Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 25

Umutegemee Yehova Wakati Uko na Mahangaiko

Umutegemee Yehova Wakati Uko na Mahangaiko

“Mimi ni . . . mwenye mahangaiko mengi.”​—1 SA. 1:15.

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, Rafiki Yangu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini tunapaswa kutii onyo la Yesu?

KATIKA unabii wake juu ya siku za mwisho, Yesu alisema hivi: “Mujiangalie ninyi wenyewe ili mioyo yenu isilemewe hata kidogo na . . . mahangaiko ya maisha,” ni kusema, mahangaiko ya maisha ya kila siku. (Lu. 21:34) Tunapaswa kutii onyo hilo. Juu ya nini? Leo, tunapaswa kupiganisha magumu ileile yenye kuleta mahangaiko, yenye kila mutu anapiganisha.

2. Ndugu na dada zetu wanapiganisha magumu gani yenye kuleta mahangaiko?

2 Wakati fulani, tunapaswa kupiganisha kwa wakati uleule magumu mbalimbali yenye kuleta mahangaiko. Ona mifano yenye kufuata. Shahidi mumoja mwenye kuitwa John, * mwenye kuwa na ugonjwa wa mufumo wa neva (sclérose), alihuzunika sana wakati bibi yake alimuacha kisha kufanya pamoja naye miaka 19 katika ndoa. Kisha, watoto wake wawili wanamuke wakaacha kumutumikia Yehova. Bwana mumoja mwenye kuitwa Bob na bibi yake Linda, walipiganisha magumu mbalimbali yenye kuwa tofauti na ile ya John. Wote wawili walipoteza kazi yao, na kisha walilazimika kutoka mu nyumba yenye walikuwa wanaishi ndani na kuenda kuishi mu nyumba ya kidogo. Zaidi ya ile magumu, Linda alivumbuliwa na ugonjwa hatari wa moyo na ugonjwa mwingine ulianza kuharibu uwezo wa mwili wake wa kujilinda na magonjwa.

3. Kulingana na Wafilipi 4:6, 7, tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

3 Tunaweza kuwa hakika kama Yehova, Muumbaji wetu na Baba yetu mwenye upendo, anaelewa namna tunajisikia wakati tuko na mahangaiko. Na anapenda kutusaidia tupiganishe magumu yenye tuko nayo. (Soma Wafilipi 4:6, 7.) Neno la Mungu linazungumuzia habari za mingi zenye kuonyesha magumu yenye watumishi wake walivumilia. Linaonyesha pia namna Yehova aliwasaidia kupiganisha hali hizo zenye kuleta mahangaiko. Tuzungumuzie basi mifano ya watu fulani.

ELIYA ALIKUWA “MUTU MWENYE HISIA KAMA ZETU”

4. Eliya alipata magumu gani, na alijisikia namna gani juu ya Yehova?

4 Eliya alimutumikia Yehova katika nyakati ngumu na alipata magumu makali. Ahabu, mufalme mumoja kati ya wafalme wa Israeli wenye hawakukuwa waaminifu, alioa Yezebeli, mwanamuke muovu mwenye alikuwa anaabudu Baali. Wote wawili walieneza ibada ya Baali katika inchi na waliua manabii wengi wa Yehova. Eliya aliweza kuponyoka. Aliendelea kupata chakula wakati wa njaa kali kwa sababu alimutegemea Yehova. (1 Fa. 17:2-4, 14-16) Tena, alimutegemea Yehova wakati alipingana na manabii wa Baali na watu wengine wenye walikuwa wanamuabudu Baali. Alitia moyo Waisraeli wamutumikie Yehova. (1 Fa. 18:21-24, 36-38) Eliya alijionea mambo mingi yenye ilimuhakikishia kama Yehova alikuwa anamutegemeza wakati huo wa mahangaiko.

Yehova alituma malaika ili kumusaidia Eliya apate nguvu tena (Picha hii inapatana na fungu la 5-6) *

5-6. Kulingana na andiko la 1 Wafalme 19:1-4, Eliya alijisikia namna gani, na namna gani Yehova alimuonyesha kama alikuwa anamupenda?

