Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 44

Fanya Urafiki Wenye Nguvu Pamoja na Wengine Mbele Mwisho Ufike

Fanya Urafiki Wenye Nguvu Pamoja na Wengine Mbele Mwisho Ufike

“Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote.”​—MEZ. 17:17.

WIMBO 101 Kufanya Kazi Pamoja kwa Umoja

KIFUPI CHA HABARI *

Tutakuwa na lazima ya marafiki wazuri wakati wa “taabu kubwa” (Picha hii inapatana na fungu la 2) *

1-2. Kulingana na 1 Petro 4:7, 8, ni nini itatusaidia kupambana na magumu?

KADIRI tunaendelea kukaribia mwisho wa “siku za mwisho,” tunaweza kupambana na magumu makali. (2 Ti. 3:1) Kwa mufano, kisha uchaguzi kufanyika katika inchi moja ya Afrika mangaribi, kulitokea muvurugo na jeuri yenye ililetwa na vikundi vya watenda-mabaya. Kwa zaidi ya miezi sita, ndugu na dada hawakuweza kutembea kwa uhuru kwa sababu walikuwa katika eneo la vita. Ni nini iliwasaidia ili wapambane na ile magumu? Wamoja walikimbia katika nyumba za ndugu wenye walikuwa wanaishi mu eneo lenye lilikuwa na usalama. Ndugu mumoja alisema hivi: “Katika hali kama ile, nilifurahia kuwa na marafiki pembeni yangu. Tulitiana moyo.”

2 Wakati “taabu kubwa” itaanza, tutafurahia kuwa na marafiki wazuri wenye kutupenda. (Ufu. 7:14) Kwa hiyo, ni jambo la haraka tufanye urafiki wenye nguvu pamoja na wengine sasa. (Soma 1 Petro 4:7, 8.) Mufano wa Yeremia unaweza kutufundisha mambo mingi. Marafiki wake walimusaidia aokoke wakati wa magumu yenye ilitangulia kuharibiwa kwa Yerusalemu. * Namna gani tunaweza kumuiga Yeremia?

MUFANO WA YEREMIA UNATUFUNDISHA NINI?

3. (a) Ni nini ingemufanya Yeremia ajitenge na wengine? (b) Yeremia alimuambia Baruku nini, na hilo lilileta matokeo gani?

3 Kwa miaka 40 hivi, Yeremia aliishi kati ya watu wenye hawakukuwa washikamanifu, kutia ndani majirani wake na pengine watu fulani wa jamaa yake kutoka katika muji wa Anatoti kwenye alizaliwa. (Yer. 11:21; 12:6) Lakini, hakujitenga na wengine. Kwa kweli, alimuambia Baruku, mwandishi wake muaminifu namna alikuwa anajisikia, na sisi pia tunajua namna alikuwa anajisikia kwa sababu ile mambo iliandikwa katika Biblia. (Yer. 8:21; 9:1; 20:14-18; 45:1) Kwa kweli, Baruku na Yeremia walifikia kupendana na kuheshimiana sana wakati Baruku alikuwa anaandika mambo yote yenye ilimufikia Yeremia.​—Yer. 20:1, 2; 26:7-11.

4. Yehova alimuomba Yeremia afanye nini, na namna gani ile kazi ilitia nguvu urafiki kati ya Yeremia na Baruku?

4 Kwa miaka mingi, Yeremia alikuwa ameonya kwa ujasiri Waisraeli juu ya mambo yenye ingefikia muji wa Yerusalemu. (Yer. 25:3) Mara ingine yenye Yehova alitia watu moyo watubu, alimuomba Yeremia aandike katika kitabu cha kukunjwa maonyo yenye alimupatia. (Yer. 36:1-4) Wakati Yeremia na Baruku waliendelea kutumika pamoja ile kazi yenye Mungu aliwapatia, yenye pengine ilifanya miezi fulani, kwa kweli, mambo yenye walikuwa wanaongea ilitia nguvu imani yao.

