Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 6

Yehova, Baba Yetu, Anatupenda Sana

Yehova, Baba Yetu, Anatupenda Sana

“Basi ninyi munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu.’”​—MT. 6:9.

WIMBO 135 Mwaliko Wenye Upendo wa Yehova: “Uwe na Hekima, Mwanangu”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Mutu alikuwa anafanya nini ili kuzungumuza na mufalme wa Uajemi?

WAZIA unaishi katika inchi ya Uajemi miaka 2 500 hivi yenye imepita. Unapenda kuzungumuza na mufalme wa inchi hiyo juu ya jambo fulani, kwa hiyo, unasafiri mupaka mu muji wa Shushani, kwenye mufalme anaishi. Lakini mbele ya kuzungumuza na mufalme, unapaswa kwanza kupata ruhusa yake. Kama unapima kuzungumuza naye bila kupata ruhusa yake, unaweza kuuawa!​—Est. 4:11.

2. Yehova anapenda tujisikie namna gani juu ya kuzungumuza naye?

2 Tuko wenye shukrani sana juu Yehova haiko kama mufalme huyo wa Uajemi! Yehova iko na mamlaka zaidi kuliko mufalme yeyote mwanadamu, lakini anapenda tuzungumuze naye wakati wowote. Anapenda tujisikie huru kuzungumuza naye. Kwa mufano, hata kama Yehova iko na majina ya cheo yenye utukufu kama vile Muumbaji Mukubwa, Mweza-yote, na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, anapenda tuzungumuze naye kwa kutumia jina la kirafiki “Baba.” (Mt. 6:9) Inafurahisha sana kuona kama Yehova anapenda tujisikie karibu sana naye!

3. Juu ya nini tunaweza kumuita Yehova “Baba,” na habari hii itazungumuzia nini?

3 Tuko na haki ya kumuita Yehova “Baba,” kwa sababu ni yeye njo alitupatia uzima. (Zb. 36:9) Juu iko Baba yetu, tunapaswa kumutii. Kama tunafanya mambo yenye anatuomba, tutapata baraka za muzuri sana. (Ebr. 12:9) Kati ya baraka hizo, kuko uzima wa milele, ikuwe mbinguni ao ku dunia. Kuko pia baraka zenye tunapata leo. Habari hii inazungumuzia namna Yehova anatenda kama Baba mwenye upendo leo na juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama hatatuacha hata kidogo wakati wenye kuja. Lakini, tuone kwanza juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Baba yetu wa mbinguni anatupenda sana na anatuhangaikia.

YEHOVA NI BABA MWENYE KUTUPENDA NA KUTUHANGAIKIA

Yehova anapenda akuwe rafiki yetu, kama vile tu baba mwenye upendo anapendaka kuwa rafiki ya watoto wake (Ona fungu la 4)

4. Juu ya nini watu fulani wanaona kama ni nguvu kumuona Yehova kuwa Baba yao?

4 Unaona kama ni nguvu kumuona Mungu kuwa Baba yako? Watu fulani wanaweza kujiona kuwa kidogo sana na wa bure kwa kujilinganisha na Yehova. Hawako hakika kama Mungu Mweza-yote anawahangaikia kipekee. Lakini, Baba yetu mwenye upendo hapendi tujisikie vile. Alitupatia uzima na anapenda tufanye urafiki pamoja naye. Kisha kuonyesha vile, mutume Paulo alifasiria wasikilizaji wake katika muji wa Atene kama Yehova “haiko mbali sana na kila mumoja wetu.” (Mdo. 17:24-29) Mungu anapenda kila mumoja wetu azungumuze naye kama vile tu mutoto anazungumuzaka na muzazi wake mwenye kumupenda na kumuhangaikia.

5. Mufano wa dada mumoja unatufundisha nini?

5 Wengine wanaweza kuona kama ni nguvu kumuona Yehova kuwa Baba yao kwa sababu baba yao mwenye aliwazaa hakuwaonyesha upendo ao aliwaonyesha upendo kidogo. Ona maelezo ya dada mumoja Mukristo. Anasema hivi: “Baba yangu alikuwa mukali sana. Wakati nilianza kujifunza Biblia, ilikuwa nguvu kwangu kujisikia kuwa karibu na Baba wa mbinguni. Lakini, wakati nilifikia kumujua Yehova, ile yote ilibadilika.” Na wewe unajisikiaka vile? Kama ni vile, ukuwe hakika kama wewe pia unaweza kufikia kumuona Yehova kuwa Baba muzuri zaidi.

