Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 3

Yehova Mungu Wako Anakuona Kuwa wa Maana!

Yehova Mungu Wako Anakuona Kuwa wa Maana!

“Alitukumbuka wakati tulikuwa katika hali ya chini.”​—ZB. 136:23.

WIMBO 33 Mtupie Yehova Mzigo Wako

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Watumishi wengi wa Yehova wanapambana na hali gani, na hali hizo zinaweza kuwafanya wajisikie namna gani?

FIKIRIA hali tatu zenye kufuata: Munganga anamuambia ndugu mumoja kijana kama iko na ugonjwa mubaya sana wenye utamufanya aendelee kuwa muzaifu. Ndugu mumoja mwenye kutumika kwa bidii mwenye kuwa na miaka zaidi ya 50 anapoteza kazi yake, anajikaza sana ili kupata kazi ingine lakini anashindwa kuipata. Dada mumoja muaminifu mwenye kuzeeka anaendelea kuwa muzaifu zaidi na kwa hiyo, hawezi tena kufanya mambo mingi katika kazi ya Yehova.

2 Kama uko katika hali moja kati ya hali zenye kutajwa pale juu, unaweza kujisikia kuwa hauko tena wa maana hata kidogo. Hali hizo zinaweza kukufanya upoteze furaha, ujisikie kuwa mutu wa bure, na kukufanya usikuwe na uhusiano muzuri pamoja na wengine.

3. Namna gani Shetani na watu wenye anachochea wanaona uzima wa mwanadamu?

3 Ulimwengu huu unaonyesha mawazo ya Shetani juu ya uzima wa mwanadamu. Sikuzote, Shetani ametendea watu kama vile hawako wa maana hata kidogo. Hata kama Shetani alikuwa anajua kwamba malipizi ya kukosa kutii ni kifo, bila huruma, alimuambia Eva kama kukosa kumutii Mungu kungemuletea uhuru. Shetani anaongoza sikuzote mashirika ya biashara, ya politike, na ya dini ya ulimwengu huu. Kwa hiyo, haishangaze kuona kuwa, kama Shetani, wafanyabiashara wengi, viongozi wengi wa politike, na viongozi wengi wa dini hawaone uzima wa mwanadamu kuwa wa maana na hawahangaikie namna watu wanajisikia.

4. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

4 Lakini, Yehova anapenda tujue kama tuko wa maana, na anatusaidia wakati tunapambana na hali zenye zinaweza kutufanya tujione kuwa watu wa bure. (Zb. 136:23; Ro. 12:3) Habari hii itazungumuzia namna Yehova anatusaidia katika hali zenye kufuata: (1) Wakati tunagonjwa, (2) wakati tuko na magumu ya kupata feza, na (3) wakati uzee unatufanya tuwaze kama hatuwezi tena kufanya jambo lolote mu kazi ya Yehova. Lakini, tuone kwanza juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anaona kila mumoja wetu kuwa wa maana.

YEHOVA ANATUONA KUWA WA MAANA

5. Ni nini inakuonyesha kama Yehova anaona wanadamu kuwa wa maana?

5 Hata kama tuliumbwa kwa mavumbi ya udongo, tuko wa maana zaidi kuliko mavumbi. (Mwa. 2:7) Fikiria tu sababu fulani zenye zinatuonyesha kama Yehova anatuona kuwa wa maana. Alituumba sisi wanadamu na uwezo wa kuiga sifa zake. (Mwa. 1:27) Kwa kufanya vile, alitufanya kuwa wa maana kuliko vitu vingine vyote vyenye aliumba ku dunia, na alitupatia mamlaka juu ya dunia na wanyama.​—Zb. 8:4-8.

6. Ni jambo gani lingine lenye kutuonyesha kama Yehova anaona wanadamu wenye hawakamilike kuwa wa maana?

6 Hata kisha Adamu kufanya zambi, Yehova aliendelea kuona wanadamu kuwa wa maana. Anatuona kuwa wa maana sana, njo maana alimutoa Yesu, Mwana wake mupendwa, kuwa bei ya ukombozi kwa ajili ya zambi zetu. (1 Yo. 4:9, 10) Yehova atatumia faida za bei ya ukombozi ili kufufua watu wote wenye wamekufa kwa sababu ya zambi ya Adamu, “wenye haki na wenye hawako wenye haki.” (Mdo. 24:15) Neno lake linaonyesha kama anatuona kuwa wa maana sana hata kama tuko wagonjwa, maskini, ao wenye kuzeeka.​—Mdo. 10:34, 35.

