Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 10

Ni Kitu Gani Kinanizuia Nisibatizwe?

Ni Kitu Gani Kinanizuia Nisibatizwe?

“Filipo na towashi wakaingia ndani ya maji, na akamubatiza.”​—MDO. 8:38.

WIMBO 52 Wakfu wa Kikristo

KIFUPI CHA HABARI *

1. Adamu na Eva walipoteza nini, na hilo lilileta matokeo gani?

UNAWAZA ni nani mwenye anapaswa kutuwekea kanuni juu ya mambo yenye kuwa ya muzuri na mambo yenye kuwa ya mubaya? Wakati Adamu na Eva walikula matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya, walionyesha wazi kama hawakumutumainia Yehova na kanuni zake. Waliamua kujiwekea kanuni zao wenyewe za mema na mabaya. (Mwa. 3:22) Lakini, fikiria mambo yenye walipoteza. Walipoteza urafiki wao pamoja na Yehova. Pia, walipoteza nafasi ya kuishi milele, na waliachia watoto wao zambi na kifo. (Ro. 5:12) Uamuzi wa Adamu na Eva ulileta taabu.

Kisha kumukubali Yesu, towashi Muetiopia alipenda kubatizwa bila kukawia (Picha hii inapatana na fungu la 2-3)

2-3. (a) Towashi Muetiopia alitenda namna gani wakati Filipo alimuhubiria? (b) Kubatizwa kunatuletea baraka gani, na tutajibu maulizo gani?

2 Linganisha namna Adamu na Eva walitenda na namna towashi Muetiopia alitenda wakati Filipo alimuhubiria. Towashi alikuwa mwenye shukrani juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walikuwa wamemufanyia na hilo lilimuchochea abatizwe palepale. (Mdo. 8:34-38) Wakati tunajitoa kwa Mungu na kubatizwa, kama vile ule Muetiopia alifanya, tunaonyesha wazi kama tuko wenye shukrani juu ya mambo yenye Yehova na Yesu wametufanyia. Tunaonyesha pia kama tunamutumainia Yehova na kama tunakubali kuwa ni yeye tu njo mwenye anapaswa kutuwekea kanuni za mema na mabaya.

3 Fikiria baraka zenye tunapata wakati tunamutumikia Yehova! Baraka moja ni hii: tuko na tumaini la kupata tena mambo yote yenye Adamu na Eva walipoteza, kutia ndani nafasi ya kuishi milele. Kwa sababu tuko na imani katika Yesu Kristo, Yehova anasamehe makosa yetu na anatusaidia kuwa na zamiri ya muzuri. (Mt. 20:28; Mdo. 10:43) Pia, tunakuwa mu familia ya watumishi wa Yehova wenye anakubali, wenye kungojea wakati muzuri sana wenye kuwa mbele yetu. (Yoh. 10:14-16; Ro. 8:20, 21) Lakini, hata kama kuko faida hizo zenye kuwa wazi, watu fulani wenye wamefikia kumujua Yehova wanasita kufuata mufano wa towashi Muetiopia. Pengine ni mambo gani inawazuia wasibatizwe? Na namna gani wanaweza kushinda vile vizuizi?

MAMBO YENYE KUZUIA WATU FULANI WASIBATIZWE

Vizuizi vyenye watu fulani wanapambana navyo mbele waamue kubatizwa

Kukosa Kujiaminia (Picha hizi zinapatana na fungu la 4-5) *

4-5. Kijana mwanaume mwenye kuitwa Avery na kijana mwanamuke mwenye kuitwa Hannah walikuwa na matatizo gani?

4 Kukosa kujiaminia. Wazazi wa Avery ni Mashahidi wa Yehova. Baba yake anajulikana kuwa mwenye sifa za muzuri sana: ni baba mwenye kuhangaikia familia yake na ni muzee muzuri wa kutaniko. Lakini, Avery alijizuia kubatizwa. Juu ya nini? Anasema hivi: “Nilifikiri kwamba sitaweza kuwa na sifa za muzuri kama za baba yangu.” Pia, Avery hakuamini kama anaweza kutimiza muzuri madaraka yenye anaweza kupewa wakati wenye kuja. Anasema tena hivi: “Niliogopa kama nitaombwa kusali mbele ya watu wengi, kutoa hotuba mbalimbali, ao kuongoza kikundi katika mahubiri.”

