Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 34

Mambo ya Kufanya Wakati Mugao Wako Unabadilika

Mambo ya Kufanya Wakati Mugao Wako Unabadilika

“Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu na upendo wenye mulionyesha kwa ajili ya jina lake.”​—EBR. 6:10.

WIMBO 38 Atakupa Nguvu

KIFUPI CHA HABARI *

1-3. Ni mambo gani fulani yenye inaweza kufanya migao ya watumishi wa wakati wote ibadilike?

ROBERT na Mary Jo wanakumbuka hivi: “Kisha kufanya miaka 21 ya muzuri mu mugao wetu wa umisionere, wazazi wetu wote ine walifikia kuwa wazaifu. Tulifurahia kuwahangaikia. Lakini, tulihuzunika kuacha mahali kwenye tulikuwa tumependa sana.”

2 William na Terrie wanasema hivi: “Tulilia wakati tulijua kama afya yetu haingeturuhusu kurudia mu mugao wetu. Sikuzote, tulikuwa tunapenda kumutumikia Yehova katika inchi ingine, lakini hatungeendelea tena kufanya vile.”

3 Aleksey anasema hivi: “Tulijua kama wapinzani wetu walipenda kufunga biro yetu ya tawi kwenye nilikuwa ninatumikia. Lakini tulivunjika moyo wakati jambo hilo lilitokea na tulipaswa kutoka ku Beteli.”

4. Tutazungumuzia maulizo gani mu habari hii?

4 Pia watumishi wengi wa wakati wote, kutia ndani wale wenye kutumikia ku Beteli, wamepewa migao ya mupya. * Ndugu na dada hao waaminifu wanaweza kuona kama ni nguvu kuacha mugao wenye walikuwa wanapenda sana. Ni nini inaweza kuwasaidia wakati mugao unabadilika? Namna gani unaweza kuwasaidia? Majibu ya ile maulizo inaweza kutusaidia tujue namna ya kuzoea hali za mupya mu maisha.

MAMBO YA KUFANYA WAKATI MUGAO WAKO UNABADILIKA

Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kwa watumishi wa wakati wote kuacha mugao wao? (Picha hii inapatana na fungu la 5) *

5. Kama mugao wetu unabadilika, tunaweza kujisikia namna gani?

5 Ikuwe tunatumikia ku Beteli ao katika aina zingine za utumishi wa wakati wote, tunaweza kufikia kupenda watu sana na hata mahali kwenye tunatumikia. Kama hali fulani inatulazimisha kuacha mugao wetu, tunaweza kuhuzunika sana. Tunaendelea kukumbuka sana ndugu na dada wenye tumeacha, na tunaendelea kujiuliza ikiwa wako mu hali gani, zaidi sana kama tulilazimika kuhama kwa sababu wapinzani wetu walikuwa wanatutesa. (Mt. 10:23; 2 Ko. 11:28, 29) Tena, wakati mutu anapata mugao mupya ao anarudia ku nyumba, mara mingi inaomba azoee desturi za mupya. Robert na Mary Jo wanasema hivi: “Tulikuwa tumesahau desturi ya kwetu na hata kuhubiri mu luga yetu ya kizalikio. Tulijisikia kama wageni katika inchi yetu.” Watu fulani wenye mugao wao unabadilika, bila kukawia, wanaweza kuwa na matatizo yenye hawakuwazia ya kupata feza. Wanaweza kuwa na wasiwasi, woga, na wanaweza kuvunjika moyo. Ni nini inaweza kuwasaidia?

Ni jambo la maana tumukaribie Yehova na kumutegemea (Picha hii inapatana na fungu la 6-7) *

6. Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kumukaribia Yehova?

6 Endelea kumukaribia Yehova. (Yak. 4:8) Namna gani tunaweza kufanya vile? Kwa kumutegemea na kusali kwake kwa sababu iko “Musikiaji wa sala.” (Zb. 65:2) Zaburi 62:8 inasema hivi: “Mumwange mioyo yenu mbele yake.” Yehova anaweza kufanya “kwa wingi zaidi kupita mambo yote yenye tunaomba ao yenye tunafikiri.” (Efe. 3:20) Hatupatie tu mambo yenye tunamuomba katika sala. Anaweza kumaliza magumu yetu katika njia yenye hatukuwazia hata kidogo.

7. (a) Ni mambo gani yenye itatusaidia tuendelee kumukaribia Yehova? (b) Kulingana na Waebrania 6:10-12, matokeo itakuwa nini kama tunaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu?

