Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 4

“Roho Yenyewe Inatoa Ushahidi”

“Roho Yenyewe Inatoa Ushahidi”

“Roho yenyewe inatoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi tuko watoto wa Mungu.”​—RO. 8:16.

WIMBO 25 Mali ya Pekee

KIFUPI CHA HABARI *

Kwa njia yenye kushangaza, Yehova alimwanga roho yake takatifu juu ya kikundi cha Wakristo karibu 120 siku ya Pentekoste (Ona fungu la 1-2)

1-2. Ni tukio gani la kushangaza lenye linatokea siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33?

NI SIKU YA YENGA asubui katika Yerusalemu. Ni mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu, na ni siku ya Pentekoste. Kikundi cha wanafunzi karibu 120 wanakusanyika pamoja mu chumba cha juu cha nyumba fulani. (Mdo. 1:13-15; 2:1) Siku kidogo mbele ya pale, Yesu alikuwa amewaamuru wabakie Yerusalemu kwa sababu walipaswa kupata zawadi ya pekee. (Mdo. 1:4, 5) Ni nini inatokea kisha?

2 ‘Mara moja kunatokea makelele mbinguni, kama ya upepo wenye nguvu, wenye unavuma.’ Makelele inajaza nyumba yote. Kisha, “ndimi kama za moto” zinatokea juu ya vichwa vya wanafunzi hao, na wote ‘wanajazwa roho takatifu.’ (Mdo. 2:2-4) Kwa njia hiyo yenye kushangaza, Yehova anamwanga roho yake takatifu juu ya wanafunzi hao. (Mdo. 1:8) Wanakuwa watu wa kwanza wenye wanatiwa mafuta kwa roho takatifu * na kupewa tumaini la kutawala pamoja na Yesu mbinguni.

MAMBO INAKUWAKA NAMNA GANI WAKATI MUTU ANATIWA MAFUTA?

3. Juu ya nini wale wenye walikuwa ku Pentekoste walikuwa hakika kabisa kama walitiwa mafuta kwa roho takatifu?

3 Kama ulikuwaka kati ya wale wanafunzi wenye walikusanyika mu chumba cha juu ile siku, haungesahau hata kidogo mambo yenye ilitokea. Kitu fulani chenye kilionekana kama ulimi wa moto kilitua juu ya kichwa chako, na ulianza kusema kwa luga! (Mdo. 2:5-12) Ungekuwa hakika kabisa kama umetiwa mafuta kwa roho takatifu. Lakini, je, wale wote wenye kutiwa mafuta kwa roho takatifu wanatiwa mafuta kwa njia fulani ya kushangaza na wakati uleule? Hapana. Juu ya nini?

4. Wakristo wote watiwa-mafuta wa wakati wa mitume walitiwa mafuta wakati uleule? Fasiria.

4 Tuzungumuzie basi ni wakati gani mutu anaweza kutiwa mafuta. Haiko tu kikundi hicho cha Wakristo karibu 120 njo wenye walitiwa mafuta kwa roho takatifu siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33. Siku ileile, kisha Wakristo hao kutiwa mafuta, wengine karibu 3 000 walipata pia roho takatifu yenye ilikuwa imeahidiwa. Walitiwa mafuta wakati walibatizwa. (Mdo. 2:37, 38, 41) Lakini, mu miaka yenye ilifuata, haiko Wakristo watiwa-mafuta wote njo walitiwa mafuta wakati walibatizwa. Wasamaria walitiwa mafuta wakati fulani kisha kubatizwa. (Mdo. 8:14-17) Na Kornelio na nyumba yake walitiwa mafuta kwa njia yenye haikukuwa ya kawaida: walitiwa mafuta mbele hata ya kubatizwa.​—Mdo. 10:44-48.

5. Kulingana na 2 Wakorinto 1:21, 22, mambo inakuwaka namna gani wakati mutu fulani anatiwa matuta kwa roho takatifu?

5 Tuzungumuzie pia mambo inakuwaka namna gani wakati mutu anatiwa mafuta kwa roho takatifu. Wakristo fulani wenye wanatiwa mafuta wanaweza kwanza kushindwa kuelewa kama Yehova amewachagua. Wanaweza kujiuliza hivi: ‘Juu ya nini Mungu alinichagua?’ Wengine hawawezi kujisikia vile. Ikuwe mutu anajisikia vile ao hapana, mutume Paulo anafasiria namna mambo inakuwaka kuhusu wale wote wenye wanatiwa mafuta. Anasema hivi: “Kisha ninyi kuamini, mulitiwa muhuri * kupitia yeye kwa roho takatifu yenye iliahidiwa, ambayo ni alama yenye kuhakikisha mbele ya wakati uriti wetu.” (Efe. 1:13, 14; maelezo ya chini) Kwa hiyo, Yehova anatumia roho yake takatifu ili kuhakikishia waziwazi kabisa Wakristo hao kama amewachagua. Kwa njia hiyo, roho takatifu ni “alama [uhakikisho ao ahadi]” yenye Mungu anatoa ili kuwahakikishia kama wakati wenye kuja, hawataishi milele ku dunia lakini wataishi milele mbinguni.​—Soma 2 Wakorinto 1:21, 22.

