Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATHAYO 20-21

“Yeyote Anayetaka Kuwa Mkubwa Kati Yenu Lazima Awe Mhudumu Wenu”

“Yeyote Anayetaka Kuwa Mkubwa Kati Yenu Lazima Awe Mhudumu Wenu”

20:28

Waandishi na Mafarisayo wenye kiburi walipenda kutambuliwa na kusalimiwa na watu sokoni

Waandishi na Mafarisayo wenye majivuno walitaka kuwapendeza wanadamu na walitamani kutukuzwa. (Mt 23:5-7) Yesu alikuwa tofauti. ‘Mwana wa binadamu alikuja, si kuhudumiwa, bali kuhudumu.’ (Mt 20:28) Je, katika ibada yetu tunajihusisha tu na mambo ambayo yatatufanya tutambuliwe na kusifiwa na wengine? Ikiwa tunataka kuwa wakuu machoni pa Yehova, tutajitahidi kuwa kama Yesu kwa kufanya yote tuwezayo kuwahudumia wengine. Mara nyingi kazi kama hizo hufanywa bila kuonekana na wengine—zinatambuliwa tu na Yehova. (Mt 6:1-4) Mhudumu mnyenyekevu . . .

  • atashiriki kusafisha na kudumisha Jumba la Ufalme

  • atachukua hatua ya kwanza kuwasaidia watu wenye umri mkubwa na watu wengine

  • anatoa michango ili kutegemeza masilahi ya Ufalme