Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 7

Tunamupenda Sana Yehova, Baba Yetu

Tunamupenda Sana Yehova, Baba Yetu

“Sisi tunapenda, kwa sababu alitupenda kwanza.”​—1 YO. 4:19.

WIMBO 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Juu ya nini Yehova alituwezesha kuingia mu familia yake, na alifanya vile namna gani?

YEHOVA ametualika ili tuingie mu familia ya waabudu wake. Huo ni mwaliko muzuri sana! Familia yetu inafanyizwa na watu wenye wamejitoa kwa Mungu na wenye wanaonyesha imani katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Mwana wake. Familia yetu ni familia yenye furaha. Tuko na maisha yenye maana leo, na tuko na furaha juu tuko na tumaini la kuishi milele, ikuwe mbinguni ao mu Paradiso hapa ku dunia.

2 Yehova alituwezesha kuingia mu familia yake juu anatupenda sana. Lakini ili kufanya vile, Yehova alilipa bei kubwa sana. (Yoh. 3:16) ‘Tulinunuliwa kwa bei.’ (1 Ko. 6:20) Kupitia bei ya ukombozi, Yehova alituwezesha tukuwe na urafiki wa sana pamoja naye. Tuko na pendeleo la kuita Mutu mukubwa zaidi katika ulimwengu kuwa Baba yetu. Na kama vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, Yehova njo Baba muzuri zaidi.

3. Tunaweza kujiuliza maulizo gani? (Ona pia kisanduku “ Yehova Ananitambua?”)

3 Kama muandikaji mumoja wa Biblia, tunaweza kujiuliza hivi: “Nitamulipa Yehova nini kwa mema yote yenye amenitendea?” (Zb. 116:12) Lakini jibu ni hili: hatuwezi hata kidogo kumulipa Baba yetu wa mbinguni. Lakini, upendo wenye anatuonyesha unatuchochea tumupende. Mutume Yohana aliandika hivi: “Sisi tunapenda, kwa sababu alitupenda kwanza.” (1 Yo. 4:19) Namna gani tunaweza kumuonyesha Baba yetu wa mbinguni kama tunamupenda?

BAKIA KARIBU NA YEHOVA

Tunaonyesha kama tunamupenda sana, Yehova, Baba yetu wa mbinguni, kwa kuendelea kumukaribia kupitia sala, kwa kumutii, na kwa kusaidia wengine ili wamupende (Ona fungu la 4-14)

4. Kulingana na Yakobo 4:8, juu ya nini tunapaswa kujikaza ili kumukaribia Yehova?

4 Yehova anapenda tumukaribie na tukuwe tunazungumuza naye. (Soma Yakobo 4:8.) Anatuomba ‘tudumu katika sala,’ na iko tayari kutusikiliza wakati wowote. (Ro. 12:12) Hawezi kuwa na mambo mingi ya kufanya yenye inaweza kumuzuia asisikilize sala zetu, na hawezi kuchoka hata kidogo ili akose kutusikiliza. Na sisi tunamusikiliza kwa kusoma Neno lake Biblia, na vichapo vyenye vinatusaidia kuelewa Biblia. Pia, tunamusikiliza kwa kufuata kwa uangalifu mikutano yetu ya Kikristo. Kama vile kuzungumuza kwa ukawaida na wazazi kunasaidia watoto waendelee kuwa marafiki wa wazazi wao, kuzungumuza na Yehova kwa ukawaida kunatusaidia tukuwe marafiki wa Yehova.

Ona fungu la 5

5. Tunaweza kufanya nini ili sala zetu zikuwe muzuri zaidi?

5 Chunguza namna unazungumuzaka na Mungu. Yehova anapenda tumwange mioyo yetu mbele yake katika sala. (Zb. 62:8) Tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Sala zangu ni za kijuu-juu tu kama vile ujumbe wenye kuchapishwa, ao ni sala zenye kutoka mu moyo kama vile barua zenye kuandikwa kwa mukono?’ Kwa kweli, unamupenda Yehova sana, na unapenda uendelee kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja naye. Ili kufanya vile, unapaswa kuzungumuza naye kwa ukawaida. Umuelezee siri zako. Umuambie mambo yenye inakuletea furaha na mambo yenye inakuletea huzuni. Ukuwe hakika kama unaweza kumuomba musaada.

