Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 11

Sikiliza Sauti ya Yehova

Sikiliza Sauti ya Yehova

“Huyu ni Mwana wangu . . . Mumusikilize.”​—MT. 17:5.

WIMBO 89 Sikiliza, Tii, Upate Baraka

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Yehova amezungumuza na wanadamu kupitia njia gani? (b) Tutazungumuzia nini mu habari hii?

YEHOVA anapenda kuzungumuza na sisi. Wakati wa zamani, alitumia manabii, malaika, na Yesu Kristo, Mwana wake, ili kutujulisha mawazo yake. (Amo. 3:7; Gal. 3:19; Ufu. 1:1) Leo, anazungumuza na sisi kupitia Neno lake, Biblia. Alitupatia Biblia ili tujue mawazo yake na tuelewe njia zake.

2 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, Yehova alisema kutoka mbinguni mara tatu. Tuzungumuzie basi mambo yenye Yehova alisema, mambo yenye maneno yake inaweza kutufundisha, na faida zenye tunapata kupitia mambo yenye alisema.

“WEWE NI MWANA WANGU, MUPENDWA”

3. Kama vile andiko la Marko 1:9-11 linaonyesha, Yehova alisema nini wakati Yesu alibatizwa, na ile maneno inahakikisha mambo gani ya maana?

3 Marko 1:9-11 inazungumuzia mara ya kwanza yenye Yehova alisema kutoka mbinguni. (Soma.) Alisema hivi: “Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.” Yesu alipaswa kuguswa moyo kabisa wakati alisikia Baba yake anasema kama anamupenda na kumutumainia! Maneno ya Yehova ilihakikisha mambo tatu ya maana juu ya Yesu. Kwanza, Yesu ni Mwana wake. Pili, Yehova anamupenda Mwana wake. Na tatu, Yehova amemukubali Mwana wake. Tuchunguze basi kwa uangalifu kila jambo kati ya ile mambo tatu.

4. Wakati Yesu alibatizwa, aliingia katika uhusiano gani mupya pamoja na Mungu?

4 “Wewe ni Mwana wangu.” Kupitia ile maneno, Yehova alionyesha kama Yesu, Mwana wake mupendwa, alikuwa ameingia katika uhusiano mupya pamoja naye. Wakati Yesu alikuwa mbinguni, alikuwa mwana wa roho wa Mungu. Lakini, wakati alibatizwa, alitiwa mafuta kwa roho takatifu. Wakati huo, Mungu alionyesha kama Yesu akiwa Mwana wake mutiwa mafuta, alikuwa sasa na tumaini la kurudia mbinguni ili akuwe Kuhani Mukubwa na Mufalme mwenye aliwekwa na Mungu. (Lu. 1:31-33; Ebr. 1:8, 9; 2:17) Kwa hiyo, wakati Yesu alibatizwa, Baba yake alikuwa na sababu ya muzuri ya kusema hivi: “Wewe ni Mwana wangu.”​—Lu. 3:22.

Tunafanya maendeleo ya muzuri wakati wengine wanatupongeza na kututia moyo (Picha hizi zinapatana na fungu la 5) *

5. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yehova wa kuonyesha wengine upendo na kuwatia moyo?

5 “Wewe ni . . . mupendwa.” Yehova alionyesha Mwana wake kama anamupenda na anamukubali; mufano wake unatukumbusha kama tunapaswa kutafuta nafasi za kutia wengine moyo. (Yoh. 5:20) Tunafanya maendeleo ya muzuri wakati mutu fulani mwenye tunapendaka anaonyesha kama anatupenda na kutupongeza juu ya mambo ya muzuri yenye tunafanya. Vilevile, ndugu na dada zetu mu kutaniko na watu wa familia yetu wako na lazima tuwaonyeshe upendo na kuwatia moyo. Wakati tunapongeza wengine, tunatia nguvu imani yao na tunawasaidia wamutumikie Yehova kwa ushikamanifu. Zaidi sana wazazi wanapaswa kutia moyo watoto wao. Wakati wazazi wanapongeza watoto wao kwa moyo wote na kuwaonyesha upendo, wanawasaidia wafanye maendeleo ya muzuri.

6. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yesu atatimiza ahadi zote za Yehova?

