Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 20

Namna ya Kufariji Wale Wenye Wametendewa Mubaya Kingono

Namna ya Kufariji Wale Wenye Wametendewa Mubaya Kingono

“Mungu wa faraja yote . . . anatufariji katika majaribu yetu yote.”​—2 KO. 1:3, 4.

WIMBO 134 Watoto Amana Kutoka kwa Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Ni mufano gani wenye kuonyesha kama wanadamu wanazaliwa na uhitaji wa kufarijiwa na uwezo wa kufariji wengine? (b) Watoto fulani wanaumizwa katika njia gani?

WANADAMU wanazaliwa na uhitaji wa kufarijiwa na uwezo wa pekee wa kufariji wengine. Kwa mufano, wakati mutoto mudogo anaanguka na kuumia kwenye magoti, anaweza kukimbilia kwa mama ao baba yake na iko analia. Wazazi hawawezi kuponyesha kidonda, lakini wanaweza kufariji mutoto wao. Wanaweza kumuuliza ni nini ilitokea, wanaweza kumupanguza machozi, kupuliza kwenye kidonda chake, na pengine wanaweza kuweka dawa kwenye kidonda hicho ao kukifunga. Bila kukawia, mutoto anaacha kulia na anaweza hata kuanza kucheza tena. Kisha wakati fulani, kidonda kitapona.

2 Lakini, wakati fulani watoto wanaumizwa katika njia za mubaya sana. Watoto fulani wanatendewa mubaya kingono. Mutoto anaweza kutendewa mubaya kingono mara moja ao mara mingi kwa kipindi cha miaka fulani. Katika hali hizo mbili, kutendewa mubaya vile kunaumiza mutoto sana na anaweza kusikia maumivu ya moyoni kwa miaka mingi. Katika hali fulani, mutu mwenye alitendea mutoto mubaya kingono anakamatwa na kupewa malipizi. Katika hali zingine, inaweza kuonekana kuwa mutu mwenye alitendea mutoto mubaya kingono hapewe malipizi hata kidogo. Lakini, hata kama anapewa malipizi bila kukawia, mutoto mwenye alitendewa mubaya kingono anaweza kuendelea kuteseka hata wakati atakuwa mutu muzima.

3. Kama vile andiko la 2 Wakorinto 1:3, 4 linaonyesha, Yehova anapenda nini, na tutazungumuzia maulizo gani?

3 Kama Mukristo fulani mwenye alitendewa mubaya kingono wakati alikuwa angali mutoto anaendelea kupambana na maumivu ya moyoni hata kama alishakuwa mutu muzima, namna gani tunaweza kumusaidia? (Soma 2 Wakorinto 1:3, 4.) Ni wazi kwamba Yehova anapenda kondoo wake waonyeshwe upendo na kupata faraja yenye wako nayo lazima. Tuzungumuzie basi maulizo hii tatu: (1) Juu ya nini wale wenye wametendewa mubaya kingono wako na lazima ya kufarijiwa? (2) Ni nani wenye wanaweza kuwatolea faraja yenye wako nayo lazima? (3) Namna gani tunaweza kuwafariji muzuri?

JUU YA NINI WAKO NA LAZIMA YA FARAJA?

4-5. (a) Juu ya nini ni jambo la lazima kujua kama watoto wako tofauti na watu wazima? (b) Kama mutoto anatendewa mubaya kingono, hilo linaweza kuwa na matokeo gani juu ya uwezo wake wa kutumainia wengine?

4 Watu fulani wazima wenye walitendewa mubaya kingono wakati walikuwa watoto, wanaweza kuwa wangali na lazima ya faraja hata kama kumepita miaka mingi tangu watendewe vile. Juu ya nini? Ili tuelewe, tunapaswa kwanza kujua kama watoto wako tofauti sana na watu wazima. Namna mutoto anajisikia wakati anatendewa mubaya iko tofauti na namna mutu muzima anajisikia wakati anatendewa mubaya. Fikiria mifano fulani.

5 Watoto wako na lazima ya kutumainia wale wenye wanawalea na kuwahangaikia na kuwa na uhusiano muzuri pamoja nao. Uhusiano huo unafanya watoto wajisikie kuwa salama na unawasaidia kutumainia watu wengine wenye kuwapenda. (Zb. 22:9) Jambo la kuhuzunisha ni hili: mara mingi watoto wanatendewa mubaya kingono katika nyumba yao, na mara mingi ni watu wa familia na marafiki wa familia njo wanawatendeaka mubaya kingono. Wakati mutoto anatendewa mubaya kingono na mutu mwenye anatumainia, hilo linaweza kufanya ashindwe kutumainia watu wengine, hata kisha miaka mingi kupita.

