Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 13

Ujitie pa Nafasi ya Wengine Katika Kazi Yako ya Kuhubiri

Ujitie pa Nafasi ya Wengine Katika Kazi Yako ya Kuhubiri

“Akawasikilia huruma . . . Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.”​—MK. 6:34.

WIMBO 70 Tafuteni Wanaostahili

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni jambo gani moja lenye kufurahisha zaidi juu ya utu wa Yesu? Fasiria.

MOJA kati ya mambo yenye kufurahisha zaidi juu ya utu wa Yesu ni uwezo wake wa kuelewa magumu yenye tuko nayo kwa sababu tuko wanadamu wenye hawakamilike. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, ‘alifurahi pamoja na wale wenye kufurahi’ na ‘kulia pamoja na wale wenye kulia.’ (Ro. 12:15) Kwa mufano, wakati wanafunzi wake 70 walirudia kisha kupata matokeo ya muzuri mu kazi yao ya kuhubiri, Yesu “akakuwa na furaha kubwa kupitia roho takatifu.” (Lu. 10:17-21) Lakini, wakati Yesu aliona namna watu wenye walikuwa wanamupenda Lazaro walihuzunika juu ya kifo chake, “akasumbuka sana ndani yake na akavurugika.”​—Yoh. 11:33.

2. Ni nini ilimusaidia Yesu asikilie watu huruma?

2 Hata kama Yesu alikuwa mukamilifu, alitendea kwa rehema na huruma watu wenye hawakamilike. Ni nini ilimusaidia kufanya vile? Kwanza kabisa, Yesu alikuwa anapenda watu. Kama vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, ‘wana wa binadamu ndio alipenda zaidi sana.’ (Mez. 8:31) Kwa sababu Yesu alipenda wanadamu, hilo lilimuchochea ajue muzuri zaidi mawazo yao. Mutume Yohana alisema hivi: “Alijua mambo yenye yalikuwa ndani ya mwanadamu.” (Yoh. 2:25) Yesu alikuwa anasikilia wengine huruma. Watu waliona kama alikuwa anawapenda na wakasikiliza ujumbe wa Ufalme wa Mungu. Wakati tunaonyesha zaidi sifa ya huruma kama vile Yesu alifanya, tutapata matokeo ya muzuri zaidi mu kazi yetu ya kuhubiri.​—2 Ti. 4:5.

3-4. (a) Kama tuko na sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine, namna gani tutaona kazi yetu ya kuhubiri? (b) Tutajifunza nini mu habari hii?

3 Mutume Paulo alijua kama alilazimika kuhubiri, na sisi tunajua vile. (1 Ko. 9:16) Lakini, kama tuko na sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine, hatutaona tu kazi yetu ya kuhubiri kuwa kazi yenye tunalazimika kufanya. Tutapenda kuonyesha kama tunahangaikia watu na tuko tayari kuwasaidia. Tunajua kama “kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Wakati tunaendelea kukumbuka jambo hilo juu ya kazi yetu ya kuhubiri, tutaifurahia zaidi.

4 Mu habari hii, tutajifunza namna ya kujitia pa nafasi ya wengine mu kazi yetu ya kuhubiri. Kwanza, tutaona mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia namna Yesu alijisikia juu ya watu wengine. Kisha, tutajifunza mambo ine yenye tunaweza kufanya ili kuiga mufano wake.​—1 Pe. 2:21.

YESU ALIJITIA PA NAFASI YA WENGINE MU KAZI YA KUHUBIRI

Sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine ilimuchochea Yesu ahubirie watu ujumbe wenye kufariji (Picha hii inapatana na fungu la 5-6)

5-6. (a) Yesu alijitia pa nafasi ya watu gani? (b) Kama vile ilitabiriwa mu andiko la Isaya 61:1, 2, juu ya nini Yesu alisikilia huruma watu wenye alihubiria?