6 “Nimekukubali.” Ile maneno inaonyesha kama Yehova alikuwa hakika kuwa Yesu angetimiza kwa uaminifu mapenzi ya Baba yake. Kwa sababu Yehova iko na uhakika huo juu ya Mwana wake, na sisi tunaweza kuwa hakika kabisa kama Yesu atatimiza ahadi zote za Yehova. (2 Ko. 1:20) Wakati tunafikiri juu ya mufano wa Yesu, tunaazimia hata zaidi kujifunza kupitia mufano wake na kufuata hatua zake. Vilevile, Yehova iko hakika kuwa watumishi wake, wakiwa kikundi, wataendelea kufuata mufano wa Mwana wake.​—1 Pe. 2:21.

“MUMUSIKILIZE”

7. Kulingana na Matayo 17:1-5, ni wakati gani Yehova alisema kutoka mbinguni, na alisema nini?

7 Soma Matayo 17:1-5. Mara ya pili yenye Yehova alisema kutoka mbinguni ilikuwa wakati Yesu ‘aligeuzwa sura.’ Yesu alikuwa amealika Petro, Yakobo, na Yohana wamusindikize juu ya mulima murefu. Wakati walikuwa kule, waliona maono ya ajabu. Sura ya Yesu na nguo zake vilingaa sana. Watu wawili, wenye walifananisha Musa na Eliya, wakaanza kuzungumuza na Yesu juu ya kifo chenye kingemupata na juu ya ufufuo wake. Hata kama mitume hao tatu walikuwa “wamelemewa na usingizi,” waliona ile maono ya kushangaza wakati walikuwa macho kabisa. (Lu. 9:29-32) Kisha, wingu lenye kungaa likawafunika, na wakasikia sauti kutoka katika lile wingu, ilikuwa sauti ya Mungu! Kama vile Yehova alifanya wakati Yesu alibatizwa, mara hii tena alisema kama alimukubali Mwana wake na kumupenda. Alisema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.” Lakini mara hii Yehova aliongeza hivi: “Mumusikilize.”

8. Namna gani maono ya kugeuzwa sura ilisaidia Yesu na wanafunzi wake?

8 Ile maono ilionyesha utukufu na uwezo wenye Yesu angekuwa nao wakati wenye kuja wakati angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Kwa kweli, Kristo alitiwa moyo na alitiwa nguvu ili kuvumilia mateso na kifo chenye maumivu chenye kingemupata. Pia, ile maono ilitia nguvu imani ya wanafunzi. Hilo liliwasaidia wajitayarishe juu ya majaribu ya uaminifu-mushikamanifu yenye ingewapata na kazi ya nguvu yenye wangepaswa kufanya kwa miaka mingi. Miaka 30 hivi kisha pale, mutume Petro alizungumuzia ile maono ya kugeuzwa sura, na hilo lilionyesha kama alikuwa angali anaikumbuka kabisa.​—2 Pe. 1:16-18.

9. Yesu alitolea wanafunzi wake mashauri gani yenye kufaa?

9 “Mumusikilize.” Yehova alionyesha wazi kama anapenda tusikilize maneno ya Mwana wake na tuitii. Yesu alisema nini wakati alikuwa ku dunia? Alisema mambo mingi ya maana yenye tunapaswa kusikiliza! Kwa mufano, kwa upendo alifundisha wanafunzi wake namna ya kuhubiri habari njema, na mara kwa mara aliwakumbusha waendelee kukesha. (Mt. 24:42; 28:19, 20) Pia, aliwaomba wajikaze sana, na aliwatia moyo wasichoke. (Lu. 13:24) Yesu alikazia kama ni jambo la lazima wanafunzi wake wapendane, waendelee kuwa na umoja, na kushika amri zake. (Yoh. 15:10, 12, 13) Ile mashauri yenye Yesu alitolea wanafunzi wake ilikuwa yenye kufaa kabisa! Na ni ya maana sana leo kama vile tu ilikuwa wakati Yesu aliitoa.

10-11. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko tunamusikiliza Yesu?

10 Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye iko upande wa ile kweli anasikiliza sauti yangu.” (Yoh. 18:37) Tunaonyesha kama tuko tunasikiliza sauti yake wakati ‘tunaendelea kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda.’ (Kol. 3:13; Lu. 17:3, 4) Tena, tunaonyesha kama tuko tunasikiliza sauti yake wakati tunahubiri habari njema kwa bidii “katika nyakati zenye kufaa na nyakati zenye kuwa ngumu.”​—2 Ti. 4:2.

