Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 47

Mambo Yenye Kitabu cha Mambo ya Walawi Kinatufundisha

Mambo Yenye Kitabu cha Mambo ya Walawi Kinatufundisha

“Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.”​—2 TI. 3:16.

WIMBO 98 Maandiko​—Yaliongozwa na Roho ya Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Leo, juu ya nini Wakristo wanapaswa kupendezwa na kitabu cha Mambo ya Walawi?

MUTUME PAULO alimukumbusha Timoteo, rafiki yake kijana, kama “kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.” (2 Ti. 3:16) Kitabu cha Mambo ya Walawi ni sehemu ya kila andiko. Uko na mawazo gani juu ya kitabu hicho cha Biblia? Watu fulani wanawaza kama kitabu hicho kiko na sheria mingi zenye hazitumike wakati wetu, lakini Wakristo wa kweli hawana ile mawazo.

2 Kitabu cha Mambo ya Walawi kiliandikwa kumepita miaka 3 500 hivi, lakini Yehova alilinda kitabu hicho “ili kutufundisha sisi.” (Ro. 15:4) Kwa sababu kitabu cha Mambo ya Walawi kinaonyesha wazi mawazo ya Yehova, tunapaswa kufurahia kujifunza kitabu hicho. Kwa kweli, kitabu hicho chenye kiliongozwa na roho ya Mungu kinaweza kutufundisha mambo mingi. Tuzungumuzie mambo ine kati ya ile mambo.

MAMBO YENYE TUNAPASWA KUFANYA ILI YEHOVA ATUKUBALI

3. Kila mwaka Siku ya Kufunika Zambi, juu ya nini zabihu zilikuwa zinatolewa?

3 Jambo la kwanza: Tunapaswa kukubaliwa na Yehova ili akubali zabihu zetu. Kila mwaka Siku ya Kufunika Zambi, Waisraeli walikuwa wanakusanyika pamoja, na kuhani mukubwa alikuwa anatoa zabihu za wanyama. Zabihu hizo zilikumbusha Waisraeli kama walikuwa na lazima ya kusamehewa zambi zao! Lakini mbele kuhani mukubwa atoe zabihu yoyote ya damu ndani ya Patakatifu Zaidi siku hiyo, alipaswa kufanya jambo lingine. Jambo hilo lilikuwa la maana zaidi kuliko kusamehewa kwa zambi za taifa.

(Picha hii inapatana na fungu la 4) *

4. Kulingana na Mambo ya Walawi 16:12, 13, kuhani mukubwa alikuwa anafanya nini wakati aliingia kwa mara ya kwanza ndani ya Patakatifu Zaidi Siku ya Kufunika Zambi? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

4 Soma Mambo ya Walawi 16:12, 13. Wazia mambo yenye inafanyika Siku ya Kufunika Zambi: Kuhani mukubwa anaingia ndani ya tabenakulo. Hii ni mara ya kwanza kati ya mara tatu zenye anapaswa kuingia ndani ya Patakatifu Zaidi siku hiyo. Katika mukono moja, anabeba chetezo chenye kujaa uvumba wenye marashi, na katika mukono ingine, anabeba chetezo chenye kujaa makaa yenye kuwaka. Anasimama mbele ya pazia (ao rido) yenye kufunika muingilio wa Patakatifu Zaidi. Kwa heshima kubwa, anaingia ndani ya Patakatifu Zaidi na kusimama mbele ya sanduku la agano. Kwa njia ya mufano, anasimama kabisa mbele ya Yehova Mungu! Sasa kwa uangalifu, kuhani anamwangia uvumba mutakatifu kwenye makaa ya moto, na chumba kinajaa harufu ya muzuri. * Kisha ataingia tena ndani ya Patakatifu Zaidi akiwa na damu ya matoleo ya zambi. Lakini, anachoma kwanza uvumba mbele ya kutoa damu ya matoleo ya zambi.

5. Kutumia uvumba Siku ya Kufunika Zambi, kunatufundisha nini?

5 Kutumia uvumba Siku ya Kufunika Zambi, kunatufundisha nini? Biblia inaonyesha kama sala za watumishi waaminifu wa Yehova zenye anakubali ziko kama uvumba. (Zb. 141:2; Ufu. 5:8) Kumbuka kama wakati kuhani alikuwa analeta uvumba mbele ya Yehova, alikuwa anafanya vile kwa heshima kubwa. Vilevile, wakati tunamukaribia Yehova katika sala, tunafanya vile kwa heshima kubwa. Tuko wenye shukrani sana kwa sababu Muumbaji wa ulimwengu wote anaturuhusu tumukaribie zaidi kama vile mutoto anamukaribiaka baba yake. (Yak. 4:8) Anakubali tukuwe marafiki wake! (Zb. 25:14) Tunafurahia sana pendeleo hilo; kwa hiyo hatupendi kumuhuzunisha hata kidogo.

6. Kuhani mukubwa alikuwa anachoma kwanza uvumba mbele atoe zabihu, hilo linatufundisha nini juu ya Yesu?

6 Kumbuka kama kuhani mukubwa alipaswa kuchoma kwanza uvumba mbele atoe zabihu. Kwa kufuata hatua zote kwa uangalifu juu ya namna ya kuchoma uvumba, kuhani mukubwa alikuwa anahakikisha kama Mungu angemukubali wakati angetoa zabihu. Jambo hilo linaweza kutufundisha nini juu ya Yesu? Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alipaswa kufanya jambo fulani la maana mbele atoe uzima wake kuwa zabihu, na jambo hilo lilikuwa la maana zaidi kuliko kuokoa wanadamu. Ni jambo gani? Alipaswa kumutii Yehova kwa ushikamanifu maisha yake yote ku dunia ili Yehova akubali zabihu yake. Kwa kufanya vile, Yesu angeonyesha kama kufanya mambo namna Yehova anapenda njo namna ya muzuri ya kuishi. Yesu angetetea ao kuonyesha kama mamlaka makubwa ya Baba yake, ni kusema, namna yake ya kutawala ni yenye kufaa na yenye haki.

7. Juu ya nini maisha yote ya Yesu ku dunia ilimufurahisha Baba yake?

7 Katika maisha yake yote ku dunia, Yesu aliendelea kutii kwa ukamilifu kanuni za haki za Yehova. Hata kama alipata majaribu na magumu na angekufa kifo chenye maumivu makali, aliazimia kuonyesha kama namna ya kutawala ya Baba yake njo ya muzuri zaidi. (Flp. 2:8) Wakati Yesu alipata magumu, alisali “kwa vilio vyenye nguvu na machozi.” (Ebr. 5:7) Sala zenye alitoa kwa moyo wote zilionyesha kama alikuwa mushikamanifu kwa Yehova na zilimusaidia aazimie hata zaidi kumutii. Yehova aliona sala za Yesu kama harufu ya uvumba muzuri sana. Mu maisha yake yote ku dunia, Yesu alimufurahisha sana Baba yake na kutetea namna yake ya kutawala.

8. Namna gani tunaweza kumuiga Yesu?

8 Tunaweza kumuiga Yesu kwa kufanya nguvu yetu yote ili kuishi maisha ya uaminifu-mushikamanifu na kushikamana na kanuni na sheria za Yehova. Wakati tunapata magumu, tunasali kwa moyo wetu wote ili kumuomba Yehova musaada kwa sababu tunapenda kumufurahisha. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tunaunga mukono namna ya Yehova ya kutawala. Tunaelewa kama Yehova hatakubali sala zetu kama tuko tunafanya mambo yenye anachukia. Lakini, kama tunaishi kulingana na kanuni zake, tunaweza kuwa hakika kama Yehova ataona sala zetu zenye tunatoa kwa moyo wote kama uvumba wenye harufu ya muzuri sana. Na tunaweza kuwa hakika kama utii na ushikamanifu wetu unamufurahisha Baba yetu wa mbinguni.​—Mez. 27:11.

TUNAMUTUMIKIA YEHOVA JUU TUKO WENYE SHUKRANI KWAKE NA TUNAMUPENDA

(Picha hii inapatana na fungu la 9) *

9. Juu ya nini watu walikuwa wanatoa zabihu za ushirika?

9 Jambo la pili: Tunamutumikia Yehova juu tuko wenye shukrani kwake. Ili kukazia jambo hilo, tuzungumuzie matoleo ya ushirika, sehemu ingine ya maana ya ibada ya kweli katika Israeli ya zamani. * Katika kitabu cha Mambo ya Walawi, tunajifunza kama Mwisraeli angetoa zabihu ya ushirika ili “kuonyesha shukrani.” (Law. 7:11-13, 16-18) Hakukuwa anatoa toleo hilo juu alilazimishwa kufanya vile, lakini juu alipenda kufanya vile. Kwa hiyo, toleo hilo lilikuwa la kujipendea lenye mutu alikuwa anatoa kwa sababu alimupenda Yehova, Mungu wake. Mutu mwenye alitoa toleo hilo, familia yake, na makuhani walikuwa wanakula nyama ya munyama mwenye alitolewa kuwa zabihu. Lakini sehemu fulani za munyama wa zabihu zilikuwa zinatolewa tu kwa Yehova. Ni sehemu gani?

(Picha hii inapatana na fungu la 10) *

10. Zabihu za ushirika zenye kuzungumuziwa mu Mambo ya Walawi 3:6, 12, 14-16, zinatufundisha nini juu ya nia yenye ilimuchochea Yesu afanye mapenzi ya Baba yake?

10 Jambo la tatu: Juu tunamupenda Yehova, tunamupatia jambo la muzuri zaidi. Yehova aliona mafuta kuwa sehemu ya muzuri zaidi ya munyama. Alisema pia kama sehemu fulani za munyama kutia ndani figo, zilikuwa za maana sana. (Soma Mambo ya Walawi 3:6, 12, 14-16.) Kwa hiyo, Yehova alifurahi zaidi sana wakati Mwisraeli alimutolea kwa kujipendea sehemu za maana na mafuta. Mwisraeli mwenye alitoa toleo kama hilo alionyesha kama alipenda sana kumutolea Mungu jambo la muzuri zaidi. Vilevile, Yesu alimutolea Yehova kwa kujipendea jambo la muzuri zaidi kwa kumutumikia kwa nafsi yake yote kwa sababu alimupenda. (Yoh. 14:31) Yesu alifurahia kufanya mapenzi ya Mungu; alipenda sana sheria ya Mungu. (Zb. 40:8) Kwa kweli, Yehova alifurahi sana wakati aliona Yesu anamutumikia vile kwa kujipendea!

Kumupenda Yehova kunatuchochea tumupatie jambo la muzuri zaidi (Picha hii inapatana na fungu la 11-12) *

11. Juu ya nini utumishi wetu uko kama zabihu za ushirika, na namna gani hilo linaweza kututia moyo?

11 Utumishi wetu kwa Yehova uko kama vile zabihu za ushirika kwa sababu utumishi huo unaonyesha namna tunamupenda Yehova sana. Tunamutolea Yehova jambo la muzuri zaidi kwa sababu tunamupenda kwa moyo wetu wote. Kwa kweli, Yehova anafurahi sana wakati anaona mamilioni ya watu wenye wanamutumikia kwa kujipendea kwa sababu wanamupenda sana na wanapenda kanuni zake! Tunaweza kutiwa moyo wakati tunakumbuka kama Yehova haonake tu mambo yenye tunafanya katika utumishi wake lakini anaona pia nia yenye kutuchochea kufanya ile mambo. Kwa mufano, kama uko mwenye kuzeeka na hauwezi tena kufanya mambo mingi kama vile ungependa kufanya, ukuwe hakika kama Yehova anaelewa mipaka yako. Unaweza kuona kama hauna tena uwezo wa kufanya mambo mingi, lakini Yehova anaona namna unamupenda sana na upendo huo unakuchochea kufanya mambo yenye unaweza kufanya. Anafurahia mambo yenye unaweza kumutolea kulingana na uwezo wako.

12. Yehova alijisikia namna gani wakati Waisraeli walikuwa wanamutolea matoleo ya ushirika, na hilo linatuhakikishia nini?

