Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 28

Endelea Kumuabudu Yehova Wakati Kazi Yetu Inakatazwa

Endelea Kumuabudu Yehova Wakati Kazi Yetu Inakatazwa

“Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.”​—MDO. 4:19, 20.

WIMBO 122 Iweni Imara, Thabiti!

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Juu ya nini hatupaswe kushangaa wakati kazi yetu inakatazwa? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

KATIKA mwaka wa 2018, wahubiri wa habari njema zaidi ya 223 000 waliishi katika inchi mbalimbali kwenye kazi yetu ilikatazwa ao kuwekewa vizuizi sana. Jambo hilo halipaswe kutushangaza. Kama vile tuliona katika habari yenye ilitangulia, Wakristo wa kweli wanatazamia kama watateswa. (2 Ti. 3:12) Hata kama tunaishi wapi, wakubwa wa serikali wanaweza kutukataza haraka na kwa kushitukia kumuabudu Yehova, Mungu wetu mwenye upendo.

2 Kama serikali ya mahali kwenye unaishi inakataza ibada ya Mashahidi wa Yehova, unaweza kujiuliza maulizo kama hii: ‘Je, mateso inaonyesha kama hatukubaliwe tena na Mungu? Tutaacha kumuabudu Yehova kwa sababu kazi yetu inakatazwa? Ninapaswa kuhamia katika inchi ingine ili niweze kumuabudu Mungu kwa uhuru?’ Katika habari hii, tutazungumuzia ile maulizo. Pia, tutaona namna tunaweza kuendelea kumuabudu Yehova wakati kazi yetu inakatazwa na mitego yenye tunapaswa kuepuka.

MATESO INAONYESHA KAMA HATUKUBALIWE TENA NA MUNGU?

3. Kulingana na andiko la 2 Wakorinto 11:23-27, mutume Paulo alipata mateso gani, na mufano wake unatufundisha nini?

3 Kama serikali fulani inakataza ibada yetu, tunaweza kukosea kwa kufikiri kama hatukubaliwe tena na Mungu. Lakini, kumbuka kama mateso haimaanishe kama Yehova hatufurahie. Tukamate mufano wa mutume Paulo. Kwa kweli, alikuwa anakubaliwa na Mungu. Alipata pendeleo la kuandika barua 14 za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, na alikuwa mutume kwa mataifa. Lakini, alipata mateso makali. (Soma 2 Wakorinto 11:23-27.) Mambo yenye ilimupata mutume Paulo inatuonyesha kama Yehova anaruhusu watumishi wake waaminifu wapate mateso.

4. Juu ya nini ulimwengu unatuchukia?

4 Yesu alionyesha juu ya nini tunapaswa kutazamia kama tutateswa. Alisema kama watu watatuchukia kwa sababu hatuko sehemu ya ulimwengu. (Yoh. 15:18, 19) Mateso haionyeshe kama hatukubaliwe tena na Yehova. Lakini, inaonyesha kama tuko tunafanya mambo yenye kuwa sawa!

WAKATI KAZI YETU INAKATAZWA, TUTAACHA KUMUABUDU YEHOVA?

5. Wanadamu bure wanaweza kusimamisha ibada ya Yehova? Fasiria.

5 Wanadamu bure wenye wanatupinga hawawezi kutufanya tuache kumuabudu Yehova, Mungu Mweza-yote. Wengi wamejaribu lakini wameshindwa. Fikiria mambo yenye ilitokea wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Wakati huo, serikali katika inchi mingi zilitesa sana watu wa Mungu. Chama cha Wanazi katika inchi ya Ujerumani kilikataza kazi yetu sisi Mashahidi wa Yehova na pia serikali ya Australia, Kanada, na inchi zingine. Lakini, ona mambo yenye ilitokea. Wakati vita hiyo ilianza katika mwaka wa 1939, kulikuwa wahubiri 72 475 mu dunia yote. Ripoti zilionyesha kama kufikia mwisho wa vita katika mwaka wa 1945, kwa baraka ya Yehova, kulikuwa wahubiri 156 299. Hesabu ya wahubiri iliongezeka mara mbili na kupita!