7. Watumishi wa Mungu wako na sababu gani zingine za kuwafanya waamini kama Yehova anawaona kuwa wa maana?

7 Tuko na sababu zingine za kutufanya tuamini kama Yehova anatuona kuwa wa maana. Ametuvuta kwake na aliona namna tulitenda wakati tulisikia habari njema. (Yoh. 6:44) Wakati tulianza kumukaribia Yehova, yeye pia alitukaribia zaidi. (Yak. 4:8) Pia, Yehova anatumia njia mingi ili kutufundisha, na kwa kufanya vile, anaonyesha kama anatuona kuwa wa maana. Anajua tuko watu wa namna gani leo na anajua kama tunaweza kufanya mabadiliko ya muzuri. Na anatutia nizamu kwa sababu anatupenda. (Mez. 3:11, 12) Ile mambo yote inaonyesha kabisa kama Yehova anatuona kuwa wa maana!

8. Maneno ya Zaburi 18:27-29 inatusaidia kuwa na mawazo gani juu ya magumu yetu?

8 Watu fulani walimuona Mufalme Daudi kuwa mutu wa bure, lakini alijua kama Yehova alimupenda na alikuwa anamusaidia. Kujua jambo hilo kulimusaidia Daudi avumilie hali yake akiwa na mawazo ya muzuri. (2 Sa. 16:5-7) Wakati tunajisikia kuwa wenye kushuka moyo ao wakati tunapata magumu, Yehova anaweza kutusaidia tuone mambo kwa njia tofauti na anaweza kutusaidia kushinda kizuizi chochote. (Soma Zaburi 18:27-29.) Wakati tunajua kama Yehova anatusaidia, hakuna kitu chenye kinaweza kufanya tuache kumutumikia kwa furaha. (Ro. 8:31) Tuzungumuzie basi hali hizo tatu; katika hali hizo tunapaswa zaidi sana kukumbuka kama Yehova anatupenda na anatuona kuwa wa maana.

WAKATI TUNATESEKA JUU YA UGONJWA

Kusoma maneno ya Yehova yenye iliongozwa na roho yake kutatusaidia kushinda mawazo yenye haifae yenye kuletwa na ugonjwa (Ona fungu la 9-12)

9. Ugonjwa unaweza kutufanya tujione namna gani?

9 Ugonjwa unaweza kutusumbua kiakili, kwa kutufanya tujisikie kama hatuko tena wa maana kwa mutu yeyote. Tunaweza kujisikia mubaya wakati watu wanatambua kama kuko jambo lenye haliendeke juu yetu ao wakati hatuwezi kufanya tena kitu bila musaada wa wengine. Hata wakati watu wengine hawatambue kama tuko wagonjwa, tunaweza kusikia haya juu hatuna tena uwezo wa kufanya mambo yenye tulikuwa tunafanya. Katika wakati huo wa magumu, Yehova anatutia moyo. Namna gani?

10. Kulingana na Mezali 12:25, ni nini inaweza kutusaidia wakati tuko wagonjwa?

10 Wakati tuko wagonjwa, “neno la muzuri” linaweza kututia moyo. (Soma Mezali 12:25.) Yehova ametia katika Biblia maneno ya muzuri yenye inatukumbusha kama anatuona kuwa wa maana hata kama tuko wagonjwa. (Zb. 31:19; 41:3) Kama tunasoma ao hata kusoma tena na tena ile maneno yenye iliongozwa na roho takatifu, atatusaidia kushinda mawazo yenye haifae yenye kuletwa na ugonjwa.

11. Namna gani ndugu mumoja aliona kama Yehova alimusaidia?

11 Fikiria mufano wa Jorge. Wakati Jorge alikuwa kijana, aligonjwa ugonjwa wenye ulifanya hali yake ikuwe mubaya haraka na ulimufanya ajisikie kuwa mutu wa bure. Jorge anasema hivi: “Sikukuwa nimejitayarisha juu ya namna ugonjwa wangu ulifanya nijisikie ao juu ya haya yenye nilisikia wakati wengine walikuwa wananiangalia. Wakati hali yangu ilifikia kuharibika zaidi, nilikuwa ninafikiria namna maisha yangu ingebadilika. Nilikuwa na huzuni sana, na nilimuomba Yehova anisaidie.” Namna gani Yehova alimusaidia? Jorge anasema hivi: “Kwa sababu nilikuwa na magumu ya kukaza akili yangu juu ya mambo fulani, nilitiwa moyo kusoma mistari kidogo mu Zaburi yenye kuonyesha kama Yehova anahangaikia watumishi wake. Nilisoma tena na tena mistari hiyo kila siku, na niliona kuwa ilikuwa inanifariji na kunitia moyo. Kisha wakati fulani, watu wengine walianza kuona kama nilianza kuonyesha zaidi sura ya kicheko. Hata walisema kama mawazo yangu ya muzuri iliwatia moyo. Nilitambua kama Yehova alikuwa amejibu sala zangu! Alikuwa amenisaidia kubadilisha namna nilikuwa ninajiona. Nilianza kukaza akili juu ya mambo yenye Neno lake linasema kuhusu namna alikuwa ananiona hata kama nilikuwa mugonjwa.”

