Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 11

Uko Tayari Kubatizwa?

Uko Tayari Kubatizwa?

“Ubatizo . . . unawaokoa ninyi sasa pia.”​—1 PE. 3:21.

WIMBO 28 Kuwa Rafiki ya Yehova

KIFUPI CHA HABARI *

1. Mutu anapaswa kufanya nini mbele ya kujenga nyumba?

WAZIA mutu mwenye anaamua kujenga nyumba. Anajua kama atajenga nyumba ya namna gani. Unawaza kama ataenda mara moja kuuza vyombo fulani na kuanza kujenga? Hapana. Mbele aanze kujenga, kuko jambo fulani la maana lenye anapaswa kufanya: kuhesabia garama yote yenye nyumba itaomba. Sababu gani? Kwa sababu anapaswa kwanza kuangalia kama iko na feza za kutosha ili kumaliza kujenga nyumba yake. Kama anahesabia garama mbele ya wakati, inawezekana kabisa kama atamaliza kujenga nyumba yake.

2. Kulingana na Luka 14:27-30, unapaswa kufikiria sana mambo gani mbele ya kubatizwa?

2 Je, kumupenda Yehova na kuwa mwenye shukrani juu ya mambo yenye amekufanyia kumekuchochea ufikirie kubatizwa? Kama ni vile, hali yako inafanana na ya mutu mwenye anataka kujenga nyumba. Juu ya nini tunasema vile? Fikiria maneno ya Yesu yenye kuwa mu Luka 14:27-30. (Soma.) Yesu alikuwa anazungumuzia mambo yenye mutu anapaswa kufanya ili akuwe mwanafunzi wake. Juu tukuwe wanafunzi wake, tunapaswa kuwa tayari kukubali “garama” yenye inaombwa, ni kusema, tunapaswa kuwa tayari kuvumilia magumu fulani na kuachana na mambo fulani. (Lu. 9:23-26; 12:51-53) Kwa hiyo, mbele ya kubatizwa, unapaswa kufikiria sana mambo yenye itakupata kama unakuwa mwanafunzi wa Kristo. Ukifanya vile, utakuwa tayari kabisa kuendelea kumutumikia Mungu kwa uaminifu kisha kubatizwa.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Je, kuwa mwanafunzi wa Kristo mwenye kubatizwa kunaleta baraka kabisa kupita magumu yenye unapaswa kupambana nayo na mambo yenye unapaswa kuachana nayo? Ndiyo kabisa! Ubatizo unafungua mulango wa kupata baraka mingi, sasa na wakati wenye kuja. Tuzungumuzie maulizo fulani ya maana kuhusu ubatizo. Kufanya vile kutakusaidia kujibu ulizo hili: “Niko tayari kubatizwa?”

MAMBO YENYE UNAPASWA KUJUA KUHUSU KUJITOA KWA MUNGU NA KUBATIZWA

4. (a) Kujitoa kwa Mungu maana yake nini? (b) Matayo 16:24 inazungumuzia ‘kujikana’ mwenyewe. Maana yake nini?

4 Kujitoa kwa Mungu maana yake nini? Mbele ya kubatizwa, unapaswa kujitoa kwanza kwa Mungu. Wakati unajitoa kwa Mungu, unamuambia katika sala yenye inatoka mu moyo kama utatumia maisha yako ili kumutumikia milele. Wakati unajitoa kwa Mungu katika sala, ‘unajikana’ mwenyewe. (Soma Matayo 16:24.) Unakuwa sasa mali ya Yehova, na ni pendeleo kubwa. (Ro. 14:8) Unamuambia kama kuanzia sasa na kuendelea, jambo lenye utatia pa nafasi ya kwanza mu maisha yako ni kumutumikia, hapana kujipendeza mwenyewe. Wakati unajitoa kwa Mungu, unafanya naziri. Naziri ni ahadi nzito yenye mutu anatoa kwa Mungu. Yehova hatukaze tufanye naziri kama hiyo. Lakini wakati tunaifanya, anataka tuitimize.​—Zb. 116:12, 14.

5. Kuko tofauti gani kati ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa?

5 Kuko tofauti gani kati ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa? Kujitoa kwa Mungu ni jambo lenye unafanya kipekee, ni kati yako na Yehova tu. Lakini ubatizo unafanywa mbele ya watu mingi, kwa kawaida ku mukusanyiko wa muzunguko ao wa eneo. Wakati unabatizwa, unaonyesha wengine kama umekwisha kujitoa kwa Yehova. * Kwa hiyo ubatizo wako unaonyesha wengine kama unamupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu yako yote na unaonyesha kama umeazimia kumutumikia milele.​—Mk. 12:30.

