Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 9

Acha Yehova Akutulize

Acha Yehova Akutulize

“Wakati mahangaiko yalinilemea, ulinifariji na kunituliza.”​—ZB. 94:19.

WIMBO 44 Sala ya Mtu wa Hali ya Chini

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni nini inaweza kutuletea mahangaiko, na mahangaiko inaweza kutufanya tukuwe na mawazo gani?

UMEKWISHA kusumbuliwa sana na mahangaiko? * Pengine uko na mahangaiko juu mambo yenye wengine walisema ao kufanya imekuumiza. Ao unaweza kuwa na mahangaiko juu ya mambo yenye ulisema ao kufanya. Kwa mufano, pengine ulifanya kosa fulani, na unaogopa kama Yehova hatakusamehe hata kidogo. Na jambo la mubaya zaidi, unaweza kuwaza kama hauna imani, na uko mutu mubaya kwa sababu mahangaiko inakulemea. Lakini, je, hiyo ni kweli?

2. Ni mifano gani ya Biblia yenye kuonyesha kama kuwa na mahangaiko hakumaanishe kama mutu hana imani?

2 Fikiria mifano ya watu fulani wenye Maandiko inazungumuzia. Hana, mwenye alifikia kuwa mama ya nabii Samweli, alikuwa mwanamuke mwenye imani kubwa. Lakini, alikuwa na mahangaiko sana wakati mutu mumoja wa mu nyumba yake alimutendea mubaya. (1 Sa. 1:7) Mutume Paulo alikuwa na imani kubwa, lakini alilemewa na “mahangaiko juu ya makutaniko yote.” (2 Ko. 11:28) Mufalme Daudi alikuwa na imani yenye nguvu na njo maana Yehova alimupenda sana. (Mdo. 13:22) Hata hivyo, Daudi alifanya makosa yenye ilimuletea mahangaiko sana. (Zb. 38:4) Yehova alifariji na kutuliza kila mumoja wao. Tuone basi mambo yenye mifano yao inaweza kutufundisha.

MAMBO YENYE TUNAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MUFANO WA HANA, MWANAMUKE MUAMINIFU

3. Namna gani maneno ya wengine inaweza kutuletea mahangaiko?

3 Wakati wengine wanasema mambo yenye kuumiza ao kututendea mubaya, jambo hilo linaweza kutuletea mahangaiko. Tunakuwa na mahangaiko zaidi kama mutu mwenye alitukwaza ni rafiki wa sana ao mutu wa familia. Tunaweza kuogopa kwamba urafiki wetu pamoja na mutu huyo umeharibika. Wakati fulani, mutu mwenye anatukwaza anaweza kusema bila kufikiri, na tunaweza kujisikia kama vile anatuchoma kwa upanga! (Mez. 12:18) Ao pengine mutu fulani anaweza kuamua kimakusudi kutumia maneno yenye kuumiza kama vile upanga. Jambo fulani kama hilo lilimufikia dada mumoja kijana. Anasema hivi: “Miaka fulani yenye imepita, mutu fulani mwenye niliona kuwa rafiki muzuri alianza kueneza habari za uongo juu yangu ku Enternete. Jambo hilo liliniumiza na kuniletea mahangaiko. Sikuelewa kabisa juu ya nini rafiki mwenye nilitumainia angeweza kuniumiza vile.” Kama rafiki wa sana ao mutu wa jamaa amekwisha kukukwaza, mufano wa Hana unaweza kukufundisha mambo mingi.