5 Soma 1 Wafalme 19:1-4. Lakini, Eliya aliogopa wakati Malkia Yezebeli alisema kama atamuua. Kwa hiyo, alikimbilia katika eneo la Beer-sheba. Alivunjika moyo sana mupaka “akaomba akufe.” Ni nini ilifanya Eliya ajisikie vile? Alikuwa mutu mwenye hakamilike, “mutu mwenye hisia kama zetu.” (Yak. 5:17) Pengine alikuwa na mahangaiko mingi na alijisikia kuwa mwenye kuchoka sana. Pengine Eliya aliwaza kama bidii yenye alikuwa amefanya ili kuendelesha ibada safi ilikuwa ya bure, aliwaza kama mambo iliendelea kuharibika katika Israeli, na kama yeye tu njo mutumishi wa Yehova mwenye alikuwa amebakia. (1 Fa. 18:3, 4, 13; 19:10, 14) Namna nabii huyo muaminifu alitenda inaweza kutushangaza. Lakini Yehova alielewa namna Eliya alikuwa anajisikia.

6 Yehova hakumukaripia Eliya kwa sababu alisema namna alikuwa anajisikia. Lakini, alimusaidia Eliya apate nguvu tena. (1 Fa. 19:5-7) Kisha, Yehova alimuonyesha Eliya nguvu zake za ajabu ili kumusaidia kwa upendo abadilishe mawazo yake. Yehova alimuambia kama alikuwa angali na watu 7 000 katika Israeli wenye walikataa kumuabudu Baali. (1 Fa. 19:11-18) Kwa kumusaidia katika njia hizo zenye kufaa, Yehova alimuonyesha Eliya kama alikuwa anamupenda.

NAMNA YEHOVA ATATUSAIDIA

7. Namna Yehova alimusaidia Eliya inatutia moyo namna gani?

7 Uko unapiganisha hali fulani yenye kuleta mahangaiko? Tunafarijiwa sana kujua kama Yehova alielewa namna Eliya alikuwa anajisikia! Tunatiwa moyo kujua kama anaelewa magumu yetu. Anajua mipaka yetu, na hata anajua mawazo yetu na namna tunajisikia. (Zb. 103:14; 139:3, 4) Kama tunamuiga Eliya kwa kumutegemea Yehova, atatusaidia tupiganishe magumu yenye kutuletea mahangaiko.​—Zb. 55:22.

8. Namna gani Yehova atakusaidia upiganishe mahangaiko?

8 Mahangaiko inaweza kukufanya uwaze kama hali yako haitabadilika hata kidogo, na inaweza kukufanya uvunjike moyo. Kama hilo linakufikia, kumbuka kama Yehova atakusaidia upiganishe mahangaiko. Atakusaidia namna gani? Anakuomba umuambie mahangaiko yako. Na atajibu vilio vyako vya kuomba musaada. (Zb. 5:3; 1 Pe. 5:7) Kwa hiyo, sali kwa Yehova tena na tena juu ya magumu yako. Hatasema na wewe moja kwa moja kama vile alisema na Eliya, lakini atasema na wewe kupitia Neno lake, Biblia, na kupitia tengenezo lake. Habari zenye unasoma katika Biblia zinaweza kukufariji na kukupatia tumaini. Pia, ndugu na dada zako wanaweza kukutia moyo.​—Ro. 15:4; Ebr. 10:24, 25.

9. Rafiki mwenye tunatumainia anaweza kutusaidia namna gani?

9 Yehova alimuambia Eliya apatie Elisha madaraka yake fulani. Kwa kufanya vile, Yehova alimupatia Eliya rafiki mwenye alikuwa naye lazima kabisa, mwenye angemusaidia kupiganisha mahangaiko yake. Sisi pia, wakati tunamuambia rafiki mwenye tunatumainia namna tunajisikia, anaweza kutusaidia kupiganisha mahangaiko yetu. (2 Fa. 2:2; Mez. 17:17) Kama unaona kuwa hauna mutu mwenye unaweza kuambia namna unajisikia, usali kwa Yehova akusaidie kupata Mukristo fulani mwenye kukomaa kiroho mwenye anaweza kukutia moyo.

10. (a) Namna gani jambo lenye lilimufikia Eliya linatusaidia tukuwe na tumaini kama sisi pia tunaweza kuvumilia? (b) Namna gani ahadi yenye kuwa katika Isaya 40:28, 29 inaweza kutusaidia?

