Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 27

Ujitayarishe Leo kwa Ajili ya Mateso

Ujitayarishe Leo kwa Ajili ya Mateso

“Wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.”​—2 TI. 3:12.

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini tunapaswa kujitayarisha kwa ajili ya mateso?

KATIKA usiku wenye ulitangulia kifo chake, Bwana wetu Yesu alisema kama wale wote wenye wanaamua kuwa wanafunzi wake watachukiwa. (Yoh. 17:14) Kuanzia wakati huo mupaka leo, watu wenye kupinga ibada ya kweli wametesa Wakristo waaminifu Mashahidi wa Yehova. (2 Ti. 3:12) Kadiri mwisho wa ulimwengu huu unaendelea kukaribia, tunatazamia kama maadui wetu watatupinga hata zaidi.​—Mt. 24:9.

2-3. (a) Tunapaswa kujua nini juu ya woga? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Tunaweza kufanya nini leo ili tukuwe tayari kuvumilia mateso? Haiko lazima tuwazie mambo yote ya mubaya yenye inaweza kutupata. Kama tunafanya vile, tunaweza kuogopa na kuhangaika sana. Tunaweza kuruhusu ile mambo yenye tunawazia ituogopeshe sana na tunaweza kuacha kumutumikia Yehova hata mbele mateso yoyote itupate. (Mez. 12:25; 17:22) Woga ni silaha yenye nguvu sana yenye “adui [yetu], Ibilisi,” anatumia ili kutupiganisha. (1 Pe. 5:8, 9) Tunaweza kufanya nini leo ili tujitayarishe kuvumilia mateso?

3 Katika habari hii, tutazungumuzia namna tunaweza kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova, na juu ya nini ni jambo la maana tufanye vile leo. Pia, tutazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya ili tukuwe na uhodari zaidi. Na kisha, tutaona namna tunaweza kuvumilia chuki ya watu wenye kutupinga.

MAMBO YA KUFANYA ILI KUTIA NGUVU URAFIKI WAKO PAMOJA NA YEHOVA

4. Kulingana na Waebrania 13:5, 6, tunapaswa kuwa hakika na jambo gani, na juu ya nini?

4 Ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na kama hatakuacha hata kidogo. (Soma Waebrania 13:5, 6.) Kumepita miaka mingi tangu wakati gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Mutu mwenye anamujua Mungu muzuri atamutegemea zaidi wakati wa majaribu.” Ile maneno ni ya kweli kabisa! Ili tuweze kuvumilia mateso, tunapaswa kumupenda Yehova na kumutegemea kabisa, hatupaswe kuwa na mashaka hata kidogo kuwa anatupenda.​—Mt. 22:36-38; Yak. 5:11.

5. Ni nini itakusaidia uone kuwa Yehova anakupenda?

5 Usome Biblia kila siku na uko na muradi wa kumukaribia Yehova zaidi. (Yak. 4:8) Wakati unasoma, kazia akili sifa za muzuri za Yehova. Ujikaze kuelewa namna mambo yenye anasema na kufanya inaonyesha kama anakupenda sana. (Kut. 34:6) Inaweza kuwa nguvu kwa watu fulani kuamini kama Mungu anawapenda kwa sababu hakuna mutu mwenye amekwisha kuwaonyesha upendo. Kama uko na ile shida, jaribu kuandika kila siku liste ya mambo yenye kuonyesha namna Yehova amekuonyesha rehema na fazili. (Zb. 78:38, 39; Ro. 8:32) Wakati unafikiria mambo yenye umejionea mu maisha yako na kufikiri sana juu ya mambo yenye umesoma katika Neno la Mungu, inawezekana kabisa kuwa utapata mambo mingi sana yenye Yehova amekufanyia ya kutia ku liste yako. Kama uko mwenye shukrani zaidi juu ya mambo yenye Yehova anafanya, urafiki wako pamoja naye utakuwa wenye nguvu zaidi.​—Zb. 116:1, 2.