5 Hannah, mwenye kuwa na miaka 18, alikuwa na tatizo kubwa la kukosa kujiaminia. Wazazi wake ni watumishi wa Yehova. Hata hivyo, alikuwa na mashaka kwamba hataweza kufuata kanuni za Yehova. Juu ya nini? Hannah alikuwa anajiona kuwa mutu wa bure sana. Wakati fulani, alikuwa anajisikia mubaya sana na hilo lilifanya ajiumize, lakini kufanya vile kuliharibisha mambo zaidi. Anasema hivi: “Sikuambia hata mutu mumoja juu ya jambo lenye nilikuwa ninafanya, sikuambia hata wazazi wangu, na niliwaza kuwa Yehova hatanikubali hata kidogo nikuwe mutumishi wake kwa sababu ya namna nilikuwa ninajitendea.”

Kuchochewa Mubaya na Marafiki (Picha hii inapatana na fungu la 6) *

6. Ni nini ilimuzuia Vanessa asibatizwe?

6 Kuchochewa mubaya na marafiki. Vanessa, mwenye kuwa na miaka 22, anasema hivi: “Nilikuwa na rafiki muzuri mwenye nilikuwa nimejuana naye kwa miaka karibu kumi.” Lakini, rafiki ya Vanessa hakuunga mukono muradi wa Vanessa wa kupenda kubatizwa. Hilo lilimuhuzunisha Vanessa. Anasema hivi: “Haiko mwepesi kwangu kuwa na marafiki, na niliogopa kama ikiwa ninakata urafiki pamoja naye, singepata tena rafiki mwingine wa sana.”

Mutu Kuogopa Kuwa Atafanya Kosa Nzito (Picha hii inapatana na fungu la 7) *

7. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Makayla aliogopa nini, na juu ya nini?

7 Mutu kuogopa kuwa atafanya kosa nzito. Makayla alikuwa na miaka tano wakati ndugu yake mukubwa alitengwa na kutaniko. Wakati alikuwa anakomaa, aliona huzuni yenye wazazi wake walikuwa nayo kwa sababu ya matendo ya ndugu yake. Makayla anasema hivi: “Niliogopa kama, ikiwa ningebatizwa, ningefanya kosa, kisha ningetengwa na kutaniko, na kuletea wazazi wangu huzuni hata zaidi.”

Kuogopa Kupingwa (Picha hii inapatana na fungu la 8) *

8. Kijana mwanaume mwenye kuitwa Miles aliogopa nini?

8 Kuogopa kupingwa. Baba ya Miles na bibi ya baba yake ni Mashahidi wa Yehova, lakini mama yake mwenye kumuzaa haiko Shahidi. Miles anasema hivi: “Niliishi na mama yangu kwa miaka 18, na niliogopa kumuambia kama nilipenda kubatizwa. Nilikuwa nimeona namna mama yangu alitenda wakati baba yangu alifikia kuwa Shahidi. Niliogopa kama angenipinga.”

UNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUSHINDA VIZUIZI HIVYO?