5. Ni nini inaonyesha kama Baruku alikuwa rafiki muzuri wa Yeremia?

5 Wakati walimaliza kuandika kitabu cha kukunjwa, Yeremia alipaswa kutuma Baruku rafiki yake, ili atangazie watu ule ujumbe. (Yer. 36:5, 6) Baruku alitimiza kwa uhodari mugao wake wenye ulikuwa hatari. Kwa kweli, Yeremia alijivunia sana Baruku wakati Baruku alienda ku hekalu na kufanya jambo lenye aliombwa afanye. (Yer. 36:8-10) Wakubwa wa Yuda walisikia habari juu ya jambo lenye Baruku alikuwa amefanya, na walimuamuru awasomee kitabu cha kukunjwa kwa sauti kubwa! (Yer. 36:14, 15) Wakubwa waliamua kumuambia Mufalme Yehoyakimu mambo yenye Yeremia alikuwa amesema. Kwa sababu walimuhangaikia Baruku, walimuambia hivi: “Uende na mujifiche, wewe pamoja na Yeremia, na musiache mutu yeyote ajue kwenye muko.” (Yer. 36:16-19) Hilo lilikuwa shauri la muzuri kabisa!

6. Namna gani Yeremia na Baruku walitenda wakati walipingwa?

6 Mufalme Yehoyakimu alikasirika sana wakati alisikia maneno yenye Yeremia aliandika; kwa hiyo, akaunguza kitabu hicho cha kukunjwa na akatoa amri Yeremia na Baruku wakamatwe. Lakini Yeremia hakuogopa. Alikamata kitabu kingine cha kukunjwa, akakipatia Baruku, na wakati Yeremia alikuwa anasema ujumbe wa Yehova, Baruku alikuwa anaandika “maneno yote ya kile kitabu cha kukunjwa chenye Mufalme Yehoyakimu wa Yuda alikuwa ameteketeza katika moto.”​—Yer. 36:26-28, 32.

7. Pengine ni nini ilitokea wakati Yeremia na Baruku walikuwa wanatumika pamoja?

7 Watu wenye wanavumilia magumu pamoja, mara mingi wanapendanaka sana. Kwa hiyo, inawezekana kabisa kama wakati Yeremia na Baruku walitumika pamoja ili kuandika tena maneno yenye ilikuwa katika kitabu cha kukunjwa chenye Mufalme muovu Yehoyakimu aliunguza, walijuana muzuri na wakakuwa marafiki wa sana. Namna gani mufano wa wanaume hao wawili waaminifu unaweza kutusaidia?

AMBIA MARAFIKI WAKO MAWAZO YAKO NA NAMNA UNAJISIKIA

8. Ni nini inaweza kutuzuia kufanya urafiki wenye nguvu pamoja na wengine, na juu ya nini hatupaswe kuvunjika moyo?

8 Tunaweza kuona kama ni nguvu kuambia wengine mawazo yetu na namna tunajisikia kwa sababu pengine mutu fulani alituvunja moyo zamani. (Mez. 18:19, 24) Ao tunaweza kuwaza kama hatuna wakati na nguvu za kufanya urafiki wenye nguvu pamoja na wengine. Lakini hatupaswe kuvunjika moyo. Kama tunapenda ndugu na dada zetu watusaidie wakati wa magumu, tunapaswa kujifunza kuwatumainia sasa kwa kuwaambia mawazo yetu na namna tunajisikia. Ile njo hatua ya maana ya kupata marafiki wa kweli.​—1 Pe. 1:22.

9. (a) Namna gani Yesu alionyesha kama alitumainia marafiki wake? (b) Namna gani kuzungumuza waziwazi na wengine kunaweza kukusaidia ukuwe na urafiki wenye nguvu? Leta mufano.