12. Wakati unavumilia ugonjwa fulani, unaweza kufanya nini ili kupata musaada wa Yehova?

12 Kama uko unavumilia ugonjwa fulani, ukuwe hakika kama Yehova anajua hali yako. Umuombe akusaidie ili ukuwe na mawazo ya muzuri juu ya hali yako. Kisha, utumie Biblia ili kupata maneno ya muzuri yenye Yehova ametia ndani kwa ajili yako. Kazia akili maandiko yenye kuonyesha namna Yehova anaona watumishi wake kuwa wa maana sana. Ukifanya vile, utaona kama Yehova ni mwema kwa wale wote wenye wanamutumikia kwa uaminifu.​—Zb. 84:11.

WAKATI TUNAPAMBANA NA MAGUMU YA KUPATA FEZA

Kukumbuka kama Yehova anaahidi kama atatutimizia mahitaji yetu kutatusaidia wakati tunakosa kazi (Ona fungu la 13-15)

13. Kupoteza kazi kunaweza kufanya kichwa cha familia ajisikie namna gani?

13 Kila kichwa cha familia anapenda kuwa na uwezo wa kutimizia watu wa familia yake mahitaji yao. Lakini, wazia kama ndugu anapoteza kazi yake, hata kama hakufanya jambo lolote la mubaya. Anajikaza sana ili kupata kazi ingine, lakini anaikosa. Juu ya hali hiyo, anaweza kujisikia kuwa mutu wa bure. Namna gani kukaza akili juu ya ahadi za Yehova kunaweza kumusaidia?

14. Juu ya nini Yehova anatimiza ahadi zake?

14 Sikuzote, Yehova anatimiza ahadi zake. (Yos. 21:45; 23:14) Kuko sababu mbalimbali zenye zinamuchochea afanye vile. Kwanza, kama hafanye vile, jina lake ao sifa yake itachafuliwa. Yehova ameahidi kama atahangaikia watumishi wake washikamanifu, na anaona kama analazimika kutimiza ahadi hiyo. (Zb. 31:1-3) Tena, Yehova anajua kama sisi wenye kuwa sehemu ya familia yake, tunaweza kuhuzunika na kuvunjika moyo kama anakosa kutuhangaikia. Anaahidi kama atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima kimwili na kiroho, na hakuna kitu chenye kitamuzuia kutimiza ahadi yake!​—Mt. 6:30-33; 24:45.

15. (a) Wakristo wa wakati wa mitume walipata magumu gani? (b) Zaburi 37:18, 19 inatuhakikishia nini?

15 Wakati tunakumbuka juu ya nini Yehova anatimiza ahadi zake, tunaweza kuwa hakika kama atatusaidia wakati tunapambana na magumu ya kupata feza. Fikiria mufano wa Wakristo wa wakati wa mitume. Wakati kulitokea mateso makubwa juu ya kutaniko katika Yerusalemu, “wote, isipokuwa mitume, walitawanywa.” (Mdo. 8:1) Wazia hilo lilileta matokeo gani: magumu ya kupata feza! Inawezekana Wakristo walipoteza nyumba zao na kazi zao. Lakini, Yehova hakuwaacha; na hawakupoteza furaha yao. (Mdo. 8:4; Ebr. 13:5, 6; Yak. 1:2, 3) Yehova alitegemeza Wakristo waaminifu hao, na sisi pia atatutegemeza.​—Soma Zaburi 37:18, 19.