9. Inawezekana kabisa kuwa utafanya nini wakati unajifunza kama Yehova iko muvumilivu na mwenye upendo sana?

9 Adamu na Eva walikamata uamuzi wa kukosa kumutumikia Yehova juu upendo wao kwake haukukuwa wenye nguvu. Hata hivyo, Mungu aliwaacha waishi wakati murefu ili wakuwe na watoto na wajiwekee kanuni zao wenyewe juu ya namna ya kulea ao kukomalisha watoto hao. Bila kukawia, matokeo ya uamuzi wa Adamu na Eva wa kuacha kumutegemea Mungu ilionyesha wazi kama walikuwa wapumbavu kabisa. Mutoto wao wa kwanza aliua ndugu yake mwenye hakukuwa na kosa, na kisha wakati fulani, wanadamu wengi walifikia kuwa wenye jeuri na wenye kujipenda wenyewe. (Mwa. 4:8; 6:11-13) Lakini, Yehova alifanya njia ya kuokoa watoto wote wa Adamu na Eva wenye wanapenda kumutumikia. (Yoh. 6:38-40, 57, 58) Wakati unaendelea kujifunza mambo mingi juu ya namna Yehova iko muvumilivu na mwenye upendo sana, inawezekana kabisa kuwa utamupenda zaidi. Utakuwa tayari kuepuka kukamata uamuzi wenye Adamu na Eva walikamata na utajitoa kwa Yehova.

Unaweza kufanya nini ili kushinda vizuizi hivi

(Picha hizi zinapatana na fungu la 9-10) *

10. Juu ya nini kufikiri sana juu ya Zaburi 19:7 kunaweza kukusaidia umutumikie Yehova?

10 Endelea kujifunza juu ya Yehova. Wakati unaendelea kujifunza mambo mingi juu ya Yehova, utakuwa hakika zaidi kama utaweza kumutumikia. Avery, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Nilianza kujiaminia wakati nilisoma na kufikiri sana juu ya ahadi yenye kupatikana mu Zaburi 19:7.” (Soma.) Wakati Avery aliona namna Yehova alitimiza ile ahadi, alimupenda zaidi. Upendo unatusaidia tujiaminie na unatusaidia tukaze akili yetu juu ya Yehova na juu ya mambo yenye anapenda. Hannah, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Kusoma na kujifunza Biblia kipekee, kulinisaidia nielewe kama wakati ninajiumiza mwenyewe, Yehova naye anaumia mu moyo wake.” (1 Pe. 5:7) Hannah akakuwa ‘mutendaji wa neno la Mungu.’ (Yak. 1:22) Alipata matokeo gani? Anasema hivi: “Wakati niliona kama kumutii Yehova kuliniletea faida, nilifikia kumupenda zaidi. Sasa, niko hakika kama Yehova ataniongoza sikuzote wakati niko na lazima ya musaada wake.” Hannah aliweza kuachana na tabia yake ya kujiumiza mwenyewe. Alijitoa kwa Yehova na kubatizwa.

(Picha hii inapatana na fungu la 11) *

11. Vanessa alifanya nini ili kupata marafiki wazuri, na mufano wake unaweza kutufundisha nini?

11 Chagua marafiki wako kwa hekima. Vanessa, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, alifikia kutambua kama rafiki yake alikuwa anamuzuia asimutumikie Yehova. Kwa hiyo, alikata urafiki huo. Lakini, Vanessa hakuishia pale. Alijikaza sana ili kutafuta marafiki wapya, mu kutaniko. Anasema kama mufano wa Noa na familia yake ulimusaidia. Anasema hivi: “Walikuwa wanazungukwa na watu wenye hawakumupenda Yehova, lakini walikuwa na uhusiano muzuri kati yao.” Kisha kubatizwa, Vanessa alianza kufanya kazi ya upainia. Sasa anasema hivi: “Kufanya vile kumenisaidia kupata marafiki wazuri, haiko tu mu kutaniko langu lakini pia mu makutaniko ingine.” Na wewe unaweza kupata marafiki wazuri kama unafanya kwa bidii kazi yenye Yehova ametupatia tufanye.​—Mt. 24:14.

