Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Kuiga Mifano ya Muzuri Kuliniletea Baraka Mingi

Kuiga Mifano ya Muzuri Kuliniletea Baraka Mingi

WAKATI nilikuwa kijana, ilikuwa nguvu kwangu kuhubiri. Wakati nilikomaa, nilipata migao yenye niliona kama sikukuwa na uwezo wa kuifanya. Niwaelezee basi juu ya mifano fulani ya muzuri yenye ilinisaidia nishinde woga na kupata baraka za muzuri mu miaka 58 yenye nilipitisha katika utumishi wa wakati wote.

Nilizaliwa mu muji wa Québec, katika jimbo la Kanada kwenye watu wanazungumuza Kifaransa. Wazazi wangu, Louis na Zélia, walinionyesha upendo. Baba yangu hakukuwa anasema sana na alipenda kusoma. Nilikuwa ninapenda kuandika na nilitumaini kama siku moja nitakuwa mutangazaji wa habari.

Wakati nilikuwa na miaka 12, Rodolphe Soucy, mumoja kati ya watu wenye walikuwa wanafanya kazi pamoja na baba, alitutembelea ku nyumba pamoja na rafiki yake. Walikuwa Mashahidi wa Yehova. Sikukuwa ninajua mambo mingi juu ya Mashahidi na sikukuwa ninapendezwa kabisa na dini yao. Lakini, nilifurahia namna yao ya muzuri na yenye kupatana na akili ya kujibu maulizo kwa kutumia Biblia. Wazazi wangu walipendezwa pia, na kwa hiyo, tukakubali funzo la Biblia.

Wakati huo, nilikuwa ninasomea ku masomo ya Wakatoliki. Mara kwa mara, nilikuwa ninazungumuza na wanafunzi wenzangu juu ya mambo yenye nilikuwa ninajifunza kupitia funzo langu la Biblia. Kisha wakati fulani, walimu, wenye walikuwa mapadri, wakajua jambo hilo. Kuliko kutumia Biblia ili kuonyesha kama mambo nilikuwa ninasema ilikuwa ya uongo, mumoja wao alinisema mbele ya wanafunzi wenzangu wote kama nilikuwa muasi! Hali hiyo ilikuwa ya kuhuzunisha sana, lakini ilinisaidia kuona kama mafundisho ya dini yenye tulikuwa tunafundishwa ku masomo haikupatana na mambo yenye Biblia inasema. Niliona kama haikukuwa muzuri nisomee pale. Wazazi wangu waliniruhusu niende ku masomo ingine.

NAMNA NILIJIFUNZA KUPENDA MAHUBIRI

Niliendelea kujifunza Biblia, lakini sikufanya haraka maendeleo ya kiroho juu nilikuwa naogopa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Kanisa Katoliki lilikuwa na mamlaka sana na lilipinga kwa ukali kazi yetu ya kuhubiri. Maurice Duplessis, kiongozi wa jimbo la Québec, alikuwa na urafiki wa sana na viongozi wa kanisa. Alitegemeza vikundi vya watu wabaya ili kusumbua na hata kushambulia Mashahidi. Iliomba kabisa uhodari ili kuhubiri wakati huo.

Ndugu mwenye alinisaidia kushinda woga ni John Rae, mwenye alimaliza somo la kenda la Masomo ya Gileadi. John, alikuwa mwenye uzoefu sana, lakini alikuwa mupole, munyenyekevu, na mwenye kukaribiwa kwa vyepesi. Mara mingi, hakunishauria moja kwa moja, lakini mufano wake muzuri ulinifundisha mambo mingi. John alikuwa na magumu ya kusema Kifaransa, kwa hiyo nilimusindikiza mara mingi katika mahubiri ili kumusaidia kuzungumuza Kifaransa. Kupitisha wakati pamoja na John kulinisaidia nifikie kuwa Shahidi wa Yehova. Nilibatizwa tarehe 26 Mwezi wa 5, 1951, miaka kumi kisha kukutana na Mashahidi kwa mara ya kwanza.

