Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 9

Upendo na Haki Katika Israeli ya Zamani

Upendo na Haki Katika Israeli ya Zamani

“Anapenda uadilifu na haki. Dunia imejaa upendo mushikamanifu wa Yehova.”​—ZB. 33:5.

WIMBO 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika, Wetu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Sisi wote tunataka nini? (b) Tunaweza kuwa hakika juu ya jambo gani?

SISI wote tunataka wengine watupende. Na sisi wote tunataka kutendewa kwa haki. Ikiwa tunatendewa kwa ukawaida bila upendo na haki, tunaweza kujiona kuwa watu wa bure na tunaweza kukosa tumaini.

2 Yehova anajua kama tunapenda kabisa kuonyeshwa upendo na kutendewa kwa haki. (Zb. 33:5) Tunaweza kuwa hakika kama Mungu wetu anatupenda sana na anapenda tutendewe kwa haki. Tunaona waziwazi jambo hilo wakati tunachunguza kwa uangalifu Sheria yenye Yehova alipatia taifa la Israeli kupitia Musa. Kama uko na huzuni sana kwa sababu wengine wamekutendea bila upendo ao bila haki, tafazali, chunguza namna Sheria ya Musa * inaonyesha namna Yehova anahangaikia watu wake.

3. (a) Kama vile Waroma 13:8-10 inafasiria, tunaona nini wakati tunajifunza Sheria ya Musa? (b) Tutajibu maulizo gani mu habari hii?

3 Wakati tunajifunza Sheria ya Musa, tunaona namna Yehova Mungu wetu ni mwenye upendo sana. (Soma Waroma 13:8-10.) Katika habari hii, tutachunguza sheria fulani tu kati ya Sheria zenye Waisraeli walipewa na tutajibu maulizo hii: Juu ya nini tunaweza kusema kama Sheria ilitegemea upendo? Juu ya nini tunaweza kusema kama Sheria ilitia watu moyo watende kwa haki? Wale wenye walikuwa na madaraka waliombwa watumie Sheria namna gani? Na Sheria ililinda zaidi sana nani? Majibu ya ile maulizo inaweza kutufariji, kutupatia tumaini, na kutusaidia tumukaribie zaidi Baba yetu mwenye upendo.​—Mdo. 17:27; Ro. 15:4.

SHERIA YENYE ILITEGEMEA UPENDO

4. (a) Juu ya nini tunaweza kusema kama Sheria ya Musa ilitegemea upendo? (b) Kama vile Matayo 22:36-40 inaonyesha, Yesu alikazia amri gani?

4 Tunaweza kusema kama Sheria ya Musa ilitegemea upendo kwa sababu mambo yote yenye Yehova anafanya inachochewa na upendo. (1 Yo. 4:8) Yehova alifanya sheria zote zenye zilifanyiza Sheria ya Musa zitegemee amri hizi mbili za musingi: kumupenda Mungu, na kumupenda jirani. (Law. 19:18; Kum. 6:5; soma Matayo 22:36-40.) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama kila amri kati ya amri zaidi ya 600 zenye kufanyiza Sheria, inaonyesha upendo wa Yehova. Tuone basi mifano fulani.

5-6. Yehova anapenda bibi na bwana wafanye nini, na anajua nini? Leta mufano.

5 Ukuwe mushikamanifu kwa bibi ao bwana yako, na uhangaikie watoto wako. Yehova anapenda bibi na bwana wapendane sana ili upendo wao uendelee maisha yao yote. (Mwa. 2:24; Mt. 19:3-6) Uzinifu ni kati ya makosa makubwa yenye kuonyesha kama mutu hana upendo kabisa. Njo maana, amri ya saba kati ya zile Amri Kumi ilikataza uzinifu. (Kum. 5:18) Ni ‘kumutendea Mungu’ zambi na ni kutendea bila huruma kabisa bibi ao bwana yako. (Mwa. 39:7-9) Bibi ao bwana ya mutu mwenye alifanya uzinifu anaweza kusikia maumivu kwa miaka mingi sana juu ya ukosefu huo wa uaminifu.