6. Kulingana na Zaburi 94:17-19, sala yenye kutoka mu moyo inaweza kukusaidia namna gani?

6 Usali kwa ukawaida. Wazia kijana mudogo mwanaume mwenye baba yake anakumbatia kwa upendo. Kijana huyo anajisikia salama sana na kwa hiyo, anazungumuza waziwazi na baba yake juu ya mambo ya muzuri na ya mubaya yenye ilimufikia siku hiyo. Unaweza kuwa na urafiki wa namna hiyo kama unamukaribia Yehova kila siku kupitia sala yenye kutoka mu moyo. (Soma Zaburi 94:17-19.) Wakati unasali kwa Yehova, “mwanga moyo wako kama maji” na kumuambia Baba yako mwenye upendo mambo yote yenye kukuogopesha na mahangaiko yako yote. (Omb. 2:19) Utapata matokeo gani? Utakuwa na jambo lenye Biblia inaita “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” (Flp. 4:6, 7) Kama unaendelea kusali kwa namna hiyo, utajisikia kuwa karibu zaidi na Yehova.​—Ro. 8:38, 39.

Kuwa na imani yenye nguvu katika Yehova na Ufalme wake kunatusaidia tukuwe na uhodari

Stanley Jones alijitia nguvu kupitia ujuzi wake juu ya Ufalme wa Mungu (Picha hii inapatana na fungu la 7)

7. Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama ahadi zenye Mungu anatoa juu ya Ufalme wake zitatimia?

7 Ukuwe hakika kama ahadi za Ufalme wa Mungu zitatimia. (Hes. 23:19) Kama hauamini kabisa kama ahadi za Mungu zitatimia, itakuwa mwepesi kwa Shetani na watu wake wakuogopeshe. (Mez. 24:10; Ebr. 2:15) Unaweza kufanya nini leo ili ukuwe na imani yenye nguvu katika Ufalme wa Mungu? Utumie wakati ili kujifunza ahadi za Mungu juu ya Ufalme wake na sababu zenye zinaweza kukufanya ukuwe hakika kama zitatimia. Kufanya vile kutakusaidia namna gani? Fikiria mufano wa Stanley Jones, mwenye alifungwa miaka saba mu gereza kwa sababu imani yake. * Ni nini ilimusaidia avumilie kwa uaminifu? Anasema hivi: “Imani yangu ilikuwa yenye nguvu kwa sababu nilikuwa na ujuzi juu ya Ufalme wa Mungu na mambo yenye utafanya, na sikukuwa na mashaka hata kidogo juu ya ile mambo. Kwa hiyo, hakuna mutu mwenye angeweza kunifanya nimuache Yehova.” Kama unaamini kabisa ahadi za Mungu, utamukaribia zaidi na hakuna mutu mwenye atakuogopesha.​—Mez. 3:25, 26.

8. Kama tunafurahia kuhuzuria mikutano, hilo linaonyesha nini? Fasiria.

8 Uhuzurie mikutano ya Kikristo kwa ukawaida. Mikutano inatusaidia tumukaribie Yehova zaidi. Kama tunafurahia kuhuzuria mikutano, hilo linaonyesha kama tutaweza kuvumilia mateso ya wakati wenye kuja. (Ebr. 10:24, 25) Juu ya nini tunasema vile? Kama tunaacha mambo ya kidogo-kidogo ituzuie kuhuzuria mikutano leo, itakuwa namna gani wakati wenye kuja ikiwa tutalazimika kujitia katika hatari ili kukutana pamoja na ndugu na dada zetu? Kwa upande mwingine, kama tunaazimia kabisa kuhuzuria mikutano, hatutaacha wakati watu wenye kutupinga wanajaribu kutufanya tuache kukutana pamoja. Leo njo wakati wa kupenda zaidi mikutano yetu. Kama tunafurahia kuhuzuria mikutano, hakuna upinzani wowote, ao hata sheria ya serikali yenye kukataza kazi yetu, yenye itatufanya tutii wanadamu kuliko kumutii Mungu.​—Mdo. 5:29.

