Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu

Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu

Yesu alifundisha wafuasi wake kusali hivi: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe. Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.” (Matayo 6:9, 10) Ufalme wa Mungu ni nini? Uko unafanya nini? Na juu ya nini tunapaswa kusali ukuje?

Yesu Ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu.

Luka 1:31-33: “Utamupatia jina Yesu. Huyo atakuwa mukubwa na ataitwa Mwana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi; na Yehova Mungu atamupatia kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, na atatawala akiwa Mufalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

Ufalme njo ilikuwa kichwa kikubwa cha mahubiri ya Yesu.

Matayo 9:35: “Yesu akatoka ili kutembelea miji na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuponyesha kila namna ya ugonjwa na kila namna ya uzaifu.”

Yesu alipatia wanafunzi wake alama yenye ingewasaidia kujua kama Ufalme uko karibu kuja.

Matayo 24:7: “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine.”

Leo, wanafunzi wa Yesu wanahubiri katika dunia yote kuhusu Ufalme.

Matayo 24:14: “Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”