Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anaona “Amina” Yako Kuwa ya Maana

Yehova Anaona “Amina” Yako Kuwa ya Maana

YEHOVA anaona ibada yenye tunamutolea kuwa ya maana. Iko ‘muangalifu na anasikiliza’ watumishi wake, na anaona kila jambo lenye wanafanya ili kumusifu, hata kama ni jambo la kidogo sana. (Mal. 3:16) Kwa mufano, fikiria neno moja lenye inawezekana kabisa tumesema mara mingi sana. Ni neno “amina.” Je, Yehova anaona hata neno hilo la mwepesi kuwa la maana? Ndiyo! Ili kujua juu ya nini, tuzungumuzie basi maana ya neno hilo na namna linatumiwa mu Biblia.

“WATU WOTE WATASEMA, ‘AMINA!’”

Neno la Kiswahili “amina” maana yake “ikuwe vile,” ao “bila shaka.” Neno hilo linatokana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “kuwa muaminifu,” “kuwa mwenye kutumainika.” Wakati fulani, lilitumiwa mu mambo ya sheria. Kisha mutu kufanya kiapo fulani, alikuwa anasema “amina” ili kuhakikisha kama mambo yenye alisema ilikuwa ya kweli na kama alikubali matokeo ya maneno yake. (Hes. 5:22) Wakati alisema “amina” mbele ya watu, alihakikisha hata zaidi kama atatimiza maneno yake.​—Ne. 5:13.

Mufano mukubwa wenye kuonyesha namna neno “amina” lilitumiwa unapatikana mu kitabu cha Kumbukumbu la Torati sura ya 27. Kisha Waisraeli kuingia mu Inchi ya Ahadi, walipaswa kukusanyika kati ya Mulima Ebali na Mulima Gerizimu ili wasikilize usomaji wa Sheria. Walikuwa pale ili kusikiliza na pia ili kuonyesha kama wanakubali sheria hiyo. Walifanya vile kwa kujibu “Amina!” wakati waliwasomea mambo yenye ingewapata ikiwa wangekosa kutii. (Kum. 27:15-26) Wazia sauti ya maelfu ya wanaume, wanamuke, na watoto wakati wanajibu kwa sauti kubwa! (Yos. 8:30-35) Kwa kweli, hawakusahau hata kidogo maneno yenye walisema ile siku. Na wale Waisraeli walitimiza neno lao, kwa sababu Biblia inasema hivi: “Israeli wakaendelea kumutumikia Yehova siku zote za Yoshua na siku zote za wazee wenye waliendelea kuishi kisha Yoshua kufa na wenye walikuwa wamejua mambo yote yenye Yehova alitendea Israeli.”​—Yos. 24:31.

Yesu naye alitumia neno “amina” ili kuhakikisha kama mambo yenye alisema ilikuwa ya kweli kabisa, lakini alifanya vile kwa njia ya pekee. Yesu hakutumia neno amina ili kujibu kisha maneno fulani kusemwa, lakini alitumia neno “amina” (lenye kutafsiriwa “kwa kweli” mu Kiswahili) mbele ya kusema maneno fulani ili kuhakikisha kama ile maneno ilikuwa ya kweli. Wakati fulani, alirudilia neno hilo kwa kusema “amina amina.” (Mt. 5:18; Yoh. 1:51) Kwa kufanya vile, alihakikishia wasikilizaji wake kama maneno yake ilikuwa ya kweli kabisa. Yesu angeweza kuzungumuza kwa uhakika huo kwa sababu ni yeye njo mwenye aliruhusiwa kufanya ahadi zote za Mungu zitimie.​—2 Ko. 1:20; Ufu. 3:14.

