Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Wakati wa zamani, mutu alikuwa anafanya mipango gani ili kusafiri kwa mashua?

KWA kawaida, mashua za kubeba watu tu hazikukuwa mu siku za Paulo. Ili kusafiri kwa kutumia mashua, mutu alikuwa anauliza watu wengine ikiwa wanajua mashua ya biashara (ao ya mizigo) yenye ilikuwa inaenda mahali kwenye ataenda na yenye ingeitika kubeba watu. (Mdo. 21:2, 3) Hata kama mutu alikuwa mu mashua yenye haikukuwa inaenda mahali kwenye alikuwa anaenda, alikuwa anashukia mu njia wakati mashua ilikuwa inasimama mahali mbalimbali na kutafuta mashua ya kuenda karibu na kwenye alikuwa anaenda.​—Mdo. 27:1-6.

Safari katika bahari ilikuwa inafanywa katika vipindi fulani vya mwaka, na mashua hazikukuwa na programu fulani ya kawaida. Zaidi ya hali ya hewa ya mubaya, watumishi wa mashua wenye waliamini ushirikina walikuwa wanachelewesha safari ikiwa waliona alama yenye ilionyesha kama watapatwa na mambo ya mubaya, alama kama vile kunguru mwenye kulia kwenye kamba za mashua, ao wakati waliona pembeni ya inchi kavu mashua ingine yenye iliharibika. Watumishi wa mashua walikuwa wanasafiri wakati upepo ulikuwa muzuri, kwa hiyo wakati upepo ulikuwa wenye kufaa, walikuwa wanaanza safari. Wakati mutu mwenye kusafiri alikuwa anapata mashua yenye iliitika kumubeba, alikuwa anaenda pembeni ya bandari (mahali mashua zinaegesha) akiwa na mizigo yake na kungojea tangazo la kuonyesha kama mashua inataka kuenda.

Mwanahistoria mumoja mwenye kuitwa Lionel Casson anasema hivi: “Roma ilikuwa na njia ya mwepesi ya kusaidia watu wapate mashua ya kusafiri nayo ili wasilazimike kutafuta mashua wao wenyewe. Bandari yake ilikuwa mahali kwenye Muto Tiberi unaingilia mu bahari. Mu muji wa Ostia wenye ulikuwa karibu, kulikuwa kiwanja kikubwa cha watu wote chenye kilizungukwa na biro mbalimbali. Biro za mingi kati ya biro hizo zilikuwa za wafanyakazi wenye kuwakilisha bandari mbalimbali: wafanyakazi wa bandari ya Narbonne [yenye kuwa katika Ufaransa ya leo] walikuwa na biro pale, wafanyakazi wa bandari ya Carthage [yenye kuwa katika Tunisia ya leo] walikuwa pia na biro pale, . . . na kulikuwa zingine. Kila mutu mwenye alikuwa anatafuta mashua ya kusafiri nayo angeweza tu kuuliza habari mu biro za miji yenye ilikuwa mu njia ya safari yake.”

Kusafiri mu bahari kulisaidia watu wafike mbio, lakini safari ya namna hiyo ilikuwa na magumu yake. Mara fulani mutume Paulo alivunjikiwa na mashua katika safari zake za umisionere.​—2 Ko. 11:25.