6. Kuliko kutuogopesha, upinzani unaweza kuleta matokeo gani ya muzuri? Leta mufano.

6 Kuliko kutuogopesha sana, upinzani unaweza kutuchochea tuazimie zaidi kumutumikia Yehova. Kwa mufano, bwana mumoja na bibi yake wenye walikuwa na mutoto mudogo mwanaume walikuwa wanaishi katika inchi kwenye serikali iliamua kukataza ibada yetu. Kuliko kuogopa sana na kupunguza bidii yao, bwana huyo na bibi yake walianza kufanya kazi ya upainia. Bibi aliacha hata kazi yake ya mushahara muzuri ili kufanya upainia. Bwana huyo alisema kama kukataza kazi yetu kulifanya watu wengi wapende kujua mambo mingi juu ya Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo, aliona kama ilikuwa mwepesi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kukataza kazi yetu kulileta matokeo ingine ya muzuri. Muzee mumoja katika inchi ileile alisema kama watu wengi wenye walikuwa wameacha kumutumikia Yehova walianza tena kuhuzuria mikutano na kuhubiri.

7. (a) Andiko la Mambo ya Walawi 26:36, 37 linatufundisha nini? (b) Utafanya nini kama kazi yetu inakatazwa?

7 Wakati maadui wetu wanakataza ibada yetu, wanatumaini kama hilo litafanya tuogope kumutumikia Yehova. Zaidi ya kukataza kazi yetu, wanaweza kueneza habari za uongo juu yetu, kutuma watu wa serikali ili wachunguze nyumba zetu, kutupeleka ku tribinali, ao hata kufunga mu gereza wamoja kati yetu. Wanatumaini kama tutaogopa sana kwa sababu walifunga mu gereza ndugu na dada zetu fulani. Kama tunawaruhusu watuogopeshe, tunaweza kupunguza bidii yetu ao hata kuacha kumutumikia Yehova. Hatupendi kuwa kama watu wenye kuzungumuziwa katika Mambo ya Walawi 26:36, 37. (Soma.) Hatutaacha woga ufanye tupunguze bidii yetu ao tuache kumutumikia Yehova. Tunamutegemea Yehova kabisa na tunaacha kuogopa. (Isa. 28:16) Tunasali kwa Yehova ili kumuomba muongozo. Tunajua kama, kupitia musaada wake, hata serikali ya wanadamu yenye nguvu zaidi haiwezi kutuzuia kumuabudu Mungu wetu kwa uaminifu.​—Ebr. 13:6.

NINAPASWA KUHAMIA KATIKA INCHI INGINE?

8-9. (a) Kila mutu ao kila kichwa cha familia anapaswa kukamata uamuzi gani? (b) Nini itasaidia mutu akamate uamuzi wenye hekima?

8 Kama serikali ya mahali kwenye tunaishi inakataza ibada yetu, unaweza kujiuliza ikiwa unapaswa kuhamia katika inchi ingine kwenye unaweza kumutumikia Yehova kwa uhuru. Huo ni uamuzi wa kipekee wenye hakuna mutu anaweza kukamata pa nafasi yako. Watu fulani wanaweza kuona kama kufikiria jambo lenye Wakristo wa wakati wa mitume walifanya wakati waliteswa kunaweza kuwasaidia. Kisha maadui kumuua Stefano kwa kumupiga majiwe, wanafunzi katika muji wa Yerusalemu walihamia Yudea na Samaria na hata mupaka Foinike, Kipro, na Antiokia. (Mt. 10:23; Mdo. 8:1; 11:19) Lakini, wengine wanaweza kuona kama, wakati upinzani mwingine mukali ulipata Wakristo wa kwanza, mutume Paulo aliamua kama hatatoka mu maeneo kwenye kazi ya kuhubiri ilikuwa inapingwa. Lakini, alijitia katika hatari ili kueneza habari njema na kutia nguvu ndugu katika miji kwenye kulikuwa mateso makali.​—Mdo. 14:19-23.