6. Mukristo mutiwa-mafuta anapaswa kufanya nini ili apate zawadi yake ya kuenda mbinguni?

6 Kama Mukristo fulani anatiwa mafuta, ni kusema kama ataenda tu mbinguni? Hapana. Iko hakika kama amechaguliwa ili kuenda mbinguni. Lakini, anapaswa kukumbuka onyo hili: “Ndugu, mujikaze sana ili kufanya mwito na kuchaguliwa kwenu kukuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe, kwa maana kama munaendelea kufanya mambo hayo, hamutashindwa hata kidogo.” (2 Pe. 1:10) Kwa hiyo, hata kama Mukristo mutiwa-mafuta amechaguliwa, ao kuitwa, ili aende mbinguni, atapata zawadi yake kama tu anabakia muaminifu.​—Flp. 3:12-14; Ebr. 3:1; Ufu. 2:10.

NAMNA GANI MUTU ANAJUAKA KAMA AMETIWA MAFUTA?

7. Namna gani Wakristo watiwa-mafuta wanajua kama wamealikwa ili waende mbinguni?

7 Lakini, namna gani mutu anajuaka kama amealikwa ili aende mbinguni? Jibu linaonekana wazi mu maneno yenye Paulo aliandikia Wakristo wa Roma “wenye waliitwa ili wakuwe watakatifu.” Aliwaambia hivi: “Hamukupokea roho ya utumwa yenye inaleta woga tena, lakini mulipokea roho ya kufanywa kuwa wana, roho yenye kupitia hiyo tunaita kwa sauti kubwa: ‘Abba, Baba!’ Roho yenyewe inatoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi tuko watoto wa Mungu.” (Ro. 1:7; 8:15, 16) Kwa hiyo, kupitia roho yake takatifu, Mungu anahakikishia waziwazi watiwa-mafuta kama amewaalika ili waende mbinguni.​—1 Te. 2:12.

8. Kulingana na 1 Yohana 2:20, 27, juu ya nini Wakristo watiwa-mafuta hawana lazima mutu yeyote awahakikishie kama wametiwa mafuta?

8 Yehova haache mashaka yoyote mu akili na mu moyo wa wale wenye anaalika ili waende mbinguni. (Soma 1 Yohana 2:20, 27.) Kwa kweli, Wakristo watiwa-mafuta wako na lazima ya kufundishwa na Yehova kupitia kutaniko kama vile tu watu wengine wote. Lakini, hawana lazima mutu yeyote awahakikishie kama wametiwa-mafuta. Yehova ametumia nguvu yake kubwa zaidi katika ulimwengu wote, ni kusema, roho yake takatifu ili kuwahakikishia kabisa kama wametiwa mafuta!

‘WANAZALIWA TENA’

9. Kulingana na Waefeso 1:18, kunatokea badiliko gani wakati mutu anatiwa mafuta?

9 Wengi kati ya watumishi wa Mungu leo wako na magumu ya kuelewa namna mambo inakuwaka wakati Mungu anatia mutu fulani mafuta. Juu ya nini? Juu wao wenyewe hawajatiwa mafuta. Mungu aliumba wanadamu ili waishi milele ku dunia, hapana mbinguni. (Mwa. 1:28; Zb. 37:29) Lakini Yehova amechagua watu fulani ili waishi mbinguni. Kwa hiyo, wakati anawatia mafuta, anabadilisha kabisa tumaini lao na namna yao ya kufikiri, ili wakuwe na hamu ya kuishi mbinguni.​—Soma Waefeso 1:18.

10. ‘Kuzaliwa tena,’ maana yake nini? (Ona pia maelezo ya chini.)

10 Wakati Wakristo wanatiwa mafuta kwa roho takatifu, ‘wanazaliwa tena’ ao ‘wanazaliwa kutoka juu.’ * Pia, Yesu alionyesha kama haiwezekane kufasiria kabisa-kabisa mutu fulani mwenye hakutiwa mafuta namna mutu anajisikiaka wakati ‘anazaliwa tena’ ao ‘kuzaliwa kwa roho.’​—Yoh. 3:3-8; maelezo ya chini.