(Picha hizi zinapatana na fungu la 12-15) *

12. Adamu na Eva hawakukuwa na woga wa aina gani, na hilo lilileta matokeo gani?

12 Ujifunze kuwa na woga wenye kufaa. Ni muzuri kuwa na aina fulani ya woga. Kwa mufano, tunapaswa kuogopa kumuchukiza Yehova. (Zb. 111:10) Adamu na Eva wangekuwa na woga wa aina hiyo, hawangemuasi Yehova. Lakini, walimuasi. Kisha kufanya vile, macho yao ilifunguliwa, ni kusema, walielewa kabisa kama walikuwa watenda-zambi. Wangeweza tu kuachia watoto wao zambi na kifo. Kwa sababu waliona, ao kuelewa, hali yao, walisikia haya juu walikuwa uchi na wakajifunika.​—Mwa. 3:7, 21.

13-14. (a) Kulingana na 1 Petro 3:21, juu ya nini hatupaswe kuogopa sana kifo? (b) Tuko na sababu gani za kumupenda Yehova?

13 Hata kama tunapaswa kuogopa kumuchukiza Yehova, hatupaswe kuogopa sana kifo. Yehova amefanya njia ya kutusaidia tupate uzima wa milele. Kama tunafanya zambi, lakini tunatubu kwelikweli, Yehova atasamehe makosa yetu. Atatusamehe kwa sababu tuko na imani katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Mwana wake. Njia moja kati ya njia za maana zaidi za kuonyesha imani ni kutoa maisha yetu kwa Mungu na kubatizwa.​—Soma 1 Petro 3:21.

14 Tuko na sababu za mingi za kumupenda Yehova. Anatupatia mambo ya muzuri yenye tunafurahia kila siku na pia anatufundisha kweli juu yake na juu ya kusudi lake. (Yoh. 8:31, 32) Ametupatia kutaniko la Kikristo ili lituongoze na kututegemeza. Anatusaidia kuvumilia magumu yetu leo, na anatupatia tumaini la kuishi milele mu hali kamilifu wakati wenye kuja. (Zb. 68:19; Ufu. 21:3, 4) Wakati tunafikiri sana juu ya mambo yote yenye tayari Yehova amefanya ili kutuonyesha kama anatupenda, tunachochewa kumupenda. Na wakati tunamupenda Yehova, tunajifunza kuwa na woga wenye kufaa. Tunaogopa kumuhuzunisha Yehova, kwa sababu tumefikia kumupenda sana.

15. Namna gani Makayla alishinda tatizo lake la kuogopa kama atafanya kosa nzito?

15 Makayla, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, alishinda tatizo lake la kuogopa kama atafanya kosa nzito wakati alielewa kama Yehova ni mwenye kusamehe sana. Anasema hivi: “Nilielewa kama sisi wote hatukamilike na tutafanya makosa. Lakini nilielewa pia kama Yehova anatupenda na atatusamehe kwa sababu tuko na imani katika bei ya ukombozi.” Upendo wake kwa Yehova ulimuchochea ajitoe kwake na kubatizwa.

(Picha hii inapatana na fungu la 16) *

16. Ni nini ilimusaidia Miles aache kuogopa kuwa mama yake atamupinga?

16 Miles, mwenye alikuwa anaogopa kama mama yake angepinga uamuzi wake wa kubatizwa, aliomba musaada kwa mwangalizi wa muzunguko. Miles anasema hivi: “Ule mwangalizi naye alikomalia mu familia yenye muzazi mumoja tu njo Shahidi. Alinisaidia nifikiri juu ya mambo yenye ningesema ili nimusadikishe mama yangu kama mimi mwenyewe njo nilikamata uamuzi wa kubatizwa na kama haiko baba yangu njo alikuwa ananisukuma nifanye vile.” Mama ya Miles hakufurahia uamuzi wake. Kisha wakati fulani, Miles alipaswa kutoka kwa mama yake, lakini alishikamana na uamuzi wake. Anasema hivi: “Kujifunza juu ya mambo ya muzuri yenye Yehova amenifanyia kulinigusa moyo. Wakati nilifikiri sana juu ya zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu, nilifikia kuona kama Yehova ananipenda sana. Wazo hilo lilinichochea nijitoe kwa Yehova na kubatizwa.”

SHIKAMANA NA UAMUZI WAKO

Tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya mambo yenye Mungu ametufanyia (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17. Tuko na nafasi ya kuonyesha nini?