6. Kulingana na Matayo 11:27, Yehova ametumia njia gani ili kutusaidia tumuone kuwa Baba yetu mwenye upendo?

6 Njia moja yenye Yehova ametumia ili kutusaidia kumuona kuwa Baba yetu mwenye upendo ni hii: alifanya maneno na matendo ya Yesu iandikwe mu Biblia. (Soma Matayo 11:27.) Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake, njo maana alisema hivi: “Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.” (Yoh. 14:9) Mara mingi, Yesu alimuita Yehova kuwa Baba. Katika Injili ine tu, Yesu alimuita Yehova kuwa “Baba” mara 165 hivi. Juu ya nini Yesu alimuita Yehova kuwa Baba mara mingi vile? Sababu moja ni hii: alipenda watu wakuwe hakika kama Yehova ni Baba mwenye upendo.​—Yoh. 17:25, 26.

7. Tunajifunza nini juu ya Yehova kupitia namna alimutendea Mwana wake?

7 Fikiria mambo yenye tunajifunza juu ya Yehova kupitia namna alimutendea Yesu, Mwana wake. Sikuzote, Yehova alisikiliza sala za Yesu. Hakusikiliza tu sala za Yesu lakini pia alijibu sala hizo. (Yoh. 11:41, 42) Katika majaribu yote yenye ilimufikia Yesu, alijisikia kuwa Baba yake alikuwa anamupenda na kumutegemeza.​—Lu. 22:42, 43.

8. Yehova alimutimizia Yesu mahitaji gani?

8 Yesu alijua kama Yehova njo mwenye alimupatia uzima na mambo yenye alikuwa nayo lazima ili aendelee kuishi. Alisema hivi: “Ninaishi kwa sababu ya Baba.” (Yoh. 6:57) Yesu alimutegemea kabisa Baba yake, na Yehova, Baba yake, alimutimizia mahitaji yake ya kimwili. Na jambo la maana zaidi, Yehova alimutimizia mahitaji yake ya kiroho.​—Mt. 4:4.

9. Namna gani Yehova alionyesha kama alikuwa Baba mwenye alimupenda Yesu na kumuhangaikia?

9 Kwa sababu Yehova ni Baba mwenye upendo, alimusaidia Yesu ajue kama alikuwa anamutegemeza. (Mt. 26:53; Yoh. 8:16) Yehova hakumulinda Yesu ili jambo lolote la mubaya lisimupate, lakini alimusaidia kuvumilia majaribu yenye ilimupata. Yesu alikuwa hakika kama jambo lolote la mubaya lenye lingemupata lingekuwa la muda. (Ebr. 12:2) Yehova alionyesha kama alimuhangaikia Yesu kwa kumusikiliza, kwa kumutimizia mahitaji yake, kwa kumuzoeza, na kumutegemeza. (Yoh. 5:20; 8:28) Tuone basi namna Baba yetu anatuhangaikia katika njia hizo.

NAMNA BABA YETU MWENYE UPENDO ANATUHANGAIKIA

10. Kulingana na Zaburi 66:19, 20, namna gani Yehova anaonyesha kama anatupenda?

10 Yehova anasikiliza sala zetu. (Soma Zaburi 66:19, 20.) Hatuombe tusali kwake mara fulani tu, lakini anatuomba tusali kwake mara mingi. (1 Te. 5:17) Tunaweza kuzungumuza kwa heshima na Mungu wetu wakati wowote, hata tukuwe wapi. Hawezi kuwa na mambo mingi ya kufanya yenye inaweza kumuzuia asisikilize sala zetu; iko tayari kila wakati kusikiliza sala zetu. Wakati tunaona kama Yehova anasikiliza sala zetu, tunamukaribia zaidi. Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: “Ninamupenda Yehova kwa sababu anasikia sauti yangu.”​—Zb. 116:1.