9 Yesu alionyesha kama alikuwa anatumainia marafiki wake kwa sababu alikuwa anazungumuza nao waziwazi na bila kuwaficha kitu. (Yoh. 15:15) Tunaweza kumuiga kwa kuambia wengine mambo yenye kutuletea furaha, mahangaiko yetu, na mambo yenye kutuvunja moyo. Usikilize kwa uangalifu wakati mutu fulani anazungumuza na wewe, na unaweza kutambua kama iko na mawazo na miradi yenye iko sawa na yako na anajisikia kama wewe. Fikiria mufano wa Cindy, dada mwenye kuwa na miaka 29. Alifanya urafiki na dada mumoja painia mwenye kuitwa Marie-Louise mwenye kuwa na miaka 67. Cindy na Marie-Louise wanahubiri pamoja kila Siku ya Ine asubui, na wanazungumuzia waziwazi mambo mbalimbali. Cindy anasema hivi: “Ninafurahia mazungumuzo mazito pamoja na marafiki wangu kwa sababu hilo linanisaidia kuwajua na kuwaelewa.” Wakati unaambia marafiki wako mawazo yako na namna unajisikia na unawasikiliza wakati wanaongea, urafiki wenu unakuwa wenye nguvu zaidi. Kama unazungumuza na wengine kwa uchangamufu na waziwazi kama vile Cindy anafanyaka, inawezekana kabisa urafiki wako pamoja nao utakuwa wenye nguvu zaidi.​—Mez. 27:9.

KUTUMIKA PAMOJA

Marafiki wazuri wanahubiri pamoja (Picha hii inapatana na fungu la 10)

10. Kulingana na Mezali 27:17, tunaweza kupata matokeo gani wakati tunatumika pamoja na ndugu na dada zetu?

10 Kama vile Yeremia na Baruku, wakati tunatumika pamoja na ndugu na dada zetu na kuona sifa zao za muzuri, tunaiga mufano wao na tunafanya urafiki wenye nguvu pamoja nao. (Soma Mezali 27:17.) Kwa mufano, unajisikia namna gani wakati uko mu mahubiri na unasikia namna rafiki yako anatetea kwa ujasiri imani yake na anaongea kwa usadikisho juu ya Yehova na juu ya makusudi yake? Inawezekana utamupenda zaidi.

11-12. Toa mufano wenye kuonyesha namna kuhubiri pamoja na wengine kunaweza kutusaidia kutia nguvu urafiki wetu pamoja na wengine.

11 Fikiria mifano mbili yenye kuonyesha namna kuhubiri pamoja na wengine kunafanya watu wakuwe marafiki. Adeline, dada mwenye kuwa na miaka 23, alimuomba, dada Candice, mumoja kati ya marafiki wake, aende pamoja naye kuhubiri katika eneo lenye halihubiriwe sana. Anasema hivi: “Tulipenda kuwa na bidii zaidi na kufurahia zaidi kazi ya kuhubiri. Sisi wawili tulikuwa na lazima ya kutiwa moyo ili tuendelee kumutumikia Yehova kulingana na uwezo wetu.” Kuhubiri pamoja kuliwaletea faida gani? Adeline anasema hivi: “Kila mangaribi, tulizungumuzia namna tulikuwa tunajisikia, mambo yenye ilitutia moyo juu ya mazungumuzo yenye tulifanya, na namna tuliona kuwa Yehova alituongoza katika mahubiri. Sisi wawili tulikuwa tunafurahia ile mazungumuzo mazito na tulifikia hata kujuana muzuri.”

12 Laïla na Marianne, dada wawili wenye hawajaolewa wa inchi ya Ufaransa, walienda kuhubiri kwa majuma tano katika Bangui, muji mukubwa wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, wenye kuwa na watu wengi. Laïla anakumbuka hivi: “Mimi na Marianne tulipata magumu, lakini kuwa na mazungumuzo ya muzuri na kuonyeshana upendo wa kweli kulifanya urafiki wetu ukuwe wenye nguvu zaidi. Wakati niliona Marianne anajipatanisha kwa vyepesi na hali za mupya, namna alipenda watu wa eneo, na bidii yake katika kazi ya kuhubiri, nilimuheshimia tena zaidi.” Haiombe uhamie katika inchi ingine ili upate zile faida. Kila wakati unahubiri mu eneo lenu pamoja na ndugu ao dada yako, uko na nafasi ya kumujua muzuri zaidi na kufanya urafiki wenu ukuwe wenye nguvu zaidi.

