Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 23

“Mufanye Angalisho ili Mutu Yeyote Asiwakamate Mateka”!

“Mufanye Angalisho ili Mutu Yeyote Asiwakamate Mateka”!

“Mufanye angalisho ili mutu yeyote asiwakamate mateka kupitia filozofia na udanganyifu wa bure kulingana na desturi ya wanadamu.”​—KOL. 2:8.

WIMBO 96 Kitabu cha Mungu Ni Hazina

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kulingana na Wakolosai 2:4, 8, namna gani Shetani anajaribu kukamata mateka akili yetu?

SHETANI anapenda kutufanya tumuache Yehova. Ili kutimiza muradi wake, anajaribu kukamata mateka akili yetu, ni kusema, kugeuza mawazo yetu na kutufanya tuanze kuwaza kama yeye. Anachochea tamaa zetu ili kujaribu kutushawishi ao kutudanganya tumufuate.​—Soma Wakolosai 2:4, 8.

2-3. (a) Juu ya nini tunapaswa kutii onyo lenye kupatikana katika Wakolosai 2:8? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Tuko kabisa katika hatari kubwa ya kudanganywa na Shetani? Ndiyo! Kumbuka kama Paulo hakuandika onyo lenye kupatikana mu Wakolosai 2:8 kwa ajili ya watu wenye hawakukuwa Wakristo, lakini ni Wakristo wenye walikuwa wametiwa mafuta kwa roho takatifu njo wenye aliandikia onyo hilo. (Kol. 1:2, 5) Wakristo hao walikuwa katika hatari ya kudanganywa na Shetani wakati huo, leo na sisi tuko katika hatari kubwa sana. (1 Ko. 10:12) Juu ya nini? Shetani ametupwa ku dunia, na anajikaza sana kudanganya watumishi washikamanifu wa Mungu. (Ufu. 12:9, 12, 17) Tena, tunaishi wakati wenye watu waovu na wajanja wanaendelea “kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.”​—2 Ti. 3:1, 13.

3 Katika habari hii, tutazungumuzia namna Shetani anatumia “udanganyifu wa bure” ili kujaribu kuchochea mawazo yetu. Tutaona matendo tatu kati ya “matendo ya ujanja” ya Shetani, ao “mipango [yake] ya mubaya.” (Efe. 6:11; maelezo ya chini) Kisha, katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna ya kuondoa matokeo yoyote ya mubaya yenye pengine ametia mu akili yetu kupitia ujanja wake. Lakini, tuzungumuzie kwanza jambo lenye tunaweza kujifunza juu ya namna Shetani alidanganya Waisraeli kisha wao kuingia mu Inchi ya Ahadi.

WALISHAWISHIWA KUABUDU SANAMU

4-6. Kulingana na Kumbukumbu la Torati 11:10-15, ni ufundi gani wa mupya juu ya mambo ya kulima wenye Waisraeli walipaswa kujifunza wakati waliingia mu Inchi ya Ahadi?

4 Shetani alitumia ujanja ili kushawishi Waisraeli waabudu sanamu. Alifanya vile namna gani? Alijua kama walikuwa na lazima ya chakula, kwa hiyo alijaribu kutumia jambo hilo ili kuwachochea wafanye mambo yenye alipenda. Wakati Waisraeli waliingia mu Inchi ya Ahadi, walipaswa kubadilisha ufundi wao wa kukomalisha chakula. Wakati Waisraeli walikuwa mu inchi ya Misri, walikuwa wanashota maji mu Muto Nile na kuimwangia mu mashamba yao. Lakini, mu Inchi ya Ahadi, hamukukuwa muto mukubwa; ili kukomalisha chakula chao, walikuwa na lazima ya maji ya mvua na pia maji ya umande. (Soma Kumbukumbu la Torati 11:10-15; Isa. 18:4, 5) Kwa hiyo, Waisraeli walipaswa kujifunza ufundi wa mupya juu ya mambo ya kulima. Haikukuwa mwepesi kufanya vile juu watu wengi kati ya wale wenye walikuwa na ufundi mu mambo ya kulima walikuwa wamekufa mu jangwa.

Namna gani Shetani aliweza kubadilisha mawazo ya Waisraeli wenye walikuwa walimaji? (Picha hii inapatana na fungu la 4-6) *

5 Yehova alifasiria watu wake kama hali zao zilikuwa zimebadilika. Kisha, aliwapatia angalisho lenye kufuata, lenye linaweza kuonekana kwanza kuwa halipatane na mambo ya kulima. Aliwaambia hivi: “Mukuwe waangalifu ili musiache mioyo yenu ishawishiwe kupotoka na kuabudu miungu mingine na kuiinamia.” (Kum. 11:16, 17) Juu ya nini Yehova aliwapatia angalisho juu ya kuabudu miungu ya uongo wakati alikuwa anazungumuzia kujifunza ufundi wa mupya juu ya mambo ya kulima?