6 Yehova anajua muzuri namna bibi na bwana wanatendeana. Alipenda bibi watendewe muzuri katika Israeli. Bwana mwenye aliheshimia Sheria alipaswa kupenda bibi yake na hangepaswa kuvunja ndoa yao kwa sababu ya mambo ya kidogo-kidogo. (Kum. 24:1-4; Mt. 19:3, 8) Lakini kama tatizo kubwa lilitokea na alipaswa kuvunja ndoa na bibi yake, alipaswa kumupatia cheti cha kuvunja ndoa. Cheti cha kuvunja ndoa kilimulinda mwanamuke ili asishitakiwe kwa uongo kuwa alifanya uasherati. Zaidi ya hilo, mbele bwana amupatie bibi yake cheti cha kuvunja ndoa, inaonekana kuwa alipaswa kwanza kuonana na wazee wa muji. Kwa kufanya vile, wazee walikuwa na nafasi ya kujaribu kusaidia bibi na bwana ili wasivunje ndoa yao. Wakati Muisraeli alivunja ndoa na bibi yake kwa sababu ya faida zake mwenyewe, Yehova hakusaidia kila mara, kwa mufano kupitia wazee ao manabii. Lakini, aliona machozi ya bibi huyo, na alielewa maumivu yake.​—Mal. 2:13-16.

Yehova alipenda watoto wajisikie salama kabisa wakati walikuwa wanakomalishwa kwa upendo na kufundishwa na wazazi wao (Picha hii inapatana na fungu la 7-8) *

7-8. (a) Yehova aliamuru wazazi wafanye nini? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.) (b) Tunajifunza mambo gani?

7 Pia, Sheria inaonyesha kama Yehova anahangaikia sana hali ya muzuri ya watoto. Yehova aliamuru wazazi watimizie watoto wao mahitaji ya kimwili na ya kiroho. Wazazi walipaswa kutumia kila nafasi ili kusaidia watoto wao wapendezwe na Sheria ya Yehova na wajifunze kumupenda. (Kum. 6:6-9; 7:13) Sababu moja kati ya sababu zenye zilifanya Yehova apatie Waisraeli azabu ao malipizi ni kwamba, walitendea watoto wao fulani kwa njia ya mubaya sana. (Yer. 7:31, 33) Wazazi hawakupaswa kuona watoto wao kuwa kitu fulani chenye wangezarau na kutendea mubaya, lakini walipaswa kuwaona kuwa uriti, zawadi kutoka kwa Yehova yenye walipaswa kufurahia.​—Zb. 127:3.

8 Mambo yenye tunajifunza: Yehova anaona muzuri sana namna bibi na bwana wanatendeana. Anapenda wazazi wapende watoto wao, na ataomba wazazi watoe hesabu juu ya namna wanatendea watoto wao.

9-11. Juu ya nini Yehova alitoa amri yenye kukataza kutamani?

9 Usitamani. Amri ya mwisho kati ya Amri Kumi ilikataza kutamani, ao kukomalisha tamaa ya mubaya juu ya kitu cha mutu mwingine. (Kum. 5:21; Ro. 7:7) Yehova alitoa sheria hiyo ili kufundisha jambo hili la maana: watu wake wanapaswa kulinda moyo wao, ni kusema, mawazo yao na hisia zao. Anajua kama mawazo ya mubaya na hisia za mubaya njo vinaongoza mutu afanye matendo ya mubaya. (Mez. 4:23) Ikiwa Muisraeli aliacha tamaa za mubaya zikomae mu moyo wake, iliwezekana kabisa atendee wengine bila upendo. Kwa mufano, Mufalme Daudi, aliangukia mu mutego huo. Kwa kawaida, alikuwa mutu muzuri. Lakini wakati fulani, alitamani bibi ya mwanaume mwingine. Tamaa yake ilimuongoza afanye zambi. (Yak. 1:14, 15) Daudi alifanya uzinifu, alijaribu kudanganya bwana ya bibi huyo, na kisha akafanya auawe.​—2 Sa. 11:2-4; 12:7-11.

10 Yehova alijua wakati Muisraeli alivunja sheria yenye ilikataza kutamani; anaweza kusoma mioyo. (1 Ny. 28:9) Sheria yenye ilikataza kutamani ilionyesha watu wake kama walipaswa kuepuka mawazo yenye inaongoza watu wafanye mambo ya mubaya. Yehova ni Baba mwenye upendo na mwenye hekima sana!

