Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 8

Juu ya Nini Tunapaswa Kuonyesha Shukrani?

Juu ya Nini Tunapaswa Kuonyesha Shukrani?

“Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.”​—KOL. 3:15.

WIMBO 46 Asante, Yehova

KIFUPI CHA HABARI *

1. Musamaria mwenye Yesu aliponyesha alifanya nini ili kuonyesha shukrani?

WANAUME kumi walikuwa mu hali ya mubaya sana. Walikuwa wanagonjwa ukoma na hawakukuwa na tumaini kama hali yao ingekuwa muzuri. Lakini siku moja walimuona Mwalimu Mukubwa Yesu, kwa mbali. Walikuwa wamesikia kama Yesu alikuwa anaponyesha magonjwa ya namna zote, na walikuwa hakika kama angewaponyesha. Kwa hiyo, walisema hivi kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwalimu, utusikilie huruma!” Wanaume hao kumi waliponyeshwa kabisa. Kwa kweli, wote walikuwa wenye shukrani juu ya wema wenye Yesu aliwaonyesha. Lakini, mumoja kati yao alifanya mengi zaidi ya kuwa tu mwenye shukrani, alimuonyesha Yesu shukrani. * Mwanaume huyo Musamaria mwenye aliponyeshwa, alichochewa kumusifu Mungu “kwa sauti kubwa.”​—Lu. 17:12-19.

2-3. (a) Juu ya nini tunaweza kukosa kuonyesha shukrani? (b) Tutazungumuzia nini mu habari hii?

2 Kama Musamaria huyo, tunapenda kuwaonyesha shukrani watu wenye wanatutendea kwa wema. Lakini, wakati fulani, tunaweza kusahau kuonyesha shukrani yetu kupitia maneno ao matendo.

3 Mu habari hii, tutazungumuzia juu ya nini ni jambo la maana kuonyesha shukrani kupitia maneno na matendo yetu. Tutajifunza mambo mingi kupitia mifano ya watu fulani wenye kuzungumuziwa mu Biblia wenye walionyesha shukrani na wenye hawakuonyesha ile sifa. Kisha, tutazungumuzia ni katika njia gani fulani tunaweza kuonyesha shukrani.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUONYESHA SHUKRANI?

4-5. Juu ya nini tunapaswa kuonyesha shukrani?

4 Yehova anatuwekea mufano wa kuonyesha shukrani. Njia moja yenye anatumia ili kufanya vile ni kubariki wale wenye wanamufurahisha. (2 Sa. 22:21; Zb. 13:6; Mt. 10:40, 41) Na Maandiko inatutia moyo ‘tukuwe waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.’ (Efe. 5:1) Kwa hiyo, sababu kubwa yenye inatuchochea tuonyeshe shukrani ni hii: tunapenda kufuata mufano wa Yehova.

5 Fikiria sababu ingine yenye inatuchochea tuonyeshe wengine shukrani. Shukrani iko kama chakula cha muzuri, tunakifurahia zaidi wakati tunakichangia na watu wengine. Tunafurahi wakati tunajua kama wengine ni wenye shukrani juu ya mambo yenye tunafanya. Wakati tunaonyesha shukrani, tunafanya wengine wafurahi. Mutu mwenye tunaonyesha shukrani anajua kama bidii yake ya kutusaidia, ao kutupatia kitu fulani chenye tulikuwa nacho lazima, ilikuwa ya maana. Hilo linafanya urafiki wetu pamoja na mutu huyo ukuwe wenye nguvu.

6. Maneno ya kuonyesha shukrani na matunda ya mutofaa yenye kufanyizwa na zahabu, inafanana katika njia gani fulani?

6 Kuonyesha shukrani ni jambo la maana sana. Biblia inasema hivi: “Kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye vyombo vya feza vyenye kupambwa ni vile pia neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa.” (Mez. 25:11) Wazia namna tunda la mutofaa lenye kufanyizwa na zahabu lenye kuwekwa kwenye chombo cha feza linaweza kupendeza sana! Na ufikirie namna linaweza kuwa la maana sana! Unaweza kujisikia namna gani kama mutu fulani anakupatia zawadi kama hiyo? Kwa kweli, maneno ya kuonyesha shukrani yenye unaambia wengine inaweza kuwa ya maana kama ile zawadi. Na fikiria kweli hii: Tunda la mutofaa lenye kufanyizwa na zahabu linaweza kufanya wakati murefu sana. Vilevile, mutu mwenye unaonyesha shukrani anaweza kupendezwa na shukrani hiyo na kuikumbuka maisha yake yote.