9 Habari hizo zinatufundisha nini? Kila kichwa cha familia anapaswa kukamata uamuzi wa kipekee juu ya kuhama. Mbele ya kukamata uamuzi, anapaswa kusali na kufikiria kwa uangalifu hali za familia yake na matokeo ya muzuri ao ya mubaya yenye kuhama kunaweza kuwaletea. Juu ya jambo hilo, kila Mukristo anapaswa ‘kubeba muzigo wake mwenyewe.’ (Gal. 6:5) Hatupaswe kuhukumu wengine juu ya uamuzi wenye wanakamata.

NAMNA GANI TUTAMUABUDU YEHOVA WAKATI KAZI YETU INAKATAZWA?

10. Biro ya tawi na wazee watatoa maagizo gani?

10 Ni nini itakusaidia uendelee kumuabudu Yehova wakati kazi yetu inakatazwa? Biro ya tawi itatolea wazee maagizo na mashauri yenye kufaa juu ya namna ya kupata chakula cha kiroho, namna ya kufanya mikutano, na namna ya kuhubiri habari njema. Kama biro ya tawi haiwezi kupashana habari na wazee, wazee watakusaidia wewe na wengine wote katika kutaniko ili muendelee kumuabudu Yehova. Watatoa muongozo wenye kutegemea Biblia na vichapo vyetu.​—Mt. 28:19, 20; Mdo. 5:29; Ebr. 10:24, 25.

11. Juu ya nini unaweza kuwa hakika kama utapata chakula cha kiroho, na unaweza kufanya nini ili kulinda Biblia na vichapo vingine?

11 Yehova ameahidi kama watumishi wake watakulishwa muzuri kiroho. (Isa. 65:13, 14; Lu. 12:42-44) Kwa hiyo, unaweza kuwa hakika kama tengenezo lake litafanya kila jambo lenye linawezekana ili kukutolea mambo yenye uko nayo lazima ili uendelee kuwa muaminifu. Lakini, na wewe unaweza kufanya jambo fulani. Wakati kazi yetu inakatazwa, tafuta nafasi ya muzuri kwenye unaweza kuficha Biblia yako na chakula kingine cha kiroho chenye unaweza kuwa nacho, ni kusema, vichapo vingine. Ukuwe muangalifu ili usiache vichapo hivyo vya maana sana mahali kwenye vinaweza kuonekana kwa vyepesi, ikuwe vyenye kuchapishwa ao vya kielektroniki. Kila mumoja kati yetu anapaswa kufanya nguvu yake yote ili aendelee kuwa nguvu kiroho.

Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kukutana bila woga ili kuabudu (Picha hii inapatana na fungu la 12) *

12. Wazee wanaweza kufanya mipango gani ili mikutano ifanyike katika njia yenye watu hawatatambua?

12 Halafu mikutano yenye tunafanyaka kila juma ili kumuabudu Yehova? Wazee watafanya mipango ili muweze kuhuzuria mikutano katika njia yenye watu wenye kutupinga hawatatambua. Wanaweza kuwapatia maagizo ili mufanye mikutano katika vikundi vya kidogo-kidogo, na wanaweza kubadilisha mara kwa mara wakati wa kufanya mikutano na mahali pa kufanyia ile mikutano. Unaweza kusaidia ili kulinda ndugu na dada zako kwa kusema kwa sauti ya chini-chini wakati munakuja ao wakati munatoka. Pia, inaweza kuwa muzuri uvae katika njia ya kawaida yenye haitafanya muvumbuliwe.

Hata kama serikali inakataza kazi yetu, hatutaacha kuhubiri (Picha hii inapatana na fungu la 13) *

