Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 18

Upendo na Haki Katika Kutaniko la Kikristo

Upendo na Haki Katika Kutaniko la Kikristo

“Muendelee kubebeana mizigo mizito, na kwa njia hiyo mutatimiza sheria ya Kristo.”​—GAL. 6:2.

WIMBO 12 Mungu Mkuu, Yehova

KIFUPI CHA HABARI *

1. Tunaweza kuwa hakika juu ya mambo gani mbili?

YEHOVA MUNGU anapenda waabudu wake. Amewapenda sikuzote, na ataendelea kuwapenda. Anapenda pia haki. (Zb. 33:5) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika juu ya mambo mbili: (1) Yehova anahuzunika wakati watumishi wake wanatendewa bila haki. (2) Atahakikisha kama watu wake wanatendewa kwa haki. Katika habari ya kwanza ya habari hizi, * tulijifunza kama Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli kupitia Musa ilitegemea upendo. Ilikazia haki; haki kwa ajili ya watu wote, hata kwa ajili ya watu wenye hawakukuwa na uwezo wa kujilinda. (Kum. 10:18) Sheria hiyo inaonyesha kama Yehova anahangaikia sana waabudu wake.

2. Tutajibu maulizo gani?

2 Sheria ya Musa ilifikia mwisho wake mu mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati kutaniko la Kikristo lilianzishwa. Wakristo wangebakia bila kulindwa na sheria yenye kutegemea upendo na yenye kukazia haki? Hapana! Wakristo walikuwa na sheria ya mupya. Katika habari hii, tutazungumuzia kwanza sheria hiyo ni sheria gani. Kisha tutajibu maulizo hii: Juu ya nini tunaweza kusema kama sheria hiyo inategemea upendo? Juu ya nini tunaweza kusema kama inakazia haki? Chini ya sheria hiyo, wale wenye kuwa na mamlaka wanapaswa kutendea wengine namna gani?

“SHERIA YA KRISTO” NI NINI?

3. “Sheria ya Kristo” yenye kutajwa katika Wagalatia 6:2, inatia ndani nini?

3 Soma Wagalatia 6:2. Wakristo wanaongozwa na “sheria ya Kristo.” Yesu hakuandika liste ya sheria kwa ajili ya wanafunzi wake, lakini aliwapatia maagizo, amri, na kanuni za kuwaongoza katika maisha yao. “Sheria ya Kristo” inatia ndani mambo yote yenye Yesu alifundisha. Ili kuelewa muzuri zaidi sheria hiyo, fikiria mambo yenye kufuata.

4-5. Yesu alifundisha kupitia njia gani, na alifundisha wakati gani?

4 Yesu alifundisha watu kupitia njia gani? Kwanza, alifundisha watu kupitia mambo yenye alisema. Maneno yake ilikuwa yenye nguvu kwa sababu alisema kweli juu ya Mungu, alifundisha kusudi la kweli la maisha, na alifundisha kama Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza mateso yote ya wanadamu. (Lu. 24:19) Yesu alifundisha pia kupitia mufano wake. Kupitia namna aliishi, alionyesha wanafunzi wake namna walipaswa kuishi.​—Yoh. 13:15.

5 Yesu alifundisha wakati gani? Alifundisha wakati alikuwa anafanya utumishi wake hapa ku dunia. (Mt. 4:23) Pia, wakati mufupi kisha kufufuliwa kwake, alifundisha wanafunzi wake. Kwa mufano, alitokea kikundi cha wanafunzi wake, pengine walikuwa zaidi ya 500, na aliwapatia amri ya ‘kufanya wanafunzi.’ (Mt. 28:19, 20; 1 Ko. 15:6) Kwa sababu Yesu njo kichwa cha kutaniko, aliendelea kufundisha wanafunzi wake kisha kurudia mbinguni. Kwa mufano, katika mwaka wa 96 hivi, Kristo alimuongoza mutume Yohana ili atie moyo Wakristo watiwa-mafuta na kuwapatia mashauri.​—Kol. 1:18; Ufu. 1:1.

6-7. (a) Mafundisho ya Yesu imeandikwa wapi? (b) Namna gani tunatii sheria ya Kristo?