Baba mwenye upendo (1) anasikiliza watoto wake, (2) anawatimizia mahitaji yao, (3) anawazoeza, na (4) kuwalinda. Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo naye anatuhangaikia katika njia hizo (Ona fungu la 10-15) *

11. Namna gani Yehova anajibu sala zetu?

11 Baba yetu hasikilize tu sala zetu lakini pia anajibu sala hizo. Mutume Yohana anatuhakikishia hivi: “Hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi [ya Mungu], yeye anatusikia.” (1 Yo. 5:14, 15) Kwa kweli, pengine Yehova hatajibu sala zetu kwa njia yenye tunawazia. Anajua mambo ya muzuri zaidi yenye inaweza kutuletea faida, njo maana wakati fulani hajibu sala yetu ao anataka tungojee.​—2 Ko. 12:7-9.

12-13. Baba yetu wa mbinguni anatutimizia mahitaji gani?

12 Yehova anatutimizia mahitaji yetu. Anafanya jambo lenye anapenda baba wote wafanye. (1 Ti. 5:8) Anatimizia watoto wake mahitaji yao ya kimwili. Hapendi tuhangaike juu ya chakula, manguo, ao makao. (Mt. 6:32, 33; 7:11) Kwa sababu iko muzazi mwenye upendo, Yehova amefanya hata mipango ili kutimiza mahitaji yetu ya wakati wenye kuja.

13 Jambo la maana zaidi, Yehova anatutimizia mahitaji yetu ya kiroho. Kupitia Neno lake, Yehova amefunua kweli juu yake, kusudi lake, maana ya maisha, na juu ya wakati wenye kuja. Alihangaikia kila mumoja wetu wakati tulijifunza kweli, kwa kutumia wazazi wetu ao mutu mwingine ili kutusaidia tufikie kumujua. Na tunaendelea kupata musaada kupitia wazee wa kutaniko wenye upendo na ndugu na dada wengine wenye kukomaa kiroho. Tena, Yehova anatufundisha kupitia mikutano yetu ya kutaniko, kwenye tunajifunza pamoja na ndugu na dada zetu. Kupitia njia hizo na njia zingine, Yehova anaonyesha kama anatuhangaikia sisi wote kama Baba.​—Zb. 32:8.

14. Juu ya nini Yehova anatuzoeza, na anafanya vile namna gani?

14 Yehova anatuzoeza. Yesu alikuwa mukamilifu, lakini sisi hatuko wakamilifu. Kwa hiyo, ili kutuzoeza, Baba yetu mwenye upendo anatupatia nizamu, wakati ni lazima kufanya vile. Neno lake linatukumbusha hivi: “Wale wenye Yehova anapenda anawatia nizamu.” (Ebr. 12:6, 7) Yehova anatutia nizamu katika njia mingi. Kwa mufano, jambo fulani lenye tunasoma katika Neno lake, ao lenye tunasikia ku mikutano yetu linaweza kuturekebisha. Ao pengine tunaweza kupata musaada wenye tuko nao lazima kupitia wazee. Hata kama Yehova anatutia nizamu katika njia gani, sikuzote anafanya vile kwa sababu anatupenda.​—Yer. 30:11.

15. Yehova anatulinda namna gani?

15 Yehova anatutegemeza wakati wa magumu. Kama vile tu baba mwenye upendo anategemeza watoto wake wakati wa magumu, Baba yetu wa mbinguni anatutegemeza wakati wa magumu. Anatupatia roho yake takatifu. Roho hiyo inatulinda juu ya kila kitu chenye kinaweza kuharibu urafiki wetu pamoja naye. (Lu. 11:13) Pia, Yehova anatulinda kwa kutusaidia wakati tunavunjika moyo. Kwa mufano, anatupatia tumaini la muzuri sana. Tumaini hilo juu ya wakati wenye kuja linatusaidia kuvumilia magumu. Fikiria jambo hili: Hata mambo gani ya mubaya itufikie, Baba yetu mwenye upendo atamaliza mambo yote yenye kututesa. Hata ikuwe tuko tunapambana na magumu gani, ile magumu ni ya muda tu, lakini baraka zenye Yehova anatupatia ni za milele.​—2 Ko. 4:16-18.

BABA YETU HATATUACHA HATA KIDOGO

16. Ni nini ilitokea wakati Adamu alikosa kumutii Baba yake wa mbinguni?

16 Tunaona kama Yehova anatupenda wakati tunafikiria jambo lenye alifanya wakati Adamu alikosa kumutii. Wakati Adamu alimuasi Baba yake wa mbinguni, alipoteza nafasi yake mu familia ya Yehova yenye furaha, alipoteza nafasi hiyo kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya wazao wake. (Ro. 5:12; 7:14) Lakini, Yehova alifanya jambo fulani ili kusaidia wazao wa Adamu.