4. Ni magumu gani ya nguvu yenye Hana alipaswa kupambana nayo?

4 Hana alipaswa kupambana na magumu fulani ya nguvu. Kwa miaka mingi, hakukuwa na uwezo wa kuzaa watoto. (1 Sa. 1:2) Mu desturi ya Waisraeli, mwanamuke mwenye alikuwa tasa alionwa kuwa mwenye kulaaniwa. Jambo hilo lilimufanya asikie haya. (Mwa. 30:1, 2) Na kulikuwa jambo lingine lenye lilifanya maisha ya Hana ikuwe nguvu zaidi: bwana yake alikuwa na bibi mwingine, Penina, mwenye alimuzalia watoto. Penina alimuona Hana kuwa mushindani wake na “alimuchokoza bila kuacha ili kumukasirisha.” (1 Sa. 1:6) Ku mwanzo, ilikuwa nguvu kwa Hana kuvumilia ile magumu ya nguvu. Alikuwa na huzuni sana, na hivyo “alikuwa analia na hakukuwa anakula.” Alikuwa na “uchungu mwingi sana” mu moyo. (1 Sa. 1:7, 10) Hana alifanya nini ili kupata faraja?

5. Namna gani sala ilimusaidia Hana?

5 Hana alimuambia Yehova katika sala namna alikuwa anajisikia. Kisha kusali, alimufasiria Eli, Kuhani Mukubwa, magumu yake. Kwa hiyo, Kuhani Mukubwa alimuambia hivi: “Uende kwa amani, na Mungu wa Israeli atimize ombi lako lenye umemuomba.” Matokeo ilikuwa nini? Hana “akaenda zake na akakula, na uso wake haukukuwa tena na huzuni.” (1 Sa. 1:17, 18) Sala ilimusaidia Hana akuwe tena na amani.

Kama Hana mwenye aliishi wakati wa zamani, tunaweza kufanya nini ili tupate tena amani ya moyo na kuendelea kuwa nayo? (Ona fungu la 6-10)

6. Tunaweza kujifunza nini juu ya sala kupitia mufano wa Hana na kupitia andiko la Wafilipi 4:6, 7?

6 Tunaweza kuwa tena na amani kama tunaendelea kusali. Hana alizungumuza na Baba yake wa mbinguni kwa wakati murefu. (1 Sa. 1:12) Sisi pia tunaweza kuzungumza na Yehova kwa wakati murefu juu ya magumu yetu, juu ya mambo yenye inatuletea woga, na juu ya uzaifu wetu. Haiko lazima sala zetu zikuwe kama mashairi (poèmes) ao zikuwe zenye kupangwa muzuri kabisa. Wakati fulani, tunaweza hata kulia wakati tunazungumuza na Yehova juu ya mahangaiko yetu. Lakini, Yehova hatachoka hata kidogo kutusikiliza. Zaidi ya kusali juu ya magumu yetu, tunapaswa kukumbuka shauri lenye kuwa mu Wafilipi 4:6, 7. (Soma.) Paulo alionyesha waziwazi kama tunapaswa kutoa sala za shukrani. Tuko na sababu mingi sana za kumushukuru Yehova. Kwa mufano, tunaweza kumushukuru kwa ajili ya uzima wenye ametupatia, kwa ajili ya vitu vya muzuri vyenye ameumba, kwa ajili ya upendo mushikaminifu wenye anatuonyesha, na kwa ajili ya tumaini lenye ametupatia. Mufano wa Hana unaweza kutufundisha jambo lingine gani?

7. Hana na bwana yake walikuwa wanafanya nini kwa ukawaida?

7 Hata kama Hana alikuwa na magumu, alikuwa anaenda kwa ukawaida pamoja na bwana yake mahali pa kumuabudia Yehova katika Shilo. (1 Sa. 1:1-5) Ni wakati Hana alikuwa ku tabenakulo njo Kuhani Mukubwa Eli alimutia moyo kwa kusema kama alitumaini kuwa Yehova atajibu sala yake.​—1 Sa. 1:9, 17.

8. Namna gani mikutano inaweza kutusaidia? Fasiria.

8 Tunaweza kuwa tena na amani kama tunaendelea kuhuzuria mikutano ya kutaniko. Mara mingi katika sala ya kuanza mikutano yetu, ndugu wanaomba roho takatifu ikuwe pamoja na sisi. Amani ni sehemu ya tunda la roho hiyo. (Gal. 5:22) Wakati tunahuzuria mikutano yetu hata kama tuko na mahangaiko, Yehova na ndugu na dada zetu wanaweza kututia moyo na kutusaidia tukuwe tena na amani ya akili na ya moyo. Sala na mikutano ni njia za maana zenye Yehova anatumia ili kututuliza. (Ebr. 10:24, 25) Tuzungumuzie basi jambo lingine lenye mufano wa Hana unaweza kutufundisha.