6 Mafundisho ya Yesu imeandikwa wapi? Mambo mingi yenye Yesu alisema na kufanya wakati alikuwa ku dunia, imeandikwa katika vitabu ine vya Injili. Vitabu vingine vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, vyenye viliandikwa na wanaume wenye waliongozwa na roho takatifu na wenye walikuwa na “akili ya Kristo,” vinatusaidia pia kuelewa mawazo ya Kristo juu ya mambo mbalimbali.​—1 Ko. 2:16.

7 Mambo yenye tunajifunza: Mafundisho ya Yesu inaweza kutusaidia katika sehemu zote za maisha. Kwa hiyo, sheria ya Kristo inahusu mambo yenye tunafanya ku nyumba, ku kazi, ku masomo, na katika kutaniko. Tunajifunza sheria hiyo kwa kusoma vitabu vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma. Tunatii sheria hiyo kwa kutumia mu maisha yetu maagizo, amri, na kanuni zenye kupatikana katika vile vitabu vyenye viliongozwa na roho ya Mungu. Wakati tunatii sheria ya Kristo, tunamutii Yehova, Mungu wetu mwenye upendo, mwenye mambo yote yenye Yesu alifundisha ilitoka kwake.​—Yoh. 8:28.

SHERIA YENYE KUTEGEMEA UPENDO

8. Musingi wa sheria ya Kristo ni nini?

8 Nyumba yenye kujengwa muzuri, yenye kujengwa kwenye musingi wenye nguvu, inafanya wale wenye kuishi ndani wajisikie kuwa salama. Vilevile, sheria yenye kujengwa juu ya musingi wenye nguvu inafanya wale wenye kuitii wajisikie salama. Sheria ya Kristo inajengwa kwenye musingi muzuri zaidi, ni kusema, upendo. Juu ya nini tunaweza kusema vile?

Wakati tunatendea wengine kwa upendo, tunatii “sheria ya Kristo” (Picha hii inapatana na fungu la 9-14) *

9-10. Ni mifano gani yenye kuonyesha kama Yesu alichochewa na upendo, na namna gani tunaweza kumuiga?

9 Kwanza, Yesu alichochewa na upendo katika mambo yote yenye alifanya. Sifa ya huruma, inaonyesha kama mutu iko na upendo. Huruma kama hiyo ilimuchochea Yesu afundishe vikundi vya watu, aponyeshe wagonjwa, akulishe watu wenye walikuwa na njaa, na kufufua watu wenye walikuwa wamekufa. (Mt. 14:14; 15:32-38; Mk. 6:34; Lu. 7:11-15) Hata kama kufanya vile kuliomba Yesu atumie wakati mingi na nguvu mingi, alikuwa tayari kutanguliza mahitaji ya wengine kuliko mahitaji yake mwenyewe. Zaidi ya yote, alionyesha upendo mukubwa kwa kutoa uzima wake kwa ajili ya wengine.​—Yoh. 15:13.

10 Mambo yenye tunajifunza: Tunaweza kumuiga Yesu kwa kutanguliza mahitaji ya wengine kuliko mahitaji yetu wenyewe. Pia, tunaweza kumuiga kwa kujifunza kuonyesha zaidi watu wa eneo letu huruma. Wakati huruma kama hiyo inatuchochea kuhubiri na kufundisha watu habari njema, tunatii sheria ya Kristo.

11-12. (a) Ni nini inaonyesha kama Yehova anatuhangaikia sana? (b) Namna gani tunaweza kuiga upendo wa Yehova?

11 Pili, Yesu alionyesha upendo wa Baba yake. Wakati wa utumishi wake, Yesu alionyesha namna Yehova anahangaikia sana waabudu wake. Alionyesha jambo hilo katika njia mingi. Kwa mufano, alifundisha jambo hili: Baba yetu wa mbinguni anaona kila mumoja wetu kuwa wa maana na mwenye samani. (Mt. 10:31) Yehova iko tayari kabisa kukaribisha kondoo mwenye alikuwa amepotea mwenye anatubu na kurudia katika kutaniko. (Lu. 15:7, 10) Yehova alituonyesha upendo wake kwa kumutoa Mwana wake kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yetu.​—Yoh. 3:16.

