Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Yehova Anaokoa Wale Wenye Kupondwa Roho

Yehova Anaokoa Wale Wenye Kupondwa Roho

Kila mutu anakuwaka na huzuni wakati fulani. Kuwa na huzuni haimaanishe kama mutu iko zaifu kiroho. Wakati fulani hata Yehova alionyesha kama alikuwa na huzuni. (Mwa 6:5, 6) Lakini tufanye nini kama tunazoea kusikia huzuni ya mingi ao ikiwa tunaisikia kila wakati?

Tafuta musaada kwa Yehova. Yehova anahangaikia sana afya yetu ya kiakili na namna tunajisikia. Anajua wakati tuko na furaha na wakati tuko na huzuni. Anaelewa juu ya nini tuko na mawazo ao hisia fulani. (Zb 7:9b) Na jambo ya maana zaidi, Yehova anatuhangaikia na anaweza kutusaidia kupambana na huzuni na hali ya kushuka moyo.—Zb 34:18.

Hangaikia afya yako ya kiakili. Mawazo ya kuvunja moyo inaweza kufanya tupoteze furaha na inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya ibada yetu. Njo maana tunapaswa kulinda moyo wetu, ni kusema hali yetu yote ya ndani.—Mez 4:23.

MUANGALIE VIDEO NAMNA NDUGU NA DADA ZETU WAKO NAFURAHIA AMANI HATA KAMA WANASHUKA MOYO, NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Nikki alifanya nini ili aweze kupambana na hali ya kushuka moyo?

  • Juu ya nini Nikki aliona kama alikuwa na lazima ya kuonana na munganga?—Mt 9:12

  • Namna gani Nikki alitafuta musaada wa Yehova?