6-7. Kulingana na 1 Petro 3:18-22, ni sababu gani mbili zenye kufanya ubatizo ukuwe wa maana?

6 Ni jambo la maana kabisa kubatizwa? Fikiria maneno yenye kuwa mu 1 Petro 3:18-22. (Soma.) Safina ilionyesha waziwazi kama Noa alikuwa na imani, vilevile ubatizo wako unaonyesha waziwazi kama umejitoa kwa Yehova. Lakini je, ubatizo ni wa maana kabisa? Ndiyo. Petro alionyesha sababu zenye zinafanya ubatizo ukuwe wa maana kabisa. Sababu ya kwanza, ubatizo ‘unakuokoa wewe.’ Ubatizo unaweza kutuokoa kama tunaonyesha kupitia matendo yetu kwamba tunamuamini Yesu na kuamini kama alikufa kwa ajili yetu, alifufuliwa na kuenda mbinguni, na sasa iko “kwenye mukono wa kuume wa Mungu.”

7 Sababu ya pili, ubatizo unatusaidia kuwa na “zamiri ya muzuri.” Wakati tunajitoa kwa Mungu na kubatizwa, tunaingia katika uhusiano wa pekee pamoja naye. Kwa sababu tumetubu kabisa na tuko na imani katika bei ya ukombozi, Mungu anasamehe zambi zetu. Kwa hiyo, tunakuwa na zamiri ya muzuri mbele ya Mungu.

8. Ni sababu gani kubwa yenye inapaswa kukuchochea uamue kubatizwa?

8 Ni nini inapaswa kukuchochea ubatizwe? Kujifunza Biblia kwa uangalifu kumekusaidia ujue mambo mingi juu ya Yehova, umejua sifa zake na njia zake. Mambo yenye umejifunza juu yake imegusa moyo wako na imekuchochea umupende sana. Kumupenda Yehova njo sababu kubwa yenye inapaswa kukuchochea uamue kubatizwa.

9. Maana yake nini kubatizwa katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kama vile Matayo 28:19, 20 inasema?

9 Sababu ingine ya kukuchochea uamue kubatizwa ni mafundisho ya kweli ya Biblia yenye unaamini sasa. Fikiria mambo yenye Yesu alisema wakati alitoa amri ya kufanya wanafunzi. (Soma Matayo 28:19, 20.) Yesu alisema kama, wale wenye kubatizwa wanapaswa kubatizwa “katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu.” Maana yake nini? Maana yake unapaswa kuamini kwa moyo wako wote mambo ya kweli yenye Biblia inafundisha juu ya Yehova; Mwana wake, Yesu; na roho takatifu. Ile mafundisho iko na nguvu sana na inaweza kugusa sana moyo wako. (Ebr. 4:12) Turudilie mafundisho fulani.

10-11. Ni mafundisho gani juu ya Baba yenye umejifunza na kuamini?

10 Fikiria tena wakati ulijifunza mafundisho hii juu ya Baba: “Jina [lake] ni Yehova,” yeye njo “Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote,” na yeye peke yake njo “Mungu wa kweli.” (Zb. 83:18; Isa. 37:16) Yeye njo Muumbaji wetu, na “wokovu ni wa Yehova.” (Zb. 3:8; 36:9) Amefanya mipango juu ya kutukomboa katika zambi na kifo na ametupatia tumaini la kuishi milele. (Yoh. 17:3) Kujitoa kwa Mungu na kubatizwa kutaonyesha kama umekuwa Shahidi wa Yehova. (Isa. 43:10-12) Utaingia mu familia ya mu dunia yote ya waabudu wenye wanajivunia kuitwa kwa jina la Mungu na kujulisha wengine jina hilo.​—Zb. 86:12.

11 Ni pendeleo kabisa kuelewa mambo yenye Biblia inafundisha juu ya Baba! Wakati unaamini ile mafundisho ya maana sana, moyo wako unakuchochea ujitoe kwa Yehova na kubatizwa.

12-13. Ni mafundisho gani juu ya Mwana yenye umejifunza na kuamini?

12 Ulijisikia namna gani wakati ulijifunza mafundisho yenye kufuata juu ya Mwana? Yesu njo mutu wa pili wa maana zaidi mu ulimwengu wote. Kwa kujipendea, alitoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yetu. Wakati tunaonyesha kupitia matendo yetu kama tunaamini bei ya ukombozi, zambi zetu zinasamehewa, tunakuwa marafiki wa Mungu, na tunakuwa na tumaini la kuishi milele. (Yoh. 3:16) Yesu ni Kuhani wetu Mukubwa. Anataka kutusaidia tupate faida ya bei ya ukombozi na tukuwe na urafiki wa sana na Mungu. (Ebr. 4:15; 7:24, 25) Kwa sababu yeye njo Mufalme wa Ufalme wa Mungu, Mungu atamutumia ili kutakasa jina lake, kumaliza uovu, na kuleta baraka za milele katika Paradiso ya wakati wenye kuja. (Mt. 6:9, 10; Ufu. 11:15) Yesu njo mufano wetu. (1 Pe. 2:21) Alituachia mufano kwa kutumia maisha yake ili kufanya mapenzi ya Mungu.​—Yoh. 4:34.

