Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yesu Alikufa Kabisa kwa Ajili Yangu?

Yesu Alikufa Kabisa kwa Ajili Yangu?

BIBLIA iko na maneno mingi yenye kutoka mu moyo yenye watu ‘wenye hisia kama zetu’ walisema. (Yak. 5:17) Kwa mufano, tunaweza kuelewa kwa vyepesi mambo yenye Paulo alimaanisha wakati alisema maneno yenye kuwa katika Waroma 7:21-24. Alisema hivi: “Wakati ninataka kufanya mambo yenye kuwa sawa, mambo ya mubaya yako pamoja na mimi. . . . Maskini mimi!” Hisia hizo zenye kutoka mu moyo zinatutia moyo wakati tunapiganisha hali yetu ya kukosa kukamilika.

Paulo alizungumuzia hisia zingine zenye kutoka mu moyo. Katika Wagalatia 2:20, alionyesha kama alikuwa hakika kuwa Yesu ‘alimupenda na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake!’ Ile maneno inaonyesha namna sisi pia tunajisikiaka? Pengine hatujisikie vile sikuzote.

Kama tunapiganisha hisia za kujisikia kuwa hatuko wa maana kwa sababu ya zambi zenye tulifanya zamani, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kukubali kama Yehova anatupenda na anasamehe, na inaweza kuwa nguvu sana tuone zabihu ya Yesu kuwa zawadi kwa ajili yetu. Je, Yesu anapenda kabisa tuelewe kama bei ya ukombozi ni zawadi? Kama ni vile, ni nini inaweza kutusaidia tuione vile? Tuzungumuzie basi ile maulizo mbili.

NAMNA YESU ANAONA ZABIHU YAKE

Kwa kweli, Yesu anapenda tuone zabihu yake kuwa zawadi kwa ajili yetu. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe hakika na jambo hilo? Wazia katika akili yako habari yenye kupatikana katika Luka 23:39-43. Mwanaume mumoja anatundikwa ku muti wa mateso pembeni ya Yesu. Anakubali kama alifanya jambo fulani la mubaya. Kosa lenye alifanya linapaswa kuwa nzito sana kwa sababu ni watenda-maovu wenye walifanya mambo ya mubaya sana njo tu wenye walikuwa wanapewa malipizi makali kama ile. Kwa sababu anahuzunika sana juu ya hali yake, anamuomba Yesu hivi: “Unikumbuke wakati utaingia katika Ufalme wako.”

Yesu alitenda namna gani? Wazia maumivu yenye alisikia wakati alipaswa kugeuza kichwa ili kumuangalia mwanaume huyo. Hata kama iko na maumivu makali, anajikaza sana ili kuonyesha sura ya kicheko na anamuhakikishia hivi: “Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” Pengine Yesu angekumbusha tu ule mwanaume kama “Mwana wa binadamu [alikuja] ili . . . atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” (Mt. 20:28) Lakini, unaona namna Yesu anakazia kwa upendo faida yenye zabihu yake ingeletea ule mutenda-maovu? Alionyesha hali ya urafiki wakati alitumia neno “utakuwa” na neno “mimi.” Na alifanya ule mwanaume aone kama zabihu yake ilimuhusu kipekee wakati alimutolea tumaini la kuishi katika dunia paradiso.

Kwa kweli, Yesu alipenda mwanaume huyo akubali kama zabihu yake ingemuletea faida kipekee. Kama Yesu aliona kuwa zabihu yake ingeletea faida ule mutenda-maovu mwenye hakukuwa amepata hata nafasi ya kutumikia Mungu, hilo linaonyesha kama zabihu yake inaletea faida hata zaidi Mukristo mwenye kubatizwa mwenye kumutumikia Mungu. Basi, ni nini inaweza kutusaidia tuamini kabisa kama zabihu ya Yesu inaweza kutuletea faida, hata kama tulifanya zambi zamani?

