Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Wachungaji Wanaowanufaisha Watu wa Yehova

Wachungaji Wanaowanufaisha Watu wa Yehova

Watu wengi wana maoni yasiyofaa kuhusu watu wenye mamlaka. Inaeleweka kwa nini wana maoni hayo. Kwa muda mrefu wanadamu wametumia mamlaka yao kwa njia mbaya ili kujinufaisha wenyewe. (Mik 7:3) Tunashukuru sana kwamba wazee katika kutaniko wamezoezwa kutumia mamlaka yao kuwanufaisha watu wa Yehova.—Est 10:3; Mt 20:​25, 26.

Tofauti na watu wenye mamlaka katika ulimwengu huu, wazee hujitahidi kufikia mapendeleo kwa sababu wanampenda Yehova na watu wake. (Yoh 21:16; 1Pe 5:​1-3) Chini ya mwongozo wa Yesu, wachungaji hao wanawasaidia wahubiri wote kuhisi wao ni sehemu ya familia ya Yehova na kuendelea kukaa karibu na Yehova. Wanatenda upesi ili kutoa msaada wa kiroho kwa kondoo wa Yehova na kusaidia kunapokuwa na dharura ya kitiba au janga linapotokea. Ikiwa unahitaji msaada, kwa nini usichukue hatua ya kwanza kuwasiliana na mzee katika kutaniko lako?—Yak 5:14.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WACHUNGAJI WANAOTUNZA KUNDI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Mariana alinufaikaje kutokana na msaada aliopata kutoka kwa wazee?

  • Elias alinufaikaje kutokana na msaada aliopata kutoka kwa wazee?

  • Masimulizi uliyotazama yanakufanya uhisije kuhusu kazi ya wazee?