Kuweka katika akili maandiko na nyimbo za Ufalme leo kunaweza kukusaidia wakati wa mateso (Picha hii inapatana na fungu la 9) *

9. Juu ya nini kuweka maandiko katika akili ni njia ya muzuri ya kujitayarisha kwa ajili ya mateso?

9 Uweke katika akili maandiko fulani yenye unapendaka sana. (Mt. 13:52) Pengine akili yako haitakumbuka kwa ukamilifu, lakini Yehova anaweza kutumia roho yake takatifu yenye nguvu ili ikusaidie kukumbuka ile maandiko. (Yoh. 14:26) Ndugu mumoja alifungwa mu gereza la Ujerumani Mashariki na alitiwa katika chumba cha gereza yeye mwenyewe. Ona mambo yenye alisema: “Ilikuwa baraka sana kuona kama wakati huo nilikuwa nimeweka mamia fulani ya maandiko katika akili! Hata kama nilikuwa peke yangu, niliendelea kufikiri sana juu ya habari mbalimbali za Biblia.” Ile maandiko ilisaidia ndugu yetu aendelee kumukaribia Yehova na kuvumilia kwa uaminifu.

(Picha hii inapatana na fungu la 10) *

10. Juu ya nini tunapaswa kuweka nyimbo zetu katika akili?

10 Uweke katika akili nyimbo za kumusifu Yehova na uzoee kuziimba. Wakati Paulo na Sila walifungwa mu gereza katika muji wa Filipi, waliimba nyimbo za kiroho zenye walikuwa wameweka katika akili. (Mdo. 16:25) Vilevile, wakati ndugu zetu katika Muungano wa Sovieti walipelekwa Siberia, walifanya nini ili kujitia nguvu? Dada Mariya Fedun alikumbuka hivi: “Tulikuwa tunaimba nyimbo zote zenye tulikuwa tunajua, nyimbo za mu kitabu cha nyimbo.” Alisema kama nyimbo hizo ziliwatia wote nguvu na ziliwasaidia wajisikie kuwa karibu zaidi na Yehova. Unajisikia kuwa mwenye nguvu wakati unaimba nyimbo za kiroho zenye unapendaka sana? Basi, weka nyimbo hizo katika akili yako leo!​—Ona kisanduku “ Unipatie Uhodari.”

MAMBO YA KUFANYA ILI UKUWE NA UHODARI ZAIDI

11-12. (a) Kulingana na 1 Samweli 17:37, 45-47, ni nini ilimusaidia Daudi akuwe na uhodari? (b) Mufano wa Daudi unatufundisha jambo gani la maana?

11 Uko na lazima ya uhodari ili kuvumilia mateso. Ukiona kama hauna sifa hiyo, unaweza kufanya nini? Ukumbuke kama uhodari wa kweli hautegemee urefu ao unene wako, nguvu zako, ao uwezo wako. Fikiria mufano wa kijana Daudi wakati alipigana na Goliati. Daudi hakukuwa murefu na munene, hakukuwa na nguvu sana, na hakukuwa na silaha za muzuri kwa kumulinganisha na mwanaume huyo murefu na munene. Daudi hakukuwa hata na upanga. Lakini, alikuwa hodari sana. Bila kuogopa, Daudi alienda kupigana na mutu huyo murefu na munene mwenye alikuwa na kiburi.

12 Ni nini ilimusaidia Daudi akuwe na uhodari sana? Aliamini kabisa kama Yehova alikuwa pamoja na yeye. (Soma 1 Samweli 17:37, 45-47.) Daudi hakukaza akili juu ya namna Goliati alikuwa murefu na munene kumupita. Lakini, alikaza akili juu ya namna Goliati hakukuwa kitu kwa kumulinganisha na Yehova. Ile habari inatufundisha nini? Tutajisikia kuwa hodari kama tuko hakika kuwa Yehova iko pamoja na sisi na kama tuko hakika kuwa watu wenye kutupinga hawako kitu kwa kuwalinganisha na Mungu Mweza-yote. (2 Ny. 20:15; Zb. 16:8) Tunaweza kufanya nini leo ili tukuwe na uhodari zaidi, mbele mateso ikuje?

13. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe na uhodari zaidi? Fasiria.

13 Kuhubiria watu habari njema ya Ufalme wa Mungu kunaweza kutusaidia tukuwe na uhodari zaidi leo. Sababu gani? Kwa sababu wakati tunahubiria wengine, tunajifunza kumutegemea Yehova na kuacha kuogopa watu. (Mez. 29:25) Kama vile mwili wetu unakuwa na nguvu wakati tunafanya mazoezi, vilevile tunakuwa na uhodari zaidi wakati tunahubiri nyumba kwa nyumba, mahali pa watu wengi, wakati wowote, na katika maeneo ya biashara. Kama tuko na uhodari wa kuhubiri leo, tutakuwa tayari kuendelea kuhubiri hata kama kazi yetu inakatazwa.​—1 Te. 2:1, 2.

Nancy Yuen alikataa kuacha kuhubiri habari njema (Picha hii inapatana na fungu la 14)

14-15. Mufano wa Nancy Yuen na Valentina Garnovskaya unaweza kutufundisha nini?

14 Mufano wa dada wawili waaminifu wenye walionyesha uhodari wa pekee unaweza kutufundisha mambo mingi. Nancy Yuen alikuwa tu na urefu wa metre 1 na nusu, lakini haikukuwa mwepesi kumuogopesha. * Alikataa kuacha kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo, alifungwa mu gereza katika inchi ya China kwa miaka zaidi ya 20. Watu wa serikali wenye walimuuliza maulizo walisema kama yeye njo alikuwa “mutu mwenye kichwa nguvu sana” katika inchi yao!

Valentina Garnovskaya alikuwa hakika kama Yehova alikuwa pamoja na yeye (Picha hii inapatana na fungu la 15)

15 Vilevile, Valentina Garnovskaya alifungwa mara tatu mu gereza kwa miaka 21 katika Muungano wa Sovieti wa zamani. * Juu ya nini? Aliazimia kabisa kuendelea kuhubiri, na kwa hiyo, watu wa serikali walimuita kuwa “mutenda-maovu mwenye alikuwa hatari sana.” Ni nini ilisaidia wanamuke hao wawili waaminifu wakuwe hodari sana? Walikuwa hakika kama Yehova alikuwa pamoja nao.

16. Siri ya kuwa na uhodari wa kweli ni nini?

16 Kama vile tumeona, ili tukuwe na uhodari zaidi, hatupaswe kutegemea nguvu zetu na uwezo wetu wenyewe. Lakini, tunapaswa kuamini kama Yehova iko pamoja na sisi na kama yeye njo iko anatupigania. (Kum. 1:29, 30; Zek. 4:6) Ile njo siri ya kuwa na uhodari wa kweli.

MAMBO YA KUFANYA WAKATI WATU WANATUCHUKIA

17-18. Kulingana na Yohana 15:18-21, Yesu alitutolea onyo gani? Fasiria.

17 Tunapenda watu wengine watuheshimie, lakini hatupaswe kuwaza kama hatuko wa maana wakati watu wanatuchukia. Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanawachukia, na wakati wanawafukuza, na wanawalaumu, na kuharibu jina lenu kwa kusema ni kitu chenye uovu kwa sababu ya Mwana wa binadamu.” (Lu. 6:22) Yesu alipenda kusema nini?