6 Yehova alijua kama Waisraeli wangeshawishiwa kuendea wapagani wenye walikuwa wanawazunguka ili kujifunza ufundi fulani wa mupya juu ya mambo ya kulima mashamba. Kwa kweli, majirani wao walikuwa na uzoefu zaidi kuwapita, na watu wa Mungu wangejifunza ufundi mbalimbali wa maana kutoka kwao, lakini kulikuwa hatari. Walimaji Wakanaani walikuwa wanamuabudu Baali, na mawazo yao ilichochewa na mambo yenye walikuwa wanaamini juu ya Baali. Waliamini kama Baali njo mwenye anga na njo mwenye anapatia watu mvua. Yehova hakupenda watu wake wadanganywe na imani hizo za uongo. Lakini, mara kwa mara, Waisraeli walichagua kumuabudu Baali. (Hes. 25:3, 5; Amu. 2:13; 1 Fa. 18:18) Sasa, ona namna Shetani aliwezaka kukamata Waisraeli mateka.

UFUNDI TATU WENYE SHETANI ALITUMIA ILI KUKAMATA WAISRAELI MATEKA

7. Namna gani imani ya Waisraeli ilijaribiwa wakati waliingia mu Inchi ya Ahadi?

7 Ufundi wa kwanza wenye Shetani alitumia ilikuwa kuchochea tamaa ya kawaida ya kupenda mvua inyeshe ili kulowanisha udongo. Mvua ilikuwa kidogo sana mu Inchi ya Ahadi kuanzia mwisho wa Mwezi wa 4 mupaka Mwezi wa 9 kila mwaka. Ili Waisraeli waishi na wapate mavuno ya mingi, walikuwa na lazima ya mvua yenye, kwa kawaida, ilikuwa inaanza mu Mwezi wa 10 hivi. Shetani alidanganya Waisraeli waamini kama ili kupata mavuno ya mingi, walipaswa kufuata desturi za majirani wao wapagani. Majirani hao waliamini kama ili wapate mvua yenye walikuwa nayo lazima, walipaswa kufanya desturi fulani ili miungu yao itende na kuwapatia mvua. Waisraeli wenye hawakukuwa na imani katika Yehova, waliamini kama ile njo ilikuwa njia moja tu ya kuwasaidia ili kipwa kisiendelee sana, kwa hiyo, walifuata desturi za wapagani za kuabudu Baali, mungu wa uongo.

8. Ni ufundi gani wa pili wenye Shetani alitumia? Fasiria.

8 Shetani alitumia ufundi wa pili ili kudanganya Waisraeli. Alichochea tamaa zao za mubaya. Wakati watu wa mataifa ya wapagani walikuwa wanaabudu miungu yao, walikuwa wanafanya matendo machafu yenye kuchukiza sana. Aina hiyo ya ibada chafu ilitia ndani ukahaba wa wanamuke na wa wanaume kwenye hekalu. Wapagani hao waliruhusu tendo la mwanaume kulala na mwanaume na mwanamuke kulala na mwanamuke na aina zingine za uasherati na waliona ile matendo kuwa yenye kukubalika! (Kum. 23:17, 18; 1 Fa. 14:24) Waliamini kama ile matendo ilichochea miungu yao ifanye udongo utoe chakula sana. Waisraeli wengi walivutiwa na desturi hizo za uasherati za wapagani na walijiacha watumikie miungu ya uongo. Kwa kweli, Shetani alikuwa amewakamata mateka.

9. Kulingana na Hosea 2:16, 17, namna gani Shetani alifanya Waisraeli wasahau Yehova ni nani kabisa?

9 Shetani alitumia ufundi wa tatu. Alifanya Waisraeli wasahau Yehova ni nani kabisa. Katika siku za nabii Yeremia, Yehova alisema kama manabii wa uongo walifanya watu wake wasahau jina lake “kwa sababu ya Baali.” (Yer. 23:27) Inaonekana kabisa kama watu wa Mungu waliacha kutumia jina la Yehova na kuliko kutumia jina hilo, walitumia jina Baali, lenye kumaanisha “Mumiliki (mwenye mutu ao kitu fulani)” ao “Bwana.” Hilo lilifanya ikuwe nguvu kwa Waisraeli kujua tofauti kati ya Yehova na Baali, kwa hiyo, walianza kuchanga desturi za ibada ya Baali na ibada ya Yehova.​—Soma Hosea 2:16, 17 na maelezo ya chini.