5 Fikiria mufano fulani wenye kuonyesha namna Yesu alijitia pa nafasi ya wengine. Wakati fulani, Yesu na wanafunzi wake walikuwa wenye kuchoka sana kwa sababu walikuwa wamehubiri habari njema bila kupumuzika. Hawakupata “hata wakati wa kula chakula.” Kwa hiyo, Yesu alipeleka wanafunzi wake “mahali kwenye hakuna watu ili wakuwe peke yao” na ‘wapumuzike kidogo.’ Lakini, watu wengi walikimbia na wakatangulia Yesu na wanafunzi wake mahali kwenye walikuwa wanaenda. Wakati Yesu alifika kule na kuona watu, alijisikia na kutenda namna gani? “Akawasikilia huruma, * kwa sababu walikuwa kama kondoo wenye hawana muchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.”​—Mk. 6:30-34.

6 Ona sababu yenye ilimufanya Yesu asikilie watu hao huruma, ao ajitie pa nafasi yao. Alitambua kwamba “walikuwa kama kondoo wenye hawana muchungaji.” Pengine Yesu aliona kama watu fulani kati yao walikuwa maskini na walikuwa wanatumika sana ili kutimiza mahitaji ya familia yao. Pengine wengine walikuwa na huzuni kwa sababu walikuwa wamefiwa na mupendwa wao. Kama ni vile, inawezekana kabisa kuwa Yesu alielewa hali yao. Kama vile tulizungumuzia mu habari yenye ilitangulia, pengine Yesu naye alipatwa na magumu fulani kati ya ile magumu. Yesu alihangaikia wengine, na alichochewa kuwahubiria ujumbe wenye uliwafariji.​—Soma Isaya 61:1, 2.

7. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yesu?

7 Mufano wa Yesu unatufundisha nini? Kama Yesu, tunazungukwa na watu wenye kuwa “kama kondoo wenye hawana muchungaji.” Wako na magumu mingi sana. Tuko na jambo lenye wako nalo lazima, ni kusema, ujumbe wa Ufalme. (Ufu. 14:6) Kwa hiyo, tunamuiga Bwana wetu na tunahubiri habari njema kwa sababu ‘tunamusikilia huruma mutu wa hali ya chini na maskini.’ (Zb. 72:13) Tunasikilia watu huruma, na tunapenda kufanya jambo fulani ili kuwasaidia.

NAMNA TUNAWEZA KUONYESHA SIFA YA KUJITIA PA NAFASI YA WENGINE

Fikiria mahitaji ya kila mutu (Picha hii inapatana na fungu la 8-9)

8. Ni jambo gani moja lenye tunaweza kufanya ili kujitia pa nafasi ya wengine mu kazi ya kuhubiri? Leta mufano.

8 Ni nini inaweza kutusaidia tujitie pa nafasi ya watu wenye tunahubiria? Tunapaswa kuwazia namna watu wenye tunakutana nao wanafikiri na kujisikia, na tunapaswa kuwatendea namna tungependa watutendee ikiwa tungekuwa mu hali kama yao. * (Mt. 7:12) Tuzungumuzie basi mambo ine yenye tunaweza kufanya ili kujitia pa nafasi ya watu wenye tunahubiria. Jambo la kwanza, fikiria mahitaji ya kila mutu. Wakati tunahubiri habari njema, kazi yetu iko sawa na kazi ya munganga. Munganga muzuri anafikiriaka mahitaji ya kila mugonjwa. Anaulizaka maulizo na kusikiliza kwa uangalifu wakati mugonjwa anamufasiria hali yake na namna anajisikia. Kuliko kuandikia mugonjwa dawa ya kwanza yenye anafikiria, munganga anaweza kufanya uchunguzi zaidi ili kujua tatizo ni gani, na kisha anaweza kumutolea matunzo yenye kufaa. Vilevile, hatupaswe kutumia ufundi uleule ili kuanzisha mazungumuzo na kila mutu mwenye tunakutana naye mu kazi yetu ya kuhubiri. Lakini, tunapaswa kufikiria hali ya kila mutu na mawazo yake.