KAZA AKILI JUU YA SIFA ZA MUZURI ZA WENGINE, NA UKUWE MWENYE KUSAMEHE

13. Tunatambua nini wakati tunatumika karibu sana na marafiki wetu?

13 Mara mingi wakati tunatumika karibu sana na marafiki wetu, tunatambua sifa zao za muzuri na pia uzaifu wao. Ni nini inaweza kutusaidia tuendelee kuwa na urafiki wenye nguvu hata kama wako na uzaifu fulani? Fikiria tena mufano wa Yeremia. Ni nini ilimusaidia aendelee kuona sifa za muzuri za wengine na asikaze akili juu ya uzaifu wao?

14. Yeremia alijifunza nini juu ya Yehova, na hilo lilimusaidia namna gani?

14 Yeremia aliandika kitabu chenye kuitwa kwa jina lake, na inawezekana aliandika pia vitabu vya Biblia vyenye kuitwa 1 Wafalme na 2 Wafalme. Kwa kweli, kazi hiyo ilimusaidia aone kama Yehova ni mwenye rehema sana kuelekea wanadamu wenye hawakamilike. Kwa mufano, alijua kama wakati Mufalme Ahabu alitubu matendo yake ya mubaya, Yehova aliamua kama hataleta uharibifu juu ya familia yake yote wakati alikuwa angali muzima. (1 Fa. 21:27-29) Vilevile, Yeremia alijua kama Manase alifanya mambo yenye ilimuchukiza Yehova sana kuliko ile yenye Ahabu alifanya. Hata hivyo, Yehova alimusamehe Manase kwa sababu alitubu. (2 Fa. 21:16, 17; 2 Ny. 33:10-13) Habari hizo zilipaswa kumusaidia Yeremia aige uvumilivu wa Mungu na rehema yake katika namna ya kutendea marafiki wake wa sana.​—Zb. 103:8, 9.

15. Namna gani Yeremia aliiga uvumilivu wa Yehova wakati Baruku alikengeushwa?

15 Fikiria namna Yeremia alimutendea Baruku wakati alikengeushwa kwa wakati fulani katika mugao wake. Kuliko kumuacha haraka Baruku, rafiki yake, Yeremia alimusaidia kwa kumuambia ujumbe muzuri na wenye ulikuwa wazi wenye ulitoka kwa Mungu. (Yer. 45:1-5) Habari hii inaweza kutufundisha nini?

Marafiki wazuri wanasameheana kwa kupenda (Picha hii inapatana na fungu la 16)

16. Kulingana na Mezali 17:9, tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na wengine?

16 Kusema kweli, hatuwezi kutazamia ukamilifu kwa ndugu na dada zetu. Kwa hiyo, kisha kufanya urafiki wenye nguvu pamoja na wengine, tunapaswa kujikaza sana ili urafiki huo uendelee. Kama marafiki wetu wanafanya makosa, tunaweza kuwatolea mashauri ya upole lakini ya wazi yenye kutegemea Neno la Mungu. (Zb. 141:5) Na kama wanatukwaza, tunapaswa kuwasamehe. Kisha kuwasamehe, tunapaswa kuepuka kuzungumuzia tena mambo yenye walitufanyiaka. (Soma Mezali 17:9.) Ni jambo la maana sana katika nyakati hizi za magumu kukaza akili juu ya sifa za muzuri za ndugu na dada zetu kuliko kukaza akili juu ya uzaifu wao! Kufanya vile kunatia nguvu urafiki wetu pamoja nao, na tutakuwa na lazima ya marafiki wa sana wakati wa taabu kubwa.