9. Katika hali ya Hana, ni nini ilibadilika, lakini ni nini haikubadilika?

9 Mambo yenye ilimuletea Hana mahangaiko haikuisha palepale. Wakati Hana alirudia ku nyumba kisha kumuabudu Yehova ku tabenakulo, alipaswa kuendelea kuishi mu nyumba ileile pamoja na Penina. Na Biblia haionyeshe kama tabia ya Penina ilibadilika. Kwa hiyo, pengine Hana alipaswa kuendelea kuvumilia maneno yenye kuumiza ya Penina. Lakini Hana alipata tena amani ya moyo na aliendelea kuwa nayo. Kumbuka kama, kisha kuacha mambo mu mikono ya Yehova, Hana hakukuwa tena na mahangaiko. Alimuacha Yehova amufariji na kumutuliza. Wakati fulani kisha pale, Yehova alimubariki Hana kwa kumusaidia azae watoto!​—1 Sa. 1:19, 20; 2:21.

10. Mufano wa Hana unatufundisha nini?

10 Tunaweza kuwa tena na amani hata kama mambo yenye kutuletea mahangaiko inaendelea. Hata kama tunasali kwa bidii na kuhuzuria mikutano kwa ukawaida, magumu fulani inaweza kuendelea. Lakini, mufano wa Hana unatufundisha kama hakuna kitu chenye kinaweza kumuzuia Yehova kutuliza moyo wetu wenye huzuni. Yehova hatatusahau hata kidogo, na hatakosa kutubariki juu ya uaminifu wetu.​—Ebr. 11:6.

MAMBO YENYE TUNAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MUFANO WA MUTUME PAULO

11. Ni mambo gani yenye ilimuletea Paulo mahangaiko?

11 Kuko mambo mingi yenye ilimuletea Paulo mahangaiko. Kwa mufano, kwa sababu alipenda ndugu na dada zake, matatizo yenye walikuwa nayo ilimuletea mahangaiko. (2 Ko. 2:4; 11:28) Wakati alikuwa anahubiri, mara mingi watu wenye walimupinga walimupiga na kumutia mu gereza. Alipaswa pia kuvumilia magumu yenye ilimuletea mahangaiko, kwa mufano “kupungukiwa na chakula.” (Flp. 4:12) Na kwa sababu alivunjikiwa na mashua karibu mara tatu mu maisha yake, inawezekana alikuwa na mahangaiko mingi wakati alikuwa anasafiri kwa mashua. (2 Ko. 11:23-27) Ni nini ilimusaidia Paulo apiganishe ile mahangaiko?

12. Ni nini ilimusaidia Paulo kupunguza mahangaiko yake?

12 Paulo alikuwa na mahangaiko juu ya ndugu na dada zake wakati walikuwa na magumu, lakini hakujaribu kumaliza magumu yao yote yeye mwenyewe. Paulo alikuwa na sifa ya kiasi. Alifanya mipango ili wengine wamusaidie kushugulikia kutaniko. Kwa mufano, alipatia madaraka wanaume fulani wenye kutumainika, kama vile Timoteo na Tito. Kwa kweli, kazi yenye wanaume hao walifanya ilimusaidia Paulo kupunguza mahangaiko yake.​—Flp. 2:19, 20; Tit. 1:1, 4, 5.

Kama mutume Paulo, tunaweza kufanya nini ili mahangaiko isitulemee? (Ona fungu la 13-15)

13. Namna gani wazee wanaweza kumuiga Paulo?

13 Omba wengine musaada. Kama Paulo, leo wazee wengi wenye upendo wako na mahangaiko juu ya ndugu na dada wa kutaniko wenye kuwa na magumu. Lakini, muzee hawezi kusaidia ndugu na dada wote wa kutaniko. Sifa ya kiasi itachochea muzee abebe muzigo huo pamoja na wanaume wengine wenye kustahili na azoeze ndugu vijana ili wamusaidie kushugulikia kundi la Mungu.​—2 Ti. 2:2.

