Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kwa Kweli, Maisha Ni ya Maana!

Kwa Kweli, Maisha Ni ya Maana!

Faizal alifanyiwa upasuaji mukubwa wa moyo mwaka moja tu kisha kifo cha bibi yake. Anasema hivi: “Wakati ninasoma kitabu cha Yobu, ninajua kama kuko sababu yenye ilifanya Yehova atie kitabu hicho ndani ya Biblia. Wakati tuko wenye kushuka moyo sana na tunasoma katika Biblia kuhusu mutu fulani mwenye alijisikia kama sisi, ile inatupatia kitulizo.” Anaongeza hivi: “Maisha ingali yenye maana.”

Tarsha alikuwa kijana wakati mama yake alikufa. Anasema hivi: “Kumujua Muumbaji wetu njo jambo lenye linafanya maisha ikuwe na kusudi, nikuwe na tumaini, na nikuwe mwenye furaha hata kama niko na magumu mingi. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo wa kututegemeza na kutusaidia kuvumilia kila siku.”

HABARI zenye zilitangulia zimeonyesha namna hali mbalimbali zenye kuumiza zinaweza kufanya ikuwe nguvu kuvumilia katika maisha. Wakati unaendelea kuvumilia peke yako, unaweza kujiuliza ikiwa maisha iko na maana ao hata ikiwa kuko mutu mwenye kukuhangaikia. Ukuwe hakika kama Mungu anaona taabu yako na anakuhangaikia. Uko wa maana sana mbele yake.

Muandikaji wa Zaburi ya 86 alionyesha kama alimutumainia Mungu kwa kusema hivi: “Ninakuitia katika siku ya taabu yangu, kwa maana utanijibu.” (Zaburi 86:7) Lakini pengine unajiuliza, ‘Namna gani Mungu anaweza kunijibu “katika siku ya taabu yangu”?’

Hata kama Mungu hawezi kumaliza matatizo yako mara moja, Neno lake Biblia, linakuhakikishia kama anaweza kukupatia amani ya akili ili kukusaidia uvumilie. Linasema hivi: “Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.” (Wafilipi 4:6, 7, maelezo ya chini) Tafazali, fikiria namna maandiko yenye kufuata ya Biblia inatuhakikishia kama Mungu anatuhangaikia kwa upendo.

Mungu Anakuhangaikia

“Mungu hamupuuze [shomoro] hata mumoja wao. . . . Ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.”​Luka 12:6, 7, maelezo ya chini.

FIKIRIA JAMBO HILI: Ndege wadogo kama shomoro, wanaweza kuonwa na watu wengi kuwa hawana maana, lakini Mungu anawahangaikia. Mungu anaonaka hata ndege shomoro mudogo sana; anaona kila shomoro kuwa kiumbe cha maana chenye kuishi. Wanadamu ni wa maana zaidi kuliko ndege shomoro. Wanadamu ndio viumbe vya maana zaidi kati ya viumbe vya Mungu vyenye kuwa ku dunia. Wameumbwa kwa “mufano” wake na wako na uwezo wa kukomalisha na kuonyesha sifa zake za maana sana.​—Mwanzo 1:26, 27.

“Ee Yehova, umenichunguza kabisa, na unanijua. . . . Unatambua mawazo yangu . . . Unichunguze, na ujue mawazo yangu yenye kuhangaisha.”​Zaburi 139:1, 2, 23.

FIKIRIA JAMBO HILI: Mungu anakujua kipekee. Anajua mahangaiko yako na namna unajisikia kwa ndani kabisa. Hata kama watu wengine hawawezi kuelewa matatizo na mahangaiko yako, Mungu anakuhangaikia na anapenda kukusaidia. Jambo hilo linafanya maisha ikuwe na maana.

Maisha Yako Iko na Maana

“Ee Yehova, sikia sala yangu; kilio changu cha kuomba musaada kikufikie. . . . Unitegee sikio lako; Unijibu haraka wakati ninaita. . . . Atasikiliza sala ya maskini.”​Zaburi 102:1, 2, 17.

FIKIRIA JAMBO HILI: Tangu mwanzo Yehova amekuwa akiona kila chozi lenye wanadamu wametosha kwa sababu ya mateso yao. (Zaburi 56:8) Anaona pia machozi yako. Mungu anakumbuka mateso na machozi yako yote kwa sababu uko wa maana sana mbele yake.

“Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia . . . mimi, Yehova Mungu wako, . . . ni mimi mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’”​Isaya 41:10, 13.

FIKIRIA JAMBO HILI: Mungu iko tayari kukusaidia. Ukianguka, atakuinua.

Kuko Tumaini la Kuwa na Wakati Wenye Kuja wa Muzuri Zaidi

“Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.”​Yohana 3:16.

FIKIRIA JAMBO HILI: Kwa sababu Mungu anakupenda sana, alimutoa Yesu, Mwana wake, kwa kupenda, ili akuwe zabihu kwa ajili yako. Zabihu hiyo inakupatia tumaini la kuishi maisha yenye kusudi na yenye furaha milele. *

Hata kama unaweza kuteseka na kuona kama hauwezi kuvumilia katika maisha yako, ujifunze kwa uangalifu Neno la Mungu na ufanye imani yako katika tumaini lenye Mungu anatoa ikuwe nguvu. Ile itafanya ukuwe mwenye furaha na ukuwe hakika kama maisha yako ni ya maana.

^ fu. 19 Ili kujua mambo mingi zaidi kuhusu namna unaweza kufaidika na zabihu ya Yesu, ona video Tukumbuke Kifo cha Yesu, ku www.pr418.com. Ona chini ya kichwa VICHAPO > VIDEO > MIKUTANO NA KAZI YETU YA MAHUBIRI.