Mufano muzuri wa John Rae (A) ulinisaidia (B) nishinde woga wa kuhubiri nyumba kwa nyumba

Katika kutaniko letu la kidogo mu muji wa Québec, watu karibu wote walikuwa mapainia. Mufano wao muzuri ulinichochea nikuwe painia. Wakati huo, tulikuwa tunahubiri nyumba kwa nyumba kwa kutumia Biblia tu. Kwa sababu hatukutumia vichapo, tulipaswa kutumia Maandiko muzuri zaidi. Kwa hiyo, nilijikaza sana ili kujua muzuri maandiko ya Biblia yenye ingenisaidia kutetea kweli. Lakini, watu wengi walikuwa wanakataa kusoma hata Biblia, kama haikukuwa Biblia yenye ilikubaliwa na Kanisa Katoliki.

Mu mwaka wa 1952, nilimuoa Simone Patry, dada mumoja muaminifu wa mu kutaniko letu. Tulihamia Montréal, na katika mwaka moja wa ndoa, Lise, mutoto wetu mwanamuke, alizaliwa. Hata kama niliacha kazi ya upainia wakati kidogo tu mbele ya kuoa, mimi na Simone tulijikaza kufanya maisha yetu ikuwe ya mwepesi ili tushiriki katika kazi za kutaniko kwa uwezo wetu wote tukiwa familia.

Miaka kumi ilipita mbele nifikirie tena kwa uzito kazi ya upainia. Mu mwaka wa 1962, wakati nilikuwa ku Masomo ya Huduma ya Ufalme yenye ilifanya mwezi moja, ku Beteli ya Kanada, nilipangishwa katika chumba kimoja na ndugu mwenye kuitwa Camille Ouellette. Camille alikuwa na bidii kwa ajili ya mahubiri, jambo hilo lilinifurahisha kabisa, zaidi sana juu alikuwa baba wa familia. Wakati huo, ndugu na dada kidogo tu katika Québec wenye walikuwa na watoto njo walikuwa mapainia; lakini huo njo ulikuwa muradi wa Camille. Katika wakati wenye tuliishi pamoja, alinitia moyo nifikiri juu ya hali yangu. Kisha miezi kidogo tu, niliona kama ningeweza tena kuwa painia wa kawaida. Ndugu na dada fulani walisema kama uamuzi wangu haukukuwa wenye hekima, lakini nilianza tena kazi ya upainia, juu nilikuwa hakika kama Yehova angenisaidia kabisa nishiriki katika kazi ya kuhubiri kwa uwezo wangu wote.

TUNARUDIA QUÉBEC NA TUKO MAPAINIA WA PEKEE

Mu mwaka wa 1964, mimi na Simone tulipewa mugao wa kuwa mapainia wa pekee mu muji wa Québec, muji wetu wa kizalikio, kwenye tulitumikia kwa miaka fulani yenye ilifuata. Wakati huo, upinzani ulikuwa umepunguka, lakini watu fulani walikuwa wangali wanatupinga.

Siku ya Posho moja kisha midi, nilikamatwa mu Sainte-Marie, muji wa kidogo wenye hauko mbali na muji wa Québec. Ofisa mumoja alinipeleka ku kituo cha polisi na kunitia mu gereza kwa sababu nilikuwa ninahubiri nyumba kwa nyumba bila kuwa na karatasi ya kuniruhusu. Kisha, nilipelekwa mbele ya muamuzi mwenye kuitwa Baillargeon, mwanaume mwenye kuogopesha. Aliniuliza ni nani angenisambia. Wakati nilitaja jina Glen How, * mwanasheria mwenye alijulikana sana mwenye alikuwa Shahidi, akasema kwa woga hivi: “Oh, hapana! Hapana ule!” Wakati huo, Glen How alijulikana muzuri kuwa mwanasheria mwenye alikuwa anatetea Mashahidi. Bila kukawia, tribinali ilinijulisha kama mashitaka yangu ilikuwa imeondolewa.

Pia, ilikuwa nguvu kulipia nafasi zenye kufaa za kufanyia mikutano kwa sababu kazi yetu ilikuwa inapingwa mu muji wa Québec. Kutaniko letu la kidogo lilipata tu nafasi ya kuwekea magari, nafasi hiyo haikukuwa na chombo cha kuleta joto. Ili kupata joto wakati wa baridi kali, ndugu walikuwa wanatumia chombo cha kuleta joto chenye kutumia mafuta. Mara mingi, tulikuwa tunakusanyika kuzunguka chombo hicho kwa saa fulani mbele ya kuanza mikutano ili kuelezeana mambo yenye kutia moyo.

