Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Chagua Kuunga Mukono Ufalme wa Mungu Leo!

Chagua Kuunga Mukono Ufalme wa Mungu Leo!

Wazia unasikia habari kama katika eneo kwenye unaishi kutatokea upepo mukubwa. Wakubwa wa serikali wako wanasema: “MUFANYE HARAKA! MUTAFUTE FASI YA KUKIMBILIA!” Utafanya nini? Bila shaka, utaenda fasi kwenye unaweza kupata usalama.

Kwa njia fulani, sisi wote tuko na tukio lenye linatungojea lenye linaweza kufananishwa na upepo mukubwa, tukio lenye Yesu aliita “taabu kubwa.” (Matayo 24:21) Hatuwezi kuenda fasi fulani ili kuepuka tukio hilo. Lakini tunaweza kufanya jambo fulani ili tupate usalama wakati wa taabu kubwa. Ni jambo gani lenye tunaweza kufanya?

Katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu Kristo alishauria watu hivi: “Basi, muendelee kutafuta kwanza Ufalme [wa Mungu] na haki yake.” (Matayo 6:33) Tunafanya vile namna gani?

Tunatafuta kwanza Ufalme wa Mungu. Ile inamaanisha kama tunapaswa kuona Ufalme wa Mungu kuwa jambo la maana sana kuliko jambo lingine lolote. (Matayo 6:25, 32, 33) Juu ya nini tunapaswa kufanya vile? Juu wanadamu hawana uwezo wa kumaliza magumu yao wenyewe. Ni Ufalme wa Mungu tu njo wenye unaweza kufanya vile.

Tunatafuta haki ya Mungu. Tunapaswa kujikaza kuishi kulingana na sheria na kanuni za Mungu za haki. Juu ya nini? Juu kama tunajiamulia sisi wenyewe mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa, matokeo itakuwa mubaya. (Mezali 16:25) Kwa upande mwingine, wakati tunaishi kulingana na kanuni za Mungu, tunamufurahisha Mungu, na zaidi ya ile tunajipatia faida sisi wenyewe.​—Isaya 48:17, 18.

Muendelee kutafuta kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake. Yesu alionya kama watu fulani wangekengeuka na kufikiri kuwa wanaweza kupata usalama kwa kutafuta feza mingi. Wengine wanaweza kuacha mahangaiko ya maisha iwalemee na kufikia kukosa wakati wa kutafuta Ufalme wa Mungu.​—Matayo 6:19-21, 25-32.

Yesu alitoa ahadi kama wale wenye wanaunga mukono Ufalme wa Mungu watapata mambo yenye wako nayo lazima sasa na kama watafurahia baraka za milele wakati wenye kuja.​—Matayo 6:33.

Hata kama wanafunzi wa Yesu wa wakati wa mitume walikuwa wanatafuta kwanza Ufalme na haki yake, hawakuona mwisho wa maumivu na mateso yote katika siku zao. Lakini walilindwa. Namna gani?

Waliishi kulingana na kanuni za Mungu za haki, na ile iliwalinda kutokana na magumu yenye wale wenye walizarau mambo yenye Mungu alisema walipata. Imani yao yenye kuwa nguvu ya kama Ufalme wa Mungu utakuja iliwasaidia kupambana hata na matatizo makubwa sana. Na Mungu aliwapatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida” ili waweze kupambana muzuri na ile matatizo.​—2 Wakorinto 4:7-9.

UTATAFUTA KWANZA UFALME?

Wakristo wa wakati wa mitume walitii amri ya Yesu ya kutafuta kwanza Ufalme. Walihubiri habari njema ya Ufalme katika eneo lao lote la dunia. (Wakolosai 1:23) Kuko watu wenye kufanya ile kazi leo?

Ndiyo! Mashahidi wa Yehova wanajua kama wakati wenye unabakia mbele Ufalme wa Mungu umalize mupangilio huu wa mambo ni mufupi. Kwa hiyo, wanafanya yote yenye wanaweza ili kuishi kulingana na maneno hii ya Yesu: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—Matayo 24:14.

Utakubali ile habari njema? Tunakutia moyo kuiga wakaaji wa wakati wa mitume wa muji wa Beroya katika eneo la Makedonia. Wakati mutume Paulo aliwatangazia habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu, walikubali ujumbe wake “kwa hamu kubwa ya akili.” Kisha ‘walichunguza Maandiko kwa uangalifu’ ili kuhakikisha kama mambo yenye walisikia ilipatana na maandiko, na walitenda kulingana na mambo yenye walijifunza.​—Matendo 17:11, 12.

Wewe pia unaweza kufanya vile. Ikiwa unatafuta kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, utapata kimbilio na ulinzi sasa, na utafurahia amani na usalama wakati wenye kuja.