12 Mambo yenye tunajifunza: Namna gani tunaweza kuiga upendo wa Yehova? (Efe. 5:1, 2) Tunaona kila ndugu na dada yetu kuwa wa maana na mwenye samani, na tunakaribisha kwa furaha “kondoo mwenye amepotea” mwenye kumurudilia Yehova. (Zb. 119:176) Tunaonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu kwa kujitoa kwa ajili yao, kama vile kuwasaidia wakati wako na lazima ya musaada. (1 Yo. 3:17) Wakati tunaonyesha wengine upendo, tunatii sheria ya Kristo.

13-14. (a) Kama vile andiko la Yohana 13:34, 35 linasema, Yesu aliamuru wanafunzi wake waonyeshe nini, na juu ya nini ile ni amri mupya? (b) Namna gani tunatii ile amri mupya?

13 Tatu, Yesu aliamuru wanafunzi wake waonyeshe upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine. (Soma Yohana 13:34, 35.) Amri ya Yesu ni ya mupya kwa sababu inatuomba tuonyeshe aina ya upendo yenye haikuombwa katika Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli: Tupende Wakristo wenzetu kama vile Yesu alitupenda. Hilo linaomba upendo wa kujitoa. * Tunapaswa kupenda ndugu na dada zetu hata kuliko namna tunajipenda sisi wenyewe. Tunapaswa kuwapenda sana mupaka tunakuwa tayari kutoa uzima wetu kwa ajili yao, kama vile Yesu alifanya kwa ajili yetu.

14 Mambo yenye tunajifunza: Namna gani tunatii ile amri mupya? Kwa kifupi, ni kwa kujitoa kwa ajili ya ndugu na dada zetu. Tuko tayari kutoa jambo kubwa zaidi kwa ajili yao, ni kusema, uzima wetu, lakini pia tuko tayari kujitoa katika mambo ya kidogo-kidogo. Kwa mufano, tunaonyesha kama tunatii sheria ya Kristo wakati tunajikaza kwa ukawaida ili kusaidia ndugu ao dada mwenye kuzeeka ahuzurie mikutano, ao wakati tuko tayari kuachana na mambo yenye tunapenda ili kupendeza Wakristo wenzetu, ao wakati tunaomba mapumuziko kwenye kazi ili kusaidia ndugu na dada zetu wakati wa musiba. Pia, tunasaidia kufanya kutaniko letu likuwe mahali kwenye kila mutu anajisikia kuwa salama.

SHERIA YENYE KUKAZIA HAKI

15-17. (a) Namna gani matendo ya Yesu ilifunua namna aliona haki? (b) Namna gani tunaweza kumuiga Yesu?

15 Wakati neno “haki” linatumiwa katika Biblia, kwa kawaida linamaanisha kufanya mambo yenye Mungu anasema kuwa ni sawa na kuifanya bila ubaguzi. Juu ya nini tunaweza kusema kama sheria ya Kristo inakazia haki?

Yesu alitendea wanamuke kwa heshima na kwa upole, kutia ndani wale wenye watu wengine walizarau (Picha hii inapatana na fungu la 16) *

16 Kwanza, fikiria namna matendo ya Yesu ilifunua namna aliona haki. Katika siku zake, viongozi wa dini ya Kiyahudi walikuwa wanachukia watu wenye hawakukuwa Wayahudi, walizarau Wayahudi wa kawaida, na hawakuheshimia wanamuke. Lakini, Yesu alitendea watu wote kwa haki na bila ubaguzi. Hakukataa watu wenye hawakukuwa Wayahudi wenye walionyesha imani kwake. (Mt. 8:5-10, 13) Alihubiria watu wote bila ubaguzi, matajiri na maskini. (Mt. 11:5; Lu. 19:2, 9) Hakutendea hata kidogo wanamuke kwa ukali ao bila huruma. Lakini, alionyesha wanamuke heshima na kuwatendea kwa upole, kutia ndani wale wenye watu wengine walizarau.​—Lu. 7:37-39, 44-50.

17 Mambo yenye tunajifunza: Tunaweza kumuiga Yesu kwa kutendea wengine bila ubaguzi na kuhubiria watu wote wenye kuwa tayari kusikiliza, bila kuangalia hali yao ya maisha ao dini yao. Wanaume Wakristo wanaiga mufano wake kwa kutendea wanamuke kwa heshima. Wakati tunafanya mambo kama ile, tunatii sheria ya Kristo.