13 Wakati unaamini mambo yenye Biblia inafundisha juu ya Yesu, unafikia kumupenda Mwana mupendwa wa Mungu. Kumupenda Yesu kunakuchochea utumie maisha yako ili kufanya mapenzi ya Mungu, sawa vile Yesu alifanya. Kwa hiyo, utakuwa na hamu ya kujitoa kwa Yehova na kubatizwa.

14-15. Ni mafundisho gani juu ya roho takatifu yenye umejifunza na kuamini?

14 Ulijisikia namna gani wakati ulijifunza mafundisho yenye kufuata juu ya roho takatifu? Roho takatifu haiko mutu, lakini ni nguvu ya utendaji ya Mungu. Yehova alitumia roho takatifu ili kuongoza wale wenye waliandika Biblia, na ile roho inatusaidia kuelewa na kutumia katika maisha yetu mambo yenye tunasoma mu Biblia. (Yoh. 14:26; 2 Pe. 1:21) Yehova anatumia roho yake takatifu juu ya kutupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” (2 Ko. 4:7) Roho takatifu inatupatia nguvu ya kuhubiri habari njema, kupinga jaribu, kupambana na hali ya kuvunjika moyo, na kuvumilia magumu. Inatusaidia kuonyesha sifa za muzuri sana zenye zinafanyiza “tunda la roho.” (Gal. 5:22) Mungu iko tayari kupatia roho yake wale wenye wanamutumainia na kumuomba roho hiyo kwa bidii.​—Lu. 11:13.

15 Inatia moyo kujua kama waabudu wa Yehova wanaweza kumuomba roho takatifu ili iwasaidie kumutumikia! Wakati unaamini mafundisho yenye umejifunza juu ya roho takatifu, utakuwa na hamu ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa.

16. Mupaka hapa tumejifunza nini?

16 Uamuzi wa kujitoa kwa Mungu na kubatizwa, ni uamuzi wa maana sana. Kama vile tumejifunza, unapaswa kuwa tayari kukubali garama yenye inaombwa, ni kusema, unapaswa kuwa tayari kuvumilia magumu fulani na kuachana na mambo fulani. Lakini baraka zenye utapata zinapita sana magumu yenye utavumilia na mambo yenye utaachana nayo. Ubatizo unaweza kukuokoa, na unakusaidia ukuwe na zamiri ya muzuri mbele ya Mungu. Sababu kubwa yenye inapaswa kukuchochea uamue kubatizwa ni kumupenda Yehova Mungu. Unapaswa pia kuamini kwa moyo wako wote mafundisho yenye umejifunza juu ya Baba, Mwana, na roho takatifu. Kisha kufikiria mambo yenye tumezungumuzia mupaka hapa, utajibu namna gani ulizo hili: “Niko tayari kubatizwa?”

MAMBO YENYE UNAPASWA KUFANYA MBELE YA KUBATIZWA

17. Mutu anapaswa kufanya mambo gani mbele abatizwe?

17 Kama unaona kwamba uko tayari kubatizwa, ile inaonyesha kama tayari umeanza kufanya mambo fulani ili kuwa na urafiki muzuri na Yehova. * Kwa sababu unajifunza Biblia kwa ukawaida, umefikia kujua mambo mingi juu ya Yehova na Yesu. Umekuwa na imani. (Ebr. 11:6) Unaamini kabisa ahadi za Mungu zenye kuwa mu Biblia, na uko hakika kama kuwa na imani katika zabihu ya Yesu kunaweza kukuokoa katika zambi na kifo. Umetubu zambi zako, ni kusema, umehuzunika sana juu ya makosa yenye ulifanya, na umemuomba Yehova musamaha. Umegeuka, ni kusema, umeachana kabisa na maisha yako ya mubaya ya zamani na umeanza kuishi maisha yenye kumupendeza Mungu. (Mdo. 3:19) Uko na hamu kabisa ya kuambia wengine mambo yenye unaamini. Ulitimiza mambo yenye inaombwa ili kuwa muhubiri mwenye hajabatizwa na ulianza kuhubiri pamoja na kutaniko. (Mt. 24:14) Yehova anajivunia wewe kwa sababu umefanya ile mambo ya lazima. Umefurahisha sana moyo wake.​—Mez. 27:11.