7 Ili uendelee kumukaribia Yehova, usome Maandiko kila siku na kufikiri sana juu ya mambo yenye unasoma. Ndugu mumoja mwenye alikuwaka misionere anasema hivi: “Uendelee kufanya ibada ya familia kwa ukawaida na kutayarisha mikutano, kama vile ulikuwa unafanya mu mugao wako wa zamani.” Pia, uendelee kuhubiri habari njema kwa uwezo wako wote katika kutaniko lako la mupya. Yehova anakumbuka wale wenye wanaendelea kumutumikia kwa uaminifu, hata kama hawawezi kufanya mambo mingi kama vile zamani.​—Soma Waebrania 6:10-12.

8. Namna gani maneno yenye kuwa mu 1 Yohana 2:15-17 inaweza kukusaidia ufanye maisha yako ikuwe mwepesi?

8 Ufanye maisha yako ikuwe mwepesi. Usiache mahangaiko ya ulimwengu wa Shetani ikuzuie kumutumikia Yehova. (Mt. 13:22) Usikubali watu wa ulimwengu ao marafiki wenye hawana nia ya mubaya ao watu wa jamaa wakuchochee utafute feza ili ukuwe na maisha ya muzuri katika ulimwengu wa Shetani. (Soma 1 Yohana 2:15-17.) Umutegemee Yehova, mwenye ameahidi kama atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima “wakati wenye kufaa.” Atatusaidia tuendelee kuwa na imani yenye nguvu, tujisikie kuwa wenye kutulia, na atatutimizia mahitaji yetu ya kimwili.​—Ebr. 4:16; 13:5, 6.

9. Kulingana na Mezali 22:3, 7, juu ya nini ni jambo la maana kuepuka madeni yenye haiko ya lazima, na nini inaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri?

9 Uepuke madeni yenye haiko ya lazima. (Soma Mezali 22:3, 7.) Inaweza kuomba feza mingi ili kuhama, na ni mwepesi kukamata madeni. Juu ya kuepuka madeni yenye haiko ya lazima, usikope feza ili kuuza vitu vyenye hauna navyo lazima kabisa. Wakati tuko katika hali yenye kuleta mahangaiko, kwa mufano, wakati tunahangaikia mupendwa wetu mwenye kuwa mugonjwa, tunaweza kushindwa kuamua ni feza ngapi zenye tunaweza kukopa. Katika hali kama hizo, ukumbuke kama “sala na sala ya kumulilia Mungu” inaweza kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri. Ili kujibu sala zako, Yehova anaweza kukupatia amani yenye ‘italinda moyo wako na nguvu zako za akili,’ ili uamue muzuri mambo yenye unaweza kufanya.​—Flp. 4:6, 7; 1 Pe. 5:7.

10. Unaweza kufanya nini ili ukuwe na marafiki wapya?

10 Endelea kuwa na marafiki wazuri. Uelezee marafiki wako wa sana namna unajisikia na magumu yenye uko nayo, zaidi sana wale wenye wamekwisha kupata magumu kama yako. Kufanya vile kunaweza kukusaidia ujisikie muzuri. (Muh. 4:9, 10) Marafiki wenye ulijifanyia mu mugao wako wa zamani wataendelea kuwa marafiki wako. Sasa, wakati mugao wako unabadilika, uko na lazima ya kujifanyia marafiki wapya. Ukumbuke kama ili upate marafiki, unapaswa kuwa mutu mwenye kufanya urafiki. Unaweza kufanya nini ili ukuwe na marafiki wapya? Uzungumuze na wengine juu ya mambo ya muzuri sana yenye umejionea mu kazi ya Yehova na uache waone kama uko na furaha katika kazi ya Yehova. Hata kama wamoja katika kutaniko lako hawaelewe juu ya nini unapenda utumishi wa wakati wote, wengine wanaweza kuiga mufano wako na kuwa marafiki wako wazuri. Lakini, ukuwe muangalifu ili usizungumuzie sana mambo yenye ulitimiza katika kazi ya Yehova, na mawazo yoyote ya mubaya yenye unaweza kuwa nayo.

11. Unaweza kufanya nini ili ndoa yenu iendelee kuwa na furaha?

11 Kama ulilazimika kuacha mugao wako kwa sababu bibi ao bwana yako amekuwa mugonjwa, usiseme kama ni kosa lake. Ao kama wewe mwenyewe uligonjwa, usione kama ni kosa lako, na kuwaza kama umevunja bibi ao bwana yako moyo. Ukumbuke kama muko “mwili mumoja,” na mulimuahidi Yehova kama kila mumoja atahangaikia mwenzake katika hali zote. (Mt. 19:5, 6) Kama mumeacha mugao wenu kwa sababu ya mimba yenye hamukutazamia, muhakikishie mutoto wenu kama iko wa maana zaidi kuliko mugao wenu wa zamani. Muhakikishie mutoto wenu kama munamuona kuwa “zawabu” kutoka kwa Mungu. (Zb. 127:3-5) Pia, muzungumuze naye juu ya mambo yenye mulijionea mu mugao wenu. Kufanya vile kunaweza kusaidia mutoto wenu naye afanye utumishi wa wakati wote.