6. Tunapaswa kufanya nini ili tubakie karibu na Baba yetu wa mbinguni?

6 Ili tubakie karibu na Baba yetu wa mbinguni, tunapaswa kuendelea kuwa wenye shukrani kwake. Tunakubaliana na muandikaji wa zaburi mwenye aliandika hivi: “Mambo yenye umefanya ni mengi sana, Ee Yehova Mungu wangu, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea. Hakuna mwenye anaweza kulinganishwa na wewe; kama ningejaribu kueleza na kuongea kuzihusu, zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!” (Zb. 40:5) Hatupaswe tu kujisikia kuwa wenye shukrani; tunapaswa kumuonyesha Yehova shukrani yetu kupitia maneno na matendo yetu. Jambo hilo linafanya tukuwe tofauti na watu wengi leo. Tunaishi mu dunia kwenye watu hawaonyeshe shukrani juu ya mambo yote yenye Mungu anawafanyia. Kwa kweli, jambo moja lenye kuonyesha kama tuko tunaishi katika “siku za mwisho” ni kwamba watu hawana shukrani. (2 Ti. 3:1, 2) Hatupendi kuwa vile hata kidogo!

7. Yehova anapenda tufanye nini, na juu ya nini?

7 Wazazi hawapendake watoto wao wakose kusikilizana lakini wanapendaka watoto wao wakuwe marafiki. Vilevile, Yehova anapenda watoto wake waishi kwa amani. Kwa kweli, upendo wenye tunaonyeshana unatutambulisha kuwa Wakristo wa kweli. (Yoh. 13:35) Tunakubaliana na muandikaji wa zaburi mwenye aliandika hivi: “Ni muzuri sana na inapendeza sana ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” (Zb. 133:1) Wakati tunapenda ndugu na dada zetu, tunamuonyesha Yehova kama tunamupenda. (1 Yo. 4:20) Inapendeza kabisa kuwa katika familia ya ndugu na dada ‘wenye fazili wao kwa wao, wenye huruma nyingi.’​—Efe. 4:32.

ONYESHA KAMA UNAMUPENDA YEHOVA KWA KUMUTII

Ona fungu la 8

8. Kulingana na 1 Yohana 5:3, ni sababu gani ya maana zaidi yenye inafanya tumutii Yehova?

8 Yehova anapenda watoto watii wazazi wao, na anapenda tumutii. (Efe. 6:1) Tunapaswa kumutii kwa sababu yeye njo Muumbaji wetu, yeye njo anatupatia mambo yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuishi, na yeye njo muzazi mwenye hekima zaidi. Lakini, sababu ya maana zaidi yenye inafanya tumutii Yehova ni juu tunamupenda. (Soma 1 Yohana 5:3.) Hata kama kuko sababu mingi zenye zinatufanya tumutii Yehova, hatulazimishe kufanya vile. Yehova alitupatia zawadi ya uhuru wa kuchagua, njo maana anafurahi wakati tunachagua kumutii kwa sababu tunamupenda.

9-10. Juu ya nini ni jambo la maana tujue sheria za Mungu na kuzitii?

9 Wazazi wanapendaka watoto wao wakuwe salama. Njo maana wanaweka sheria za mwenendo, zenye zinaletea watoto wao faida. Wakati watoto wanatii sheria hizo, wanaonyesha kama wanatumainia wazazi wao na wanawaheshimia. Kwa hiyo, ni jambo la maana zaidi tujue sheria za Baba yetu wa mbinguni na tuzitii. Wakati tunafanya vile, tunamuonyesha Yehova kama tunamupenda na tunamuheshimia na pia tunajiletea faida sisi wenyewe. (Isa. 48:17, 18) Lakini, wale wenye wanamukataa Yehova na sheria zake wanajiletea magumu wao wenyewe.​—Gal. 6:7, 8.

10 Wakati tunaishi kwa njia yenye inamupendeza Yehova, tunalindwa na hatari za kimwili, kihisia, na kiroho. Yehova anajua mambo ya muzuri zaidi yenye inaweza kutuletea faida. Aurora, mwenye kuishi mu inchi ya Amerika, anasema hivi: “Ninajua kama kumutii Yehova sikuzote kunafanya tukuwe na maisha ya muzuri zaidi.” Sisi wote tunaona kama jambo hilo ni la kweli. Wewe, umepata faida gani kwa kutii muongozo wenye Yehova anatutolea kwa upendo?

11. Sala inatusaidia namna gani?

11 Sala inatusaidia tukuwe watiifu, hata wakati ni nguvu kufanya vile. Wakati fulani, haiko mwepesi kumutii Yehova kwa sababu tuko watenda-zambi, lakini sikuzote tunapaswa kujikaza sana ili kupiganisha mwelekeo wetu wa kufanya zambi. Muandikaji mumoja wa zaburi alimuomba Mungu hivi: “Uchochee ndani yangu utayari wa kukutii.” (Zb. 51:12) Denise, mwenye iko painia wa kawaida, anasema hivi: “Kama ninaona kuwa ni nguvu kutii amri fulani ya Yehova, ninasali ili kupata nguvu za kufanya mambo yenye kuwa sawa.” Tunaweza kuwa hakika kama, sikuzote Yehova atajibu sala ya namna hiyo.​—Lu. 11:9-13.