14. Paulo hakuogopa nini, na mufano wake unaweza kutufundisha nini?

14 Ukubali kama uko na lazima ya kufarijiwa. Paulo alikuwa munyenyekevu, njo maana alijua kama marafiki wake wangeweza kumutia moyo. Kwa kweli, hakuogopa kama wengine wataona kama iko muzaifu kwa sababu marafiki wake walimutia moyo. Wakati Paulo alimuandikia Filemoni, alisema hivi: “Nilifurahi sana na kupata kitulizo wakati nilisikia juu ya upendo wako.” (Flm. 7) Paulo alitaja majina ya wafanyakazi wenzake wengine wengi wenye walikuwa wamemufariji sana wakati alikuwa na mahangaiko. (Kol. 4:7-11) Wakati tunaonyesha unyenyekevu na kukubali kama tuko na lazima ya kitia-moyo, ndugu na dada zetu watafurahi kutupatia musaada wenye tuko nao lazima.

15. Paulo alifanya nini wakati alikuwa mu hali yenye kuleta mahangaiko?

15 Tegemea Neno la Mungu. Paulo alijua kama Maandiko ingeweza kumufariji. (Ro. 15:4) Maandiko ingemupatia pia hekima ya kupambana na magumu yoyote. (2 Ti. 3:15, 16) Wakati Paulo alifungwa Roma kwa mara ya pili, aliona kama alikuwa anakaribia kufa. Katika hali hiyo yenye kuleta mahangaiko, Paulo alifanya nini? Alimuomba Timoteo akuje haraka na amuletee “vile vitabu vya kukunjwa.” (2 Ti. 4:6, 7, 9, 13) Juu ya nini? Juu vile vitabu vya kukunjwa vilikuwa sehemu ya Maandiko ya Kiebrania, Paulo angeweza kuvitumia ili kufanya funzo lake la pekee la Biblia. Wakati tunamuiga Paulo kwa kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida, Yehova atatumia Maandiko ili kututuliza, hata kama tuko na magumu gani.

MAMBO YENYE TUNAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MUFANO WA MUFALME DAUDI

Kama Mufalme Daudi, ni nini inaweza kutusaidia ikiwa tumefanya zambi nzito? (Ona fungu la 16-19)

16. Daudi alijiletea mahangaiko gani?

16 Zamiri ya Daudi ilimusumbua kwa sababu alikuwa amefanya jambo fulani la mubaya sana. Alikuwa amefanya uzinifu na Bat-sheba, alifanya mupango ili bwana yake auawe, na alijaribu kuficha zambi zake kwa wakati fulani. (2 Sa. 12:9) Ku mwanzo, Daudi hakusikiliza zamiri yake. Na kwa hiyo, aliteseka kiroho, kiakili, na pia kimwili. (Zb. 32:3, 4) Ni nini ilimusaidia Daudi apiganishe mahangaiko yenye alijiletea, na ni nini inaweza kutusaidia kama tunafanya kosa nzito?

17. Namna gani maneno ya Zaburi 51:1-4 inaonyesha kama Daudi alitubu kwa moyo wote?

17 Uombe musamaha katika sala. Kisha, Daudi alisali kwa Yehova. Alitubu kwa moyo wake wote na kumuambia Yehova mambo yenye alikuwa amefanya. (Soma Zaburi 51:1-4.) Kufanya vile kulimusaidia atulie kabisa! (Zb. 32:1, 2, 4, 5) Kama unafanya zambi nzito, usijaribu kuficha zambi yako. Lakini, tubu waziwazi zambi yako kwa kumuambia Yehova mambo yote katika sala. Kama unafanya vile, utajisikia kuwa mwenye kutulia zaidi na hautajisikia tena kuwa mwenye hatia sana. Lakini, kama unapenda kurudisha urafiki wako pamoja na Yehova, unapaswa kufanya jambo lingine zaidi ya kusali.

