Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Polisi Wayahudi wa hekalu walikuwa nani? Walikuwa na kazi gani?

Walawi fulani wenye hawakukuwa makuhani walikuwa na kazi zingine, kwa mufano walikuwa maofisa wa polisi. Waliongozwa na kapiteni wa hekalu. Ili kueleza kazi mbalimbali za wale maofisa, Philo, muandikaji mumoja Muyahudi alisema hivi: “Wamoja kati ya [Walawi] hao walikuwa wanasimama kwenye kila muingilio ili kufanya kazi ya ulinzi, wengine walikuwa [katika eneo la hekalu] mbele ya patakatifu ili kuzuia watu wenye hawastahili wasiingie pale kimakusudi, ao bila kukusudia. Wengine walikuwa wanazunguka eneo la hekalu ili kulilinda. Walikuwa wanagomboana: wamoja muchana, wengine usiku.”

Sanhedrini ingeweza kuomba polisi hao wawasaidie. Ni wao tu njo Wayahudi wenye utawala wa Roma uliruhusu kubeba silaha.

Joachim Jeremias, mutu mumoja mwenye elimu, anasema kama wakati maofisa walimukamata Yesu, aliwauliza juu ya nini hawakumukamata wakati alikuwa anafundisha mu hekalu. (Mt. 26.55) Anasema pia kama Yesu hangewauliza vile ikiwa hawangekuwa polisi wa hekalu. Muandikaji huyo anaamini kama wale wenye walitumwa mbele ya pale ili kumukamata Yesu walikuwa pia polisi wa hekalu. (Yoh. 7:32, 45, 46) Kisha, Sanhedrini ilituma kapiteni wa hekalu na maofisa fulani ili walete wanafunzi wa Yesu mbele ya Sanhedrini na inaonekana kama ni polisi wa hekalu njo walimukokotea Paulo inje ya hekalu.​—Mdo. 4:1-3; 5:17-27; 21:27-30.