11 Mambo yenye tunajifunza: Yehova haone tu namna mutu anaonekana kwa inje. Anaona namna tuko kabisa ndani ya moyo wetu. (1 Sa. 16:7) Hatuwezi kumuficha wazo fulani, jambo fulani lenye kuwa mu moyo wetu, ao tendo fulani. Yehova anatafuta sifa za muzuri zenye kuwa ndani ya moyo wetu, na anapenda tukomalishe sifa hizo za muzuri. Lakini anapenda tutambue na kuzuia mawazo ya mubaya mbele ituongoze kufanya mambo ya mubaya.​—2 Ny. 16:9; Mt. 5:27-30.

SHERIA YENYE ILIKAZIA HAKI

12. Sheria ya Musa inakazia jambo gani?

12 Pia Sheria ya Musa inakazia kama Yehova anapenda haki. (Zb. 37:28; Isa. 61:8) Alionyesha mufano mukamilifu juu ya namna ya kutendea wengine kwa haki. Yehova alibariki Waisraeli wakati walitii sheria zenye aliwapatia. Lakini, waliteseka wakati walikataa kutii kanuni zake za uadilifu na haki. Fikiria tena amri zingine mbili kati ya zile Amri Kumi.

13-14. Amri mbili za kwanza kati ya zile Amri Kumi ziliomba Waisraeli wafanye nini, na namna gani kutii zile amri kungewaletea faida?

13 Umuabudu Yehova tu. Amri mbili za kwanza kati ya zile Amri Kumi ziliomba Waisraeli wamuabudu Yehova tu na ziliwaonya juu ya kuabudu sanamu. (Kut. 20:3-6) Haiko Yehova njo alipata faida kupitia amri hizo. Lakini, watu wake njo walipata faida kupitia amri hizo. Wakati watu wake waliendelea kuwa washikamanifu kwake, walikuwa na hali ya muzuri. Lakini waliteseka wakati waliabudu miungu ya mataifa ingine.

14 Fikiria Wakanaani. Waliabudu sanamu zenye hazina uzima kuliko kumuabudu Mungu wa kweli na mwenye kuishi. Matokeo ni kwamba, walifanya mambo yenye kuchukiza sana. (Zb. 115:4-8) Katika ibada yao, walikuwa wanafanya matendo machafu ya ngono na matendo yenye kuogopesha ya kutoa watoto kuwa zabibu. Vilevile, wakati Waisraeli walimuacha Yehova na kuamua kuabudu sanamu, walifanya mambo yenye kuchukiza sana na kuumiza familia zao. (2 Ny. 28:1-4) Wale wenye walikuwa na mamlaka waliacha kanuni za Yehova za haki. Walitumia mubaya mamlaka yao na walionea watu wazaifu na wale wenye hawakukuwa na uwezo wa kujilinda. (Eze. 34:1-4) Yehova alionya Waisraeli kama angeleta hukumu juu ya wale wenye walitendea mubaya watu wenye hawakukuwa na uwezo wa kujilinda, kama vile wanamuke na watoto. (Kum. 10:17, 18; 27:19) Lakini, Yehova alibariki watu wake wakati walikuwa washikamanifu kwake na wakati walikuwa wanatendeana kwa haki.​—1 Fa. 10:4-9.

Yehova anatupenda na anajua wakati tunatendewa bila haki (Picha hii inapatana na fungu la 15)

15. Tunajifunza mambo gani juu ya Yehova?

15 Mambo yenye tunajifunza: Haiko kosa la Yehova wakati wale wenye wanasema kuwa wanamutumikia wanakosa kufuata kanuni zake na kutendea mubaya watu wake. Hata hivyo, Yehova anatupenda na anajua wakati tunatendewa bila haki. Anaelewa kabisa maumivu yetu kuliko namna mama anaelewa mateso ya mutoto wake mudogo. (Isa. 49:15) Hata kama pengine hatende mara moja ili kumaliza hali hiyo, kwa wakati wenye kufaa atahukumu watenda-zambi wenye hawatubu juu ya namna wametendea wengine.

NAMNA GANI SHERIA ILIPASWA KUTUMIWA?

16-18. Sheria ya Musa ilitumiwa katika sehemu gani mbalimbali za maisha, na tunajifunza mambo gani?

16 Sheria ya Musa ilizungumuzia sehemu mingi za maisha ya Muisraeli, kwa hiyo, ilikuwa jambo la maana wazee wenye waliwekwa wahukumu watu wa Yehova kwa hukumu ya haki. Hawakukuwa tu na daraka la kushugulikia mambo yenye kuhusu ibada kwa Yehova, lakini walipaswa pia kushugulikia hali za kukosa kuelewana kati ya watu na makosa makubwa yenye watu walifanya. Ona mifano yenye kufuata.