10 Yehova alimusaidia Eliya apiganishe mahangaiko yake na amutumikie kwa uaminifu kwa miaka mingi. Mufano wa Eliya unatupatia tumaini. Wakati fulani, tunaweza kupiganisha mahangaiko makali yenye inaweza kutufanya tuchoke kimwili na kiakili. Lakini, kama tunamutegemea Yehova, atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kumutumikia.​—Soma Isaya 40:28, 29.

HANA, DAUDI, NA MUANDIKAJI MUMOJA WA ZABURI WALIMUTEGEMEA YEHOVA

11-13. Wakati wa zamani, mahangaiko ilifanya watumishi tatu wa Mungu wajisikie namna gani?

11 Watu wengine wenye kuzungumuziwa mu Biblia walipiganisha pia mahangaiko makali. Kwa mufano, Hana alivumilia haya ya kukosa kuzaa na pia alivumilia kuchokozwa mubaya na bibi-mushindani wake. (1 Sa. 1:2, 6) Mahangaiko makali yenye Hana alikuwa nayo ilimufanya akuwe mwenye uchungu sana, na hilo lilikuwa linamufanya alie na kukosa hamu ya kula chakula.​—1 Sa. 1:7, 10.

12 Wakati fulani, Mufalme Daudi alikuwa na mahangaiko ya mingi sana. Fikiria magumu yenye alipata. Alijisikia kuwa mwenye hatia kabisa kwa sababu ya makosa ya mingi yenye alikuwa amefanya. (Zb. 40:12) Mwana wake mupendwa Absalomu alimuasi, na jambo hilo lilimuletea Absalomu kifo. (2 Sa. 15:13, 14; 18:33) Na rafiki mumoja wa sana wa Daudi alimusaliti. (2 Sa. 16:23–17:2; Zb. 55:12-14) Zaburi za mingi kati ya zaburi zenye Daudi aliandika, zinaonyesha namna alikuwa anajisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo na pia namna alimutegemea Yehova kabisa.​—Zb. 38:5-10; 94:17-19.

Ni nini ilimusaidia muandikaji wa zaburi apate tena furaha ya kumutumikia Yehova? (Picha hii inapatana na fungu la 13-15) *

13 Kisha wakati fulani, muandikaji mumoja wa zaburi alianza kutamani maisha ya watu waovu. Pengine alikuwa muzao wa Mulawi Asafu, na alitumikia mu “patakatifu pakubwa pa Mungu.” Muandikaji huyo wa zaburi alikuwa na mahangaiko yenye ilimufanya akose furaha na asikuwe mwenye kutosheka. Hata alianza kuona kama baraka zenye alipata kwa kumutumikia Mungu hazikutosha.​—Zb. 73:2-5, 7, 12-14, 16, 17, 21.

14-15. Mifano ya watu tatu wenye kuzungumuziwa mu Biblia wenye walimuomba Yehova musaada inatufundisha nini?

14 Watumishi hao tatu wa Yehova wenye tunatoka kuzungumuzia, wote walimutegemea Yehova ili awasaidie. Walikuwa wanasali kwa bidii kwa Yehova ili kumuambia mahangaiko yao. Walizungumuza naye waziwazi ili kumuonyesha juu ya nini walikuwa na mahangaiko sana. Na waliendelea kuenda mahali pa kumuabudia Yehova.​—1 Sa. 1:9, 10; Zb. 55:22; 73:17; 122:1.

15 Kwa huruma, Yehova alimusaidia kila mumoja wao. Hana alipata amani ya akili. (1 Sa. 1:18) Daudi aliandika hivi: “Magumu ya mwenye haki ni mengi, lakini Yehova anamuokoa katika magumu hayo yote.” (Zb. 34:19) Na kisha wakati fulani, ule muandikaji wa zaburi alijisikia kuwa Yehova alikuwa ‘ameshika mukono [wake] wa kuume,’ na kumuongoza kwa shauri lenye upendo. Aliimba hivi: “Lakini mimi, kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri kwangu. Nimemufanya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova kuwa kimbilio langu.” (Zb. 73:23, 24, 28) Ile mifano inatufundisha nini? Wakati fulani, tutapata magumu makali sana ya kutuletea mahangaiko. Lakini tunaweza kuishinda kama tunafikiri sana juu ya namna Yehova amesaidia wengine, kama tunamutegemea kupitia sala, na kama tunamutii kwa kufanya mambo yenye anatuomba.​—Zb. 143:1, 4-8.