17 Wakati Eva alikula tunda la muti fulani wenye ulikuwa mu bustani ya Edeni, alimukataa Baba yake. Wakati Adamu alijiunga naye, alionyesha kama hakukuwa mwenye shukrani juu ya mambo yote ya muzuri yenye Yehova alikuwa amemufanyia. Sisi wote tuko na nafasi ya kuonyesha kama hatukubaliane hata kidogo na uamuzi wenye Adamu na Eva walikamata. Wakati tunabatizwa, tunaonyesha kama tunaamini kama Yehova iko na mamlaka ya kutuwekea kanuni za mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. Tunaonyesha kama tunamupenda Baba yetu na tunamutegemea.

18. Unaweza kufanya nini ili ukuwe na matokeo ya muzuri katika utumishi wako kwa Yehova?

18 Kisha kubatizwa, tunapaswa kufuata kanuni za Yehova kila siku mu maisha yetu, hapana kanuni zetu wenyewe. Mamilioni ya watu wanafanya vile kila mwaka. Unaweza kuwaiga ikiwa unaendelea kujikaza ili kuelewa muzuri zaidi Neno la Mungu, Biblia; kujiunga kwa ukawaida na ndugu na dada zako; na kuwa na hamu ya kuambia wengine mambo yenye umejifunza juu ya Baba yako mwenye upendo. (Ebr. 10:24, 25) Wakati unakamata maamuzi, usikilize mashauri yenye Yehova anakutolea kupitia Neno lake na tengenezo lake. (Isa. 30:21) Ukifanya vile, mambo yote yenye unafanya itakuwa na matokeo ya muzuri.​—Mez. 16:3, 20.

19. Unapaswa kuendelea kukumbuka jambo gani, na juu ya nini?

19 Wakati unaendelea kukumbuka kama kuongozwa na Yehova kunakuletea faida za mingi, utamupenda zaidi na utapenda zaidi kanuni zake. Ukifanya vile, hakuna jambo lolote lenye Shetani anakutolea lenye litafanya uache kumutumikia Yehova. Wazia kunapita miaka elfu moja kuanzia leo. Utakumbuka uamuzi wa kubatizwa wenye ulikamata na kuona kama njo uamuzi muzuri zaidi wenye ulikamata mu maisha yako!

WIMBO 28 Kuwa Rafiki ya Yehova

^ fu. 5 Kuamua kama utabatizwa ao hapana, njo uamuzi wa maana zaidi wenye utakamata mu maisha yako. Juu ya nini uamuzi huo ni wa maana sana? Habari hii itajibu ulizo hilo. Pia, itasaidia wale wenye wanafikiria kubatizwa washinde vizuizi vyenye pengine vinawafanya wasibatizwe.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Kukosa kujiaminia: Kijana mwanaume anaogopa kutoa majibu kwenye mikutano.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Marafiki: Shahidi kijana mwenye iko na rafiki mubaya anasikia haya wakati anaona Mashahidi wenzake.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Mutu kuogopa kuwa atafanya kosa nzito: Wakati ndugu yake anatengwa na kutaniko na kutoka kwao, kijana mwanamuke anaogopa kuwa yeye pia atafanya kosa nzito.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Kupingwa: Kijana mwanaume anaogopa kusali wakati mama yake mwenye haiko Shahidi iko anamuangalia.

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA: Kukosa kujiaminia: Kijana mwanaume anafanya muzuri zaidi funzo lake la pekee.

^ fu. 67 MAFASIRIO YA PICHA: Marafiki: Shahidi kijana anajifunza kujivunia kuwa Shahidi.

^ fu. 69 MAFASIRIO YA PICHA:Mutu kuogopa kuwa atafanya kosa nzito: Kijana mwanamuke anashikamana na kweli na anabatizwa.

^ fu. 71 MAFASIRIO YA PICHA:Kupingwa: Kijana mwanaume anamufasiria mama yake bila woga mambo yenye anaamini.