6. Juu ya nini kutendea watoto mubaya kingono ni kukosa huruma na ni jambo lenye kuumiza sana?

6 Watoto hawana uwezo wa kujilinda, na kutendea watoto mubaya kingono ni kukosa huruma na ni jambo lenye kuumiza sana. Kukaza watoto wafanye mambo ya ngono miaka mingi mbele wakomae kimwili, kihisia, na kiakili ili kuwa tayari kwa ajili ya ngono katika ndoa, kunaweza kuwaumiza sana. Kutendea mutoto mubaya kingono, kunaweza kuharibisha sana mawazo yake juu ya ngono, juu ya namna anajiona, ao juu ya mutu yeyote mwenye anatafuta kumukaribia.

7. (a) Juu ya nini watu wadanganyifu wenye kutendea watoto mubaya kingono wanaweza kudanganya watoto kwa vyepesi, na namna gani watu hao wanaweza kufanya vile? (b) Uongo huo unaweza kuwa na matokeo gani?

7 Watoto hawajajua muzuri namna ya kuwaza, kukamata maamuzi, ao kutambua na kuepuka hatari. (1 Ko. 13:11) Kwa hiyo, ni vyepesi sana kwa watu wadanganyifu wenye kutendea watoto mubaya kingono kudanganya watoto. Watu wenye kutendea watoto mubaya kingono wanawaambia uongo wa mubaya sana, kama vile ni mutoto njo mwenye kosa, kama jambo lenye alitendewa linapaswa kubakia siri, na kama hakuna mutu mwenye atamuamini ao kumusaidia ikiwa anaeleza juu ya jambo hilo, ao kama kufanya matendo ya ngono kati ya mutu muzima na mutoto ni jambo lenye kuonyesha upendo wa kweli kabisa. Uongo huo unaweza kuharibu uwezo wa mutoto wa kufikiri na inaweza kuomba miaka mingi ili aelewe kama ile mambo yote yenye aliambiwa ilikuwa ya uongo. Mutoto kama huyo anaweza kukomaa na mawazo ya kuona kama ameharibishwa, amechafuliwa, na hastahili kupendwa ao kufarijiwa.

8. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anaweza kufariji wale wenye wameumizwa?

8 Kwa hiyo, hatuwezi kushangaa kuona kama, kutendea watoto mubaya kingono kunaweza kuleta maumivu ya muda murefu. Hilo ni kosa la mubaya sana! Kuenea kwa tendo hilo la mubaya kunaonyesha wazi kama tunaishi mu siku za mwisho, wakati wenye watu wengi “hawana upendo wa asili” na wakati wenye “watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.” (2 Ti. 3:1-5, 13) Njia za udanganyifu za Shetani ni zenye uovu kabisa, na inahuzunisha wakati wanadamu wanafanya mambo yenye kumufurahisha Ibilisi. Lakini, Yehova iko na nguvu zaidi kuliko Shetani ao watumishi wake. Sikuzote Yehova anajua njia zote za udanganyifu za Shetani. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova anajua muzuri maumivu yenye tunapambana nayo, na anaweza kutupatia faraja yenye tuko nayo lazima. Tunabarikiwa kwa sababu tunatumikia “Mungu wa faraja yote, mwenye anatufariji katika majaribu yetu yote ili tuweze kufariji wengine wenye kuwa katika jaribu la namna yoyote kupitia faraja yenye tunapokea kutoka kwa Mungu.” (2 Ko. 1:3, 4) Sasa, Yehova anatumia nani ili kutoa faraja?

NI NANI WENYE WANAWEZA KUTOA FARAJA?

9. Kulingana na maneno ya Mufalme Daudi yenye kupatikana mu Zaburi 27:10, Yehova atafanya nini kwa ajili ya wale wenye wameachwa na watu wa familia yao?

9 Wale wenye wameachwa na wazazi wao ao wale wenye wametendewa mubaya kingono na watu wa karibu njo wenye wako zaidi sana na lazima ya faraja. Daudi, muandikaji mumoja wa zaburi, alijua kama tunaweza kutumainia kuwa Yehova atatufariji sikuzote. (Soma Zaburi 27:10.) Daudi alikuwa na imani kama Yehova anahangaikia wale wenye wameachwa na wapendwa wao. Namna gani Yehova anafanya vile? Anatumia watumishi wake waaminifu. Ndugu na dada zetu katika kutaniko ni familia yetu ya kiroho. Kwa mufano, Yesu aliita wale wenye walijiunga naye ili kumuabudu Yehova kuwa ndugu zake, dada zake, na mama yake.​—Mt. 12:48-50.