WALIONYESHA SHUKRANI

7. Kama vile Zaburi 27:4 inaonyesha, namna gani Daudi na waandikaji wengine wa zaburi walionyesha shukrani yao?

7 Watumishi wengi wa zamani wa Mungu walionyesha shukrani. Mumoja kati yao alikuwa Daudi. (Soma Zaburi 27:4.) Aliona ibada safi kuwa ya maana na alionyesha jambo hilo kupitia matendo yake. Alitoa muchango wa mali mingi kwa ajili ya ujenzi wa hekalu. Wazao wa Asafu walionyesha shukrani kwa kuandika zaburi mbalimbali, ao nyimbo za sifa. Katika wimbo moja, walimushukuru Mungu na kusema namna walipendezwa sana na “kazi [za Yehova] za ajabu.” (Zb. 75:1) Kwa kweli, Daudi na wazao wa Asafu walipenda kumuonyesha Yehova namna walikuwa wenye shukrani sana kwa ajili ya baraka zote zenye alikuwa amewapatia. Unaweza kufikiria ni katika njia gani unaweza kuiga waandikaji hao wa zaburi?

Barua ya Paulo kwa Waroma inatufundisha nini juu ya kuona wengine kuwa wa maana? (Picha hii inapatana na fungu la 8-9) *

8-9. Namna gani Paulo alionyesha kama aliona ndugu na dada zake kuwa wa maana, na hilo lilipaswa kuwa na matokeo gani?

8 Mutume Paulo aliona ndugu na dada zake kuwa wa maana na alionyesha jambo hilo kupitia maneno yenye alisema juu yao. Sikuzote, alimushukuru Mungu juu yao katika sala zake za kipekee. Pia alionyesha namna aliwaona kuwa wa maana kupitia barua zenye aliwaandikia. Kwa mufano, katika mistari 15 ya kwanza ya sura ya 16 ya barua kwa Waroma, Paulo anataja majina 27 ya Wakristo wenzake. Paulo alikumbuka zaidi sana kama Prisila na Akila ‘walitia shingo zao wenyewe katika hatari’ kwa ajili yake, na alionyesha kama Foibe alikuwa “muteteaji wa wengi,” kutia ndani Paulo. Alipongeza ndugu na dada hao wapendwa wenye walikuwa wafanyakazi wenye bidii.​—Ro. 16:1-15.

9 Paulo alijua kama ndugu na dada zake hawakukuwa wakamilifu, lakini wakati alimalizia barua yake kwa Waroma, aliamua kukazia sifa zao za muzuri. Fikiria namna ndugu na dada hao walipaswa kutiwa moyo sana wakati walisikia ile maneno ya Paulo inasomwa kwa sauti kubwa mu kutaniko! Kwa hiyo, urafiki wao pamoja na mutume Paulo ulipaswa kutiwa nguvu. Je, unazoea kuonyesha shukrani juu ya mambo ya muzuri yenye ndugu na dada wa kutaniko lenu wanasema na kufanya?