UMUTEGEMEE YEHOVA ILI UPIGANISHE MUZURI MAHANGAIKO

Kwanza, dada mumoja aliona kuwa alikuwa anajitenga na wengine, lakini mambo ilibadilika wakati alitafuta njia za kusaidia wengine (Picha hizi zinapatana na fungu la 16-17)

16-17. (a) Juu ya nini hatupaswe kujitenga na wengine? (b) Ni nini inaweza kutusaidia kupata nguvu tena?

16 Ile mifano tatu inatufundisha jambo lingine la maana: hatupaswe kujitenga na Yehova na watu wake. (Mez. 18:1) Nancy, mwenye alipiganisha mahangaiko makali wakati bwana yake alimuacha, anasema hivi: “Siku za mingi, sikupenda kuona mutu yeyote ao kuzungumuza na mutu yeyote. Lakini, kadiri niliendelea kujitenga na wengine, niliendelea kuwa na huzuni zaidi.” Mambo ilibadilika wakati Nancy alitafuta njia za kusaidia wengine wenye walikuwa na magumu. Anasema hivi: “Nilikuwa ninasikiliza wakati wengine walikuwa wananielezea magumu yao. Niliona kama wakati nilisikilia wengine huruma, sikujifikiria sana mimi mwenyewe na magumu yangu.”

17 Kuenda ku mikutano ya kutaniko kunaweza kutusaidia kupata nguvu tena. Wakati tuko ku mikutano, tunamupatia Yehova nafasi zingine za kujionyesha kuwa ‘musaidizi na mufariji’ wetu. (Zb. 86:17) Ku mikutano, anatutia nguvu kupitia roho yake takatifu, Neno lake, na watu wake. Ku mikutano, tunaweza kupata nafasi ya kuwa na “ubadilishanaji wa kitia-moyo.” (Ro. 1:11, 12) Dada mumoja mwenye kuitwa Sophia alisema hivi: “Yehova na ndugu na dada zangu walinisaidia kuvumilia. Na jambo lenye niliona kuwa la maana zaidi ilikuwa mikutano ya kutaniko. Nimetambua kama wakati ninajitoa zaidi mu kazi ya kuhubiri na kazi za kutaniko, ninapata nguvu zaidi ili kupiganisha mahangaiko na wasiwasi.”

18. Wakati tunajisikia kuwa wenye kuvunjika moyo, Yehova anaweza kutupatia nini?

18 Wakati tunajisikia kuwa wenye kuvunjika moyo, tukumbuke basi kama Yehova hatuahidi tu kuwa atamaliza mahangaiko wakati wenye kuja, lakini pia anaahidi kama atatusaidia kupiganisha mahangaiko yetu leo. Anatupatia “hamu na pia nguvu” ya kushinda mawazo ya kujisikia kuwa wenye kuvunjika moyo na kukosa tumaini.​—Flp. 2:13.

19. Andiko la Waroma 8:37-39 linatuhakikishia nini?

19 Soma Waroma 8:37-39. Mutume Paulo anatuhakikishia kama hakuna kitu chenye kinaweza kututenganisha na upendo wa Mungu. Namna gani tunaweza kusaidia ndugu na dada zetu wenye wako wanajikaza kupiganisha mahangaiko? Habari yenye kufuata itazungumuzia namna tunaweza kumuiga Yehova kwa kuonyesha huruma na kutegemeza ndugu na dada zetu wakati wako na mahangaiko.

WIMBO 44 Sala ya Mtu wa Hali ya Chini

^ fu. 5 Mahangaiko mingi ao yenye kuendelea inaweza kutuletea matokeo ya mubaya kimwili na kiakili. Namna gani Yehova anaweza kutusaidia? Tutazungumuzia namna Yehova alimusaidia Eliya apiganishe mahangaiko. Mifano ya watu wengine wenye kuzungumuziwa mu Biblia itatuonyesha namna tunaweza kumuomba Yehova musaada wakati tuko na mahangaiko.

^ fu. 2 Majina imebadilishwa katika habari hii.

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Kwa upole, malaika wa Yehova anamuamusha Eliya na kumupatia mukate na maji.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Muandikaji wa zaburi mwenye pengine alikuwa muzao wa Asafu, anafurahia kuandika zaburi na kuimba pamoja na Walawi wenzake.