Ilifurahisha sana kuona matokeo ya muzuri ya kazi ya kuhubiri kadiri miaka iliendelea kupita. Mu miaka ya 1960, kulikuwa tu makutaniko kidogo katika eneo la muji wa Québec, eneo la Côte-Nord, na Peninsula ya Gaspé (sehemu ya inchi yenye inaingia mu bahari). Leo, kuko mizunguko zaidi ya mbili katika ile maeneo, na ndugu wanafanyia mikutano mu Majumba ya Ufalme ya muzuri sana.

TUNAALIKWA KUFANYA KAZI YA KUSAFIRI

Katika mwaka wa 1977, nilihuzuria mukutano wa waangalizi wenye kusafiri wenye ulifanywa katika Toronto, Kanada

Mimi na Simone tulialikwa kufanya kazi ya muzunguko mu mwaka wa 1970. Kisha, mu mwaka wa 1973, tulipewa mugao wa kufanya kazi ya wilaya. Katika miaka hiyo, nilijifunza mambo mingi kupitia mufano wa ndugu wenye uwezo kama vile Laurier Saumur * na David Splane, * wote wawili walikuwa waangalizi wenye kusafiri. Kisha kila mukusanyiko, mimi na David tulikuwa tunapatiana mapendekezo juu ya namna ya kufundisha muzuri zaidi. Ninakumbuka wakati fulani David aliniambia hivi: “Léonce, nilifurahia hotuba yako ya mwisho. Ilikuwa muzuri, lakini ningeweza kufanya hotuba tatu katika habari zote zenye ulizungumuzia!” Nilikuwa ninazungumuzia habari mingi sana mu hotuba zangu. Nilipaswa kujifunza namna ya kusema mambo kwa kifupi.

Nilitumikia mu miji mbalimbali katika sehemu ya mashariki ya Kanada

Waangalizi wa wilaya walikuwa na daraka la kutia moyo waangalizi wa muzunguko. Lakini, wahubiri wengi mu Québec walinijua muzuri. Mara mingi, walikuwa wanapenda kuhubiri pamoja na mimi wakati nilikuwa ninatembelea mizunguko yao. Hata kama nilikuwa ninafurahia kuhubiri pamoja nao, sikukuwa ninapitisha wakati wa kutosha pamoja na mwangalizi wa muzunguko. Wakati fulani, mwangalizi mumoja wa muzunguko mwenye upendo aliniambia hivi: “Ni muzuri kuona kama unapenda kupitisha wakati pamoja na ndugu zetu, lakini usisahau kama hili ni juma langu. Mimi pia niko na lazima ya kutiwa moyo!” Shauri hilo la upendo lilinisaidia nikuwe na usawaziko zaidi.

Jambo la kuhuzunisha ni hili: Mu mwaka wa 1976 jambo fulani la mubaya sana lenye sikutazamia lilinifikia. Simone, bibi yangu mupendwa, aligonjwa sana na akakufa. Alikuwa mwanamuke muzuri sana juu alikuwa na roho ya kujinyima na alimupenda Yehova sana. Kuhubiri sana kulinisaidia kabisa nivumilie huzuni ya kufiwa, na ninamushukuru Yehova kwa sababu alinitegemeza kwa upendo wakati huo wa magumu. Kisha, nilimuoa Carolyn Elliott, painia mwenye bidii mwenye kuzungumuza Kiingereza mwenye alihamia Québec ili kutumikia mahali kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Carolyn ni dada mwenye kukaribiwa kwa vyepesi na mwenye kupendezwa kabisa na wengine, zaidi sana wale wenye kuwa na haya ao wenye kujisikia kuwa peke yao. Alionekana kuwa baraka kabisa kwangu wakati alijiunga na mimi katika kazi ya kusafiri.

MWAKA WA MAANA SANA

Katika Mwezi wa 1, 1978, nilipewa mugao wa kufundisha Masomo ya kwanza ya Mapainia mu Québec. Niliogopa sana, juu ile masomo ilikuwa mupya kwangu na hata kwa wanafunzi. Jambo la kufurahisha ni hili: mu somo la kwanza lenye nilifundisha, kulikuwa mapainia wengi wenye uzoefu. Hata kama mimi njo nilikuwa mwalimu, nilijifunza mambo mingi kutoka kwa wanafunzi!

