Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 5

Tutaenda Pamoja na Ninyi

Tutaenda Pamoja na Ninyi

“Tunataka kuenda pamoja na ninyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu iko pamoja na ninyi.”​—ZEK. 8:23.

WIMBO 26 Mlinitendea Mimi

KIFUPI CHA HABARI *

Kondoo wengine (“watu kumi”) wako na pendeleo la kumuabudu Yehova pamoja na watiwa-mafuta (“Muyahudi”) (Ona fungu la 1-2)

1. Yehova alisema kutatokea nini katika siku zetu?

YEHOVA alitabiri hivi juu ya siku zetu: “Watu kumi (10) kutoka katika luga zote za mataifa watashika, ndiyo, watashika kwa nguvu kanzu ya Muyahudi, wakisema: ‘Tunataka kuenda pamoja na ninyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu iko pamoja na ninyi.’” (Zek. 8:23) “Muyahudi” huyo anafananisha wale wenye Mungu ametia mafuta kwa roho takatifu. Wanaitwa pia “Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:16) “Watu kumi” wanafananisha wale wenye kuwa na tumaini la kuishi milele ku dunia. Wanajua kwamba Yehova amebariki kikundi hicho cha watiwa-mafuta na wanaona kuwa ni pendeleo kumuabudu Yehova pamoja nao.

2. Namna gani “watu kumi” ‘wanaenda pamoja na’ watiwa-mafuta?

2 Hata kama haiwezekane kujua majina ya watiwa-mafuta wote wenye kuwa ku dunia leo, * wale wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia wanaweza “kuenda pamoja” na watiwa-mafuta. Namna gani? Biblia inasema kama “watu kumi (10) watashika kwa nguvu kanzu ya Muyahudi, wakisema: ‘Tunataka kuenda pamoja na ninyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu iko pamoja na ninyi.’” Sehemu ya kwanza ya andiko inataja Muyahudi mumoja. Lakini sehemu yenye kufuata inatumia neno “ninyi.” Maana yake Muyahudi huyo haiko mutu moja tu lakini anafananisha kikundi chote cha watiwa-mafuta. Wale wenye hawako watiwa-mafuta wanamutumikia Yehova pamoja na watiwa-mafuta. Lakini, hawaone watiwa-mafuta kuwa viongozi wao; wanajua kama Yesu njo Kiongozi wao.​—Mt. 23:10.

3. Tutajibu maulizo gani katika habari hii?

3 Juu kungali Wakristo watiwa-mafuta kati ya watu wa Mungu leo, watu fulani wanaweza kujiuliza hivi: (1) Watiwa-mafuta wanapaswa kujiona namna gani? (2) Namna gani tunapaswa kutendea wale wenye wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho? (3) Tunapaswa kuhangaika ikiwa hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai inaongezeka? Tutajibu ile maulizo katika habari hii.

WATIWA-MAFUTA WANAPASWA KUJIONA NAMNA GANI?

4. Ni onyo gani lenye kupatikana mu 1 Wakorinto 11:27-29 lenye watiwa-mafuta wanapaswa kufikiria sana, na juu ya nini?

4 Watiwa-mafuta wanapaswa kufikiria sana onyo lenye kupatikana mu 1 Wakorinto 11:27-29. (Soma.) Namna gani mutiwa-mafuta anaweza kula mukate na kunywa divai “bila kustahili” siku ya Ukumbusho? Anaweza kufanya vile kama anakula mukate na kunywa divai lakini hatii kanuni za haki za Yehova. (Ebr. 6:4-6; 10:26-29) Watiwa-mafuta wanajua kama wanapaswa kubakia waaminifu ikiwa wanapenda kupokea “zawadi ya mwito wa Mungu wa kuenda juu kupitia Kristo Yesu.”​—Flp. 3:13-16.

5. Wakristo watiwa-mafuta wanapaswa kujiona namna gani?

5 Roho takatifu ya Yehova inasaidia watumishi wake wakuwe wanyenyekevu, na waepuke kuwa na kiburi. (Efe. 4:1-3; Kol. 3:10, 12) Kwa hiyo, watiwa-mafuta hawajione kuwa wao ni wazuri zaidi kuliko wengine. Wanajua kama Yehova hawapatie roho takatifu zaidi kuliko watumishi wake wengine. Hawafikiri kama wanaelewa kweli za Biblia muzuri zaidi kuliko wengine wote. Tena, hawaambie hata kidogo mutu fulani kama yeye pia ametiwa mafuta na anapaswa kuanza kula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho. Lakini, ni wanyenyekevu na wanajua kama ni Yehova tu njo anaalika watu kuenda mbinguni.