11. Wakati mutu anatiwa mafuta, mawazo yake inabadilika namna gani? Fasiria.

11 Namna gani mawazo ya Wakristo inabadilika wakati wanatiwa mafuta? Mbele Yehova awatie mafuta, walikuwa wanafurahia sana tumaini lao la kuishi milele ku dunia. Walikuwa wanangojea kwa hamu sana wakati wenye Yehova atatosha mambo yote ya mubaya na kufanya dunia ikuwe paradiso. Pengine walikuwa wanajiwazia wako wanakaribisha mutu wa familia ao rafiki yao mwenye amekufa. Lakini, kisha kutiwa mafuta, mawazo yao ilibadilika. Juu ya nini? Haiko kusema kama hawakufurahia tena tumaini la kuishi milele ku dunia. Hawakubadilisha namna yao ya kufikiri kwa sababu walivunjika moyo ao kuteseka sana. Hawakuanza mara moja kuona kama kuishi milele ku dunia kutawachokesha. Lakini, Yehova alitumia roho yake takatifu ili kubadilisha namna yao ya kufikiri na tumaini lenye walifurahia sana.

12. Kulingana na 1 Petro 1:3, 4, Wakristo watiwa-mafuta wanajisikia namna gani juu ya tumaini lao?

12 Mutu fulani mwenye ametiwa mafuta anaweza kujiona kuwa hastahili kupata pendeleo hilo la muzuri sana. Lakini, hana mashaka hata kidogo kwamba Yehova amemuchagua. Iko mwenye furaha sana na mwenye shukrani wakati anafikiria tumaini lake la kuishi mbinguni.​—Soma 1 Petro 1:3, 4.

13. Namna gani Wakristo watiwa-mafuta wanaona maisha yao hapa ku dunia?

13 Sasa, ni kusema kama Wakristo watiwa-mafuta wanapendaka kufa? Mutume Paulo anajibu ulizo hilo. Alifananisha mwili wao wa kibinadamu na hema na akasema hivi: “Kwa kweli, sisi wenye tuko katika hema hii tunalia kwa maumivu, na tunalemewa, kwa sababu hatutaki kuvua hema hii, lakini tunataka kuvaa ile ingine, ili uzima umeze kile chenye kinaweza kufa.” (2 Ko. 5:4) Wakristo hao hawachoke na maisha ku dunia, na kupenda wakufe haraka. Lakini, wanapenda kuishi na kumutumikia Yehova pamoja na watu wa familia zao na marafiki wao kila siku. Hata hivyo, katika kila jambo lenye wanafanya, wanakumbuka kila siku tumaini la muzuri sana lenye wako nalo juu ya wakati wenye kuja.​—1 Ko. 15:53; 2 Pe. 1:4; 1 Yo. 3:2, 3; Ufu. 20:6.

YEHOVA AMEKUTIA MAFUTA?

14. Ni nini haionyeshe kama Mukristo ametiwa mafuta kwa roho takatifu?

14 Pengine uko unajiuliza ikiwa umetiwa mafuta kwa roho takatifu. Kama ni vile, fikiria maulizo hii ya maana: Unapenda sana kufanya mapenzi ya Mungu? Unajisikia kuwa uko na bidii sana mu kazi ya kuhubiri? Unafurahia sana kusoma Neno la Mungu na kujifunza juu ya “mambo mazito ya Mungu”? (1 Ko. 2:10) Unaona kama Yehova amekusaidia kupata matokeo ya muzuri sana mu kazi ya kuhubiri? Unaona kama uko na daraka kubwa la kusaidia wengine wamutumikie Yehova? Kuko mambo yenye inakuhakikishia kama Yehova amekusaidia katika sehemu mbalimbali za maisha yako? Kama unajibu ndiyo kwa ile maulizo yote, ile inaonyesha umealikwa ili kuenda mbinguni? Hapana. Juu ya nini? Juu watumishi wote wa Mungu wanaweza kujisikia vile, ikuwe wako watiwa-mafuta ao hapana. Na Yehova anaweza kutumia roho yake takatifu ili kupatia watumishi wake wote uwezo uleule, hata kama wako na tumaini la kuishi mbinguni ao ku dunia. Kwa kweli, kama unajiuliza ikiwa utaenda mbinguni, maana yake hauna mwaliko wa kuenda mbinguni. Wale wenye Yehova amealika hawajiulize ikiwa wametiwa mafuta ao hapana! Wanajua!