18-19. Yesu alifundisha nini juu ya haki, na tunajifunza mambo gani kupitia mafundisho yake?

18 Pili, fikiria mambo yenye Yesu alifundisha juu ya haki. Alifundisha kanuni zenye zingesaidia wanafunzi wake watendee wengine kwa haki. Kwa mufano, fikiria kanuni yenye kusema kama tunapaswa kutendea wengine namna tunapenda watutendee. (Mt. 7:12) Sisi wote tunapenda kutendewa kwa haki. Kwa hiyo, tunapaswa kutendea wengine kwa haki. Kama tunafanya vile, hilo linaweza kuwachochea watutendee kwa haki. Halafu kama tumetendewa bila haki? Yesu alifundisha wanafunzi wake watumainie kama Yehova ‘atahakikisha kuwa haki imefanywa kwa ajili ya [wale] wenye wanamulilia muchana na usiku.’ (Lu. 18:6, 7) Kwa kweli, ile maneno inatoa ahadi hii: Mungu wetu mwenye haki anajua magumu yote yenye tunapambana nayo katika siku hizi za mwisho, na atahakikisha kuwa haki imefanywa kwa ajili yetu kwa wakati wake wenye kufaa.​—2 Te. 1:6.

19 Mambo yenye tunajifunza: Wakati tunafuata kanuni zenye Yesu alifundisha, tutatendea wengine kwa haki. Na kama tumetendewa bila haki katika ulimwengu wa Shetani, tunaweza kupata faraja kwa kujua kama Yehova atahakikisha kuwa haki imefanywa kwa ajili yetu.

NAMNA GANI WALE WENYE KUWA NA MAMLAKA WANAPASWA KUTENDEA WENGINE?

20-21. (a) Namna gani wale wenye kuwa na mamlaka wanapaswa kutendea wengine? (b) Namna gani bwana anaweza kuonyesha upendo wa kujitoa, na namna gani baba anapaswa kutendea watoto wake?

20 Chini ya sheria ya Kristo, namna gani wale wenye kuwa na mamlaka wanapaswa kutendea wengine? Kwa sababu sheria hiyo inategemea upendo, wale wenye kuwa na mamlaka wanapaswa kutendea kwa heshima na kwa upendo wale wenye kuwa chini ya uongozi wao. Wanapaswa kukumbuka kama Kristo anapenda tuonyeshe upendo katika mambo yote yenye tunafanya.

21 Katika familia. Bwana anapaswa kupenda bibi yake “kama vile Kristo anatendea kutaniko.” (Efe. 5:25, 28, 29) Bwana anapaswa kuiga upendo wa kujitoa wa Kristo kwa kutanguliza mahitaji ya bibi yake, kuliko kutanguliza mahitaji yake mwenyewe. Wanaume fulani wanaweza kuona kama ni vigumu kuonyesha upendo kama huo, pengine kwa sababu mahali kwenye walikomalia, watu hawakuona kuwa ni jambo la maana kutendea wengine kwa haki na kwa upendo. Inaweza kuwa vigumu kwao kubadilisha tabia za mubaya, lakini wanapaswa kufanya ile mabadiliko ili watii sheria ya Kristo. Kama bwana anaonyesha upendo wa kujitoa, bibi yake atakuwa tayari kumuheshimia. Baba mwenye kupenda kabisa watoto wake hawezi hata kidogo kuwaumiza kupitia maneno ao matendo yake. (Efe. 4:31) Lakini, anaonyesha kama anapenda watoto wake na kuwafurahia, na hilo linawafanya wajisikie kuwa salama. Watoto wanakuwa tayari kupenda na kutumainia baba kama huyo.

22. Kama vile 1 Petro 5:1-3 inaonyesha, “kondoo” ni wa nani, na namna gani wanapaswa kutendewa?

22 Katika kutaniko. Wazee wanapaswa kukumbuka kama “kondoo” hawako wao. (Yoh. 10:16; soma 1 Petro 5:1-3.) Maneno “kundi la Mungu,” “mbele ya Mungu,” na “uriti wa Mungu” inakumbusha wazee kama kondoo ni wa Yehova. Anapenda kondoo wake watendewe kwa upendo na kwa upole. (1 Te. 2:7, 8) Wazee wenye wanatimiza kwa upendo daraka lao la uchungaji wanakubaliwa na Yehova. Pia, kama wazee wanafanya vile, ndugu na dada zao wanakuwa tayari kuwapenda na kuwaheshimia.