10. Namna Yesu alionyesha wanafunzi wake shukrani, inaweza kutufundisha nini?

10 Katika ujumbe wake kwa makutaniko fulani ya Asia Ndogo, Yesu alionyesha shukrani kwa ajili ya kazi yenye wanafunzi wake walifanya. Kwa mufano, kwa kutaniko lenye lilikuwa katika Tiatira, alianza ujumbe wake kwa kusema hivi: “Ninajua matendo yako, na upendo wako na imani na utumishi na uvumilivu wako, na kwamba matendo yako ya karibuni yanapita mambo yenye ulifanya pale mwanzo.” (Ufu. 2:19) Yesu hakuzungumuzia tu namna matendo yao ya muzuri ilikuwa imeongezeka, lakini pia aliwapongeza juu ya sifa zenye ziliwachochea kuonyesha ile matendo ya muzuri. Hata kama Yesu alipaswa kutolea watu fulani mashauri katika Tiatira, alianza na kumalizia ujumbe wake kwa maneno yenye kutia moyo. (Ufu. 2:25-28) Kwa sababu Yesu ni kichwa cha makutaniko yote, fikiria mamlaka yenye iko nayo. Halazimike kutushukuru juu ya kazi yenye tunamufanyia. Lakini, iko tayari kuonyesha shukrani. Huo ni mufano muzuri sana wenye aliachia wazee wa kutaniko!

HAWAKUONYESHA SHUKRANI

11. Kulingana na Waebrania 12:16, namna gani Esau aliona mambo matakatifu?

11 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu fulani wenye kuzungumuziwa mu Biblia hawakuonyesha shukrani. Kwa mufano, hata kama wazazi wenye kumupenda na kumuheshimia Yehova njo walikomalisha Esau, hakuheshimia, ao hakuonyesha shukrani juu ya mambo matakatifu. (Soma Waebrania 12:16.) Namna gani roho yake ya kukosa shukrani ilionekana wazi? Bila kufikiri, Esau alimuuzishia Yakobo, mudogo yake, haki yake ya kuzaliwa, kwa ajili tu ya bakuli la muchuzi. (Mwa. 25:30-34) Kisha wakati fulani, Esau alihuzunika sana juu ya uamuzi wenye alikuwa amekamata. Lakini kwa sababu hakukuwa ameonyesha shukrani juu ya jambo lenye alikuwa nalo, hakukuwa na sababu ya kunungunika wakati hakupewa baraka ya muzaliwa wa kwanza.

12-13. Namna gani Waisraeli walikosa kuonyesha shukrani, na hilo lilikuwa na matokeo gani?

12 Waisraeli walikuwa na sababu za mingi za kuonyesha shukrani. Walikombolewa kutoka mu utumwa kisha Yehova kuletea Wamisri Mapigo Kumi. Kisha Mungu aliwaokoa ili wasipatwe na musiba kwa kuharibu jeshi lote la Misri mu Bahari Nyekundu. Waisraeli walikuwa wenye shukrani sana, kwa hiyo, waliimba wimbo wa ushindi ili kumusifu Yehova. Lakini, je, waliendelea kuwa wenye shukrani?

13 Wakati Waisraeli walipatwa na matatizo ya mupya, walisahau bila kukawia mambo yote ya muzuri yenye Yehova alikuwa amewafanyia. Kwa hiyo, wakaonyesha namna walikuwa wenye kukosa shukrani. (Zb. 106:7) Namna gani? “Mukusanyiko wote wa Waisraeli ukaanza kumunungunikia Musa na Haruni;” kwa kweli, Yehova njo walikuwa wananungunikia. (Kut. 16:2, 8) Tabia ya watu wake ya kukosa shukrani ilimuhuzunisha. Kisha alitabiri kwamba kizazi hicho chote cha Waisraeli kingekufa katika jangwa, isipokuwa tu Yoshua na Kalebu. (Hes. 14:22-24; 26:65) Tuone basi namna tunaweza kuepuka kuiga mifano hiyo ya mubaya na namna tunaweza kuiga mifano ya muzuri.

ONYESHA SHUKRANI LEO

14-15. (a) Namna gani bibi ao bwana anaweza kuonyesha kama anaona mwenzake kuwa wa maana? (b) Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao kuonyesha shukrani?

14 Katika familia. Familia yote inapata faida wakati kila mutu katika familia anaonyesha shukrani. Wakati bibi na bwana wanaendelea kuonyeshana shukrani, hilo linafanya uhusiano wao ukuwe wenye nguvu zaidi. Na inakuwa mwepesi kwa kila mumoja wao kusamehe makosa ya mwingine. Bwana mwenye anaona bibi yake kuwa wa maana haone tu mambo ya muzuri yenye bibi yake anasema na kufanya, lakini pia “anasimama na kumusifu.” (Mez. 31:10, 28) Na bibi mwenye hekima anaelezea waziwazi bwana yake mambo mbalimbali yenye kufanya amuonyeshe shukrani.