Yehova alitumia roho yake takatifu ili kupatia Abrahamu, Sara, Daudi, na Yohana Mubatizaji uwezo wa kufanya mambo ya ajabu, lakini hakutumia roho hiyo ili kuwapatia tumaini la kuishi mbinguni (Ona fungu la 15-16) *

15. Ni nini inatuonyesha kama haiko watu wote wenye wamepata roho takatifu njo wamechaguliwa ili kuenda mbinguni?

15 Biblia inazungumuzia mifano ya watu wengi wenye imani wenye walipata roho takatifu; lakini, hawakukuwa na tumaini la kuishi mbinguni. Kwa mufano, Daudi aliongozwa na roho takatifu. (1 Sa. 16:13) Roho takatifu ilimusaidia kuelewa mambo mazito juu ya Yehova na ilimuongoza pia kuandika sehemu fulani za Biblia. (Mk. 12:36) Lakini, mutume Petro alisema kama Daudi “hakupanda mbinguni.” (Mdo. 2:34) Yohana Mubatizaji ‘alijazwa roho takatifu.’ (Lu. 1:13-16) Yesu alisema kama hapakukuwa mutu mukubwa zaidi kama Yohana, lakini kisha alisema kama Yohana hangetawala katika Ufalme wa mbinguni. (Mt. 11:10, 11) Yehova alitumia roho yake takatifu ili kupatia watu hao uwezo wa kufanya mambo ya ajabu, lakini hakutumia roho yake ili kuwachagua waishi mbinguni. Ni kusema kama watu hao hawakukuwa waaminifu sana kama wale wenye kuchaguliwa ili kutawala mbinguni? Hapana. Ni kusema tu kama Yehova atawafufua ili waishi mu Paradiso hapa ku dunia.​—Yoh. 5:28, 29; Mdo. 24:15.

16. Leo, watumishi wengi wa Mungu wako na tumaini gani?

16 Watumishi wengi wa Mungu wenye kuwa ku dunia leo hawana tumaini la kuishi mbinguni. Kama vile Abrahamu, Sara, Daudi, Yohana Mubatizaji, na wanaume na wanamuke wengine wengi wa zamani, wanangojea kwa hamu kuishi ku dunia wakati Ufalme wa Mungu utawatawala.​—Ebr. 11:10.

17. Tutazungumuzia maulizo gani mu habari yenye kufuata?

17 Leo, kungali watiwa-mafuta fulani kati ya watu wa Mungu, kwa hiyo, tunaweza kujiuliza maulizo fulani. (Ufu. 12:17) Kwa mufano, watiwa-mafuta wanapaswa kujiona namna gani? Kama mutu fulani katika kutaniko lenu anaanza kula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho, unapaswa kumutendea namna gani? Na tuseme nini kama hesabu ya wale wenye wanasema kama ni watiwa-mafuta inaendelea kuongezeka? Unapaswa kuhangaika juu ya jambo hilo? Tutajibu ile maulizo mu habari yenye kufuata.

^ fu. 5 Kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 mupaka leo, Yehova amepatia Wakristo fulani tumaini la muzuri sana, ni kusema, tumaini la kutawala pamoja na Mwana wake mbinguni. Lakini, namna gani Wakristo hao wanajuaka kama wamechaguliwa ili kupata pendeleo hilo la muzuri sana? Ni nini inatokea wakati mutu anapata mwaliko huo? Habari hii inategemea habari moja yenye ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 1, 2016. Itajibu ile maulizo yenye kupendeza.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Kutiwa mafuta kwa roho takatifu: Yehova anatumia roho yake takatifu ili kuchagua mutu kusudi atawale pamoja na Yesu mbinguni. Kupitia roho yake, Mungu anapatia mutu huyo ahadi kwa ajili ya wakati wenye kuja, ao “alama yenye kuhakikisha mbele ya wakati.” (Efe. 1:13, 14) Wakristo watiwa-mafuta wanaweza kusema kama roho takatifu “inatoa ushahidi,” ao inawahakikishia waziwazi kama wako na tumaini la kuenda mbinguni.​—Ro. 8:16.

^ fu. 5 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Muhuri. Muhuri huo ni wa muda tu; unakuwa wa kudumu wakati mutu anakufa na iko muaminifu ao wakati fulani mbele taabu kubwa ianze.​—Efe. 4:30; Ufu. 7:2-4; ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 4, 2016 (SW).

^ fu. 10 Ili kupata mafasirio zaidi juu ya maana ya ‘kuzaliwa tena,’ ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 4, 2009, ukurasa wa 3-4, ukurasa wa 5, ukurasa wa 5-6, ukurasa wa 7-8, ukurasa wa 8-9, ukurasa wa 10-11, na ukurasa wa 11-12.

WIMBO 27 Kufunuliwa kwa Wana wa Mungu

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Ikuwe tunafungwa juu ya imani yetu ao tuko huru kuhubiri na kufundisha wengine kweli, tunaweza kungojea kwa hamu kuishi ku dunia wakati Ufalme wa Mungu utatutawala.