6. Kulingana na 1 Wakorinto 4:7, 8, Wakristo watiwa-mafuta wanapaswa kujiendesha namna gani?

6 Hata kama watiwa-mafuta wanaona kuwa ni pendeleo kualikwa kuenda mbinguni, hawatazamie wengine wawatendee kwa njia ya pekee. (Flp. 2:2, 3) Wanajua pia kama wakati Yehova aliwatia mafuta, hakujulisha mutu mwingine yeyote. Njo maana mutiwa-mafuta hashangae ikiwa watu fulani hawakubali mara moja kama ametiwa mafuta. Anaelewa kama Biblia inatuomba tusiamini haraka-haraka mutu fulani mwenye anasema kama Mungu amemupatia daraka fulani la pekee. (Ufu. 2:2) Kwa sababu mutiwa-mafuta hatazamie wengine wamutendee kwa njia fulani ya pekee, hataambia wale wenye anakutana nao kama yeye ni mutiwa-mafuta. Pia, hatajisifu mbele ya wengine juu ya jambo hilo.​—Soma 1 Wakorinto 4:7, 8.

7. Wakristo watiwa-mafuta wanaepuka kufanya nini, na juu ya nini?

7 Wakristo watiwa-mafuta hawaone kama wanapaswa kupitisha wakati pamoja na watiwa-mafuta wenzao tu, kama vile wao ni watu wa kikundi fulani cha pekee. Hawatafute watiwa-mafuta wengine ili kuzungumuzia habari juu ya kutiwa mafuta kwao ao ili kuanzisha vikundi vyao vya kujifunza Biblia. (Gal. 1:15-17) Kama watiwa-mafuta wanafanya vile, kutaniko halitakuwa na umoja. Kufanya vile ni kupinga muongozo wa roho takatifu, yenye inasaidia watu wa Mungu wakuwe na amani na umoja.​—Ro. 16:17, 18.

NAMNA GANI TUNAPASWA KUTENDEA WATIWA-MAFUTA?

Hatupaswe kutendea watiwa-mafuta ao watu wengine wenye kuongoza kama vile ni watu wenye kujulikana sana (Ona fungu la 8) *

8. Juu ya nini unapaswa kuwa muangalifu juu ya namna unatendea wale wenye wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho? (Ona pia maelezo ya chini.)

8 Namna gani tunapaswa kutendea ndugu na dada wenye wametiwa mafuta? Ni mubaya kusifu-sifu mutu fulani, hata kama iko ndugu mutiwa-mafuta wa Kristo. (Mt. 23:8-12) Wakati Biblia inazungumuzia wazee, inatutia moyo ‘tuige imani yao,’ lakini haituambie kama tunaweza kufanya mwanadamu fulani akuwe kiongozi wetu. (Ebr. 13:7) Ni kweli, Biblia inasema kama watu fulani “wanastahili heshima mara mbili.” Wanastahili heshima hiyo kwa sababu “wanasimamia kwa njia ya muzuri” na “wanafanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha,” lakini haiko kwa sababu wako watiwa-mafuta. (1 Ti. 5:17) Kama tunasifu-sifu sana watiwa-mafuta na kuwatendea kwa njia ya pekee sana, hilo linaweza kuwafanya wajisikie mubaya. * Na jambo la mubaya zaidi, hilo linaweza kuwafanya wakuwe na kiburi. (Ro. 12:3) Hakuna mutu kati yetu mwenye anaweza kupenda afanye jambo fulani lenye linaweza kuchochea mumoja wa ndugu watiwa-mafuta wa Kristo afanye kosa hilo nzito!​—Lu. 17:2.

9. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia Wakristo watiwa-mafuta?