15 Wazazi, namna gani munaweza kufundisha watoto wenu kuonyesha shukrani? Mukumbuke kama watoto wenu wataiga mambo yenye munasema na kufanya. Kwa hiyo, muonyeshe mufano muzuri kwa kusema aksanti wakati watoto wenu wanawafanyia mambo fulani. Pia, mufundishe watoto wenu kusema aksanti wakati watu wanawafanyia mambo fulani. Musaidie watoto wenu waelewe kama kuonyesha shukrani kunatoka katika moyo na kama maneno yao inaweza kuwa na matokeo ya muzuri sana. Kwa mufano, dada mumoja kijana mwenye kuitwa Clary anasema hivi: “Wakati mama yangu alikuwa na miaka 32, baba yangu alipelekwa kwa kushitukia katika gereza na kumuacha na watoto tatu wenye alipaswa kukomalisha yeye mwenyewe. Wakati nilieneza miaka 32, nilifikiria namna ilipaswa kuwa vigumu kwa mama yangu wakati alikuwa na ile miaka. Kwa hiyo, nilimuambia kama niko mwenye shukrani sana kwa mambo yote yenye alijiima ili kutukomalisha mimi na ndugu zangu. Hivi majuzi, Mama aliniambia kama angali anaona maneno yangu kuwa ya maana sana, na kama mara mingi anafikiri sana juu ya ile maneno, na inamuletea furaha sikuzote.”

Fundisha watoto wako kuonyesha shukrani (Picha hizi zinapatana na fungu la 15) *

16. Namna gani kuonyesha wengine shukrani kunaweza kuwatia moyo? Leta mufano.

16 Katika kutaniko. Wakati tunaonyesha ndugu na dada zetu shukrani, tunawatia moyo. Kwa mufano, Jorge, muzee wa kutaniko mwenye kuwa na miaka 28, aligonjwa sana. Hakuweza kuhuzuria mikutano kwa mwezi moja. Hata wakati alianza kuhuzuria tena mikutano, hakukuwa na uwezo wa kufanya migao wakati wa mikutano. Jorge anasema hivi: “Nilijiona kuwa mutu wa bure kwa sababu sikuweza tena kufanya mambo fulani na sikuweza tena kushugulikia madaraka yangu katika kutaniko. Lakini kisha mukutano moja, ndugu mumoja aliniambia hivi: ‘Ninapenda kukushukuru kwa sababu ya mufano wako muzuri wenye umeonyesha familia yangu. Tumefurahia kabisa hotuba zenye umetoa kwa miaka kidogo yenye imepita. Zimetusaidia kukomaa kiroho.’ Ile maneno ilinigusa moyo sana mupaka nikaanza kulia. Maneno yenye alisema njo yenye nilikuwa na lazima kabisa ya kusikia.”

17. Kulingana na Wakolosai 3:15, namna gani tunaweza kumuonyesha Yehova shukrani juu ya ukarimu wake?

17 Kwa Mungu wetu mukarimu. Yehova ametupatia chakula mingi cha kiroho. Kwa mufano, tunapata mafundisho yenye kutusaidia kupitia mikutano yetu, magazeti yetu, na adresi zetu za Enternete. Pengine umekwisha kusikia hotuba fulani, kusoma habari fulani, ao kuangalia programu fulani ya JW Télédiffusion na kufikiri hivi: ‘Hii njo habari yenye nilikuwa nayo lazima kabisa.’ Tunaweza kufanya nini ili kumuonyesha Yehova shukrani yetu? (Soma Wakolosai 3:15.) Njia moja ni kumushukuru kwa ukawaida katika sala zetu juu ya zawadi hizo za muzuri.​—Yak. 1:17.

Kusaidia katika kazi ya kusafisha Jumba la Ufalme ni njia ya muzuri sana ya kuonyesha shukrani yetu (Picha hii inapatana na fungu la 18)

18. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya Jumba letu la Ufalme?

