Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Umutegemee Yehova Wakati Wengine Wanakuonea

Umutegemee Yehova Wakati Wengine Wanakuonea

Watu wenye kutuonea wanaweza kutuletea maumivu ya kimwili na hata huzuni. Wanaweza hata kuregeza uhusiano wetu pamoya na Yehova ikiwa tunaogopa wakati wanapinga ibada yetu. Namna gani tunaweza kujilinda kutokana na watu hao?

Waabudu wengi wa Yehova walimutegemea Yehova na waliweza kupambana na watu wenye walipenda kuwaonea. (Zb 18:17) Kwa mufano, Esta alizungumuza na mufalme na kumuambia mupango mubaya wa mutu mwenye aliitwa Hamani. (Est 7:1-6) Mbele afanye vile alionyesha kama anamutegemea Yehova kwa kufunga. (Est 4:14-16) Yehova alibariki matendo ya Esta na alimulinda yeye na watu wake.

Kijana, ikiwa unakutana na mutu mwenye anapenda kukuonea, uombe Yehova akusaidie na uzungumuze na mutu mwenye kukomaa, sawa vile muzazi, kuhusu ile tatizo. Unaweza kuwa hakika kama Yehova atakusaidia sawa tu vile alisaidia Esta. Unaweza kufanya nini ingine ili kujua namna ya kutenda wakati wengine wanakuonea ao kukuchokoza?

MUANGALIE VIDEO MAISHA YANGU YA UJANA—NIFANYE NINI KAMA VIJANA WENZANGU WANANICHOKOZA? NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Mufano wa Charlie na Ferin unaweza kufundisha vijana nini?

  • Maneno ya Charlie na Ferin kuhusu namna ya kusaidia watoto wakati wengine wanawaonea inaweza kufundisha wazazi nini?