11 Yesu alisema hivi: “Kondoo wangu wanasikiliza sauti yangu.” (Yoh. 10:27) Wanafunzi wa Kristo wanaonyesha kama wanasikiliza sauti ya Yesu kwa kukazia uangalifu maneno yake na kuitii. Hawakengeushwe na “mahangaiko ya maisha.” (Lu. 21:34) Lakini, kutii amri za Yesu njo jambo lenye wanaona kuwa la maana sana mu maisha yao, hata wakati wanapatwa na magumu. Ndugu na dada zetu wengi wanavumilia magumu makali, kutia ndani kushambuliwa na wapinzani, umaskini wa sana, na misiba ya asili. Mu ile magumu yote, wanaendelea kuwa waaminifu, hata kutokee nini. Yesu anawahakikishia hivi: “Kila mutu mwenye kuwa na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye mwenye ananipenda. Na kila mutu mwenye ananipenda atapendwa na Baba yangu.”​—Yoh. 14:21.

Kazi yetu ya kuhubiri inatusaidia tuendelee kusikiliza sauti ya Yesu (Picha hii inapatana na fungu la 12) *

12. Tunaonyesha kama tuko tunamusikiliza Yesu kupitia njia gani ingine?

12 Njia ingine ya kuonyesha kama tuko tunamusikiliza Yesu ni hii: kuunga mukono wale wenye ameweka ili watuongoze. (Ebr. 13:7, 17) Tengenezo la Mungu limefanya mabadiliko mingi mu miaka ya hivi majuzi, kutia ndani kutumia vyombo vya mupya mu mahubiri na njia za mupya za kuhubiri, namna ya kufanya mukutano wetu wa katikati ya juma, na namna tunajenga, tunarekebisha, na kutunza Majumba yetu ya Ufalme. Tuko wenye shukrani kabisa juu ya muongozo huo wenye upendo na wenye kufikiriwa kwa uangalifu! Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atabariki bidii yenye tunafanya ili kufuata muongozo wenye tengenezo linatutolea kwa wakati wenye kufaa.

13. Tunapata faida gani wakati tunamusikiliza Yesu?

13 Tunapata faida wakati tunasikiliza mambo yote yenye Yesu alifundisha. Yesu aliahidi wanafunzi wake kama mafundisho yake ingewapumuzisha. Alisema hivi: “Mutapata pumuziko kwa ajili yenu. Kwa maana nira yangu haiko yenye kuumiza, na muzigo wangu ni mwepesi.” (Mt. 11:28-30) Neno la Mungu, lenye kutia ndani vitabu ine vya Injili vyenye kuzungumuzia maisha na utumishi wa Yesu, linatupumuzisha, linaturudishia nguvu ya kiroho, na linatufanya tukuwe wenye hekima. (Zb. 19:7; 23:3) Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!”​—Lu. 11:28.

‘NITATUKUZA JINA LANGU’

14-15. (a) Kama vile andiko la Yohana 12:27, 28 linaonyesha, ni wakati gani Yehova alizungumuza kutoka mbinguni kwa mara ya tatu? (b) Juu ya nini maneno ya Yehova ilipaswa kumufariji Yesu na kumutia nguvu?

14 Soma Yohana 12:27, 28. Injili ya Yohana inazungumuzia mara ya tatu yenye Yehova alisema kutoka mbinguni. Siku kidogo mbele ya kifo chake, Yesu alikuwa Yerusalemu ili kufanya Pasaka yake ya mwisho. Alisema hivi: “Ninavurugika.” Kisha akasali hivi: “Baba, tukuza jina lako.” Kisha kusali vile, Baba yake alisema hivi kutoka mbinguni: “Nimelitukuza na nitalitukuza tena.”

15 Yesu alivurugika kwa sababu ya daraka kubwa lenye alikuwa nalo la kubakia muaminifu kwa Yehova. Yesu alijua kama alikuwa karibu kuteswa mubaya sana na kufa kifo chenye maumivu makali. (Mt. 26:38) Zaidi ya mambo ingine yote, Yesu alipenda kutukuza jina la Baba yake. Yesu alishitakiwa kuwa alimutukana Mungu, na alihangaika kuwa kifo chake kingefanya jina la Mungu lichafuliwe. Maneno ya Yehova ilipaswa kumusaidia Yesu akuwe na uhakika kabisa! Angeweza kuwa hakika kama jina la Yehova lingetukuzwa. Maneno ya Baba yake ilipaswa kumufariji kabisa na kumutia nguvu ili avumilie mateso yenye ingemupata. Hata kama kati ya watu wenye walikuwa pale, pengine Yesu tu njo mwenye alielewa maneno yenye Baba yake alisema wakati huo, Yehova alifanya maneno yake iandikwe kwa ajili yetu sisi wote.​—Yoh. 12:29, 30.