“WATU WOTE WAKASEMA, ‘AMINA!’ NA WAKAMUSIFU YEHOVA”

Waisraeli walitumia pia neno “amina” wakati walimusifu Yehova na wakati walisali kwake. (Ne. 8:6; Zb. 41:13) Kwa kusema neno hilo ku mwisho wa sala, wale wenye walikuwa wanasikiliza walionyesha kama walikubaliana na sala hiyo. Kwa kufanya vile, watu wote wenye walikuwa pale walishiriki katika sala, na hilo lilifanya tukio hilo la kiroho lifurahishe zaidi. Njo vile mambo ilikuwa wakati Mufalme Daudi alipeleka Sanduku la Yehova mu muji wa Yerusalemu. Wakati wa tukio lenye lilifuata, alitoa sala yenye ilitoka mu moyo wake yenye kuwa kama wimbo; sala hiyo inapatikana mu 1 Mambo ya Nyakati 16:8-36. Wale wote wenye walikuwa pale waliguswa moyo kupitia maneno yake na kwa hiyo “watu wote wakasema, ‘amina!’ na wakamusifu Yehova.” Kwa kweli, walifurahi sana kumuabudu Yehova pamoja ile siku.

Wakristo wa wakati wa mitume nao walikuwa wanatumia neno “amina” wakati walikuwa wanamusifu Yehova. Mara mingi waandikaji wa Biblia walitumia neno hilo katika barua zao. (Ro. 1:25; 16:27; 1 Pe. 4:11) Kitabu cha Ufunuo kinasema kama Yohana aliona katika maono hata viumbe vya roho mbinguni viko vinamutukuza Yehova kwa kusema: “Amina! Mumusifu Yah!” (Ufu. 19:1, 4) Wakristo wa kwanza-kwanza walizoea kusema “amina” ku mwisho wa sala zenye zilitolewa ku mikutano yao. (1 Ko. 14:16) Lakini, hawakupaswa kurudilia-rudilia neno hilo bila kufikiri.

JUU YA NINI “AMINA” YAKO NI YA MAANA?

Kisha kuzungumuzia namna neno “amina” lilikuwa linatumiwa, tunaelewa juu ya nini ni jambo la maana kabisa kusema neno hilo ku mwisho wa sala. Wakati tunasema neno hilo ku mwisho wa sala yetu, tunaonyesha kama mambo yenye tunasema inatoka mu moyo wetu. Na wakati tunachochewa kusema “amina,” hata kimya-kimya, ku mwisho wa sala yenye kutolewa mbele ya watu wengi, tunaonyesha kama tunakubaliana na mambo yenye imesemwa. Fikiria sababu zingine zenye kuonyesha kama “amina” yetu ni ya maana.

Tunasikiliza kwa uangalifu wakati mutu mwingine anasali kwa sababu hiyo ni sehemu ya ibada yetu. Tunamuabudu Yehova wakati wa sala kupitia maneno yenye tunasema, na pia kupitia namna tunajiendesha. Kwa sababu tunapenda kusema “amina” yenye kutoka mu moyo, hilo linatuchochea tukuwe na mutazamo muzuri na tukaze akili yetu juu ya sala.

Tunakuwa na umoja sisi waabudu wa Yehova. Wakati sala inatolewa mbele ya watu wote mu kutaniko, hilo linafanya tukaze akili juu ya mambo ileile yenye ndugu na dada wengine wote wanasikiliza. (Mdo. 1:14; 12:5) Wakati tunachochewa kusema “amina” pamoja na ndugu na dada zetu, hilo linafanya tukuwe na umoja zaidi. Ikuwe tunasema “amina” kwa sauti ao mu moyo wetu, sala yetu inaweza kuchochea Yehova afanye mambo yenye tumemuomba.

“Amina” yetu inachangia kumusifu Yehova

Tunamusifu Yehova. Yehova anaona mambo yote yenye tunafanya mu ibada yetu. (Lu. 21:2, 3) Anaona nia yetu na mambo yenye kuwa mu moyo wetu. Hata kama tunapaswa kusikiliza mukutano kupitia telefone, tunaweza kuwa hakika kama Yehova hakose kusikia “amina” yetu yenye tunasema kwa unyenyekevu. Wakati tunasema “amina,” tunajiunga na wengine wenye kuwa ku mikutano ili kumusifu Yehova.

“Amina” yetu inaweza kuonekana kuwa haina maana, lakini ni ya maana sana. Kitabu kimoja chenye kutoa maelezo juu ya Biblia kinasema hivi: “Kwa kutumia neno hilo moja, watumishi wa Mungu wanaweza kuonyesha uhakika, wanaweza kukubaliana kabisa, na kuonyesha tumaini la kweli lenye kuwa mu moyo wao.” Basi, kila “amina” yenye tunasema imupendeze Yehova.​—Zb. 19:14.