Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na Hekima Yenye Kutoka kwa Mungu

Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na Hekima Yenye Kutoka kwa Mungu

Moja kati ya njia za muzuri zaidi yenye wazazi wanaweza kutumia ili kusaidia watoto wao wakuwe na hekima yenye kutoka kwa Mungu, ni kuwasaidia wafaidike na mikutano ya Kikristo. Mambo yenye watoto wanaona, wanasikia, na maelezo yenye wanatoa ku mikutano, inaweza kuwasaidia wajifunze mambo mingi juu ya Yehova na wakuwe marafiki wake. (Kum 31:12, 13) Kama uko muzazi, namna gani unaweza kusaidia mutoto wako afaidike kabisa na mikutano?

  • Ujikaze sana kufika ku Jumba ya Ufalme kwa ajili ya mikutano.—Zb 22:22

  • Mbele ao kisha mukutano, pitisha wakati na ndugu na dada ku Jumba ya Ufalme.—Ebr 10:25

  • Hakikisha kama kila mutu mu familia iko na vichapo vyenye vitatumiwa ku mukutano, ikuwe vya kielektroniki ao vyenye kuchapishwa

  • Saidia mutoto wako atoe maelezo kwa kutumia maneno yake mwenyewe.—Mt 21:15, 16

  • Sema mambo ya muzuri kuhusu mikutano na mambo yenye tunajifunza ku mikutano

  • Saidia watoto wako wafanye mambo mbalimbali sawa vile kusaidia kusafisha Jumba ya Ufalme na kuzungumuza na ndugu na dada wenye kukomaa mu kutaniko

Ni kazi mingi kusaidia watoto wako wamukaribie Yehova, na wakati fulani inaweza kukulemea. Lakini ukuwe hakika kama Yehova atakusaidia.—Isa 40:29.

MUANGALIE VIDEO WAZAZI, MUTEGEMEE YEHOVA NA NGUVU YAKE, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Kuchoka kulikuwa na matokeo gani juu ya Zack na Leah?

  • Juu ya nini wazazi wanapaswa kumuomba Yehova awapatie nguvu?

  • Ni mu njia gani Zack na Leah walimutegemea Yehova ili wapate matokeo ya muzuri?