9. Hatupaswe kuwaza nini? Fasiria.

9 Wakati unakutana na mutu fulani mu kazi ya kuhubiri, usiwaze kama unajua hali yake ao mambo yenye anaamini na juu ya nini anaamini ile mambo. (Mez. 18:13) Lakini, umuulize maulizo kwa ufundi ili ujue jambo fulani juu yake na mambo yenye anaamini. (Mez. 20:5) Kama haiko mubaya mu desturi yenu, umuulize maulizo juu ya kazi yake, familia yake, maisha yake, na mawazo yake. Wakati tunauliza watu maulizo, tunawachochea watuelezee juu ya nini wako na lazima ya kusikia habari njema. Wakati tunajua mahitaji yao, tunaweza kujitia pa nafasi yao, na tunaweza kuwatolea musaada wenye wako nao lazima, kama vile Yesu alikuwa anafanya.​—Linganisha na 1 Wakorinto 9:19-23.

Wazia maisha yenye pengine mutu fulani mwenye unahubiria iko nayo (Picha hii inapatana na fungu la 10-11)

10-11. Kulingana na 2 Wakorinto 4:7, 8, ni jambo gani la pili lenye tunaweza kufanya ili kujitia pa nafasi ya wengine? Leta mufano.

10 Jambo la pili, jaribu kuwazia maisha yenye pengine wako nayo. Tunaweza kuelewa hali yao kwa njia fulani. Kwa kweli, juu sisi pia hatuko wakamilifu, tuko na magumu yenye watu wote wako nayo. (1 Ko. 10:13) Tunajua kama maisha iko nguvu sana mu ulimwengu huu. Ni Yehova tu njo anatusaidia kuvumilia. (Soma 2 Wakorinto 4:7, 8.) Lakini, fikiria watu wenye wanajikaza kupambana na magumu katika ulimwengu huu bila kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova. Kama Yesu, tunawasikilia huruma, na tunachochewa kuwahubiria “habari njema za jambo la muzuri zaidi.”​—Isa. 52:7.

11 Fikiria mufano wa ndugu mwenye kuitwa Sergey. Mbele Sergey ajifunze kweli, alikuwa mutu wa kimya-kimya sana na mwenye haya sana. Ilikuwa nguvu sana kwake kuzungumuza na watu wengine. Kisha wakati fulani, alikubali kujifunza Biblia. Sergey anasema hivi: “Wakati niliendelea kujifunza Biblia, nilijua kama Wakristo wanapaswa kuambia wengine mambo yenye wanaamini. Niliamini kabisa kama singeweza kufanya vile hata siku moja.” Lakini, alifikiria watu wenye walikuwa hawajasikia jambo lolote juu ya kweli, na aliona kama maisha yao inapaswa kuwa nguvu sana kwa sababu hawamujue Yehova. Anasema hivi: “Mambo ya mupya yenye nilikuwa ninajifunza ilinisaidia nikuwe na furaha sana na nikuwe na amani ya moyo. Nilijua kama watu wengine walikuwa pia na lazima ya kujua ile mambo.” Wakati Sergey aliendelea kukomalisha sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine, aliona kama alipata uhodari zaidi ili kuhubiri. Anasema hivi: “Nilishangaa sana wakati niliona kama kuzungumuza na wengine juu ya Biblia kulinisaidia kabisa nikuwe na uhodari zaidi. Na kuzungumuza na wengine juu ya mambo yenye ninaamini kulitia nguvu imani yangu.” *

Inaweza kuomba wakati ili watu fulani wafanye maendeleo ya kiroho (Picha hii inapatana na fungu la 12-13)

12-13. Juu ya nini tunapaswa kuonyesha uvumilivu watu wenye tunafundisha mu kazi yetu ya kuhubiri? Leta mufano.

12 Jambo la tatu, uonyeshe uvumilivu wale wenye unafundisha. Kumbuka kama pengine hawajafikiria hata siku moja mafundisho fulani ya Biblia yenye sisi tunajua muzuri sana. Na watu wengi wanaamini sana mambo yenye wamefundishwa. Wanaweza kuona kama mambo yenye wamefundishwa mu dini yao inawaunganisha na watu wa familia yao, desturi yao, na watu wa eneo lao. Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia?