18 Yesu hakupenda kusema kama Wakristo wanapaswa kufurahi wakati watu wanawachukia. Lakini, alikuwa anatoa onyo juu ya mambo yenye ingetufikia. Hatuko sehemu ya ulimwengu huu. Tunafuata mafundisho ya Yesu mu maisha yetu na tunahubiri ujumbe wenye alihubiri. Na hilo linafanya ulimwengu utuchukie. (Soma Yohana 15:18-21.) Tunapenda kumufurahisha Yehova. Kama watu wanatuchukia kwa sababu tunamupenda Baba yetu, kazi yao!

19. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa mitume?

19 Usiache hata kidogo jambo lolote lenye watu bure wanaweza kusema ao kutenda likufanye usikie haya ya kuwa Shahidi wa Yehova. (Mik. 4:5) Tunaweza kujifunza kuacha kuogopa watu kwa kuchunguza mufano wenye mitume walionyesha katika Yerusalemu kisha tu Yesu kuuawa. Walijua kama viongozi wa dini ya Wayahudi walikuwa wanawachukia sana. (Mdo. 5:17, 18, 27, 28) Hata hivyo, kila siku waliendelea kuenda ku hekalu na kujitambulisha mbele ya watu kuwa wao ni wanafunzi wa Yesu. (Mdo. 5:42) Hawakuacha woga uwazuie kufanya vile. Na sisi tunaweza kuacha kuogopa watu kwa kujitambulisha kwa ukawaida mbele ya watu kuwa tuko Mashahidi wa Yehova, ku kazi, ku masomo, na katika eneo letu.​—Mdo. 4:29; Ro. 1:16.

20. Juu ya nini mitume walikuwa wenye furaha hata kama watu waliwachukia?

20 Juu ya nini mitume walikuwa wenye furaha? Walijua juu ya nini watu waliwawachukia, na waliona kuwa ni heshima kutendewa mubaya kwa sababu ya kufanya mapenzi ya Yehova. (Lu. 6:23; Mdo. 5:41) Kisha wakati fulani, mutume Petro aliandika hivi: “Hata kama munateseka kwa sababu ya haki, ninyi ni wenye furaha.” (1 Pe. 2:19-21; 3:14) Wakati tunaelewa kama tunachukiwa juu ya kufanya mambo yenye kuwa sawa, hatutaacha hata kidogo kumutumikia Yehova kwa sababu watu wanatuchukia.

UTAPATA FAIDA KAMA UNAJITAYARISHA

21-22. (a) Umeamua kufanya nini ili kujitayarisha kwa ajili ya mateso? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

21 Hatujue ni wakati gani watu wanaweza kuanza kututesa ao ni wakati gani serikali inaweza kukataza kazi yetu. Lakini, tunajua kama tunaweza kujitayarisha leo kwa kufanya urafiki wetu pamoja na Yehova ukuwe wenye nguvu, kuwa na uhodari zaidi, na kujua mambo ya kufanya wakati watu wanatuchukia. Matayarisho yenye tunafanya leo itatusaidia tukuwe imara wakati wenye kuja.

22 Lakini, tutafanya nini kama serikali inakataza ibada yetu? Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia kanuni za Biblia zenye zitatusaidia tuendelee kumutumikia Yehova hata wakati kazi yetu inakatazwa.

WIMBO 118 “Tupe Imani Zaidi”

^ fu. 5 Hatupendi watu watuchukie. Lakini siku moja, sisi wote tutalazimika kuvumilia mateso. Habari hii itatusaidia tupambane na mateso kwa uhodari.

^ fu. 7 Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 4, 1966 uku. 212-224 (katika Kifaransa).

^ fu. 14 Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 1979, uku. 4-7. Ona pia video Jina la Yehova Litajulikana ku JW Télédiffusion. Fungua sehemu KUULIZWA MAULIZO NA USHUHUDA.

^ fu. 15 Ona Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2008, uku. 191-192.

^ fu. 67 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa ibada ya familia, wazazi wanatumia karte ili kusaidia watoto wao waweke maandiko katika akili.

^ fu. 70 MAFASIRIO YA PICHA: Watu wa familia moja wanajizoeza kuimba nyimbo za Ufalme mu motokari wakati wanaenda ku mukutano.