Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Wachungaji Wenye Wanasaidia Watu wa Yehova

Wachungaji Wenye Wanasaidia Watu wa Yehova

Watu wengi wako na mawazo yenye haifae juu ya wenye kuwa na mamlaka. Ile inaeleweka juu kwa miaka mingi wanadamu wametumia mubaya mamlaka yao ili kujitafutia faida. (Mik 7:3) Tuko wenye shukrani sana juu wazee katika makutaniko wanazoezwa kutumia mamlaka yao muzuri juu ya kusaidia watu wa Yehova.—Est 10:3; Mt 20:25, 26.

Tofauti na watu wenye mamlaka mu hii ulimwengu, wazee wanajikaza kufikia madaraka kwa sababu wanamupenda Yehova na watu wake. (Yoh 21:16; 1Pe 5:1-3) Chini ya uongozi wa Yesu, wale wachungaji wanasaidia kila muhubiri ajisikie muzuri mu familia ya waabudu wa Yehova na aendelee kuwa karibu na Yehova. Wako tayari kutolea kondoo wa Yehova musaada wa kiroho na kuwasaidia wakati kunatokea magonjwa yenye inaomba kushugulikia haraka ao wakati musiba unatokea. Kama uko na lazima ya musaada, kamata hatua ya kuzungumuza na muzee fulani mu kutaniko yenu—Yak 5:14.

MUANGALIE VIDEO WACHUNGAJI WENYE KUHANGAIKIA KONDOO, NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Namna gani wazee walisaidia Mariana?

  • Namna gani wazee walisaidia Elias?

  • Hii mifano inafanya ukuwe na mawazo gani juu ya kazi ya wazee?