18 Pia, tunamuonyesha Yehova shukrani yetu kwa kufanya nafasi yetu ya kufanyia ibada iendelee kuwa safi na yenye kupangwa muzuri. Kwa kawaida, tunasaidia kusafisha na kutunza Jumba letu la Ufalme, na wale wenye kushugulikia vyombo vya kuongeza sauti na vyombo vya kusaidia kuonyesha video wako waangalifu ili wasiviharibishe. Kama tunajikaza kutunza muzuri Majumba yetu ya Ufalme, haitaharibika mbio na haitakuwa na lazima ya marekebisho mingi makubwa. Hilo linasaidia tukuwe na feza zaidi za kujenga na kutengeneza upya Majumba ingine ya Ufalme mu dunia yote.

19. Mufano wa mwangalizi mumoja na bibi yake unakufundisha nini?

19 Kwa wale wenye kutumika sana kwa ajili yetu. Wakati tunaonyesha shukrani, maneno yetu inaweza kufanya mutu abadilishe mawazo yake juu ya magumu fulani yenye anapambana nayo. Fikiria mufano wa mwangalizi mumoja wa muzunguko na bibi yake. Kisha kupitisha siku muzima mu mahubiri wakati wa baridi kali, walirudia kwenye makao yao wakiwa wenye kuchoka sana. Kulikuwa baridi sana mupaka bibi akalala na koti yake ya baridi. Asubui, aliambia bwana yake kuwa anaona kama hataweza tena kuendelea na kazi ya kusafiri. Kisha katika asubui ileile, walipata barua kutoka kwenye biro ya tawi, na barua hiyo ilikuwa ya bibi yake. Barua hiyo ilimupongeza sana kwa sababu ya utumishi wake na uvumilivu wake. Barua hiyo ilionyesha kama haiko mwepesi kabisa kubadilisha makao kila juma. Bwana yake anasema hivi: “Ile maneno ya pongezi iligusa sana moyo wake; kwa hiyo, hakuzungumuza tena hata siku moja juu ya kuacha kazi ya kusafiri. Kwa kweli, mara mingi alinitia moyo niendelee wakati nilifikiria kuacha kazi ya kusafiri.” Bibi na bwana hao waliendelea kufanya kazi ya kusafiri kwa miaka karibu 40.

20. Tunapaswa kujikaza kufanya nini kila siku, na juu ya nini?

20 Tujikaze basi kila siku kuonyesha shukrani kupitia maneno na matendo yetu. Maneno yetu yenye kutoka mu moyo na matendo yetu, inaweza kuwa njo jambo lenye mutu mwingine iko nalo lazima ili kupambana na magumu na mahangaiko yake ya kila siku katika ulimwengu huu, kwenye watu wengi hawaonyeshe shukrani. Na wakati tunaonyesha shukrani, hilo litatusaidia kufanya urafiki wenye nguvu wenye unaweza kuendelea milele. Na jambo la maana zaidi, tutamuiga Yehova, Baba yetu mukarimu na mwenye kuonyesha shukrani.

WIMBO 20 Ulimtoa Mwana Wako Mpendwa

^ fu. 5 Mufano wa Yehova, wa Yesu, na wa Musamaria mwenye alikuwa na ukoma, unaweza kutufundisha nini juu ya kuonyesha shukrani? Habari hii itazungumuzia ile mifano na mifano ingine. Tutazungumuzia juu ya nini ni jambo la maana sana kuonyesha shukrani na tutaona ni katika njia gani fulani tunaweza kuonyesha sifa hiyo.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Kuonyesha shukrani kwa mutu fulani ao kwa ajili ya kitu fulani, maana yake kuelewa kama ule mutu ni wa maana ao kitu hicho ni cha maana. Neno hilo linaweza kuwa na maana ya kujisikia kuwa mwenye shukrani kwa moyo wote.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Barua ya Paulo inasomwa mu kutaniko la Roma; Akila, Prisila, Foibe, na wengine wanafurahi kusikia majina yao inatajwa.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Mama mumoja anasaidia mutoto wake mwanamuke kuonyesha shukrani juu ya mufano muzuri wenye dada mwenye kuzeeka ameonyesha.