17. Kisha Adamu kuasi, Yehova alifanya nini palepale?

17 Yehova alimupatia Adamu azabu ao malipizi, lakini hakuacha bila tumaini wazao wa Adamu wenye walikuwa hawajazaliwa. Aliahidi palepale kama wanadamu wenye kumutii wangerudishwa katika familia yake. (Mwa. 3:15; Ro. 8:20, 21) Yehova alifanya jambo hilo liwezekane kupitia zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu, Mwana wake mupendwa. Kwa kutoa Mwana wake kwa ajili yetu, Yehova alionyesha kama anatupenda sana.​—Yoh. 3:16.

Kama tumemuacha Yehova kwa wakati fulani, lakini tunatubu, Yehova, Baba yetu mwenye upendo iko tayari kutukaribisha (Ona fungu la 18)

18. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anapenda tukuwe mu familia yake, hata kama tumemuacha kwa wakati fulani?

18 Hata kama hatukamilike, Yehova anapenda tukuwe mu familia yake, na hatuone kuwa muzigo hata kidogo. Tunaweza kumuhuzunisha ao kumuacha kwa wakati fulani, lakini Yehova anaendelea kutumaini kama tutarudia. Yesu alieleza habari ya mwana mupotevu ili kuonyesha namna Yehova anapenda sana watoto wake. (Lu. 15:11-32) Baba mwenye kuzungumuziwa katika mufano huo aliendelea kutumaini kama mwana wake angerudia. Wakati mwana alirudia ku nyumba, baba yake alimukaribisha kwa furaha. Kama tumemuacha Yehova kwa wakati fulani, lakini tunatubu, tunaweza kuwa hakika kama Baba yetu mwenye upendo iko tayari kutukaribisha.

19. Namna gani Yehova atamaliza mambo ya mubaya yenye Adamu alileta?

19 Baba yetu atamaliza mambo yote ya mubaya yenye Adamu alileta. Kisha Adamu kuasi, Yehova aliamua kuchagua kati ya wanadamu watu 144 000 na kuwafanya kuwa wana wake ili wakuwe wafalme na makuhani mbinguni pamoja na Yesu, Mwana wake. Yesu na wale watawala wenzake watasaidia wanadamu wenye kutii wakuwe wakamilifu katika ulimwengu mupya. Kisha wale wanadamu kushinda jaribu la mwisho la utii, Mungu atawapatia uzima wa milele. Wakati huo, Baba yetu atafurahi kuona dunia inajaa watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke wakamilifu. Utakuwa wakati muzuri sana!

20. Namna gani Yehova ameonyesha kama anatupenda sana, na habari yenye kufuata itazungumuzia nini?

20 Yehova ameonyesha kama anatupenda sana. Yehova ni Baba muzuri zaidi. Anasikiliza sala zetu na anatutimizia mahitaji yetu, ya kimwili na ya kiroho. Anatuzoeza na kututegemeza. Pia, atatufanyia mambo ya muzuri sana wakati wenye kuja. Tunafurahi sana kujua kama Baba yetu anatupenda na kutuhangaikia! Habari yenye kufuata itazungumuzia ni katika njia gani sisi watoto wake tunaweza kumuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya upendo wake.

WIMBO 108 Upendo Mshikamanifu wa Mungu

^ fu. 5 Mara mingi, tunamuona Yehova kuwa Muumbaji wetu na Mutawala wetu Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi. Lakini, tuko na sababu za kumuona Yehova kuwa Baba mwenye anatupenda na kutuhangaikia. Habari hii itazungumuzia sababu hizo. Pia, tutajifunza juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova hawezi kutuacha hata kidogo.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Kila picha kati ya picha hizi ine inaonyesha baba pamoja na mutoto wake: baba anamusikiliza mutoto wake mwanaume kwa uangalifu, baba anamutimizia mutoto wake mwanamuke mahitaji yake, baba anamuzoeza mutoto wake mwanaume, na baba anamufariji mutoto wake mwanaume. Mukono wa Yehova wenye kuchapwa nyuma ya picha hizo ine unatukumbusha kama Yehova naye anatuhangaikia katika njia hizo.