SAIDIA WENGINE WAMUPENDE BABA YETU

12. Kulingana na Waefeso 5:1, tunapaswa kufanya nini?

12 Soma Waefeso 5:1. Kwa sababu tuko “watoto wapendwa” wa Yehova, tunajikaza sana ili kumuiga. Tunaiga sifa zake wakati tunatendea wengine kwa upendo, kwa fazili, na kuwasamehe. Wakati wale wenye hawamujue Mungu wanaona mwenendo wetu muzuri, hilo linaweza kuwachochea wajifunze mambo mingi juu yake. (1 Pe. 2:12) Wazazi Wakristo wanapaswa kumuiga Yehova katika namna wanatendea watoto wao. Wakati wanafanya vile, watoto wao wanaweza kupenda wakuwe pia marafiki wa Baba yetu mwenye upendo.

Ona fungu la 13

13. Tunapaswa kufanya nini ili tusikuwe na woga?

13 Mutoto mudogo anajivunia baba yake na anafurahia kuongea juu yake. Sisi pia tunajivunia Yehova, Baba yetu wa mbinguni, na tunapenda wengine wafikie kumujua. Katika mioyo yetu, sisi wote tunajisikia kama Mufalme Daudi, mwenye aliandika hivi: “Nitajisifu katika Yehova.” (Zb. 34:2) Halafu kama tuko watu wenye haya? Ni nini inaweza kutusaidia tusikuwe na woga? Tunashinda woga wakati tunakaza akili juu ya namna tunaweza kumufurahisha Yehova sana na namna wengine watapata faida sana kama wanajifunza juu yake. Yehova atatupatia uhodari wenye tuko nao lazima. Alisaidia Wakristo wa wakati wa mitume wasikuwe na woga, na atatusaidia sisi pia.​—1 Te. 2:2.

14. Juu ya nini ni jambo la maana tuhubiri na kufanya wanafunzi?

14 Yehova hana ubaguzi, na anafurahi wakati anatuona tunaonyesha wengine upendo, hata kama walitoka wapi. (Mdo. 10:34, 35) Moja kati ya njia za muzuri zaidi za kuonyesha wengine upendo ni kuwahubiria habari njema. (Mt. 28:19, 20) Kazi hiyo inaweza kuleta matokeo gani? Wale wenye wanatusikiliza wanaweza kufanya maisha yao ikuwe muzuri leo na wanapata tumaini la kuishi milele wakati wenye kuja.​—1 Ti. 4:16.

UMUPENDE BABA YETU NA UTAKUWA NA FURAHA

15-16. Tuko na sababu gani za kuwa wenye furaha?

15 Yehova ni muzazi mwenye upendo, kwa hiyo, anapenda familia yake ikuwe na furaha. (Isa. 65:14) Kuko sababu mingi zenye zinaweza kutufanya tukuwe na furaha leo, hata kama pengine tuko na magumu fulani. Kwa mufano, tuko hakika kama Baba yetu wa mbinguni anatupenda sana. Tuko na ujuzi wenye hauna makosa wa Biblia, Neno la Mungu. (Yer. 15:16) Na tuko mu familia ya pekee yenye kufanyizwa na watu wenye wanamupenda Yehova, wanapenda kanuni zake za juu za mwenendo, na wanapendana.​—Zb. 106:4, 5.

16 Tunaweza kuendelea kuwa wenye furaha kwa sababu tuko na tumaini hakika kama maisha itakuwa muzuri sana wakati wenye kuja. Tunajua kama hivi karibuni Yehova atatosha watu waovu wote na kama wakati wa utawala wa Ufalme wake, dunia itarudishwa kuwa Paradiso. Pia, tuko na tumaini la muzuri sana kama watu wenye wamekufa watafufuliwa na kuishi tena pamoja na wapendwa wao. (Yoh. 5:28, 29) Hiyo itakuwa furaha sana! Na jambo la maana zaidi, tuko hakika kama hivi karibuni, kila mutu mbinguni na ku dunia atamupatia Baba yetu mwenye upendo heshima, sifa, na ibada yenye anastahili.

WIMBO 12 Mungu Mkuu, Yehova

^ fu. 5 Tunajua kama Yehova, Baba yetu, anatupenda sana na ametuingiza mu familia ya waabudu wake. Na jambo hilo linatuchochea tumupende. Namna gani tunaweza kumuonyesha Baba yetu mwenye upendo kama tunamupenda? Habari hii itazungumuzia mambo fulani yenye tunaweza kufanya.