18. Namna gani Daudi alitenda wakati alipewa nizamu?

18 Ukubali nizamu. Wakati Yehova alimutuma nabii Natani kwa Daudi ili kumuonyesha zambi yake, Daudi hakujitetea ao kujaribu kuonyesha kama zambi yake haikukuwa nzito sana. Mara moja, alikubali kama alikuwa amemutendea zambi bwana ya Bat-sheba na zaidi sana, alikuwa amemutendea Yehova zambi. Daudi alikubali nizamu kutoka kwa Yehova, na Yehova alimusamehe. (2 Sa. 12:10-14) Kama tumefanya zambi nzito, tunapaswa kuzungumuza na wale wenye Yehova ameweka ili kutuchunga. (Yak. 5:14, 15) Na hatupaswe kujitetea. Kama tunakubali na kutumia haraka zaidi nizamu yoyote yenye tunapewa, tutapata tena haraka zaidi amani na furaha yetu.

19. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

19 Uazimie kutorudilia makosa ileile. Mufalme Daudi alijua kama alikuwa na lazima ya musaada wa Yehova ili aepuke kufanya zambi zilezile. (Zb. 51:7, 10, 12) Kisha Yehova kumusamehe, Daudi aliazimia kuepuka mawazo ya mubaya. Kufanya vile kulimusaidia akuwe tena na amani ya moyo.

20. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya musamaha wa Yehova?

20 Tunaonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya musamaha wa Yehova wakati tunasali kwake ili atusamehe, wakati tunakubali nizamu, na kujikaza sana ili tusirudilie makosa yetu. Wakati tunafanya vile, tutakuwa tena na amani ya moyo. James, ndugu mumoja mwenye alifanya zambi nzito, aliona kama ile ni kweli. Anasema hivi: “Wakati nilielezea wazee zambi yangu, nilisikia kama vile muzigo muzito umetoka ku mabega yangu. Nilianza kuwa tena na amani ya akili.” Inatia moyo sana kujua kama “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kupondwa roho”!​—Zb. 34:18.

21. Tunaweza kufanya nini ili kumuacha Yehova atutulize?

21 Kwa sababu tunakaribia sana mwisho, inawezekana mambo yenye kuleta mahangaiko itaongezeka. Wakati uko na mawazo yenye kuleta mahangaiko, tafuta haraka musaada wa Yehova. Ujifunze Biblia kwa bidii. Ujifunze kupitia mufano wa Hana, Paulo, na Daudi. Sali kwa Baba yako wa mbinguni akusaidie kujua mambo yenye inakuletea mahangaiko. (Zb. 139:23) Acha akusaidie kubeba mizigo yako, zaidi sana ile yenye hauwezi kubeba wewe mwenyewe. Kama unafanya vile, unaweza kuwa kama muandikaji wa zaburi mwenye alimuimbia Yehova hivi: “Wakati mahangaiko yalinilemea, ulinifariji na kunituliza.”​—Zb. 94:19.

WIMBO 4 “Yehova Ni Mchungaji Wangu”

^ fu. 5 Wakati fulani, sisi wote tunapata magumu yenye inatuletea mahangaiko. Habari hii inazungumuzia mifano ya watumishi tatu wa zamani wa Yehova wenye walipambana na mahangaiko. Pia, inazungumuzia namna Yehova alifariji na kutuliza kila mumoja wao.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mahangaiko ni kujisikia kuwa mwenye wasiwasi ao mwenye woga. Tunaweza kuwa na mahangaiko kwa sababu ya matatizo ya feza, matatizo ya afya, matatizo ya familia, ao magumu ingine. Pia, tunaweza kuwa na mahangaiko juu ya makosa fulani yenye tulifanya zamani ao juu ya magumu yenye tunawazia kama tutapata wakati wenye kuja.