UFUNDI MBALIMBALI WENYE SHETANI ANATUMIA LEO

10. Ni ufundi gani mbalimbali wenye Shetani anatumia leo?

10 Leo, Shetani anatumia ufundi uleule wenye alitumia zamani. Anakamata watu mateka kwa kuchochea tamaa zao za kawaida, kwa kuchochea uasherati, na kufanya watu wasahau Yehova ni nani kabisa. Tuzungumuzie kwanza ufundi huo wa mwisho.

11. Namna gani Shetani anafanya watu wasahau Yehova ni nani kabisa?

11 Shetani anafanya watu wasahau Yehova ni nani kabisa. Kisha kifo cha mitume wa Yesu, watu fulani wenye walijiita kuwa Wakristo walianza kueneza mafundisho ya uongo. (Mdo. 20:29, 30; 2 Te. 2:3) Waasi-imani hao walianza kusahau Mungu mumoja tu wa kweli ni nani kabisa. Kwa mufano, waliacha kutumia jina la Mungu katika maandishi yao ya Biblia na mahali pa jina hilo walitumia jina “Bwana” ao majina ingine ya cheo. Wakati walitosha jina la pekee la Mungu na kutumia jina “Bwana,” walifanya mutu mwenye kusoma Biblia ashindwe kuona tofauti yenye kuwa kati ya Yehova na “mabwana” wengine wenye kuzungumuziwa katika Maandiko. (1 Ko. 8:5) Walitumia jina “Bwana” ili kuzungumuzia Yehova na Yesu, na hilo lilifanya ikuwe vigumu kuelewa kama Yehova na Mwana wake ni watu tofauti. (Yoh. 17:3) Muvurugo huo ulifanya waanzishe fundisho la Utatu, lenye halipatikane katika Neno la Mungu. Kwa sababu ya fundisho hilo, watu wengi wanamuona Mungu kuwa fumbo na wanaamini kama hatuwezi kumujua. Huo ni uongo kabisa!​—Mdo. 17:27.

Namna gani Shetani ametumia dini ya uongo ili kuchochea tamaa za mubaya? (Picha hii inapatana na fungu la 12) *

12. Dini ya uongo imechochea nini, na hilo limeleta matokeo gani kulingana na andiko la Waroma 1:28-31?

12 Shetani anachochea tamaa za mubaya. Wakati wa Waisraeli wa zamani, Shetani alitumia dini ya uongo ili kuchochea uasherati. Na leo anafanya vile. Dini ya uongo inaachilia na hata kuchochea uasherati. Kwa hiyo, watu wengi wenye wanasema kama wanamutumikia Mungu wameacha kufuata kanuni zake za mwenendo muzuri zenye kuwa wazi. Mutume Paulo alionyesha matokeo ya jambo hilo katika barua yenye aliandikia Waroma. (Soma Waroma 1:28-31.) Kati ya “mambo yenye hayafae” kuko aina zote za uasherati, kutia ndani tendo la mwanaume kulala na mwanaume na mwanamuke kulala na mwanamuke. (Ro. 1:24-27, 32; Ufu. 2:20) Ni jambo la maana sana tushikamane na mafundisho ya Biblia yenye kuwa wazi!

13. Ni ufundi gani mwingine wenye Shetani anatumia?

13 Shetani anachochea tamaa za kawaida. Tuko na tamaa ya kawaida ya kujifunza ufundi wenye unaweza kutusaidia kutimiza mahitaji yetu wenyewe na mahitaji ya watu wa familia zetu. (1 Ti. 5:8) Mara mingi, tunaweza kupata ufundi huo kwa kuenda ku masomo ao kwa kujifunza kwa bidii. Lakini, tunapaswa kuwa waangalifu. Katika inchi za mingi, masomo inafundisha wanafunzi ufundi mbalimbali wa kuwasaidia katika maisha na inafundisha hata filozofia ya wanadamu. Wanafunzi wanachochewa wakuwe na mashaka ikiwa Mungu iko na wakose kuheshimia Biblia. Wanaambiwa kama fundisho la mageuzi tu njo linatoa maelezo yenye kupatana na akili juu ya namna uzima ulianzaka. (Ro. 1:21-23) Mafundisho kama ile inapinga “hekima ya Mungu.”​—1 Ko. 1:19-21; 3:18-20.