13. Mufano wa ndugu zetu katika Muungano wa Sovieti wa zamani unaweza kutufundisha nini?

13 Juu ya kazi ya kuhubiri, hali hazitakuwa sawasawa katika maeneo yote. Lakini, juu tunamupenda Yehova na tunafurahia kuambia wengine juu ya Ufalme wake, tutatafuta nafasi ya kuhubiri. (Lu. 8:1; Mdo. 4:29) Mwanahistoria Emily Baran alitoa maelezo fulani juu ya kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova katika Muungano wa Sovieti wa zamani. Alisema hivi: “Wakati serikali iliambia Mashahidi wa Yehova kama hawapaswe kuhubiria wengine, Mashahidi wa Yehova walikuwa wanazungumuza [na] majirani wao, wafanyakazi wenzao, na marafiki wao. Wakati Mashahidi walipelekwa mu kambi za kazi ngumu kwa sababu ya kufanya vile, walikuwa wanahubiria wafungwa wenzao.” Hata kama kazi yao ilikatazwa, ndugu zetu katika Muungano wa Sovieti hawakuacha kuhubiri. Kama siku moja kazi ya kuhubiri inakatazwa mahali kwenye unaishi, wewe pia uazimie kufanya vile!

MITEGO YENYE TUNAPASWA KUEPUKA

Tunapaswa kujua wakati wa kunyamaza (Picha hii inapatana na fungu la 14) *

14. Zaburi 39:1 inaweza kutusaidia kuepuka mutego gani?

14 Ukuwe muangalifu juu ya habari zenye unaambia wengine. Wakati kazi yetu inakatazwa, tunapaswa kutambua “wakati wa kunyamaza.” (Muh. 3:7) Tunapaswa kuchunga habari zenye zinapaswa kubakia siri, kama vile majina ya ndugu na dada zetu, mahali kwenye tunafanyia mikutano, namna tunafanya kazi yetu ya kuhubiri, na namna tunapata chakula cha kiroho. Hatupaswe kuambia wakubwa wa serikali habari hizo, ao marafiki na watu wa jamaa yetu wenye kuishi mu inchi yetu ao mu inchi zingine, hata kama hawana nia ya mubaya. Kama tunaangukia katika mutego huo, tunaweza kutia ndugu na dada zetu katika hatari.​—Soma Zaburi 39:1.

15. Shetani atajikaza kufanya nini, na namna gani tunaweza kuepuka mutego wake?

15 Usiruhusu mambo ya kidogo-kidogo ilete migawanyiko kati yetu. Shetani anajua kama nyumba yenye kugawanyika haiwezi kusimama. (Mk. 3:24, 25) Ataendelea kujikaza ili alete migawanyiko kati yetu. Wakati anafanya vile, anawaza kama tutaanza kupigana sisi wenyewe kuliko kumupiganisha yeye.

16. Dada Gertrud Poetzinger alituachia mufano gani muzuri?

16 Hata Wakristo wenye kukomaa kiroho wanapaswa kuwa waangalifu ili wasiangukie katika mutego huo. Fikiria mufano wa dada wawili watiwa-mafuta, Gertrud Poetzinger na Elfriede Löhr. Walifungwa mu gereza pamoja na dada wengine Wakristo katika kambi moja ya mateso ya Wanazi. Gertrud alisikia wivu wakati Elfriede alitolea dada wengine wenye walikuwa mu kambi hotuba mbalimbali zenye kutia moyo. Kisha wakati fulani, Gertrud alisikia haya na akamuomba Yehova musaada. Aliandika hivi: “Wakati wengine wako na uwezo mukubwa ao wanapewa madaraka zaidi kuliko sisi, tunapaswa kujifunza kukubali jambo hilo.” Gertrud alifanya nini ili ashinde wivu wake? Alikazia akili sifa za muzuri za Elfriede na hali yake ya kuwa mutu muchangamufu. Kwa kufanya vile, alirudisha uhusiano wake wa muzuri pamoja na Elfriede. Wote wawili waliokoka katika kambi ya mateso na walimutumikia Yehova kwa uaminifu mupaka mwisho wa maisha yao hapa ku dunia. Kama tunajikaza sana ili kumaliza hali za kukosa kuelewana na ndugu na dada zetu, hatutaacha kitu chochote kilete migawanyiko kati yetu.​—Kol. 3:13, 14.