Yehova atatukuza jina lake na kukomboa watu wake (Picha hii inapatana na fungu la 16) *

16. Juu ya nini wakati fulani tunaweza kuhangaika juu ya kuchafuliwa kwa jina la Mungu?

16 Kama Yesu, sisi pia tunaweza kuhangaika juu ya kuchafuliwa kwa jina la Yehova. Pengine tunatendewa bila haki kama Yesu. Ao tunaweza kuhangaika juu ya habari za uongo zenye wapinzani wanaeneza juu yetu. Tunaweza kufikiria namna habari hizo zinachafua jina la Yehova na tengenezo lake. Wakati kama huo, ile maneno ya Yehova yenye kupatikana katika Yohana 12:27, 28 inaweza kutufariji sana. Hatupaswe kuhangaika sana. Tunaweza kuwa hakika kama “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo [yetu] na nguvu [zetu] za akili kupitia Kristo Yesu.” (Flp. 4:6, 7) Yehova hatakosa hata siku moja kutukuza jina lake. Kupitia Ufalme wake, atatosha mambo yote ya mubaya yenye Shetani na ulimwengu wake wanaletea watumishi wake waaminifu.​—Zb. 94:22, 23; Isa. 65:17.

NAMNA SAUTI YA YEHOVA INATULETEA FAIDA LEO

17. Kulingana na Isaya 30:21, Yehova anasema na sisi kupitia njia gani leo?

17 Yehova angali anasema na sisi leo. (Soma Isaya 30:21.) Kwa kweli, hatusikie sauti ya Mungu inasema na sisi kutoka mbinguni. Lakini, anatutolea muongozo kupitia Neno lake, Biblia, lenye kuandikwa. Tena, roho ya Yehova inachochea “musimamizi-nyumba muaminifu” ili aendelee kupatia watumishi wake chakula cha kiroho. (Lu. 12:42) Kwa kweli, tunapata chakula mingi cha kiroho kupitia habari zenye kuchapishwa na zenye kuwa ku Enternete, kupitia video, na vichapo vya kusikiliza tu!

18. Namna gani maneno ya Yehova inatia nguvu imani yako na kukupatia uhodari?

18 Basi tuendelee kukumbuka maneno yenye Yehova alisema wakati Mwana wake alikuwa ku dunia! Maneno ya Mungu, yenye kuandikwa mu Biblia, itupatie basi uhakika kama Yehova iko na uwezo juu ya mambo yote na kama atatosha mambo yote ya mubaya yenye Shetani na ulimwengu wake mubaya wametuletea. Na tuazimie kusikiliza kwa uangalifu sauti ya Yehova. Tukifanya vile, tutaweza kuvumilia magumu yoyote yenye tunapambana nayo leo na magumu yoyote ya wakati wenye kuja. Biblia inatukumbusha hivi: “Muko na lazima ya uvumilivu, ili kisha kufanya mapenzi ya Mungu, mupokee utimizo wa ile ahadi.”​—Ebr. 10:36.

WIMBO 4 “Yehova Ni Mchungaji Wangu”

^ fu. 5 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, Yehova alizungumuza mara tatu kutoka mbinguni. Mara moja kati ya mara hizo tatu, Yehova aliomba wanafunzi wa Kristo wamusikilize Mwana wake. Leo, Yehova anasema na sisi kupitia Neno lake lenye kuandikwa, lenye kutia ndani mafundisho ya Yesu, na pia anasema na sisi kupitia tengenezo lake. Habari hii itazungumuzia faida zenye tunapata wakati tunamusikiliza Yehova na Yesu.

^ fu. 52 MAFASIRIO YA PICHA: Muzee mumoja anaona mutumishi wa huduma iko anasaidia kutunza Jumba la Ufalme na iko anasaidia kutumika ku meza ya vichapo. Muzee huyo anamupongeza kwa furaha.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana mu inchi ya Sierra Leone wanatolea mualiko wa mukutano mwanaume mumoja wa eneo lao mwenye anavuaka samaki.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Mashahidi mu inchi fulani kwenye kazi yetu imewekewa vizuizi, wanafanya mukutano mu nyumba ya ndugu fulani. Wanavaa kwa njia ya kawaida ili wasivumbuliwe.