14. Filozofia ya wanadamu inachochea watu waonyeshe nini?

14 Filozofia ya wanadamu inakataa ao kupinga kanuni za Yehova za haki. Haichochee watu waonyeshe sifa za tunda la roho ya Mungu, lakini inawachochea waonyeshe “matendo ya mwili.” (Gal. 5:19-23) Inachochea watu wakuwe na kiburi na majivuno, na hilo linawafanya wakuwe “wenye kujipenda wenyewe.” (2 Ti. 3:2-4) Tabia hizo hazipatane na roho ya unyenyekevu yenye Mungu anapenda watumishi wake wakuwe nayo. (2 Sa. 22:28) Wakristo fulani wenye wameenda ku masomo ya juu wameacha mawazo ya Mungu na kukubali mawazo ya ulimwengu. Tuzungumuzie basi mufano moja wenye kuonyesha namna jambo hilo linaweza kutokea.

Namna gani filozofia ya wanadamu inaweza kuharibu mawazo yetu? (Picha hizi zinapatana na fungu la 14-16) *

15-16. Jambo lenye lilimufikia dada mumoja linakufundisha nini?

15 Dada mumoja mwenye amefanya utumishi wa wakati wote kwa miaka zaidi ya 15 anasema hivi: “Kwa sababu niko Shahidi mwenye kubatizwa, nilikuwa nimesoma na kusikia habari juu ya hatari za kusoma masomo ya juu, lakini nilizarau maonyo kama ile. Niliwaza kama ile mashauri haikunihusu.” Hilo lilimuletea magumu gani? Anasema hivi: “Kujifunza mambo yangu ya masomo kulinikamata wakati na nguvu mingi, kwa hiyo, sikukuwa tena na wakati wa kutosha ili kusali kwa Yehova kama vile nilizoea kufanya, na kwa sababu ya kuchoka sana, sikufurahia tena kuzungumuza na watu juu ya Biblia na kutayarisha muzuri mikutano. Jambo la kufurahisha ni hili: wakati tu nilitambua kama kutumia wakati mingi mu mambo ya masomo ya juu kulikuwa kunaharibu urafiki wangu pamoja na Yehova, niliona kama nilipaswa kuacha. Na nilifanya vile.”

16 Namna gani masomo ya juu ilibadilisha mawazo ya ule dada? Anajibu hivi: “Ninasikia haya kusema kama masomo ya juu yenye nilifuatia ilinifundisha kuchambua-chambua wengine, zaidi sana ndugu na dada zangu, kutazamia wafanye mambo yenye kupita uwezo wao, na kujitenga nao. Iliomba wakati ili niachane kabisa na tabia hizo. Kupitia jambo hilo, niliona kama ni hatari sana kuzarau maonyo yenye Baba yetu wa mbinguni anatupatia kupitia tengenezo lake. Yehova alinijua muzuri kupita vile nilijijua mimi mwenyewe. Ingekuwa muzuri kama ningemusikiliza!”

17. (a) Tunapaswa kuwa na azimio gani? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Uazimie kabisa ili usikamatwe mateka hata siku moja “kupitia filozofia na udanganyifu wa bure” wa ulimwengu wa Shetani. Usiache hata kidogo Shetani akudanganye kupitia ufundi wake. (1 Ko. 3:18; 2 Ko. 2:11) Usimuache hata kidogo akufanye usahau Yehova ni nani kabisa. Utii kanuni za juu za Yehova za mwenendo muzuri. Na usiache Shetani akudanganye uzarau mashauri ya Yehova. Lakini, utafanya nini ukitambua kama mawazo ya ulimwengu imekwisha kukuambukia? Habari yenye kufuata itaonyesha namna Neno la Mungu linaweza kutusaidia kupindua mawazo na tabia zenye ‘zimetia mizizi kabisa.’​—2 Ko. 10:4, 5.

WIMBO 49 Kufurahisha Moyo wa Yehova

^ fu. 5 Shetani iko fundi wa kudanganya watu. Amedanganya watu wengi waamini kama wako huru, hata kama kwa kweli wako wafungwa wake. Habari hii itazungumuzia ufundi mbalimbali wenye Shetani anatumia ili kudanganya watu.

^ fu. 48 MAFASIRIO YA PICHA: Waisraeli wanajiunga na Wakanaani na wanashawishiwa kuabudu Baali na kufanya uasherati.

^ fu. 51 MAFASIRIO YA PICHA: Tangazo la kanisa lenye kukubali tendo la mwanaume kulala na mwanaume na mwanamuke kulala na mwanamuke.

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Dada kijana amejiandikisha ku masomo ya juu. Yeye na wanafunzi wenzake wamedanganywa na wazo la mwalimu, lenye kuonyesha kama sayansi na teknolojia vinaweza kumaliza magumu ya watu. Kisha, wakati iko ku Jumba la Ufalme, hapendezwe na anachambua-chambua wengine.