18. Ni mambo gani ingine yenye unapaswa kufanya mbele ya kubatizwa?

18 Kuko mambo ingine fulani yenye unapaswa kufanya mbele ya kubatizwa. Kama vile tumejifunza, unapaswa kujitoa kwa Mungu. Usali kwake kwa moyo wote wakati uko peke yako, na umuahidi kama utatumia maisha yako ili kufanya mapenzi yake. (1 Pe. 4:2) Kisha, uambie muratibu wa baraza la wazee kama unapenda kubatizwa. Ataomba wazee fulani wazungumuze na wewe. Tafazali, usiogope wakati watazungumuza na wewe. Tayari ndugu hao wapendwa wanakujua na wanakupenda. Watachunguza na wewe mafundisho ya musingi ya Biblia yenye umejifunza. Wanapenda kuhakikisha ikiwa unaelewa ile mafundisho na ikiwa unajua kama kujitoa kwa Mungu na kubatizwa ni hatua za maana sana. Wakiona kama uko tayari kubatizwa, watakuambia kama utabatizwa ku mukusanyiko wa muzunguko ao wa eneo wenye kufuata.

MAMBO YENYE UNAPASWA KUFANYA KISHA KUBATIZWA

19-20. Unapaswa kufanya nini kisha kubatizwa, na ni mambo gani inaweza kukusaidia kufanya vile?

19 Kisha kubatizwa, unapaswa kufanya nini? * Kumbuka kama kujitoa kwa Mungu ni naziri na kama Yehova anakuomba uitimize. Kwa hiyo, kisha kubatizwa, unapaswa kutimiza naziri yenye ulifanya wakati ulijitoa kwa Mungu. Ni mambo gani inaweza kukusaidia kufanya vile?

20 Endelea kuwa karibu na ndugu na dada zako. Kwa sababu umebatizwa, uko sasa katika ‘ushirika wa ndugu.’ (1 Pe. 2:17) Ndugu na dada zako mu kutaniko lako wako familia yako ya kiroho. Wakati unahuzuria mikutano kwa ukawaida, unafanya urafiki wako pamoja nao ukuwe nguvu. Soma Neno la Mungu kila siku na ufikiri sana juu ya mambo yenye unasoma. (Zb. 1:1, 2) Kisha kusoma sehemu fulani ya Biblia, tumia wakati fulani ili kufikiri sana juu ya mambo yenye umesoma. Ukifanya vile, mambo yenye umesoma itagusa moyo wako. ‘Sali bila kuacha.’ (Mt. 26:41) Sala zako zenye kutoka mu moyo zitakusaidia umukaribie Yehova zaidi. ‘Endelea . . . kutafuta kwanza Ufalme.’ (Mt. 6:33) Unaweza kufanya vile kwa kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza mu maisha yako. Wakati unahubiri kwa ukawaida, unaendelea kufanya imani yako ikuwe nguvu, na unaweza kusaidia wengine waingie mu barabara yenye inaongoza kwenye uzima wa milele.​—1 Ti. 4:16.

21. Ubatizo utakuletea faida gani?

21 Uamuzi wa kujitoa kwa Mungu na kubatizwa njo uamuzi wa maana sana kupita maamuzi yote yenye unaweza kukamata mu maisha. Ni kweli kwamba unapaswa kuvumilia magumu fulani na kuachana na mambo fulani. Lakini je, baraka zenye utapata zinapita kabisa magumu yenye unapaswa kuvumilia na mambo yenye unapaswa kuachana nayo? Ndiyo kabisa! Magumu yoyote yenye unaweza kupata katika ulimwengu huu muovu ni ‘ya wakati kidogo na ni ya mwepesi.’ (2 Ko. 4:17) Lakini, ubatizo utakusaidia ukuwe na maisha yenye furaha zaidi sasa na “uzima wa kwelikweli” wakati wenye kuja. (1 Ti. 6:19) Kwa hiyo, tafazali, ufikiri sana na usali juu ya jibu lako kwa ulizo hili: “Niko tayari kubatizwa?”

WIMBO 50 Sala Yangu ya Wakfu

^ fu. 5 Uko unafikiria kubatizwa? Kama ni vile, habari hii imetayarishwa kabisa kwa ajili yako. Tutazungumuzia maulizo fulani ya maana kuhusu ubatizo. Majibu yako kwa ile maulizo itakusaidia kuamua ikiwa uko tayari kubatizwa.

^ fu. 19 Kama haujamaliza kujifunza kitabu Biblia Inatufundisha Nini? na Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu, unapaswa kuendelea kujifunza na mwalimu wako wa Biblia mupaka umalize vile vitabu viwili.