Kisha, mu mwaka wa 1978, Mukusanyiko wa Kimataifa wenye kichwa “Imani Yenye Ushindi,” ulifanywa mu Kiwanja cha Michezo cha Olimpiki katika Montréal. Ule njo mukusanyiko mukubwa zaidi wenye ulikuwa umefanywa mu Québec, watu zaidi 80 000 walihuzuria. Nilipewa mugao wa kutumika katika idara yenye inashugulikia habari zenye zinahusu mukusanyiko. Nilizungumuza na watangazaji wengi wa habari na nilifurahi sana kuona kama waliandika mambo mingi ya muzuri juu yetu. Waliongoza vipindi vya kutuuliza maulizo ku televizyo na ku radio kwa saa zaidi ya 20, na walichapisha habari mingi sana. Ushahidi mukubwa sana ulitolewa!

TUNAHAMIA KATIKA ENEO LINGINE

Badiliko kubwa lilitokea katika maisha yangu mu mwaka wa 1996. Kisha kutumikia mu jimbo la Québec kwenye watu wanazungumuza Kifaransa kuanzia wakati nilibatizwa, nilipewa mugao wa kutumikia mu wilaya ya Toronto kwenye watu wanazungumuza Kiingereza. Nilijisikia kuwa singeweza na niliogopa kutoa hotuba mbalimbali katika Kiingereza changu cha kukata na shoka. Nilipaswa kusali mara mingi zaidi na kumutegemea Yehova zaidi.

Lakini, ninaweza kusema kabisa kama nilifurahia miaka mbili yenye nilitumikia mu eneo la Toronto. Carolyn alinisaidia kwa uvumilivu ili nianze kuzungumuza Kiingereza bila woga, na ndugu walinitegemeza na kunitia moyo sana. Bila kukawia, tulipata marafiki wengi wapya.

Zaidi ya kazi zingine na kutayarisha mikusanyiko yenye ilifanywa ku mwisho wa juma, mara mingi, nilikuwa ninapitisha saa moja hivi mu kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kila Siku ya Tano mangaribi. Pengine watu fulani walijiuliza hivi: ‘Juu ya nini kuhubiri mbele tu ya mukusanyiko wa mwisho wa juma wakati kuko mambo mingi ya kufanya?’ Lakini, niliona kama kuwa na mazungumuzo ya muzuri na watu mu mahubiri kulinitia moyo. Hata leo, kuhubiria watu kunaniletea furaha sikuzote.

Katika mwaka wa 1998, Mimi na Carolyn tulirudia tena mu muji wa Montréal tukiwa mapainia wa pekee. Kwa miaka mingi, mugao wangu ulitia ndani kupanga mahubiri ya pekee ya mahali pa watu wengi na kutumika na watangazaji wa habari ili kusaidia watu wasikuwe na mawazo ya mubaya juu ya Mashahidi wa Yehova. Leo, mimi na Carolyn tunafurahia kuhubiria watu wa inchi zingine wenye wamehamia Kanada hivi karibuni na wenye mara mingi wako na hamu ya kujifunza mambo mingi juu ya Biblia.

Mimi na bibi yangu Carolyn

Wakati ninafikiria miaka 68 yenye nimefanya tangu wakati nilibatizwa na kuwa mutumishi wa Yehova, ninajisikia kuwa mwenye kubarikiwa kabisa. Kujifunza kupenda mahubiri na kusaidia watu wengi wafikie kujua kweli kumeniletea baraka sana. Wakati mutoto wangu, Lise, na bwana yake walikomalisha watoto wao, wakakuwa mapainia wa kawaida. Wakati ninaona kama angali mwenye bidii katika kazi ya kuhubiri, hilo linaniletea furaha. Niko mwenye shukrani sana kwa Wakristo wenzangu wenye mufano wao muzuri na mashauri yao yenye hekima vilinisaidia nikomae kiroho na kushugulikia migao mbalimbali ya kiteokrasi. Nimevumbua kama tunaweza kubakia waaminifu katika mugao fulani kama tu tunategemea roho takatifu ya Yehova yenye nguvu. (Zb. 51:11) Ninaendelea kumushukuru Yehova kwa sababu amenipatia pendeleo la muzuri sana la kusifu jina lake!​—Zb. 54:6.

^ fu. 16 Ona habari juu ya maisha ya Glen How, “Vita Si Yenu Bali Ni ya Mungu,” katika Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 4, 2000.

^ fu. 20 Ona habari juu ya maisha ya Laurier Saumur, J’ai trouvé quelque chose pour lequel il vaut la peine de lutter,” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 2, 1977.

^ fu. 20 David Splane anatumikia katika Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova.