Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Ufalme wa Mungu ni nini? Unafanya nini? Na kwa nini tunapaswa kusali uje?

Yesu ni Mfalme wa Ufalme wa Mungu.

Luka 1:31-33: “Nawe utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi, na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

Ufalme ulikuwa kichwa kikuu cha mahubiri ya Yesu.

Mathayo 9:35: “Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuponya kila aina ya ugonjwa na kila aina ya udhaifu.”

Yesu aliwaeleza wanafunzi wake kuhusu ishara ambayo ingewasaidia kutambua Ufalme umekaribia kuja.

Mathayo 24:7: “Kwa maana taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali.”

Leo wanafunzi wa Yesu wanahubiri kuhusu Ufalme wa Mungu duniani kote.

Mathayo 24:14: “Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.”

Wanafurahia amani na umoja katika familia kwa sababu wenzi wa ndoa wanapendana na kuheshimiana.​WAEFESO 5:22, 23, 33.

Wana furaha na wanaishi maisha yenye kuridhisha kwa sababu “[wanatambua] uhitaji wao wa kiroho.”​MATHAYO 5:3.