MAMBO YENYE ILIMUSAIDIA PAULO

Utumishi ao kazi ya kuhubiri ulichochea namna Paulo aliona zabihu ya Yesu. Namna gani? Alisema hivi: “Mimi ni mwenye shukrani kwa Kristo Yesu Bwana wetu, mwenye alinipatia nguvu, kwa sababu aliniona kuwa muaminifu kwa kunipatia utumishi, hata kama zamani nilikuwa mutu mwenye kumutukana Mungu na mutesaji na mutu mwenye zarau.” (1 Ti. 1:12-14) Kazi yenye Paulo alipewa ilimuhakikishia kama Yesu alimupenda, alimuonyesha rehema, na alimutumainia. Sisi pia Yesu alitupatia utumishi. (Mt. 28:19, 20) Utumishi wetu unaweza pia kutusaidia tuelewe kama Yesu alikufa kwa ajili yetu?

Albert, mwenye alimurudilia Yehova hivi karibuni kisha kutengwa na kutaniko kwa miaka karibu 34, anasema hivi: “Zambi zangu ziko mbele yangu sikuzote. Lakini wakati niko katika mahubiri, kama Paulo, ninajisikia kuwa mimi kipekee nimepewa utumishi kutoka kwa Yesu. Utumishi unafanya nikuwe mwenye furaha zaidi na nikuwe na mawazo ya muzuri juu yangu mwenyewe, juu ya maisha yangu, na juu ya wakati wangu wenye kuja.”​—Zb. 51:3.

Wakati unajifunza na watu wa namna zote, uwahakikishie kama Yesu anawaonyesha rehema na anawapenda

Allan, mwenye alifanya makosa mingi mazito na mwenye alikuwa mwenye jeuri mbele ajifunze kweli, anasema hivi: “Ninaendelea kuwaza juu ya mambo yote ya mubaya yenye nilitendea watu. Wakati fulani, hilo linanifanya nishuke moyo. Lakini ninamushukuru Yehova kwa sababu anaruhusu mutenda-zambi kama mimi ahubirie wengine habari njema. Wakati ninaona watu wanakubali habari njema, hilo linanikumbusha kama Yehova ni mwema na mwenye upendo sana. Ninajisikia kuwa ananitumia ili kusaidia wengine wenye wamefanya pia mambo ya mubaya.”

Wakati tuko katika mahubiri, tunafanya jambo fulani la muzuri na tunafikiri juu ya mambo ya muzuri. Kazi ya kuhubiri inatuhakikishia kama Yesu anatuonyesha rehema, anatupenda, na anatutumainia.

YEHOVA NI MUKUBWA KULIKO MIOYO YETU

Mupaka wakati ulimwengu mubaya wa Shetani utahabaribiwa, mioyo yetu inaweza kuendelea kutuhukumu juu ya makosa yenye tulifanyaka zamani. Ni nini itatusaidia tusiendelee kujisikia vile?

Jean, mwenye zamiri yake inasumbua mara mingi juu ya maisha ya unafiki yenye alikuwa anaishi wakati alikuwa kijana, anasema hivi: “Niko mwenye furaha juu ‘Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu.’” (1 Yo. 3:19, 20) Na sisi tunaweza kupata faraja kwa kujua kama Yehova na Yesu wanaelewa muzuri zaidi hali yetu ya zambi kuliko sisi. Kumbuka kama, kwa sababu ya upendo wao, walitoa bei ya ukombozi, haiko kwa ajili ya wanadamu wakamilifu, lakini kwa ajili ya watenda-zambi wenye wanatubu.​—1 Ti. 1:15.

Tunahakikishia mioyo yetu kweli hiyo ya maana wakati tunafikiri sana juu ya namna Yesu alitendea wanadamu wenye hawakamilike na wakati tunafanya nguvu yetu yote ili kutimiza utumishi wenye alitupatia. Wakati tunafanya vile, kama Paulo, tunaweza kusema hivi: Yesu “alinipenda na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.”