10. Mutume Paulo alisema nini juu ya kazi yake akiwa muzee?

10 Tuchunguze mufano wenye kuonyesha namna Wakristo wenzetu mu kutaniko wako kama familia yetu. Mutume Paulo alikuwa muzee muaminifu mwenye kufanya kazi kwa bidii. Alionyesha mufano muzuri sana, na hata aliongozwa na roho ya Mungu ili kuambia wengine wamuige kama vile yeye alimuiga Kristo. (1 Ko. 11:1) Wakati fulani, Paulo alisema hivi juu ya kazi yake akiwa muzee: “Tulikuwa wapole katikati yenu, kama vile wakati mama mwenye kunyonyesha anahangaikia kwa upendo watoto wake mwenyewe.” (1 Te. 2:7) Leo, wazee washikamanifu wanaweza pia kutumia maneno yenye upole na yenye kuonyesha huruma wakati wanatumia Maandiko ili kufariji wale wenye wako na lazima ya musaada.

Mara mingi, dada wenye kukomaa kiroho wanafariji kwa njia ya muzuri (Picha hii inapatana na fungu la 11) *

11. Ni nini inaonyesha kama haiko wazee tu njo wanaweza kufariji wengine?

11 Je, ni wazee tu njo wanaweza kufariji wale wenye walitendewa mubaya kingono? Hapana. Sisi wote tuko na daraka la ‘kuendelea kufarijiana.’ (1 Te. 4:18) Zaidi sana dada wenye kukomaa kiroho wanaweza kufariji dada wenye kuwa na lazima ya faraja. Ni jambo lenye kufaa kuona kama Yehova Mungu anajifananisha na mama mwenye kufariji mwana wake. (Isa. 66:13) Biblia inazungumuzia mifano ya wanamuke wenye walifariji watu wenye walikuwa na huzuni. (Yob. 42:11) Yehova anafurahi sana wakati anaona namna dada Wakristo leo wanafariji dada wenzao wenye wanapiganisha maumivu ya moyoni! Katika hali fulani, wazee wanaweza kuomba kwa siri dada mwenye kukomaa kiroho asaidie dada mwenye kuteseka katika njia hiyo. *

NAMNA GANI TUNAWEZA KUTOA FARAJA?

12. Tunapaswa kuepuka kufanya nini?

12 Kwa kweli, tunakuwa waangalifu ili tusijiingize katika mambo yenye Mukristo mwenzetu hapendi kuzungumuzia. (1 Te. 4:11) Lakini, tunaweza kufanya nini kwa ajili ya wale wenye kuwa na lazima ya musaada na faraja? Tuzungumuzie basi njia tano zenye kutegemea Maandiko za kufariji watu wengine.

13. Kama vile andiko la 1 Wafalme 19:5-8 linaonyesha, malaika wa Yehova alimufanyia Eliya jambo gani, na namna gani tunaweza kumuiga?

13 Toa musaada wenye kufaa. Wakati nabii Eliya alikuwa anakimbia ili kuokoa uzima wake, alikuwa mwenye kuvunjika moyo sana na alipenda akufe. Yehova alimutuma malaika mwenye nguvu ili amutembelee mwanaume huyo mwenye alikuwa amevunjika moyo. Malaika huyo alimupatia Eliya musaada wenye kufaa. Alimupatia Eliya chakula cha moto na akamutia moyo akule. (Soma 1 Wafalme 19:5-8.) Habari hiyo inaonyesha kweli hii ya maana: Wakati fulani tendo la kidogo lenye kuonyesha wema linaweza kusaidia sana. Pengine kupatia ndugu ao dada mwenye amevunjika moyo chakula, zawadi ya kidogo, ao kumuandikia barua yenye kutia moyo, kunaweza kumuonyesha kama tunamupenda na kumuhangaikia. Kama hatujisikie huru kuzungumuzia mambo ya kipekee sana ao yenye kuhuzunisha, pengine tunaweza kutoa musaada fulani wenye kufaa kama huo.