17 Ikiwa Muisraeli aliua mutu fulani, hakupaswa kuuawa palepale. Wazee wa muji wake walipaswa kuchunguza kwanza hali mbele ya kuamua ikiwa mutu huyo alipaswa kupewa hukumu ya kifo. (Kum. 19:2-7, 11-13) Wazee walipaswa pia kushugulikia mambo mbalimbali ya maisha ya kila siku, kama vile mabishano kati ya watu juu ya vitu na hali za kukosa kuelewana katika ndoa. (Kut. 21:35; Kum. 22:13-19) Wakati wazee walitenda kwa haki na wakati Waisraeli walitii Sheria, kila mutu alipata faida, na taifa lote lilimuletea Yehova utukufu.​—Law. 20:7, 8; Isa. 48:17, 18.

18 Mambo yenye tunajifunza: Yehova anaona kila sehemu ya maisha yetu kuwa ya maana. Anapenda tutendee wengine kwa haki na kwa upendo. Na anajua mambo yenye tunasema na kufanya, hata kama tuko pekee yetu mu nyumba.​—Ebr. 4:13.

19-21. (a) Namna gani wazee na waamuzi walipaswa kutendea watu wa Mungu? (b) Namna gani Sheria ya Musa ililinda watu kwa njia ya pekee, na tunajifunza mambo gani?

19 Yehova hakupenda watu wake waambukizwe tabia za mubaya za mataifa yenye iliwazunguka. Kwa hiyo, aliomba wazee na waamuzi watumie Sheria bila ubaguzi. Lakini, wale wenye walihukumu watu wake hawakupaswa kuwatendea kwa njia ya mubaya ao kwa ukali. Walipaswa kupenda haki.​—Kum. 1:13-17; 16:18-20.

20 Yehova anasikilia watu wake huruma, kwa hiyo anatoa sheria ili watu wasitendewe bila haki. Kwa mufano, Sheria ilifanya isikuwe mwepesi mutu ashitakiwe mambo ya uongo. Mutu mwenye alishitakiwa alikuwa na haki ya kujua mwenye alimushitaki. (Kum. 19:16-19; 25:1) Na mbele ahukumiwe kuwa mwenye kosa, mashahidi wawili hivi walipaswa kuhakikisha jambo hilo. (Kum. 17:6; 19:15) Tuseme nini juu ya Muisraeli mwenye alifanya kosa kubwa lenye shahidi mumoja tu aliona? Hakupaswa kufikiri kama hatapewa malipizi juu ya kosa lake. Yehova aliona jambo lenye alifanya. Mu familia, baba walipewa mamlaka, lakini mamlaka yao ilikuwa na mipaka. Katika matatizo fulani ya familia, wazee walikuwa na daraka la kuingilia kati na kukamata uamuzi wa mwisho.​—Kum. 21:18-21.

21 Mambo yenye tunajifunza: Yehova anatuonyesha mufano mukamilifu; hatende hata kidogo kwa ukosefu wa haki. (Zb. 9:7) Anabariki wale wenye wanatii kanuni zake za haki, lakini anapatia azabu wale wenye kutumia mubaya mamlaka yao. (2 Sa. 22:21-23; Eze. 9:9, 10) Watu fulani wanaweza kufanya mambo ya mubaya na kuonekana kuwa hawapewe azabu, lakini Yehova anawahukumu kwa wakati wake wenye kufaa. (Mez. 28:13) Na kama hawatubu, hivi karibuni watajifunza kama “ni jambo lenye kuogopesha kuanguka katika mikono ya Mungu mwenye kuishi.”​—Ebr. 10:30, 31.

SHERIA ILILINDA ZAIDI SANA NANI?

Wakati wazee walikuwa wanashugulikia hali za kukosa kuelewana, walipaswa kuiga sifa ya Yehova ya kupenda watu na ya kupenda haki (Picha hii inapatana na fungu la 22) *

22-24. (a) Sheria ililinda zaidi sana nani, na tunajifunza nini juu ya Yehova? (b) Ni onyo gani lenye kupatikana mu andiko la Kutoka 22:22-24?