9 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia wale wenye Yehova ametia mafuta? Tunaepuka kuwauliza namna gani walitiwa mafuta. Hilo ni jambo la kipekee lenye hatuna haki ya kujua. (1 Te. 4:11; 2 Te. 3:11) Tena, hatupaswe kufikiri kama bwana ao bibi, wazazi, ao watu wengine wa familia yao ni watiwa-mafuta pia. Mutu hariti tumaini la kuenda mbinguni kutoka kwa familia yake. Ni Mungu njo anapatiaka mutu tumaini hilo. (1 Te. 2:12) Tunapaswa pia kuepuka kuuliza maulizo yenye inaweza kukwaza wengine. Kwa mufano, tunapaswa kuepuka kuuliza bibi ya ndugu mutiwa-mafuta ikiwa anajisikia namna gani juu ya kuishi milele ku dunia bila bwana yake. Lakini, tunaweza kuwa hakika kabisa kama mu dunia mupya, Yehova ‘atatimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.’​—Zb. 145:16.

10. Namna gani tunajilinda sisi wenyewe wakati tunaepuka ‘kusifu-sifu wengine’?

10 Ikiwa hatutendee watiwa-mafuta kama watu wa maana sana kuliko wengine, tunajilinda pia sisi wenyewe. Namna gani? Biblia inatuambia kama watiwa-mafuta fulani wanaweza kukosa kuendelea kuwa waaminifu. (Mt. 25:10-12; 2 Pe. 2:20, 21) Lakini kama tunaepuka ‘kusifu-sifu wengine,’ hatutakuwa hata kidogo wafuasi wa watu wengine, hata wale wenye wametiwa mafuta, ao wale wenye kujulikana, ao wale wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi. (Yud. 16) Kwa hiyo, ikiwa wanakosa uaminifu ao wanaacha kutaniko, hatutapoteza imani yetu katika Yehova ao kuacha kumutumikia.

TUNAPASWA KUHANGAIKA JUU YA HESABU YA WALE WENYE KULA MUKATE NA KUNYWA DIVAI?

11. Mambo imekuwa namna gani juu ya hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho?

11 Kwa miaka mingi yenye imepita, hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho iliendelea kupunguka. Lakini mu miaka ya hivi karibuni, hesabu hiyo imeendelea kuongezeka kila mwaka. Jambo hilo linapaswa kutuhangaisha? Hapana. Tuone basi juu ya nini hatupaswe kuhangaika.

12. Juu ya nini hatupaswe kuhangaika juu ya hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho?

12 “Yehova anajua wenye kuwa wake.” (2 Ti. 2:19) Yehova anajua kabisa ni nani kwa kweli mwenye ametiwa mafuta, lakini ndugu wenye kuhesabu wale wenye wanakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho hawajue jambo hilo. Kwa hiyo, katika hesabu hiyo, kuko wale wenye wanafikiri kama wako watiwa-mafuta lakini hawako watiwa-mafuta. Kwa mufano, watu fulani wenye walikuwa wanakula mukate na kunywa divai walifikia kuacha. Pengine kwa sababu ya matatizo ya akili ao ya kihisia, wengine wanaweza kuamini kama watatawala pamoja na Kristo mbinguni. Kwa hiyo, hatujue kabisa hesabu ya watiwa-mafuta wenye wangali ku dunia.

13. Biblia inaonyesha ni watiwa-mafuta ngapi watakuwa wangali ku dunia wakati taabu kubwa itaanza?

13 Kutakuwa watiwa-mafuta katika sehemu mingi za dunia wakati Yesu atakuja kuwachukua ili waende mbinguni. (Mt. 24:31) Biblia inasema kama mu siku za mwisho, kutakuwa kungali hesabu kidogo ya watiwa-mafuta ku dunia. (Ufu. 12:17) Lakini haiseme ni watiwa-mafuta ngapi watakuwa wangali ku dunia wakati taabu kubwa itaanza.