12 Zabihu za ushirika zinaweza kutufundisha nini? Wakati moto ulikuwa unaunguza sehemu za muzuri sana za munyama, moshi ulikuwa unapanda juu na Yehova alikuwa anafurahi. Kwa hiyo, ukuwe hakika kama Yehova anafurahia utumishi wenye unamutolea kwa kujipendea na kwa nafsi yako yote. (Kol. 3:23) Wazia namna anakufurahia. Mambo yenye unafanya katika kazi yake, ikuwe mingi ao kidogo, anaiona kuwa ya maana sana na ataikumbuka milele.​—Mt. 6:20; Ebr. 6:10.

YEHOVA IKO ANABARIKI TENGENEZO LAKE

13. Kulingana na Mambo ya Walawi 9:23, 24, Yehova alifanya nini ili kuonyesha kama alikubali Haruni na wana wake wenye waliwekwa kuwa makuhani?

13 Jambo la ine: Yehova iko anabariki sehemu ya ku dunia ya tengenezo lake. Fikiria jambo lenye lilitokea mu mwaka wa 1512 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati tabenakulo ilisimamishwa kwenye sehemu ya chini ya Mulima Sinai. (Kut. 40:17) Musa aliongoza sherehe ya kumuweka Haruni na wana wake ili wakuwe makuhani. Taifa la Israeli lilikusanyika ili kuona namna makuhani watatoa zabihu zao za kwanza za wanyama. (Law. 9:1-5) Yehova alifanya nini ili kuonyesha kama alikubali makuhani wapya wenye waliwekwa? Wakati Musa na Haruni walikuwa wanabariki watu, Yehova alishusha moto kutoka mbinguni na ukateketeza sehemu ya zabihu yenye ilibakia ku mazabahu.​—Soma Mambo ya Walawi 9:23, 24.

14. Yehova alionyesha kama alikubali Haruni na wana wake wenye waliwekwa kuwa makuhani, juu ya nini jambo hilo ni la maana kwetu?

14 Moto wenye ulishuka kutoka mbinguni ulionyesha nini? Yehova alituma moto kutoka mbinguni ili kuonyesha kama alikubali na kutegemeza Haruni na wana wake wenye waliwekwa ili wakuwe makuhani. Wakati Waisraeli waliona ushuhuda wenye ulionyesha waziwazi kama Yehova alikuwa anategemeza makuhani hao, walielewa kama wao pia walipaswa kuwategemeza kabisa. Juu ya nini jambo hilo ni la maana kwetu? Juu ukuhani katika Israeli ulifananisha ukuhani mukubwa zaidi. Kristo njo Kuhani Mukubwa zaidi, na kuko watu 144 000, wenye kuwa makuhani na wafalme wenye watatumika pamoja naye mbinguni.​—Ebr. 4:14; 8:3-5; 10:1.

Yehova iko anabariki na kuongoza tengenezo lake. Tunategemeza tengenezo hilo kwa moyo wetu wote (Picha hizi zinapatana na fungu la 15-17) *

15-16. Ni nini imeonyesha kama Yehova anamukubali “mutumwa muaminifu na mwenye busara”?

15 Katika mwaka wa 1919, Yesu aliweka kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta ili wakuwe “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” Mutumwa huyo anaongoza kazi ya kuhubiri na anatolea wanafunzi wa Kristo “chakula chao kwa wakati wenye kufaa.” (Mt. 24:45) Tunaona ushuhuda wenye kuwa wazi wenye kuonyesha kama Mungu anamukubali mutumwa muaminifu na mwenye busara?

16 Shetani na wale wenye kumuunga mukono wanajikaza kusimamisha kazi ya mutumwa muaminifu. Bila musaada wa Yehova, mutumwa huyo hangeweza kufanya kazi hiyo. Ijapokuwa matokeo ya vita mbili za ulimwengu, mateso yenye kuendelea, matatizo ya feza katika dunia yote, na kutendewa bila haki, mutumwa muaminifu na mwenye busara anaendelea kutolea chakula cha kiroho wanafunzi wa Yesu hapa ku dunia. Fikiria chakula mingi sana cha kiroho chenye tunapata leo bila kulipa, katika luga zaidi ya 900! Huo ni ushuhuda wenye kuwa wazi wenye kuonyesha kama Mungu anaendelea kumutegemeza mutumwa huyo. Fikiria ushuhuda mwingine wenye kuonyesha kama Yehova anabariki mutumwa huyo: kazi ya kuhubiri. Habari njema inahubiriwa kabisa “katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Mt. 24:14) Kwa kweli, Yehova anaongoza na kubariki sana tengenezo lake leo.

17. Namna gani tunaweza kutegemeza tengenezo lenye Yehova iko anatumia?

17 Tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Niko mwenye shukrani kwa sababu niko katika sehemu ya ku dunia ya tengenezo la Yehova?’ Yehova ametupatia ushuhuda wenye kusadikisha kabisa kama vile moto wenye ulitoka mbinguni katika siku za Musa na Haruni. Tunapaswa kuwa wenye shukrani kwa Yehova kwa sababu tuko mu tengenezo lake. (1 Te. 5:18, 19) Namna gani tunaweza kutegemeza tengenezo lenye Yehova iko anatumia? Tunafanya vile wakati tunafuata muongozo wenye kutegemea Biblia wenye tunapewa mu vichapo vyetu, ku mikutano, na mikusanyiko yetu. Tena, tunaweza kufanya vile kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha kwa bidii kulingana na uwezo wetu.​—1 Ko. 15:58.

18. Unaazimia kufanya nini?

18 Tuazimie basi kutumia mambo yenye kitabu cha Mambo ya Walawi kimetufundisha. Tujikaze kukubaliwa na Yehova ili akubali zabihu zetu. Tumutumikie Yehova kwa sababu tuko wenye shukrani kwake. Tuendelee kumutolea Yehova jambo la muzuri zaidi kwa sababu tunamupenda kwa moyo wetu wote. Na tutegemeze kwa moyo wetu wote tengenezo lenye iko anatumia leo. Kama tunafanya ile mambo yote, tunaweza kumuonyesha Yehova kama sisi Mashahidi wake tunafurahia pendeleo lenye tuko nalo la kumutumikia!

WIMBO 96 Kitabu cha Mungu Ni Hazina

^ fu. 5 Kitabu cha Mambo ya Walawi kiko na sheria zenye Yehova alipatia taifa la zamani la Israeli. Sisi Wakristo, hatuongozwe na sheria hizo, lakini zinaweza kutufundisha mambo fulani. Katika habari hii, tutazungumuzia mambo ya maana sana yenye kitabu cha Mambo ya Walawi kinatufundisha.

^ fu. 4 Uvumba wenye ulikuwa unachomwa katika tabenakulo ulionwa kuwa mutakatifu, na katika Israeli ya zamani uvumba ulitumiwa tu katika ibada ya Yehova. (Kut. 30:34-38) Hakuna habari yenye kuonyesha kama Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanachoma uvumba katika ibada yao.

^ fu. 9 Ili kupata habari zaidi juu ya matoleo ya ushirika, ona kitabu Étude perspicace des Écritures, Buku la 2, uku. 847.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Siku ya Kufunika Zambi, kuhani mukubwa katika Israeli alikuwa anaingia ndani ya Patakatifu Zaidi na iko na uvumba na makaa yenye kuwaka, ili kujaza chumba harufu ya uvumba wenye harufu ya muzuri. Kisha, aliingia tena ndani ya Patakatifu Zaidi akiwa na damu ya matoleo ya zambi.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Mwisraeli fulani anamupatia kuhani kondoo kwa ajili ya zabihu ya ushirika, ili kuonyesha kama familia yake iko yenye shukrani kwa Yehova.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa utumishi wake ku dunia, Yesu alionyesha kama anamupenda sana Yehova kwa kuendelea kutii amri zake na kwa kusaidia wanafunzi wake pia wafanye vile.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Dada mwenye kuzeeka, hata kama hana tena nguvu za kimwili, anamupatia Yehova jambo la muzuri zaidi kwa kuandikia watu barua ili kuwahubiria.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Katika Mwezi wa 2, 2019, Ndugu Gerrit Lösch wa Baraza Lenye Kuongoza alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mupya yenye kurekebishwa katika luga ya Kijerumani. Wasikilizaji walikuwa wenye shukrani sana na wenye furaha. Kama dada hawa wawili, leo wahubiri katika Ujerumani wanafurahi kutumia Biblia yao ya mupya mu mahubiri.