ONYESHA UPENDO MUSHIKAMANIFU

17. Namna gani Yeremia alijionyesha kuwa rafiki wa kweli wakati wa magumu?

17 Nabii Yeremia alijionyesha kuwa rafiki wa kweli wakati wa magumu. Kwa mufano, Ebed-meleki, ofisa wa makao ya mufalme alimuokoa Yeremia ili asikufe katika tangi la murefu lenye lilikuwa na matope. Kisha kufanya vile, aliogopa kama wakubwa wangemutendea mubaya. Wakati Yeremia alijua jambo hilo, hakunyamaza, na kuwaza kama rafiki yake angevumilia kwa nguvu yake mwenyewe. Hata kama Yeremia alikuwa mufungwa, alifanya nguvu yake yote ili kumuambia Ebed-meleki, rafiki yake, ahadi yenye kufariji kutoka kwa Yehova.​—Yer. 38:7-13; 39:15-18.

Marafiki wazuri wanasaidia ndugu na dada zao wenye kuwa na lazima ya musaada (Picha hii inapatana na fungu la 18)

18. Kulingana na Mezali 17:17, tunapaswa kutenda namna gani wakati rafiki yetu anapata magumu?

18 Leo, ndugu na dada zetu wako na magumu mbalimbali. Kwa mufano, wengi wanateseka juu ya misiba ya asili ao misiba yenye kuletwa na mwanadamu. Wakati ile misiba inatokea, wamoja kati yetu wanaweza kuwa na uwezo wa kukaribisha marafiki hao katika nyumba zao. Wengine wanaweza kuwa na uwezo wa kutoa feza ili kuwasaidia. Lakini sisi wote tunaweza kumuomba Yehova asaidie ndugu na dada zetu. Wakati tunapata habari kama ndugu ao dada yetu amevunjika moyo, tunaweza kukosa jambo la kusema ao namna ya kutenda. Lakini sisi wote tunaweza kusaidia. Kwa mufano, tunaweza kupitisha wakati fulani pamoja na rafiki yetu. Tunaweza kumusikiliza kwa huruma wakati iko anazungumuza. Na tunaweza kuzungumuzia pamoja naye andiko fulani lenye tunapendaka sana. (Isa. 50:4) Jambo la maana zaidi ni kuwa pamoja na marafiki wako wakati wako na lazima yako.​—Soma Mezali 17:17.

19. Namna gani kufanya urafiki wenye nguvu sasa kutatusaidia wakati wenye kuja?

19 Tunapaswa kuazimia kukomalisha na kuendeleza urafiki wenye nguvu pamoja na ndugu na dada zetu sasa. Juu ya nini? Juu maadui wetu watajaribu kuleta migawanyiko kati yetu kwa kutumia habari za uongo. Watajaribu kutufanya tuache kutumainia na kutegemeza ndugu na dada zetu. Lakini, hawataweza kufanya vile. Hawataweza kutufanya tuache kupendana. Hakuna jambo lenye wanaweza kufanya ili kuharibu urafiki wenye tumekwisha kufanya pamoja na ndugu na dada zetu. Kwa kweli, urafiki huo hautaendelea tu mupaka mwisho wa mupangilio huu wa mambo lakini utaendelea milele!

WIMBO 24 Njooni Kwenye Mlima wa Yehova

^ fu. 5 Kadiri mwisho unaendelea kukaribia, sisi wote tuko na lazima ya kufanya urafiki wenye nguvu pamoja na ndugu na dada zetu. Katika habari hii, tutazungumuzia mambo yenye mufano wa Yeremia unaweza kutufundisha. Pia, tutazungumuzia namna kufanya urafiki wenye nguvu pamoja na wengine kutatusaidia wakati wa magumu.

^ fu. 2 Matukio yenye kuzungumuziwa mu kitabu cha Yeremia haiandikwe kulingana na namna ilifuatana.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Picha hii inaonyesha mambo yenye inaweza kutokea wakati wa “taabu kubwa.” Ndugu na dada fulani wanakutana katika chumba chenye kuwa katika sehemu ya juu ya nyumba. Kwa sababu wako marafiki, wanafarijiana wakati huo wa magumu. Picha hizi tatu zenye kufuata zinaonyesha kama ndugu na dada hao walikuwa wamefanya urafiki wenye nguvu mbele taabu kubwa ianze.