14. Habari juu ya Eliya inaweza kutufundisha nini?

14 Fanya watu wenye huzuni wajisikie kuwa salama na wajisikie muzuri. Habari juu ya Eliya inaweza kutufundisha jambo lingine. Kwa njia ya muujiza, Yehova alimupatia nabii huyo musaada wenye alikuwa nao lazima ili kutembea njia murefu mupaka ku Mulima Horebu. Pengine Eliya alijisikia salama kwenye nafasi hiyo ya mbali, kwenye Yehova alikuwa amefanya agano pamoja na watu wake, miaka mingi mbele ya pale. Pengine alijisikia kuwa mwishowe alikuwa mbali sana na watu wenye walikuwa wanatafuta kumutendea mubaya. Hilo linaweza kutufundisha nini? Kama tunapenda kufariji wale wenye wametendewa mubaya kingono, tunapaswa kwanza kuwasaidia wajisikie kuwa salama. Kwa mufano, wazee wanapaswa kukumbuka kama dada mwenye kuwa na huzuni anaweza kujisikia muzuri na salama zaidi wakati wanazungumuza naye ku nyumba kuliko kuzungumuza naye ku Jumba la Ufalme. Mutu mwingine anaweza kufurahia zaidi kuzungumuza ku Jumba la Ufalme.

Tunaweza kuponyesha wengine kwa kuwasikiliza kwa uvumilivu, kusali kwa bidii, na kuchagua maneno yenye kufariji (Picha hizi zinapatana na fungu la 15-20) *

15-16. Kuwa musikilizaji muzuri kunatia ndani nini?

15 Ukuwe musikilizaji muzuri. Biblia inatoa shauri hili lenye kuwa wazi: “Kila mutu anapaswa kuwa mwepesi wa kusikiliza, hapana mwepesi wa kusema.” (Yak. 1:19) Je, tuko wasikilizaji wazuri? Tunaweza kuwaza kama ili kuwa musikilizaji muzuri inaomba kumuangalia tu mutu bila kusema kitu. Lakini, kuwa musikilizaji muzuri kunatia ndani mambo mingi zaidi. Kwa mufano, mwishowe Eliya alimuambia Yehova namna alikuwa anajisikia mubaya sana, na Yehova alimusikiliza kabisa. Yehova alitambua kama Eliya alikuwa na woga, alijisikia kuwa peke yake, na aliwaza kama kazi yake yote yenye alikuwa amefanya ilikuwa ya bure. Yehova alishugulikia kwa upendo mahangaiko yake yote. Alionyesha kama alikuwa amemusikiliza Eliya kabisa.​—1 Fa. 19:9-11, 15-18.

16 Wakati tunamusikiliza ndugu ao dada fulani, namna gani tunaweza kumuonyesha huruma, sifa yenye kuonyesha kama tunamupenda? Wakati fulani, maneno kidogo yenye kuonyesha utambuzi na uchangamufu inaweza kuonyesha namna tunajisikia. Unaweza kusema hivi: “Pole sana juu ya jambo lenye lilikufikia! Hakuna mutoto mwenye anapaswa kutendewa vile!” Pengine unaweza kuuliza ulizo moja ao maulizo mbili ili kuhakikisha kama unaelewa mambo yenye rafiki yako mwenye kuwa na huzuni iko anasema. Unaweza kumuuliza hivi: “Tafazali, unaweza kunisaidia kuelewa jambo lenye unapenda kusema?” ao “Wakati ulisema vile, niliwaza . . . Ni vile ulipenda kusema?” Maneno kama ile yenye kuonyesha upendo inaweza kuhakikishia mutu huyo kama unamusikiliza kabisa, na kama unajikaza kumuelewa.​—1 Ko. 13:4, 7.

17. Juu ya nini tunapaswa kuonyesha uvumilivu na hatupaswe kuwa ‘wepesi wa kusema’?

17 Lakini, ukuwe muangalifu ili usikuwe “mwepesi wa kusema.” Usikatize mutu ili kumupatia shauri ao ili kurekebisha mawazo yake. Na uonyeshe uvumilivu! Mwishowe, wakati Eliya alimuambia Yehova namna alikuwa anajisikia, alitumia maneno ya huzuni sana. Kisha Yehova kutia nguvu imani ya Eliya, Eliya alimuambia tena Yehova namna alikuwa anajisikia kwa kutumia maneno ileile. (1 Fa. 19:9, 10, 13, 14) Hilo linatufundisha nini? Wakati fulani, watu wenye huzuni wako na lazima ya kueleza zaidi ya mara moja namna wanajisikia. Kama Yehova, tunapenda kuwasikiliza kwa uvumilivu. Kuliko kujaribu kuwaambia mambo yenye wanapaswa kufanya ili kumaliza matatizo yao, tunawaonyesha huruma.​—1 Pe. 3:8.