WAKATI TUNAVUMILIA MAGUMU YENYE KULETWA NA UZEE

Kukaza akili juu ya mambo yenye tunaweza kufanya, hata wakati tumezeeka, kutatusaidia tukuwe hakika kama Yehova anatuona kuwa wa maana na kazi yetu ya uaminifu (Ona fungu la 16-18)

16. Ni hali gani yenye inaweza kutufanya tuwaze kama Yehova haone ibada yetu kuwa ya maana?

16 Wakati tunaendelea kuzeeka, tunaweza kuanza kuwaza kama hatuwezi tena kufanya kitu katika kazi ya Yehova. Pengine Mufalme Daudi alikuwa na mawazo ya namna ile wakati aliendelea kuzeeka. (Zb. 71:9) Namna gani Yehova anaweza kutusaidia?

17. Mufano wa dada mwenye kuitwa Jheri unaweza kutufundisha nini?

17 Fikiria mufano wa dada mumoja mwenye kuitwa Jheri. Alialikwa kufuata mazoezi ku Jumba la Ufalme juu ya namna ya kutunza majengo mbalimbali yenye inatumiwa kwa ajili ya kazi ya Yehova, lakini hakupenda kuenda. Alisema hivi: “Niko mwenye kuzeeka, niko mujane, na sina hata ufundi moja wenye Yehova anaweza kutumia. Niko mutu wa bure.” Usiku wenye ulitangulia ile mazoezi, alimuelezea Yehova mambo yenye ilikuwa mu moyo wake. Wakati alifika ku Jumba la Ufalme siku yenye ilifuata, alikuwa angali anajiuliza ikiwa alistahili kabisa kuwa pale. Wakati wa mazoezi, mumoja kati ya wasemaji alikazia kama kuwa tayari kufundishwa na Yehova njo ufundi wa maana sana wenye tuko nao. Jheri anakumbuka hivi: “Niliwaza, ‘niko na ufundi huo!’ Nilianza kulia wakati nilitambua kama Yehova alikuwa anajibu sala yangu. Alikuwa ananihakikishia kama nilikuwa na jambo fulani la maana sana la kumutolea na kama alikuwa tayari kunifundisha!” Wakati Jheri anakumbuka jambo hilo, anasema hivi: “Wakati niliingia katika mukutano huo, nilikuwa na woga, mwenye kuvunjika moyo na mwenye huzuni. Lakini, wakati nilitoka ku mukutano huo, sikukuwa tena na woga, nilijisikia mwenye kutiwa moyo, na nilijisikia kuwa mutu wa maana!”

18. Namna gani Biblia inaonyesha kama Yehova anaendelea kuona ibada yetu kuwa ya maana wakati tunaendelea kuzeeka?

18 Wakati tunaendelea kuzeeka, tunaweza kuwa hakika kama Yehova angali anaweza kututumia. (Zb. 92:12-15) Yesu alituhakikishia kama Yehova anafurahia mambo yoyote yenye tunaweza kufanya katika kazi yake, hata kama uwezo wetu unapunguka namna gani ao hata kama mambo yenye tuko na uwezo wa kufanya inaonekana kuwa haina tena maana. (Lu. 21:2-4) Kwa hiyo, kaza akili juu ya mambo yenye unaweza kufanya. Kwa mufano, unaweza kuambia wengine juu ya Yehova, kusali kwa ajili ya ndugu na dada zako, na kutia wengine moyo waendelee kuwa waaminifu. Yehova anakuona kuwa mufanyakazi mwenzake, haiko juu ya mambo yenye unaweza kufanya, lakini juu uko tayari kumutii.​—1 Ko. 3:5-9.

19. Andiko la Waroma 8:38, 39 linatuhakikishia nini?

19 Tuko wenye shukrani sana juu ya pendeleo lenye tuko nalo la kumuabudu Yehova, Mungu mwenye anaona kabisa watu wenye kumutumikia kuwa wa maana! Alituumba ili tufanye mapenzi yake, na ibada ya kweli njo inafanya tukuwe na furaha mu maisha yetu. (Ufu. 4:11) Hata kama watu wa ulimwengu wanaweza kutuona kuwa watu wa bure, Yehova yeye hatuone vile. (Ebr. 11:16, 38) Wakati tunajisikia kuwa wenye kuvunjika moyo juu ya ugonjwa, magumu ya kupata feza, ao uzee, tukumbuke kama hakuna kitu kinaweza kututenganisha na upendo wa Baba yetu wa mbinguni.​—Soma Waroma 8:38, 39.

^ fu. 5 Umepambana na hali fulani mu maisha zenye zilikufanya ujisikie kuwa mutu wa bure? Habari hii itakukumbusha namna Yehova anakuona kuwa wa maana sana. Itazungumuzia namna unaweza kuendelea kujiona kuwa wa maana hata kutokee nini mu maisha yako.

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, Rafiki Yangu