugonjwa mbaya.