13 Fikiria mufano huu: Watu wanafanyaka nini wakati inaomba kujenga kilalo cha mupya ili kikamate nafasi ya kilalo cha zamani chenye kimeharibika? Mara mingi wakati kilalo cha mupya kiko kinajengwa, watu wanaendelea kutumia kilalo cha zamani. Wakati kilalo cha mupya kinakuwa tayari, wanaweza sasa kubomoa kile cha zamani. Vilevile, mbele tuombe watu waachane na mafundisho ya “zamani” yenye wanaamini na yenye wanapenda sana, tunapaswa kwanza kuwasaidia wapendezwe sana na kweli za “mupya,” ni kusema, mafundisho ya Biblia yenye hawakukuwa wanajua. Kama tu tunafanya vile, watakuwa tayari kuachana na mambo yenye walikuwa wanaamini zamani. Inaweza kuomba wakati ili kusaidia watu wafanye ile mabadiliko.​—Ro. 12:2.

14-15. Namna gani tunaweza kusaidia watu wenye hawajue mambo mingi ao hawajue jambo lolote juu ya tumaini la kuishi milele mu Paradiso hapa ku dunia? Leta mufano.

14 Kama tunaonyesha watu uvumilivu mu kazi yetu ya kuhubiri, hatutatazamia kama wataelewa ao kukubali kweli ya Biblia wakati wanaisikia kwa mara ya kwanza. Lakini, sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine itatuchochea tuwasaidie wafikiri juu ya Maandiko kwa kipindi fulani. Kwa mufano, ona namna tunaweza kufikiri na mutu fulani juu ya tumaini la kuishi milele mu Paradiso hapa ku dunia. Watu wengi hawajue mambo mingi ao hawajue jambo lolote juu ya fundisho hilo. Pengine wanaamini kama kifo njo mwisho wa mambo yote. Ao pengine wanawaza kama watu wote wazuri wanaendaka mbinguni wakati wanakufa. Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia?

15 Ndugu mumoja anaeleza ufundi wenye anatumiaka ili kusaidia watu waelewe fundisho hilo. Kwanza, anasomaka Mwanzo 1:28. Kisha, anauliza musikilizaji ni wapi Mungu alipenda watu waishi na alipenda wakuwe na maisha ya namna gani. Watu wengi wanajibu hivi: “Alipenda waishi ku dunia, na wakuwe na maisha ya muzuri.” Kisha ndugu huyo anasomaka Isaya 55:11 na kuuliza ikiwa kusudi la Mungu limebadilika. Mara mingi, musikilizaji anajibu hapana. Ku mwisho, ndugu huyo anasomaka Zaburi 37:10, 11 na kuuliza musikilizaji ikiwa wakati wenye kuja wa wanadamu utakuwa namna gani. Kwa kutumia ufundi huo wa kufikiri na watu juu ya Maandiko, amesaidia watu wengi waelewe kama Mungu angali anapenda watu wazuri waishi milele mu Paradiso hapa ku dunia.

Tendo la kidogo la wema, kama vile kutumia mutu barua yenye kutia moyo, linaweza kuleta matokeo ya muzuri (Picha hii inapatana na fungu la 16-17)

16-17. Kulingana na Mezali 3:27, tunaweza kujitia pa nafasi ya wengine mu njia gani fulani? Leta mufano.

16 Jambo la ine, tafuta njia za kuonyesha watu kama unawahangaikia. Kwa mufano, kama tumetembelea mutu kwa wakati wenye unaonekana kuwa haufae, tunaweza kuomba musamaha na kumuambia kama tutarudia wakati wenye kufaa. Tutafanya nini kama musikilizaji iko na lazima ya musaada ili kufanya kazi fulani ya kidogo? Ao tutafanya nini kama mutu fulani mwenye hawezi kutoka mu nyumba iko na lazima ya mutu wa kutuma mahali fulani? Mu hali kama hizo, tunaweza kusaidia.​—Soma Mezali 3:27.