Tunapaswa kutenda namna gani kama mutu fulani anakula mukate na kunywa divai ku Ukumbusho? (Ona fungu la 14)

14. Kulingana na Waroma 9:11, 16, tunapaswa kuelewa nini juu ya kuchaguliwa kwa watiwa-mafuta?

14 Ni Yehova njo anaamua wakati wa kuchagua watiwa-mafuta. (Ro. 8:28-30) Yehova alianza kuchagua watiwa-mafuta kisha kufufuliwa kwa Yesu. Inaonekana kama, wakati wa mitume, Wakristo wote walikuwa watiwa-mafuta. Miaka mingi kisha pale, wengi kati ya wale wenye walikuwa wanajiita kuwa Wakristo, hawakumufuata kabisa Kristo. Hata hivyo, Yehova alitia mafuta hesabu kidogo ya wale wenye walikuwa Wakristo wa kweli mu miaka hiyo. Walifananishwa na ngano zenye Yesu alisema kama zingekomaa katikati ya magugu. (Mt. 13:24-30) Mu siku hizi za mwisho, Yehova ameendelea kuchagua watu wenye watakuwa kati ya wale 144 000. * Kwa hiyo, kama Mungu anaamua kuchagua watu fulani ili wakuwe kati ya watu hao mbele tu mwisho ufike, kwa kweli, hatupaswe kuwa na mashaka juu ya hekima yake. (Soma Waroma 9:11, 16.) * Tunapaswa kuwa waangalifu ili tusitende kama wafanyakazi wenye Yesu alizungumuzia katika mufano wake mumoja. Walimunungunikia bwana wao juu ya namna alitendea wale wenye walianza kutumika saa ya mwisho.​—Mt. 20:8-15.

15. Wakristo wote watiwa-mafuta wanafanyiza “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” mwenye kutajwa mu Matayo 24:45-47? Fasiria.

15 Wakristo wote wenye kuwa na tumaini la kuishi mbinguni hawafanyize “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Soma Matayo 24:45-47.) Kama vile tu wakati wa mitume, Yehova na Yesu wanatumia ndugu kidogo ili kukulisha, ao kufundisha, watu wengi. Wakati wa mitume, ni Wakristo watiwa-mafuta kidogo tu njo walitumiwa ili kuandika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Leo pia, ni Wakristo watiwa-mafuta kidogo tu njo wenye kuwa na daraka la kupatia watu wa Mungu ‘chakula kwa wakati wenye kufaa.’

16. Umejifunza nini katika habari hii?

16 Tumejifunza nini katika habari hii? Yehova ameamua kupatia watu wake wengi uzima wa milele ku dunia na kupatia wale wenye watatawala pamoja na Yesu uzima mbinguni. Yehova anapatia zawadi watumishi wake wote, ni kusema, ule “Muyahudi” na pia wale “watu kumi (10),” na anawaomba wote waheshimie amri zilezile na waendelee kuwa waaminifu. Wote wanapaswa kuendelea kuwa wanyenyekevu. Wote wanapaswa kumutumikia pamoja na kuwa na umoja. Na wote wanapaswa kujikaza ili kuendeleza amani mu kutaniko. Kwa sababu tunaendelea kukaribia mwisho, sisi wote tunapaswa kuendelea kumutumikia Yehova na kumufuata Kristo tukiwa “kundi moja.”​—Yoh. 10:16

^ fu. 5 Mwaka huu, Ukumbusho wa Kifo cha Kristo utafanywa Siku ya Pili, tarehe 7 Mwezi wa 4. Namna gani tunapaswa kuona wale wenye watakula mukate na kunywa divai mangaribi hiyo? Tunapaswa kuhangaika kwa sababu hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai inaendelea kuongezeka? Tutapata majibu ya ile maulizo katika habari hii, yenye kutegemea habari yenye ilitolewa mu gazeti Munara wa Mulinzi la Mwezi wa 1, 2016.

^ fu. 2 Kulingana na Zaburi 87:5, 6, wakati wenye kuja, pengine Mungu atafunua majina ya wale wote wenye watatawala pamoja na Yesu mbinguni.​—Ro. 8:19.

^ fu. 8 Ona kisanduku “Upendo ‘Haujiendeshe Bila Adabu’” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 1, 2016.

^ fu. 14 Hata kama andiko la Matendo 2:33 linaonyesha kama roho takatifu inamwangwa kupitia Yesu, ni Yehova njo mwenye anaalika kila mutu.

^ fu. 14 Ili kupata habari zaidi, ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2007.

WIMBO 34 Kutembea kwa Utimilifu

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Wazia namna itakuwa kukosa heshima kabisa ikiwa mujumbe wa makao makubwa na bibi yake wanazungukwa na watu wengi hivi wenye wanatafuta kuwakamata picha kwenye mukusanyiko!