22 Sheria ililinda zaidi sana wale wenye hawakukuwa na uwezo wa kujilinda, kama vile mayatima, wajane, na wakaaji wageni. Waamuzi katika Israeli waliambiwa hivi: “Haupaswe kupotosha hukumu ya mukaaji mugeni ao ya mutoto mwenye hana baba, na haupaswe kukamata nguo ya mujane kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo.” (Kum. 24:17) Mu taifa la Israeli, Yehova alihangaikia kwa upendo wale wenye hawakukuwa kabisa na uwezo wa kujilinda. Na alipatia azabu wale wenye walikuwa wanawatendea mubaya.​—Soma Kutoka 22:22-24.

23 Pia Sheria ililinda watu wa familia kwa kukataza ngono kati ya watu wote wa jamaa. (Law. 18:6-30) Tofauti na watu wa mataifa yenye ilizunguka taifa la Israeli, wenye waliachilia ao hata kukubali tabia hiyo, watu wa Yehova walipaswa kuona kosa hilo kubwa kama vile Yehova analiona, ni kusema, tendo lenye kuchukiza.

24 Mambo yenye tunajifunza: Yehova anapenda wale wenye kuwa na madaraka watendee kwa upendo wale wenye kuwa chini ya uongozi wao. Anachukia matendo ya ngono yenye haifae na anapenda kuhakikisha kama watu wote wanapata ulinzi na kutendewa kwa haki, zaidi sana wale wenye hawana uwezo wa kujilinda.

SHERIA, “KIVULI CHA MAMBO YA MUZURI YENYE YATAKUJA”

25-26. (a) Juu ya nini tunaweza kusema kama upendo na haki viko kama pumuzi na uzima? (b) Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata kati ya habari ine zenye kuzungumuzia juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anatuhangaikia?

25 Upendo na haki viko kama pumuzi na uzima, ku dunia, kimoja hakiwezi kuwa bila kingine. Wakati tuko hakika kama Yehova anatutendea kwa haki, tunamupenda zaidi. Na wakati tunapenda Mungu na kanuni zake za haki, hilo linatuchochea kupenda wengine na kuwatendea kwa haki.

26 Agano la Sheria ya Musa lilisaidia Waisraeli wakuwe na urafiki wa sana pamoja na Yehova. Lakini, Sheria ilifikia mwisho wake kisha Yesu kutimiza Sheria hiyo, na jambo la muzuri zaidi lilichukua nafasi ya Sheria hiyo. (Ro. 10:4) Mutume Paulo alionyesha kama Sheria ni “kivuli cha mambo ya muzuri yenye yatakuja.” (Ebr. 10:1) Habari yenye kufuata kati ya habari ine, zenye kuzungumuzia juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anatuhangaikia, itazungumuzia mambo fulani kati ya ile mambo ya muzuri. Itazungumuzia pia namna upendo na haki ni mambo ya maana sana mu kutaniko la Kikristo.

WIMBO 109 Pendaneni Sana Kutoka Moyoni

^ fu. 5 Hii ni habari ya kwanza kati ya habari ine zenye zitazungumuzia juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anatuhangaikia. Habari tatu zenye kubakia zitazungumuziwa mu gazeti Munara wa Mulinzi la Mwezi wa 5, 2019. Habari hizo zitazungumuzia namna Yehova anaonyesha upendo na haki katika kutaniko la Kikristo, namna wazee wanalinda kutaniko na namna wazazi wanaweza kulinda watoto wao ili wasitendewe mubaya kingono, na namna tunaweza kufariji wale wenye walitendewa mubaya kingono wakati walikuwa watoto.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Sheria zaidi ya 600 zenye Yehova alipatia Waisraeli kupitia Musa zinaitwa “Sheria,” “Sheria ya Musa,” na “amri.” Tena, vitabu tano vya kwanza vya Biblia (Mwanzo mupaka Kumbukumbu la Torati) mara mingi vinaitwa Sheria. Wakati fulani, neno hilo linatumiwa ili kuzungumuzia Maandiko yote ya Kiebrania.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati mama Muisraeli iko anatayarisha chakula, anafurahia mazungumuzo yenye kupendeza pamoja na watoto wake wanamuke. Pembeni, baba anazoeza mutoto wake mwanaume kuhangaikia kondoo.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Kwenye mulango mukubwa wa muji, wazee wanasaidia kwa upendo mujane na mutoto wake wenye wametendewa mubaya na mufanya-biashara fulani wa mu eneo lao.