18. Juu ya nini kusali pamoja na wale wenye kuwa na huzuni kunaweza kuwafariji?

18 Sali kwa bidii pamoja na mutu mwenye kuwa na huzuni. Mutu mwenye kushuka moyo sana anaweza kushindwa kusali. Anaweza kujisikia kuwa hastahili kumukaribia Yehova. Kama tunapenda kufariji mutu kama huyo, tunaweza kusali pamoja naye, na kutaja jina lake katika sala. Tunaweza kumuelezea Yehova kama sisi na kutaniko tunamupenda sana mutu huyo mwenye kuvunjika moyo. Tunaweza kumuomba Yehova amutulize na kumufariji kondoo wake huyo wa maana sana. Sala kama hizo zinaweza kufariji kabisa.​—Yak. 5:16.

19. Ni nini inaweza kutusaidia tujitayarishe ili kufariji mutu fulani?

19 Uchague maneno yenye kuponyesha na yenye kufariji. Ufikiri mbele ya kusema. Maneno yenye kusemwa bila kufikiri inaweza kuumiza wengine. Maneno ya muzuri inaweza kuponyesha. (Mez. 12:18) Kwa hiyo, usali kwa Yehova ili akusaidie kupata maneno ya muzuri, yenye kufariji, na yenye kutuliza. Ukumbuke kama hakuna maneno yenye kuwa na nguvu zaidi kuliko maneno ya Yehova yenye kuwa katika Biblia.​—Ebr. 4:12.

20. Ndugu na dada fulani wenye walitendewa mubaya kingono zamani wanaweza kujisikia namna gani, na tunapenda kuwakumbusha nini?

20 Ndugu na dada fulani wenye walitendewa mubaya kingono zamani wanaweza kujisikia kuwa wachafu, wenye hawana maana, wenye hawapendwe ao hata kuwa hawawezi kupendwa na mutu yeyote. Huo ni uongo mubaya sana! Kwa hiyo, utumie Maandiko ili kuwakumbusha kama Yehova anawaona kuwa wa maana sana. (Ona kisanduku “ Faraja Kutoka Katika Maandiko.”) Kumbuka namna, kwa upendo, malaika alimutia nguvu nabii Danieli wakati alikuwa anajisikia kuwa muzaifu na mwenye kushuka moyo. Yehova alitaka mwanaume huyo mupendwa ajue kama alikuwa wa samani ao wa maana sana. (Da. 10:2, 11, 19) Vilevile, Yehova anaona ndugu na dada zetu wenye huzuni kuwa wa maana sana!

21. Watenda-zambi wenye hawatubu watapatwa na nini, lakini sisi wote tunapaswa kuazimia kufanya nini mbele wakati huo ufike?

21 Wakati tunafariji wengine, tunawakumbusha kama Yehova anawapenda. Na hatupaswe kusahau hata kidogo kuwa Yehova iko pia Mungu mwenye haki. Anajua kila mutu mwenye ametendewa mubaya kingono, hata kama hakuna mutu mwingine mwenye anajua jambo hilo. Yehova anaona kila kitu, na hatakosa kupatia azabu ao malipizi watenda-zambi wenye hawatubu. (Hes. 14:18) Mbele wakati huo ufike, tufanye basi nguvu yetu yote ili kuonyesha upendo wale wenye wametendewa mubaya kingono. Tena, inafariji sana kujua kama Yehova ataponyesha milele wale wote wenye wametendewa mubaya na Shetani na ulimwengu wake! Hivi karibuni, hatutakumbuka tena ile mambo yenye kuumiza, na haitaingia tena mu moyo wetu.​—Isa. 65:17.

WIMBO 109 Pendaneni Sana Kutoka Moyoni

^ fu. 5 Wale wenye walitendewa mubaya kingono wakati walikuwa watoto wanaweza kupambana na magumu mingi hata kisha miaka mingi kupita. Habari hii itatusaidia kuelewa sababu. Tutazungumuzia pia ni nani wenye wanaweza kufariji watu hao. Mwishowe, tutazungumuzia ni katika njia gani za muzuri tunaweza kuwafariji.

^ fu. 11 Mutu mwenye alitendewa mubaya kingono anaweza kuamua yeye mwenyewe ikiwa atatafuta musaada wa munganga.

^ fu. 76 MAFASIRIO YA PICHA: Dada mumoja mwenye kukomaa kiroho anafariji dada mwenye kuwa na maumivu ya moyoni.

^ fu. 78 MAFASIRIO YA PICHA: Wazee wawili wanatembelea dada huyo mwenye kuwa na huzuni. Amealika ule dada mwenye kukomaa kiroho ili akuwe pale.