23-24. (a) Wazee wako na daraka gani katika kushugulikia hali zenye kuhusu zambi nzito? (b) Wakati wazee wanashugulikia hali kama hizo, wanapaswa kukumbuka nini?

23 Wazee wako na daraka gani katika kushugulikia hali zenye kuhusu zambi nzito? Daraka la wazee liko tofauti na daraka la waamuzi na wazee wenye walikuwa chini ya Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli. Chini ya Sheria hiyo, wanaume wenye walikuwa na madaraka walipaswa kushugulikia mambo yenye kuhusu ibada kwa Yehova, na walipaswa kushugulikia hali za kukosa kuelewana kati ya watu na makosa makubwa yenye watu walifanya. Lakini chini ya sheria ya Kristo, daraka la wazee ni kushugulikia zambi nzito zenye kuhusiana na ibada ya Yehova. Wanaelewa kama wakubwa wa serikali wako na mamlaka yenye Mungu amewapatia ya kushugulikia hali za kukosa kuelewana kati ya watu na makosa makubwa yenye watu wanafanya. Hilo linatia ndani mamlaka ya kutoa hukumu ya kulipa amande ao kufunga watu katika gereza.​—Ro. 13:1-4.

24 Namna gani wazee wanashugulikia zambi nzito zenye kuhusiana na ibada ya Yehova? Wanatumia Maandiko ili kuchunguza mambo na kukamata maamuzi. Wanaendelea kukumbuka kama upendo njo musingi wa sheria ya Kristo. Upendo unachochea wazee wachunguze jambo hili: Ni mambo gani yenye inapaswa kufanywa ili kusaidia mutu yeyote katika kutaniko mwenye ametendewa mubaya? Kuhusu mutenda-zambi, upendo unachochea wazee wachunguze jambo hili: Ni mwenye kutubu? Tunaweza kumusaidia akuwe tena na urafiki muzuri pamoja na Yehova?

25. Habari yenye kufuata itazungumuzia nini?

25 Sisi ni wenye shukrani sana kwa sababu tuko chini ya sheria ya Kristo! Wakati sisi wote tunajikaza sana ili kutii sheria hiyo, tunasaidia kufanya kutaniko likuwe mahali kwenye kila mutu anajisikia kuwa anapendwa, kuwa ni wa maana, na salama. Lakini, tunaishi katika ulimwengu kwenye “watu waovu” wameendelea “kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.” (2 Ti. 3:13) Tunapaswa kuendelea kuwa waangalifu. Namna gani kutaniko la Kikristo linaonyesha haki ya Mungu wakati linashugulikia zambi ya kutendea watoto mubaya kingono? Habari yenye kufuata itajibu ulizo hilo.

WIMBO 15 Msifuni Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!

^ fu. 5 Habari hii na habari mbili zenye kufuata ziko kati ya habari ine zenye kuzungumuzia juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova ni Mungu mwenye upendo na haki. Anapenda watu wake watendewe kwa haki na anafariji wale wenye wametendewa bila haki katika ulimwengu huu muovu.

^ fu. 1 Ona habari yenye kichwa “Upendo na Haki Katika Israeli ya Zamani,” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2019.

^ fu. 13 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Upendo wa kujitoa unatuchochea kutanguliza mahitaji na faida za wengine kuliko kutanguliza mahitaji na faida zetu wenyewe. Tuko tayari kuachana na jambo fulani ao kujiima jambo fulani ili kusaidia wengine ao kuwaletea faida.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anamuangalia mujane mwenye mwana wake mumoja tu amekufa. Yesu anachochewa na huruma kisha anafufua kijana huyo mwanaume.

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu anakula chakula mu nyumba ya Mufarisayo mumoja mwenye kuitwa Simoni. Mwanamuke mumoja, pengine kahaba, ananawisha Yesu miguu na machozi yake, anapanguza miguu hiyo na nywele zake, na anamwangia mafuta kwenye miguu ya Yesu. Simoni hafurahie ile mambo yenye mwanamuke huyo anafanya, lakini Yesu anamutetea.