Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Mtegemee Yehova Unaposhughulika na Mtu Anayekuonea

Mtegemee Yehova Unaposhughulika na Mtu Anayekuonea

Waoneaji wanaweza kutusababishia maumivu ya kimwili na ya kihisia. Hata wanaweza kutudhuru kiroho ikiwa tutaogopa wanapopinga ibada yetu. Unaweza kujilindaje dhidi ya mtu anayekuonea?

Waabudu wengi wa Yehova wamemtegemea yeye na wamefaulu kushughulika na watu wanaowaonea. (Zb 18:17) Kwa mfano, Esta alimshtaki mwoneaji mwovu aliyeitwa Hamani na hivyo kufunua njama zake. (Est 7:​1-6) Kabla ya kufanya hivyo, alionyesha kwamba anamtegemea Yehova kwa kufunga kula. (Est 4:​14-16) Yehova alibariki matendo ya Esta kwa kulimlinda yeye na Wayahudi.

Kijana, unapokabiliwa na mwoneaji, mwombe Yehova msaada na uzungumzie tatizo lako na mtu mzima mkomavu, kama vile mzazi. Uwe na uhakika kwamba Yehova atakusaidia kama tu alivyomsaidia Esta. Unaweza kufanya nini kingine ili kukabiliana na watu wanaokuonea?

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MAISHA YANGU YA UTINEJA—NITAFANYA NINI NIKIONEWA? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Vijana wanaweza kujifunza nini kutokana na mifano ya Charlie na Ferin?

  • Wazazi wanaweza kujifunza nini kutokana na maelezo ya Charlie na Ferin kuhusu kuwasaidia watoto kukabiliana na mtu anayewaonea?