NAMNA WENGINE WANAWEZA KUSAIDIA

12. (a) Namna gani tunaweza kusaidia wale wenye kuwa katika utumishi wa wakati wote waendelee mu mugao wao? (b) Namna gani tunaweza kuwasaidia wale wenye mugao wao umebadilika ili wazoee hali yao ya mupya?

12 Inafurahisha kuona kama, makutaniko mingi na ndugu na dada wengi wanafanya yote yenye wanaweza ili kusaidia wale wenye kuwa katika utumishi wa wakati wote wabakie mu mugao wao. Wanafanya vile kwa kuwatia moyo waendelee kufanya kazi yao, kwa kuwapatia feza ao vitu vingine vya kimwili, ao kwa kuwasaidia kuhangaikia watu wa familia yao wenye wanaishi mbali nao. (Gal. 6:2) Kama wale wenye walikuwa katika utumishi wa wakati wote wanatumwa katika kutaniko lenu wakati mugao wao unabadilika, usiwaze kama ile mabadiliko inaonyesha kama walifanya jambo fulani la mubaya mu mugao wao wa zamani. * Lakini, uwasaidie wazoee kwa vyepesi hali yao ya mupya. Uwakaribishe kwa furaha na kuwapongeza juu ya kazi yenye wamefanya, hata kama afya haiwaruhusu tena kufanya mambo mingi. Ujikaze kuwajua muzuri. Uache wakusaidie kupitia ujuzi wao, mazoezi yao, na uzoefu wao.

13. Ni musaada gani tunaweza kupatia wale wenye mugao wao umebadilika?

13 Ku mwanzo, wale wenye mugao wao umebadilika wanaweza kuwa na lazima ya musaada wako juu ya kupata nyumba, kazi, namna ya kusafiri, na mambo ingine ya lazima. Pia, wanaweza kuwa na lazima ya habari za sasa juu ya mambo ya kawaida, kama vile namna ya kulipa kodi (taxe), na namna ya kupata matunzo ya muzuri. Lakini zaidi sana, wako na lazima uwaelewe kuliko kuwasikilia tu huruma. Pengine wanapiganisha magumu ya afya yao wenyewe ao ya watu wa jamaa yao. Pengine wako na huzuni juu mupendwa wao amekufa. * Na pengine wako pia na huzuni, hata kama hawaionyeshe waziwazi, kwa sababu wanakumbuka marafiki wenye walikuwa nao mu mugao wao wa zamani. Mara mingi kujisikia vile kunaweza kufanya wavurugike, na inaomba wakati ili waache kujisikia vile.

14. Namna gani wahubiri wa eneo fulani walisaidia dada mumoja azoee mugao wake mupya?

14 Kama unahubiri nao na kuwatia moyo kupitia mufano wako, unaweza kuwasaidia wazoee hali yao ya mupya. Dada mumoja mwenye alitumikia kwa miaka mingi katika inchi ingine anasema hivi: “Mu mugao wangu wa zamani, nilikuwa ninaongoza mafunzo ya Biblia kila siku. Wakati mugao wangu ulibadilika, ilikuwa nguvu kupata hata nafasi ya kufungua Biblia ao kuonyesha video mu mahubiri. Lakini wahubiri wa eneo hilo walikuwa wananiomba niwasindikize wakati walienda kurudilia watu ao kuongoza mafunzo ya Biblia. Kuona namna ndugu na dada hao wenye bidii na wenye uhodari wanaongoza mafunzo ya Biblia yenye kufanya maendeleo, kulinisaidia nikuwe na mawazo ya muzuri juu ya watu wa eneo hilo. Nilijifunza namna ya kuanzisha mazungumuzo katika eneo hilo la mupya. Ile mambo yote ilinisaidia nikuwe tena na furaha.”

ENDELEA KUFANYA YOTE YENYE UNAWEZA!

Fikiria namna mbalimbali za kupanua utumishi wako katika eneo la kwenu (Picha hii inapatana na fungu la 15-16) *

15. Unaweza kufanya nini ili upate matokeo ya muzuri wakati mugao wako unabadilika?

15 Unaweza kupata matokeo ya muzuri wakati mugao wako unabadilika. Usione kama umeshindwa ao umerudia nyuma kwa sababu mugao wako umebadilika. Ufikirie namna Yehova anaendelea kukusaidia na uendelee kuhubiri. Uige mufano wa Wakristo waaminifu wa wakati wa mitume. Kila mahali kwenye walijikuta, ‘walipita katika inchi wakitangaza habari njema ya lile neno.’ (Mdo. 8:1, 4) Bidii yako ya kuendelea kuhubiri inaweza kuleta matokeo ya muzuri. Kwa mufano, mapainia fulani wenye walifukuzwa katika inchi moja walihamia katika inchi ya karibu, kwenye kulikuwa pia lazima kubwa ya wahubiri katika luga yenye walikuwa wanazungumuza. Mu miezi kidogo, vikundi vya mingi vilianzishwa mu ile luga.