17 Juu ya nini tunapaswa kuepuka kimbelembele?

17 Uepuke kimbelembele. Kama tunafuata maagizo yenye ndugu wenye kutumainika wenye kutuongoza wanatutolea, tutaepuka magumu mingi. (1 Pe. 5:5) Kwa mufano, katika inchi moja kwenye kazi yetu inakatazwa, ndugu wenye kuongoza walikuwa wamepatia ndugu na dada maagizo juu ya kuhubiri wakati wowote, bila kuachia watu vichapo. Lakini, ndugu mumoja painia katika eneo hilo aliona kama yeye njo anajua mambo muzuri na aliachia watu vichapo. Hilo lilileta matokeo gani? Wakati tu yeye na wahubiri wengine walimaliza kuhubiri, polisi waliwauliza maulizo. Inaonekana kuwa, watu wa serikali walikuwa wanawafuata na walikamata vichapo vyenye walikuwa wametolea watu. Jambo hilo linatufundisha nini? Tunapaswa kufuata maagizo hata kama tunaona kuwa tunajua mambo muzuri. Yehova anatubariki sikuzote wakati tunaunga mukono ndugu wenye amewekwa ili watuongoze.​—Ebr. 13:7, 17.

18. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kuwekea wengine sheria zenye haziko za lazima?

18 Usiweke sheria zenye haziko za lazima. Kama wazee wanaweka sheria zenye haziko za lazima, watawekea wengine muzigo. Ndugu Juraj Kaminský alikumbuka mambo yenye ilitokea wakati kazi yetu ilikuwa inakatazwa katika inchi yenye zamani iliitwa Chekoslovakia. Alisema hivi: “Kisha wazee wengi kufungwa katika gereza, wazee fulani wenye walibakia wenye walikuwa wanaongoza katika makutaniko na katika mizunguko walianza kuwekea wahubiri sheria juu ya mwenendo, walifanya liste ya mambo ya kufanya na mambo ya kuepuka.” Yehova hakutupatia haki ya kuwekea ndugu na dada zetu sheria. Mutu mwenye anawekea ndugu na dada sheria zenye haziko za lazima halinde usalama wao, lakini anajaribu kujifanya kuwa bwana juu ya imani yao.​—2 Ko. 1:24.

USIACHE HATA KIDOGO KUMUABUDU YEHOVA

19. Hata Shetani ajikaze namna gani, andiko la 2 Mambo ya Nyakati 32:7, 8 linatupatia sababu gani ya kutufanya tusikuwe na woga?

19 Adui yetu mukubwa, Shetani Ibilisi, hataacha kujikaza ili kutesa watumishi waaminifu wa Yehova. (1 Pe. 5:8; Ufu. 2:10) Shetani na watu wake watajaribu kutukataza kumuabudu Yehova. Lakini, hatuna sababu ya kuogopa sana na kuacha kumutumikia Yehova! (Kum. 7:21) Yehova iko pamoja na sisi, na ataendelea kutusaidia hata kama kazi yetu inakatazwa.​—Soma 2 Mambo ya Nyakati 32:7, 8.

20. Unaazimia kufanya nini?

20 Basi, tuazimie kufanya kama vile ndugu zetu wa wakati wa mitume walifanya. Waliambia viongozi wa siku zao hivi: “Kama ni jambo lenye kuwa sawa mbele ya macho ya Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko kumusikiliza Mungu, muamue ninyi wenyewe. Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.”​—Mdo. 4:19, 20.

WIMBO 73 Tupe Ujasiri

^ fu. 5 Tunapaswa kufanya nini kama serikali inatukataza kumuabudu Yehova? Habari hii itatutolea mashauri yenye kufaa juu ya mambo ya kufanya na mambo ya kuepuka ili tusiache hata kidogo kumuabudu Mungu wetu!

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Picha zote zinaonyesha Mashahidi wenye kutumikia mu inchi kwenye kazi yetu inawekewa vizuizi. Kikundi kidogo cha ndugu na dada kinakutana ili kufanya mukutano mu depo ya ndugu mumoja.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Dada Mukristo (kushoto) mwenye iko anazungumuza na mwanamuke mumoja kwa njia ya kirafiki anatafuta namna ya kuzungumuza juu ya Yehova.

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mumoja mwenye polisi wanauliza maulizo anakataa kuwaambia habari juu ya kutaniko lao.