17 Dada mumoja alipata matokeo ya muzuri kisha kufanya tendo fulani la wema lenye lingeweza kuonekana kuwa la kidogo. Sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine ilimuchochea aandike barua na kuitumia watu wa familia moja wenye walifiwa na mutoto. Barua hiyo ilikuwa na maandiko fulani ya Biblia yenye kufariji. Watu wa familia hiyo walijisikia namna gani? Mama mwenye alifiwa na mutoto aliandika hivi: “Jana nilikuwa ninajisikia mubaya sana. Barua yako ilitusaidia sana. Niko mwenye shukrani sana juu ya barua yako yenye ilitufariji sana. Jana, inawezekana nilisoma barua yako mara 20 hivi. Nilishangaa sana juu ya namna ilikuwa na maneno ya huruma, yenye kuonyesha kama unatuhangaikia, na yenye kutia moyo. Tunashukuru kwa moyo wetu wote.” Kwa kweli, tunaweza kupata matokeo ya muzuri wakati tunajitia pa nafasi ya watu wenye kuteseka na kisha tunafanya jambo fulani ili kuwasaidia.

TUELEWE MAMBO YENYE YEHOVA ANATAZAMIA TUFANYE

18. Kulingana na 1 Wakorinto 3:6, 7, juu ya nini tunapaswa kuelewa mambo yenye Yehova anatazamia tufanye?

18 Kwa kweli, ni muzuri kuelewa mambo yenye Yehova anatazamia tufanye mu kazi yetu ya kuhubiri. Tunaweza kufanya sehemu fulani ili kusaidia watu wamujue Mungu, lakini haiko sisi njo tunafanya sehemu ya maana zaidi. (Soma 1 Wakorinto 3:6, 7.) Yehova njo mwenye anavuta watu kwake. (Yoh. 6:44) Mwishowe, ikiwa mutu atakubali ao atakataa habari njema, hilo linategemea hali ya moyo wake. (Mt. 13:4-8) Kumbuka kama watu wengi hawakukubali ujumbe wa Yesu, hata kama alikuwa Mwalimu mukubwa zaidi mwenye amepata kuishi! Kwa hiyo, hatupaswe kuvunjika moyo ikiwa watu wengi kati ya watu wenye tunajikaza kusaidia hawakubali ujumbe wetu.

19. Tutapata faida gani wakati tunajitia pa nafasi ya wengine mu kazi yetu ya kuhubiri?

19 Tutapata matokeo ya muzuri wakati tunajitia pa nafasi ya wengine mu kazi yetu ya kuhubiri. Tutafurahia zaidi kazi yetu ya kuhubiri. Tutapata furaha kubwa yenye mutu anapata wakati anatoa. Na tunasaidia wale wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” wakubali habari njema kwa vyepesi. (Mdo. 13:48) Kwa hiyo, “wakati tungali na nafasi, tutendee watu wote mambo ya muzuri.” (Gal. 6:10) Tukifanya vile, tutapata furaha ya kumuletea utukufu Baba yetu wa mbinguni.​—Mt. 5:16.

WIMBO 64 Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha

^ fu. 5 Wakati tunajitia pa nafasi ya wengine, tunaweza kupata furaha zaidi mu kazi yetu ya kuhubiri, na watu wanaweza kuwa tayari zaidi kusikiliza ujumbe wetu. Juu ya nini? Mu habari hii, tutaona mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia mufano wa Yesu, na mambo ine yenye tunaweza kufanya ili kujitia pa nafasi ya watu wenye tunahubiria.

^ fu. 5 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu habari hii, neno huruma maana yake kujitia pa nafasi ya mutu fulani mwenye kuteseka ao mwenye ametendewa mubaya. Kufanya vile kunaweza kumuchochea mutu afanye kila jambo lenye anaweza ili kusaidia watu.

^ fu. 8 Ona habari “Namna ya Kuwatendea Wengine Katika Mahubiri,” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 5, 2014.