16. Unaweza kufanya nini ili upate furaha wakati mugao wako unabadilika?

16 “Shangwe ya Yehova ni nguvu yenu.” (Ne. 8:10, maelezo ya chini) Urafiki wetu pamoja na Yehova njo wenye unapaswa kutuletea shangwe ao furaha, hapana mugao wetu, hata kama tunaupenda sana. Kwa hiyo, uendelee kutembea pamoja na Yehova, umutegemee ili akupatie hekima, muongozo, na musaada. Ukumbuke kama ulifikia kupenda mugao wako kwa sababu ulijikaza sana ili kusaidia watu. Upende sana mugao wako wa sasa na uone namna Yehova anakusaidia upende mugao huo pia.​—Muh. 7:10.

17. Tunapaswa kukumbuka nini juu ya mugao wenye tuko nao sasa?

17 Tunapaswa kukumbuka kama tutamutumikia Yehova milele, lakini mugao wenye tuko nao sasa ni wa muda. Katika dunia mupya, migao yetu sisi wote inaweza kubadilika. Aleksey, mwenye tulizungumuzia ku mwanzo wa habari hii, anasema kama kubadilika kwa mugao wake kunamusaidia akuwe tayari juu ya mabadiliko ya wakati wenye kuja. Aleksey anasema: “Sikuzote nilijua kama Yehova iko kabisa na kama ulimwengu mupya haiko jambo la kuwazia tu, lakini kwa njia fulani niliona kuwa Yehova alikuwa mbali na mimi na kuwa ulimwengu mupya ulikuwa mbali. Sasa ninamuona Yehova kuwa karibu sana na mimi na ninaona kuwa ulimwengu mupya hauko tena mbali.” (Mdo. 2:25) Hata kama tuko na mugao gani, tuendelee basi kutembea pamoja na Yehova. Hatatuacha hata kidogo, lakini atatusaidia tuendelee kupata furaha katika mambo yote yenye tunaweza kufanya katika utumishi wake, hata tukuwe wapi.​—Isa. 41:13.

WIMBO 90 Tianeni Moyo

^ fu. 5 Wakati fulani, ndugu na dada wenye kuwa katika utumishi wa wakati wote wanaweza kulazimika kuacha mugao wao ao wanaweza kupewa mugao mupya. Habari hii inazungumuzia magumu yenye wanaweza kupambana nayo na mambo yenye inaweza kuwasaidia kuzoea hali yao ya mupya. Inazungumuzia pia mambo yenye wengine wanaweza kufanya ili kuwatia moyo na kuwategemeza, na pia kanuni zenye zinaweza kutusaidia sisi wote wakati kunakuwa mabadiliko mu maisha yetu.

^ fu. 4 Vilevile, kisha kueneza miaka fulani, ndugu wengi wenye kuwa na madaraka wameachia ndugu vijana madaraka yao. Ona habari yenye kichwa “Wakristo Wenye Kuzeeka​—Yehova Anapendezwa Sana na Ushikamanifu Wenu,” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 9, 2018, na “Endelea Kuwa na Amani ya Akili Hata Kama Hali Zinabadilika,” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 10, 2018.

^ fu. 12 Wazee wa kutaniko kwenye walikuwa wanatumikia wanapaswa kuandika barua ya kuwatambulisha bila kukawia, ili waendelee kutumika kama mapainia, wazee, ao watumishi wa huduma.

^ fu. 13 Ona habari zenye kichwa “Musaada kwa Wale Wenye Wamefiwa na Mupendwa Wao” katika Amuka! Na. 3 ya mwaka wa 2018.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Bwana mumoja na bibi yake wenye wanalazimika kuacha mugao wao wa umisionere katika inchi ingine, wanalia wakati wanaaga kutaniko lao.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati bwana huyo na bibi yake wanarudia katika inchi yao, wanamuomba Yehova kwa bidii ili awasaidie kupambana na magumu yao.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Yehova anasaidia bwana huyo na bibi yake kurudilia tena utumishi wa wakati wote. Wanatumia luga yenye walijifunza wakati walikuwa wamisionere ili kuhubiria habari njema watu wenye kuhamia katika eneo la kutaniko lao mupya.